Mabadiliko ya mwonekano JamiiForums - Juni 2022

Mabadiliko ya mwonekano JamiiForums - Juni 2022

Kuwa na heshima, Melo ni Kama Baba tukiwa humu😂😂😂😂🤭🤭
Chengine wekeni kitufe cha kuomba msamaha ban ya wiki mbili sio mchezo nyie..!

Max melo uje ujaribu nawewe kujipiga ban uone utamu kunoga..😂
 
Tunayasubiri kwa hamu kubwa hayo maboresho.

Kingine mjitahidi kuzingatia maadili. Lugha za matusi na zisizo za kistaarabu zimeshamiri sana. Watu wanatukana matusi mazito sana humu. Lifanyieni kazi.
 
Wakuu,

Tupo kwenye hatua za mwisho kuja na JF yenye mwonekano mpya ambayo inaendana na mabadiliko ya teknolojia. Ndani ya saa 72 zijazo mabadiliko haya yataonekana kwa wengi.

Katika mabadiliko haya, huenda ukakutana na kitu kikakufurahisha, kikakuchanganya, kikakufanya uone kuna haja ya kuongeza au kupunguza n.k - usisite kutujulisha kupitia uzi huu.

Thread hii itatumika kukusanya maoni yenu na yatazingatiwa ajili ya kujenga sehemu bora na salama zaidi kwa ajili ya kila mmoja wetu.

Kwa wale watumiaji wa App, tunashauri kujaribu App Mpya ya JamiiForums: Fuata hatua hizi kwani itaendana vema zaidi na kinachokuja.

Tunawashukuru kwa ushirikiano mnaotupa kila mara kwani hadi toleo hili ni tokana na maoni yenu.

Kutakuwa na features kadhaa hazitakuwa released mapema hadi zikamilike kufanyiwa testing ndipo ziwe applied.

Tunawapenda, tunawajali na tunaahidi kuendelea kutoa huduma bora.

Asanteni sana!
Namna hiyo, kazi nzuri...

Muupigeni mwingi kwenye huo muonekano mpya.
 
Pamoja sana Mr.Max, JF is our sanctuary, our temple where we learn and unlearn, our hub of "just be whoever you are" , voice of justice and so much more.. we thank you for this precious gift.. keep it up!!
 
Ahsante , nashauri app yenu iliyopo play store kwa watumiaji wa mfumo wa Android iboreshwe, msiitoe maana Kuna sehemu niliona mnataka /mna mpango wa kuitoa ili tuwe tunatumia app iliyoko kwa website yetu kitu ambacho nimejaribu kuitumia na kubaini kuwa haina Radha kabisa,

Binafsi sijawahi kuielewa kabisa app yenu iliyoko kwa site kuliko ya play store. Mkiitoa huko play store mtanitesa sana
 
Shukran sana mkuu
So logo yetu itabadilika pia au itabaki kama ilivyo manake tumeizoea sana
 
Back
Top Bottom