Kwa akili yako unadhani "katulizwa"? Mbona ndio kama amesukumwa na kupewa nguvu zaidi ya kudai hayo hayo, na pengine zaidi?
Watu wengine huwa hamtumii akili kutambua hali halisi ya mambo ilivyo.
Kwanza wewe mwenyewe angalia unavyojichanganya. Kama Mbowe alikuwa "anashinikiza kukutana na mama", huoni sasa kakutana naye, tena mama hakuwa na subira ya kumwacha apumzike kidogo kabla ya kumkaribisha ikulu? Wewe unadhani mama hajui anachofanya, bali wewe ndio mjuaji? Bure kabisa.