Mabadiliko ya mwonekano JamiiForums - Juni 2022

Mabadiliko ya mwonekano JamiiForums - Juni 2022

Nataka kuona post, Niki click Recent thread zinaonekana za mwanzo za mbele sio, anajua
 
JF kwa sasa mwonekano wake umekua kama blog fln hv. Haina tena mwonekano wa forum. Pitieni reddit au quora labda mnaweza pata idea.

Yaan ile radha ya forum imetoka kabisa hasahasa baada ya kuondoa forum listing kwenye landing page upande wa mobile.

Font size nayo duuh.
Inakosesha ata raha yani... Mods na Bwana Melo bring back our JF!

Na kingine sisi ndo walaji na nadhani mmeshapata maoni, wengi wetu atujapenda maboresho yenu ya kipindi hiki!
 
Katika eneo ambalo halikuhitaji mabadiriko , ni kuihamisha general forum na kuiweka pembeni badala yake trending ndo inakuwa ya Kwanza , na pia kubadili font na kuyakuza maneno Yani kama vitabu vya darasa la pili kuandika ...boring Sana aisee
 
Ongezeni jukwaa la hoja mijadala ya kidini.
Hapa ni mambo yote kuhusu dini Ukristo, Uislamu, Uchawi, Rastafarian, nk.
 
Wamechemka sana... Inakosesha ata raha yani... Mods na Bwana Melo bring back our JF!

Na kingine sisi ndo walaji na nadhani mmeshapata maoni, wengi wetu atujapenda maboresho yenu ya kipindi hiki!
Mbona forum zipo
 
mi naomba Jf iende ifike mahala tuwe na option ya kuwa portal zetu wenyewe kama ilivyo Facebook na zinginezo... where we can login using genuine userID's.
 
where we can login using genuine userID's.
Halafu jukwaa la siasa liwe hatariii🙄
Ukitoa maoni flani, kutekwa nje nje!!!

Ila hata saivi ukiamua kutumia majina yako halisi humu inawezekana tu. Kuna wanaofanya Hivyo.

Hata huko Fb, Twitter... siyo kila mtu anatumia real name
 
app ya zamani nilikua siwezi kuplay media moja kwa moja kwenye app mpaka ni download sjui kama sasa mmelirekebisha hilo
 
Halafu jukwaa la siasa liwe hatariii🙄
Ukitoa maoni flani, kutekwa nje nje!!!

Ila hata saivi ukiamua kutumia majina yako halisi humu inawezekana tu. Kuna wanaofanya Hivyo.

Hata huko Fb, Twitter... siyo kila mtu anatumia real name
Tusiogope..mambo yamebadilika si kama wakati ule wajinga wajinga wanaua watu werevu.
 
Wakuu,

Tupo kwenye hatua za mwisho kuja na JF yenye mwonekano mpya ambayo inaendana na mabadiliko ya teknolojia. Kwa wanaohitaji kuwa sehemu ya majaribio, mnakaribishwa...

Katika mabadiliko haya, huenda ukakutana na kitu kikakufurahisha, kikakuchanganya, kikakufanya uone kuna haja ya kuongeza au kupunguza n.k - usisite kutujulisha kupitia uzi huu.

Thread hii itatumika kukusanya maoni yenu na yatazingatiwa ajili ya kujenga sehemu bora na salama zaidi kwa ajili ya kila mmoja wetu.

Kwa wale watumiaji wa App, tunashauri kujaribu App Mpya ya JamiiForums: Fuata hatua hizi kwani itaendana vema zaidi na kinachokuja.

Tunawashukuru kwa ushirikiano mnaotupa kila mara kwani hadi toleo hili ni tokana na maoni yenu.

Kutakuwa na features kadhaa hazitakuwa released mapema hadi zikamilike kufanyiwa testing ndipo ziwe applied.

Tunawapenda, tunawajali na tunaahidi kuendelea kutoa huduma bora.

Asanteni sana!

===== UPDATES======

Changes on the new version:

1) Kuna urahisi wa kufichua mambo mazito bila data zako zozote kuchukuliwa na bila post kwenda public kwanza (utaona button ya Fichua Uovu). Hii itasaidia hata wasio wanachama (baadae) kushiriki kikamilifu kupinga ufisadi na rushwa kwa ujumla.

2) Faragha ya mwanachama imelindwa zaidi, hakuna wa kujua wewe ni nani on JF bila wewe kumpa access ya kifaa chako (simu, tablet au pc). Tulipata vilio vya watu kuchunguliwa IDs tukaja na suluhu.

3) Unaweza kuchagua kutumia JF ikiwa light version, dark mode au dark blue mode (my favorite).

4) Maandishi ya sasa yanasomeka kirahisi zaidi na wenzetu wenye uoni hafifu. Wasioona kabisa lakini wana vifaa vya kusomea wataweza kuitumia JF kwa urahisi zaidi.

5) Soon kuna mambo mapya yanaanza kufanyika via JF, mabadiliko haya yamelenga kupokea yajayo kuanzia mwezi huu na kuendelea.

6) Ukiwa kwenye forum yoyote, huhitaji kubonyeza Page 2, Page 3, Page 4. Wewe vuta kwenda chini tu, mada zitakuja (scroll down).

Nitaendelea…
Is it possible to have different italic options from this new current one?
 
Mods najua mmeshika mpini na sisi tumeshika makali lakini hamjatutendea haki kwa kuondoa Uzi wa kupigia kura muonekano mpya wa jamii forum niliouanzisha jana saa 7:20pm

niwe muwazi sijawahi soma vigezo & masharti vya JF lakini sizani kama kuna sheria nimeivunja kwa kuuweka huo uzi hapo jukwaani

kwa hisia zangu nahisi Uzi umeondolewa kwa sababu ya kuonekana kura nyingi zilikuwa zikionesha kutokufurahishwa na mwonekano mpya wa Jamii Forum

please Maxence Melo naomba angalia namna ya kuurudisha huo uzi au anzisheni nyie uzi mwingine wa kupigia kura mabadiliko ya mwonekano wa JF
 
Yan JF hata mimi kwasasa inanipa uzito sana na siifurahii kabisaaaa kila napopata wazo la kuingia..Yana it is BORING yan ni kama wameamua kuendana na features za kwenye Linked in na Quora..VERY VERY VERY BORING INDEED
 
Back
Top Bottom