Mabenki yaanza kukusanya Tozo za Serikali kwenye miamala wanayofanya wateja

Nilipata hiyo message niliingia kwenye statement kucheki yàani wamelamba akiba yangu yote ya kula na wanangu ukizingatia kipindi Hicho niliwatumia pesa watu mbali mbali.

Kwa kweli nimebaki kuwa mnyonge saana
 
Muwe mnafuatilia kauli za serikali,walisema watakusanya pesa kwenye miamala yote ya kifedha kwenye simu na mabenki

Miamala ya mabenki maana yake nini?

Niki deposit pesa kwenye account yangu au mtu aki deposit pesa kwenye account yangu huo ni muamala wa kutolewa tozo?

Ufafanuzi huo ulitolewa wapi na rates ziko je?

Binafsi ninawafuatilia sana manunda hawa wasiokuwa na chembe ya uchungu na sisi zaidi yao na familia zao.

Niliacha kutumia miamala ya simu. Nikikuta tunarambana tozo kinyemela benki, tutaulizana.

Hata SABAYA alidhani alikuwa akiitendea mema nchi.
 
Ukiona ume deposit wamekata ujue ni madeni ila ku deposit hawakati bali ku withdrawal,, kwenye miamala ya simu ukideposit hawakati ila ku draw au kutuma na kwenye mabenki ni hivyo hivyo.

Kopa kwenye mtandao au benk afu deposit uone moto.

Lipa kodi kwa maendeleo ya nchi.
 
Aliemwambia Mama hizi 200 za kukata watu kihuni zinaweza kuendesha nchi kampoteza sanaa yani Huu ni wizii... Bora alikubali Viatu vya Magu haviwezi maana huu ni Upuuzi na kuumiza maskini..!!
 
Labda unamaanisha kuwa hela ya kununulia ndege lazima ipatikane maana tumeshaambiwa kuwa mkopo wa IMF ndo unatumika kujenga hivyo vitu ulivyovitaja(vituo vya afya, madaraa etc)
 

Huna unalolijua chawa wa mama na CCM wewe.

Tozo za uzalendo uchwara ziko kwenye kutumia pesa kwenda kwa mtu mwingine ambapo mitandao ya simu inatumika.

Ndiyo maana tulioamua kuachana na kutuma pesa au kumpa boda boda apeleke tumepishana nazo na Mwigulu anaugulia maumivu.



Hakuna taarifa ya tozo kwenye ku deposit au ku withdraw pesa kwenye account yako benki au Mpesa bali kwenye transfer.

Kama chawa hujaelewa kaeleweshwe ili uimbe mapambio yenu kwa usahihi:

Your browser is not able to display this video.


Usijikite kwenye kuleta vipya usivyovijua.
 
Huyo ndo Samia[emoji16][emoji16][emoji16].
Maumivu Yale Yale tofauti NI mtoa adhabu.yule alikuwa anatupiga huku anatuambia ila huyu kimya kimya.
Crdb ukiangalia kila ukiangalia salio wanakata sh 100 salio la kawaida.
 
Unadhani usipolipa kodi pesa ya kujenga itatoka wapi? Lipa kodi hakuna njia za mkato saizi.
Kodi zina taratibu zake, mimi ni mlipa kodi haswa, inavyoonekana sasa ni double taxation ndio tunalalamika,pia tunaweza tukawa tunalipa kodi nyingi lakini kama zinatumiwa hovyo hakuna maendeleo yoyote tutakayopata. Na mwisho mnaojifanya wazalendo wa kulipa kodi mnakuwa sio walipaji kodi ndio maana hamujui sisi tunaolipa kodi tunavyoumia kwa kukatwa hovyo hovyo wakati hukukwingine tayari tumeshalipa hizo kodi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…