Tetesi: Machache aliyonieleza mfanyakazi wa TPA yana ukweli?

Tetesi: Machache aliyonieleza mfanyakazi wa TPA yana ukweli?

Sio kweli serikali itateua watu wale wale kuongoza hiyo authority kama kina Chenge, Hawa Ghasia n.k Sasa unategemea ufanisi au uhuru wa taasisi? Hao ndio wataiba kweli kweli
Nyie kila siku mnajinadi kuwa vipo vyombo vya usalama makini kama vile Polisi na TISS. Sasa mbona hao mnaosema ni wezi na mafisadi hawashughulikiwi na hizo taasisi zenu?
 
Utapatikana ufanisi na wingi wa mapato halafu? Tutarudi tena kujadili matumizi ya hayo mapato.

Tutaziba mirija ya watu huko bandarini hali ya kuwa kwengineko huko mirija yao bado inaendelea kufanya kazi.
 
Sasa wanaambiwa muachane na Biashara ya simu mbaki na mkongo wa Taifa tu unategemea nini? Mbona "Rudi nyumbani kumenoga" ilishika kasi! Na kweli kweli tukarudi, Sasa isiweje tuambiwe Tena Leo imepiteza wateja laki mbili?
Shida ya serikali inalea wezi na wezi wenyewe wapo kwenye serikali na ni viongozi wakubwa.
Halotel ni ya juzi tu lkn huwezi kuilinganisha na TTCL.
Ukitafuta laini ya Voda, Tigo, Airtel na Halotel zipo nyingi sana mtaani, tafuta ya TTCL utajua shirika lishakufa.
Na kwasasa, TTCL hata waweke mkongo wa taifa tayari ishakufa. Watanzania wengi hawana pesa ya kumudu gharama za internet.
Leo ili utumie 5GB inatakiwa uweka na 10,000 kwa maisha gani?
 
Nani kakwambia uwekezaji maana yake umeshindwa kuendesha?

Hizo fikra mgando ndo zinawafanya kila siku muwe nyuma kimaendeleo
Usifananishe uwekezaji wa nchi zenye akili na huu wakwetu ambao mnaohubiri wenyewe kushindwa kusimamia uendeshaji wa bandari hadi wizi kukithiri.
 
Sahihi.Mm nimeshalisema hili.Hatujawa serious na Bandari.Mbona TRA,Maliasili,Tanroads nk zinaendeshwa na wabongo na hawacheki na Raia.Hawa jamaa ukiingia kwenye anga zao utawatambua.
 
Naeleza kwa ufupi. Wenye kuelewa haraka hongereni.
  1. Bajeti ya Bandari inakata Sept 2023 ambapo kwa mujibu wake anasema kuanzia Oktoba TPA itakuwa ktk wakati mgumu kwenye kujiendesha
  2. DPW walipaswa kuanza shuguli bandarini mnamo Oktoba 2023. Lakini mpaka sasa seems deal halijafikia muafaka.
  3. Siyo kweli kwamba Watanzania hawana uwezo wa kuendesha bandari bali ufanisi hauonekani kwa sababu watawala wamekinga mirija yao bandarini.
  4. Endapo serikali ingeunda mamlaka inayojiendesha kibiashara kusimamia bandari na kuwepo nanusimamizi wa kizalendo, bandari zetu zingeweza kuleta tija mara kumi zaidi ya kinachotarajiwa kuletwa na DPW
Najua humu JF wapo wenye kuyaelewa haya mambo yanavyokwenda, je hizi taarifa zimekaaje?
Ni kweli kabisa tunaweza kutengeneza faida zaidi ya tutakayopata toka DPW. Hii ya kumpa DPW kwa sababu tu ya upigaji na wizi ni kituo cha wala. Hivi DPW ni police. Inawezekanaje majeshi yetu haya na vyombo vya usalama kushindwa kudhibiti wizi!?

Kama report ya CAG imetoka na watu hawachukuliei hatua Unadhani kweli Rais na team yake wako serious na ubadhirifu unaoendelea nchini. Report ya CAG mpaka sasa imefichwa chini ya carpet.
 
Not true, makadirio ya Mapato na matumizi say bajeti yalishapitishwa tokea July huko so haiwezekani iwe na pesa ya miezi 3 tu!!

Kwa mkataba upi? Na hata wangeanza ni Gati kama 3 pekee Sasa hizo zingine zitaendeshwa kwa bajeti ipi maana Dp world haito cover huko at least for now.

Ni kweli ila hao TPA ni mafisadi sana tu, ingawa DP world ni wageni ila wanatafuta faida so lazima watafanya kazi sana Ili waingize faida juu ya mgao wanaotupa. Ila mbadala wa DP world kamwe sio TPA kuendesha bandari ila mwekezaji mwingine mwenye tija na usawa.


Sio kweli serikali itateua watu wale wale kuongoza hiyo authority kama kina Chenge, Hawa Ghasia n.k Sasa unategemea ufanisi au uhuru wa taasisi? Hao ndio wataiba kweli kweli kuliko hao TPA au DP World!!.

We jiulize tu hata TRA ukusanyaji Mapato hauna ufanisi kabisa mfano kitengo Cha International Tax Unit kinatakiwa kikague transfer pricings kwenye MNCs Zenye matrilion ya mtaji Cha ajabu huwa wanakagua 10% pekee ya hayo makampuni!! Ila Cha ajabu ukiwapa kazi say Deloitte au PwC unashangaa watakagua mashirika yote!!

Hizi taasisi za umma ziko corrupt and inefficient tunapoelekea hata TRA itakuja kubinafsishwa maana hawana ubunifu, hawana ufanisi kazi kuomba rushwa tu na kuongeza tozo!!
Unaposema TPA ni mafisadi sijakuelewa?....Malipo yote yanafanyika baada ya kupata Control namba. Pesa inaenda Hazina. Bila control namba uwezi pata huduma. Sasa hapo ufisadi upo wapi?
 
