Madereva wa mikoani, tabia na utaratibu wa kupaki mabasi sehemu ya chakula chenye bei juu mnaumiza abiria wenye kipato kidogo

Nyumbani nakula na hicho chakula kitafanya kazi.. sasa umekaa tu napo unakula nn?
• Mechanism ya mfumo wa chakula haupo hivyo, ( mwili unahitaji glucose ili ukamilishe mambo yake)
• Kama ingekuwa hivyo basi watu wasinge jisumbua kufanya kazi, tungelala tu ndani, ili njaa isiume
 
Jamani the only best part kwenye masafari ya marefu ni tule tuchakula kwenye foil, ni vitamu and yet so small. Unataka kushiba kuwa kama wapare kama kina Mshana Jr wao huwa wanabeba hotpot la Makande cha jioni watakula kwa mwenyeji wao.
 
Kilichopo nyuma ya pazia nikuwa huwa kuna fedha inawarudia sina hakika km ni hao madereva au kampuni kwa ujumla na hili nilithibitishiwa na mmoja wa mabosi wa kampuni ****** tulitoka moro kwenda dar kufika mdaula kuna sehemu sio ya miaka mingi sana ya kuchimba dawa hapo ndyo huyo boss ilivyo julikana yupo humo ndani akaletewa chakula tena akibembelezwa apokee yule boss akasema anataka na hesabu ya mabasi ya kampuni yake yaliyo leta wateja wakasema wataiandaa na kuiweka kwenye group.
Nika muhoji kwani kuna chochote kinaingia kwa huu mfumo? Akanijibu kuwa biashara ni fursa ya bishara nyengine
 
Huendagi madukani au?
Kuna foil box
Kuna vi lunch box siku hizi vya kila dizain
Sio ile mihot pot ya enzi za Nyerere
• Familia nyingi zinakaa huku Interior Angle(kidegembye), Rais mpaka leo wanajua ni Nyerere. Sasa mtu wa aina hii, hata maana ya foil hajui,
 
Ukiwa na safari na watoto wabebee hata makande toka nyumbani utanishukuru.
😀😀, Wakiaza kutoa carbon kwenye Gari, mithili ya panya aliye kufa... Ndo utajua umuhimu wa basi kusimama maeneo maalum.
 
Mtanzania anachuuzwa km bidhaa, ulipe nauli bado wakufanyie biashara tena, unapelekwa hotel wanayotaka wenye basi, na ni dili. Wafanyakazi wa basi wanakula bure na mwisho wa mwezi mwenye hoteli awapa posho. Hizo hotel vyakula vyao ni viporo na bei ya juu. Hotel ziko porini ili usiende kwenye migahawa ya bei ya chini. Ukiingia Highway Korogwe kwanza wanavyojisikia na kudharau abiria, sahani ya wali 8000 na vinyago 3 vya nyama. Abiria hushindia biscuit. Unateswa ndani ya nchi yako na walafi wachache. Kwanini LATRA isitoe maelekezo abiria wapate chakula mjini sehemu zenye migahawa mingi? Mtu mweusi ni laana, hatosheki, mlaku. Hizo hoteli hasa Dar-Arusha ni za wenye mabasi wamezijenga porini usiwe na option
 
Uko sahihi, hivi kile chama cha kutetea haki za abiria majukumu yake ni yepi. Wamekalia mjini tu
 
• Upo sahihi kabisa mkuu, ila siyo kila mtu anauwezo wa kutembea na kuku,
• Unakuta familia haina kuku, familia haina bata,
• Familia inaishi kwa kula ugali wa dona, na maharagwe

• Mkuu hapa tuzungumzie kwa watu wote, kuazia safari za maskini mpaka safari za mwenye Kipato cha juu. Je hizo kuku atazihimili? MENEMENE TEKERI NA PERESI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…