Mzee wa kupambania
JF-Expert Member
- Aug 14, 2022
- 21,111
- 53,092
Anayenunua Mchina tatu badala ya Polo moja ndiye mwenye akili ya biasharaKatarama moja unanunua Mchina tatu
Kufa tutakufa tu mkuu ajali popote inaweza kutokea hata ukiwa unasafiri na daladalaNyie mnaoshabikia mwendo kasi siku usikie basi limeua mkeo, mumeo, mtoto au ndugu yako yeyote wa karibu sidhani kama utaendelea kushangilia huu upuuzi, juzi johanvia ya musoma dar imeua pale morogoro chanzo ni mwendokasi
Wanazi wa Katarama ni wajinga sana yaani wanaongeaga pumba sanaHii ligi huwa inanishangaza kitu kimoja tu, hizo katarama ukikuta wanazi wanavozifia alafu kaangalie mikeka sasa utashangaa mwenyewe.
Yaani kwenye mikeka ni tofauti na wanavozisifia,
Mikeka ya mwezi mzima ally's ndo huwa inafungua geti mara nyingi kuliko gari zote ila sasa wanazi wakute wanasifia katarama!
Kuna jamaa anasema katarama anafika dodoma saa 3 asubui kama vile ni jambo la ajabu!! Wakati hao wote wanatoka saa 9 usiku dodoma wanapitaga wote saa 3
ww panda Najimunisa au ZuberiTutajieni zinazoenda mwendo wa kobe mimi hizo za ligi hapana kwakweli
Allys ana gari nyingi sana na zilizofungiwa ni ebf 3 na dxs 3 bado kuna farsi weupe EBG, kuna EBU,DVA sasa huyo katarama ana gari tatu zote zimepigwa banIla kwa wapenzi wa hayo mabasi bado wataendelea yasubiri.
Hao wengine watakosa masoko vile vile.
Hapo imefanyika kufungia basi zote. Ila watalalamika kwa Sagini watafunguliwa
huyu mshereheshaji ndio amewaponza.!View attachment 2662535
Uamuzi huo umetolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Ardhini (LATRA) baada ya kubaini Mabasi hayo kuchezea Mfumo wa Kufuatilia Mwendo (VTS) kwa lengo la kusafiri kwa Mwendokasi ili kushindana kufika Stendi.
Kwa mujibu wa LATRA, watoa huduma hao wamekuwa wakitumia fursa ya kuanza safari mapema (Saa 9 Usiku hadi 11 Alfajiri) kwa kufanikisha malengo ya kufanya mashindano huku kukiwa na wanaobashiri Basi linalofika mapema wakipata ushindi kwenye Kamari.
Mabasi 6 ya Allys Star na Matatu ya Katarama yamerudishwa kwenye ratiba ya ya kuanza safari Saa 12:00 Asubuhi kuanzia Juni 21, 2023. Aidha Kampuni ya Isamilo imepewa onyo kali la mwisho kabla ya kuchukuliwa hatua stahiki.
--
View attachment 2662579View attachment 2662580View attachment 2662581
Anaua gari sasa, service za haraka nanma hiyo sidhani kama zinafanyika kwa viwango sahihi.usiku kwa usiku babake akuna kudozi.
Soma vzr ilitoka saa9 usiku dar ikafika bariad saa 2 usikuIlifika Bariadi SAA 9 ikitokea wapi?
Huyo farasi mweupe EBG ana balaaAllys ana gari nyingi sana na zilizofungiwa ni ebf 3 na dxs 3 bado kuna farsi weupe EBG, kuna EBU,DVA sasa huyo katarama ana gari tatu zote zimepigwa ban
Ndio mkuu, Ally's ana akili sana. Katarama kapewa akina DXS roho za paka wamchekeche humo road, muda huohuo zipo DVA na EBG zinatembea zimerelax.Allys ana gari nyingi sana na zilizofungiwa ni ebf 3 na dxs 3 bado kuna farsi weupe EBG, kuna EBU,DVA sasa huyo katarama ana gari tatu zote zimepigwa ban
Kufa tutakufa tu na kufa ni vizuriKufa tutakufa tu mkuu ajali popote inaweza kutokea hata ukiwa unasafiri na daladala
Kwa polo abiria 60 kwa Hela ya polo mchina una abiria 180 mchina fasta mtaji unarudii polo hadi miaka 10 mchina miaka 3Anayenunua Mchina tatu badala ya Polo moja ndiye mwenye akili ya biashara
Si umeona kampuni kongwe kama Abood na Shabiby wamehama kutoka Scania Marcopolo na Volvo sasa hivi ni mwendo wa Yutong
Safari yoyote ukifika salama ni kushukuru MunguKufa tutakufa tu na kufa ni vizuri
Shida ni kukatika viungo afu unabaki mzima unaanza kuwa omba omba
Hii ndio maana ya biasharaKwa polo abiria 60 kwa Hela ya polo mchina una abiria 180 mchina fasta mtaji unarudii polo hadi miaka 10 mchina miaka 3
Hiyo itakuwa ya Morogoro. Upo shy sehemu gani weye?Nilishangaa sa kumi na moja kasoro ally's mwanza dar anapita pale shinyanga
Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app