Maandamano ya leo ya CHADEMA yamedhihirisha unafiki wa Watanzania hasa vijana tofauti na Wakenya

Tumia akili ...chadema ni genge la mafisadi na vibaraka wa mafisadi wa ndani na wa nje ya nchi hakuna mzalendo hata mmoja. Nikama zitto kabwe tu.. chama cha chadema hakina tofauti na mchawi....ambaye anajidai mwema kumbe usiku ana wanga ...
Una uhakika na unachonena?
 
Wao waliandamana kupinga finance bill , sisi tumeandamana kupinga utekaji , kwahiyo hamna excuse
Tatizo mmetanguliza wanasiasa misukule ambao mpaka watoto wadogo wanajua ni wehu hao.

Gen z walijiteua wenywe wakaandamana kwa kauli moja ndo maana walifanikiwa.

Mtu kama mbowe wa kutuambia nini sisi tumsikilize??
 
Maandamano ya Kenya usiyafananishe na huu upuuzi wa huku Tanzania, maandamano ya kupinga serikali yanafanywa na wananchi na sio wanasiasa.
Wanasiasa nawao ni wananchi kama wewe
yaani hii comment yako inaonyesha uwezo wa watanzania wengi ni mdogo sana
 
Una uhakika na unachonena?
1000% majuzi tundu lissu kasema kuhusu rushwa ya ccm kwa viongozi wa chadema .... chadema ilikuwa inatumiwa na genge la wahuni na raia feki kina rostam azizi kupinga maendeleo ya nchi yetu chini ya JPM kwa kupigania maslai ya kina rostam azizi kama kupinga kujengwa kwa bwawa la umeme la nyerere hili fisadi rostam na genge lake waendelee kuwakamua watz kwa bei ya juu ya gesi maana walijua kuwa chini ya Jpm bwawa likikamilika bei ya umeme ingeshushwa kwa nusu na kuvuluga ubiashara yao ya kuwanyovya watz kwenye gesi.
 
Tatizo mmetanguliza wanasiasa misukule ambao mpaka watoto wadogo wanajua ni wehu hao.

Gen z walijiteua wenywe wakaandamana kwa kauli moja ndo maana walifanikiwa.

Mtu kama mbowe wa kutuambia nini sisi tumsikilize??
yaani wewe unayetumia jina bandia huwezi jiweka sentensi moja na mbowe
 
Huyo jpm alimpigia rostam magoti akamuomba arudi aje awekeze
 
Huyo jpm alimpigia rostam magoti akamuomba arudi aje awekeze
Magufuli alikuwa mjanja sana kwenye mbinu ya kupambana na mafisadi lengo nikurudisha mali alizo pora kisha anamalizwa maana huyo rostam ni jambazi kubwa sana nchini .
 
Sio kweli watu walianza kudhibitiwa na kutishwa na kukamatwa tangu Alhamisi last week
 
Sio kweli watu walianza kudhibitiwa na kutishwa na kukamatwa tangu Alhamisi last weekView attachment 3104659
 
Magufuli alikuwa mjanja sana kwenye mbinu ya kupambana na mafisadi lengo nikurudisha mali alizo pora kisha anamalizwa maana huyo rostam ni jambazi kubwa sana nchini .
Alirudisha zipi nawakati na kiwanda alifungua cha Taifa gas acha uongo na mpaka leo anakula faida
 
Wameandamana mapolisi. This time jwtz halijajihusisha kabisa na hizi drama
 
Wanahatarisha maisha kwa watu ambao wapo bize na Simba na Yanga. Ni kuwaacha tu wakipigika kisawasawa watazinduka na kutetea haki zao bila kuhitaji Kiongozi wa kuwasemea.
 
Si unafiki bali elimu ya uraia kwa vijana wa Kitanzania bado. Pia elimu ya Wakenya ipo juu kwa ujumla hivyo wanajitambua.
 
Angalia haya maeneo ya Kibera, Mathare hapa ambapo ni kilometres sita toka Nairobi.



Hakuna Mtanzania Dar es Salaam anayeishi kwenye uchafu kama huu

 
Watanzania sio wajinga.
 
Wanasiasa nawao ni wananchi kama wewe
yaani hii comment yako inaonyesha uwezo wa watanzania wengi ni mdogo sana
Sina uwezo mdogo, ila nmeongea kitu ambacho hakijakufurahisha bila kujali n sahihi au siyo.
Kwahy samia n sawa na wananchi wa kawaida?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…