Binafsi nafanya kazi za bandali, nikijionea micontenar inayotoka na kuingia kila siku nasikitika kwanini inchi yetu haisongi mbele. Kunasiku supervisor mmoja alinambia kua, mzunguko wa siku hiyo ilikua contener Mia nane, akisema kua hiyo ni takwimu yakawaida, wakati mwingine zinafika hadi miatsa au elfu moja, na hiyo ni kwaupande mmoja tu ule aliokua amekodishiwa ticts.

Kumbuka pia na TPA Wana upande wao ambao pia mzunguko wake unazidiwa kma 40%. Na kumbuka kila contenar huacha pesa si chini ya milioni moja.
Pesa zote zinakwenda Hazina. TPA wakiomba pesa kwa ajili ya kununulia vifaa vya kazi, Hazina wanasema hakuna pesa. Sasa hapo lawama ya nani?
 
Unaposema TPA ni mafisadi sijakuelewa?....Malipo yote yanafanyika baada ya kupata Control namba. Pesa inaenda Hazina. Bila control namba uwezi pata huduma. Sasa hapo ufisadi upo wapi?
Mafisadi in terms of rushwa maana unaelewa urasimu uliopo. Hata mizigo huwa inapotea sana mazingira ya kutatanisha.

Kingine ufanisi wao upo chini sana na serikali pia CAG amekiri wameshindwa kazi. Sasa solution ni kufanya outsourcing tu maana hata ukibadili wafanyakazi wanaokuja ni Wezi zaidi.

Cha ajabu watu wanakazania ooh bandari itauzwa wanasahau hata sahivi haijauzwa ila Kuna mafisadi machache yanakula hiko hiko kidogo kinachopatikana
 
Pesa zote zinakwenda Hazina. TPA wakiomba pesa kwa ajili ya kununulia vifaa vya kazi, Hazina wanasema hakuna pesa. Sasa hapo lawama ya nani?
Sio kweli hili, bajeti huandaliwa mapema kulingana na makadirio ya Mapato na huidhinishwa, Sasa kivipi pesa ikosekane? Huwa Wana miradi hewa kibao ndio inakula Hela Wala shida Yao sio vifaa ila wizi tu. Unakumbuka kesi ya flow meter kuzimwa? Au Makinikia kusafirishwa bila kukaguliwa kama kilichokua delcared kwenye karatasi ndio kipo ndani ya container?

TPA are bunch of embezzlers, hiyo bandari mara 10 wapewe hata JWTZ pengine tutaona Mapato yakipaa ila hao TPA Are shit.
 
Watanzania tunajifanya wajuaji sana hata katika tusivyovijua, huu uzalendo tunaoutaka ushawahi kuua kiwanda cha Nyama cha Tanganyika Packers, tulimnyang’anya Mzungu aliyekuwa anaendesha kiwanda tukakiweka chini ya serikali ili tunufaike kikafeli baada ya Nyama za Tanzania kushindwa kununuliwa kwenye soko la dunia, Kumbe tuliyemtimua ndo aliyekuwa ameshika soko la Nyama huko Duniani.

Dunia ya Sasa ni ya Ubepari na ubepari upo kuanzia maisha yetu ya kila siku, unaajiri mfanyakazi anazalisha milioni nyingi ila unampa kiduchu ya anacho zalisha, Mindset zetu zinatakiwa kukomaa na kuondoa uoga wa jinsi ya ku survive kwenye dunia ya ubepari
Kwenye ubepari hutengenezi monopoly ya taasis Fulani kushikilia platform za uchumi. Ni ulimwengu wa ushindani . Huyu DPW anatengenezewa mazingira ku monopoly uchumi wa Tanzania
 
Mafisadi in terms of rushwa maana unaelewa urasimu uliopo. Hata mizigo huwa inapotea sana mazingira ya kutatanisha.

Kingine ufanisi wao upo chini sana na serikali pia CAG amekiri wameshindwa kazi. Sasa solution ni kufanya outsourcing tu maana hata ukibadili wafanyakazi wanaokuja ni Wezi zaidi.

Cha ajabu watu wanakazania ooh bandari itauzwa wanasahau hata sahivi haijauzwa ila Kuna mafisadi machache yanakula hiko hiko kidogo kinachopatikana
Vipengele vya mkataba boss. Wengi tunaunga mkono uwekezaji ila mkataba uboreshwe
 
Naeleza kwa ufupi. Wenye kuelewa haraka hongereni.
  1. Bajeti ya Bandari inakata Sept 2023 ambapo kwa mujibu wake anasema kuanzia Oktoba TPA itakuwa ktk wakati mgumu kwenye kujiendesha
  2. DPW walipaswa kuanza shuguli bandarini mnamo Oktoba 2023. Lakini mpaka sasa seems deal halijafikia muafaka.
  3. Siyo kweli kwamba Watanzania hawana uwezo wa kuendesha bandari bali ufanisi hauonekani kwa sababu watawala wamekinga mirija yao bandarini.
  4. Endapo serikali ingeunda mamlaka inayojiendesha kibiashara kusimamia bandari na kuwepo nanusimamizi wa kizalendo, bandari zetu zingeweza kuleta tija mara kumi zaidi ya kinachotarajiwa kuletwa na DPW
Najua humu JF wapo wenye kuyaelewa haya mambo yanavyokwenda, je hizi taarifa zimekaaje?

mimi natamani wanipe niendeshe banandari.

nahisi point ya 3 ina ka ukweli fulani. Tanzania tuna matajiri wengi why wasipewe tenda hii kwa mkataba mzuri ?
 
Back
Top Bottom