Mabadiliko Baraza la Mawaziri: Doto Biteko ateuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Makamba Mambo ya Nje, Pindi Chana Katiba na Sheria

Mabadiliko Baraza la Mawaziri: Doto Biteko ateuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Makamba Mambo ya Nje, Pindi Chana Katiba na Sheria

Rais Samia Suluhu amefanya mabadiliko na teuzi za sura mpya kwenye baraza la mawaziri. Uapisho utafanyika September 1, Ikulu ndogo Zanzibar saa tano kamili asubuhi.
1. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Doto Biteko kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Awali alikuwa Waziri wa Madini.

2. Amemteua January Makamba kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali alikuwa Waziri wa Nishati.

3. Amemhamisha Balozi Pindi Chana kuwa Waziri wa Katiba na Sheria. Awali alikuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo.

4. Amemhamisha Steven Byabato kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali, Byabato alikuwa Naibu Waziri wa Nishati.

5. Amemteua Jerry Silaa kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Silaa ni Mbunge wa Ukonga, Dar es Salaam.

6. Rais amemteua Anthony Mavunde kuwa waziri wa madini, mwanzo alikuwa naibu waziri wa kilimo.

7. Prof Makame Mbarawa aliyekuwa waziri wa ujenzi na uchukuzi amekuwa waziri wa uchukuzi.

8. Innocent Bashungwa amekuwa waziri wa ujenzi, mwanzo alikuwa waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa.

9. Godfrey Kasekenya aliyekuwa Naibu waziri wa Ujenzi na uchukuzi ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Ujenzi

10. Alexander Mnyeti ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Kilimo

11. David Mwakiposa Kihenzile ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Uchukuzi. Ni mbunge wa Jimbo la Mufindi

12. Judith Kapinga ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa nishati, ni mbunge wa viti maalum Ruvuma.

13. Dunstan Kitandula ameteuliwa Naibu Waziri wa maliasili na Utalii, ni mbunge wa Mkinga

14. Stergomena Tax amehamishwa wizara ya mambo ya Nje kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

15. Angellah Kairuki amehamishwa kutoka TAMISEMI na kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii

16. Dkt. Damas Ndumbaro amehamishwa kutoka Wizara ya Katiba ba Sheria na kuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo.




View: https://www.youtube.com/watch?v=7bLEuvgVGG4

======

View attachment 2733279
View attachment 2733280
View attachment 2733281
View attachment 2733282

Kassimu majaliwa unapewa ujumbe hapa. Je unapwaya au hawakutaki? kwanini umepewa msaidizi Tena kinyume cha katiba?
Lakini uteuzi huu wa naibu waziri mkuu na huyo mnyeti ni danganya toto kwa wasukuma ambao wameoneka kuwa na mwitikio mkubwa katika oparesheni za Chadema na ni dhahiri hawataki kusikia kuhusu sa100.
 
Rais anao uwanda mpana wa kubadili wizara na kuwaweka Mawaziri kwa kadri atakavyo.

Kwa uzoefu wangu sikuwahi kusikia Kiongozi aliyewahi kuwa Naibu Waziri mkuu.

Hata hivyo kama Rais ana Makamu wake iweje Waziri mkuu asiwe na Naibu?

Nilipochanganyikiwa zaidi ni Kiongozi mmoja kuwa Naibu Waziri na Waziri ktk serikali hiyohiyo. Inawezekanaje?

Kwamba Pale bungeni na huko mitaani hakuna wanachama wa CCM wenye weledi kiasi cha kumtwisha majukumu mazito ndugu Dotto?

Tuombe Mungu uteuzi huu uwe na malengo ya kuimarisha ustawi wa wananchi wote na si kumdhoofisha mtu flani kwa manufaa ya watu wachache.
 
Huyu mama utawala wake itakuja kuwa na makosa mengi sana na skendo kibao. Tujipe muda maana inaonekana kama mama anashauriwa vibaya yaani "Anapigwa saundi" na anakubali.
 
Mwinyi awamu ya pili alimteua mrema kuwa Naibu waziri mkuu sasa awamu ya sita kaja na Naibu waziri mkuu tena.
 
Rais angejiuzuru tuchangue mtu anayejielewa. Huwezi kuteua cheo ambacho hakipo kikatiba
Lakini japo hakipo kikatiba, lakini kilishawahi kulazimishwa kipindi kile cha Rais Mwinyi, akamteua Mrema!! Mrema kuwa naibu waziri mkuu!! Mrema Alipoteuliwa kuwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa anaingilia kila wizara kama akinusa kuna harufu ya ufisadi. Mawaziri wakawa wanamlalamikia kuwa anaingilia wizara zao!! Mwinyi alipoona hivyo akaamua kumfanya Waziri wa mambo ya ndani na naibu waziri mkuu!! Kwa nafasi hiyo alikuwa na mamlaka ya kuhoji utendaji na ubadhirifu kwenye wizara yoyote!! Mrema alifanya kazi hiyo kwa mafanikio sana!! Hilo ndilo lilikuwa ni lengo. Tujiulize kwa leo lengo ni lipi?
 
Rais anao uwanda mpana wa kubadili wizara na kuwaweka Mawaziri kwa kadri atakavyo.

Kwa uzoefu wangu sikuwahi kusikia Kiongozi aliyewahi kuwa Naibu Waziri mkuu.

Hata hivyo kama Rais ana Makamu wake iweje Waziri mkuu asiwe na Naibu?

Nilipochanganyikiwa zaidi ni Kiongozi mmoja kuwa Naibu Waziri na Waziri ktk serikali hiyohiyo. Inawezekanaje?

Kwamba Pale bungeni na huko mitaani hakuna wanachama wa CCM wenye weredi kiasi cha kumtwisha majukumu mazito ndugu Dotto?

Tuombe Mungu uteuzi huu uwe na malengo ya kuimarisha ustawi wa wananchi wote na si kumdhoofisha mtu flani kwa manufaa ya watu wachache.
Nadhani marehemu Lyatonga Mrema aliwahi kuwa Naibu Waziri Mkuu kama sikosei
 
DP World imembeba Jerry Silaa
Huyo mtoto yupo kwenye Circe yao kitambo, ameshakuwa meya wa Ilala na mjumbe wa Kamati kuu ya Ccm, huwezi kupata hizo nafasi hivihivi.

Ingekuwa upambe tu unalipa hata Pascal Mayalla angepata uteuzi lakini wapi hata ukuu wa wilaya hajawahi kufikiriwa pamoja na kujitowa akili kote.
 
Back
Top Bottom