Madhara ya kuoa Mwanamke ambaye hajasoma na Golikipa ni haya!

Madhara ya kuoa Mwanamke ambaye hajasoma na Golikipa ni haya!

Mpeleke mkeo ambaye hajasoma na hana kazi yoyote Kwenu siku ukitokea msiba uone jinsi atakavyotumikishwa kwa kusugua masufuria na makazi yasiyo na hadhi. Wakati huo Wake wa ndugu zao wamekaa mguu juu na hakuna kima yeyote atakayewasogelea isipokuwa wao wenyewe waamue.
Asee hii ilitaka kunitokea kipindi fulani wife anamtoto mmoja.
Wife wangu ni mpole sana na anapenda kufanya kazi hasa akiwa sehemu za misiba au sherehe anajituma mpka unaweza sema huyu ni mfanya kazi nn... kuna ndugu hawamjui na wanajiskia sasa sijui walimuonaje wakaanza kumtuma mara hiki mara kile ikafika muda mtoto hataki kukaa na mimi nikamuita wife tukawa tumekaa kwenye gari akaja ndugu yangu mmoja akamwambia kule kazi haijaisha......
Wife akamuuliza kwani unanionaje mbona kazi nyingi nasukumiwa mimi kwakua namjua wife nikamwambia ndugu yangu hebu tuache tuna maongezi ndio ananipa mkanda maana mimi nilikua na baba zangu na wajomba tunapiga stori nikamwambia wasikuchanganye fanya kwa kiasi hawa watu wanaangalia nani wanamuweza wanampa makazi kibao..... Tulipomaliza msiba kukawa na kakikao na kutambuana basi ndipo nikawatambulisha ndugu kwa mke na mke kwa ndugu ndipo heahima ikaja na wengine walimuheahimu zaidi walipokuja kwangu.....

Ngozi nyeusi tuna shida moja kudharauliana kulingana na nini tunacho ukiona mtu kapoa basi unahisi ni wakumkandamiza wengine wamelelewa hivyo kuwa wapole ila sio wanyonge maana wife kasoma na mbali ya kusoma ni mpambanaji (namshukuru sana Mungu) ila kwenye swala la upole dah hadi nakasirika maana kazidisha na ndivyo alivyo habadiliki japo namsema sana na kumuelekeza tukifika kwa ndugu fanya hiki na hiki ila lazima atakugeuka utamkuta anachakarika kwenye vyombo kupika yaani hadi najiskia vibaya.
 
Kwenye taasisi ambazo kazi ni za mikataba miaka mitatu au mikataba ya muda mfupi,ma hr wanatumia sana hiyo kama njia ya kumpa mwanamke wako apate mkataba mpya hata kama ni mgumu vipi akaambiwe toa k nikuongezee contract Wala haruki,Kuna washikaji flani hivi walikuwa wanasimuliana namna wanagegeda wake za watu Kwa mfumo huo.kwa kifupi kama mke wako anabosi mwanamume kazi unayo,usijiwekee bima ndugu yangu.wewe endelea kujisifu mke wangu anafanya kazi benki,au ofisi fulani.wengi wa wanawake wanaofanya kazi ni wachepukaji wakubwa sana.mwanamke anapaswa kulea watoto tuu ,Kwa kifupi tunatakiwa kuwa Kama wapemba.ndoa ndoano
Kweli mwanamke anatakiwa kulea watoto nyumbani lakini akipata kazi lazima achepuke, akitongozwa na wanaume ishirini lazima atatokea mmoja atamkubalia tu.
 
😄😄
Siku ukipata Stroke au umestaafu au kufukuzwa kazi au kufa alafu umeacha watoto wadogo ndio utajua jinsi ulivyokuwa na mawazo mgando.

Pesa ya Mwanamke inaweza isikusaidie wewe lakini ikasaidia wàtoto wako.
Kuna wale wanaosema ukiwa na 100k na mke akawa na 100k jumla ni 200k ila ndani mnakua na 100k nashangaa sana maana mbona wanawake wana huruma upendo na wanajituma njiu yetu lakini tukiwa wakweli na kuwapenda..... Mimi kuna muda hadi nashangaa watu wapo dunia gani kulalamikia wanawake wakati ukipata wa kufanana nae basi mambo yanaenda na hakuna ubinafsi
 
Elimu ya darasani ni moja ya indicator ya Maendeleo sijui kama unajua hilo?

Nimeakuambia nenda jamii zilioelimika alafu njoo ambazo hazijaelimika uone zipo zenye Utu.

Ni ngumu kama huna elimu ukawa na utu.

Tunaweza kujadili kwa hoja alafu mwisho utaelewa kuwa elimu ndio inaibua na kuchochea thamani na utu wa mwanadamu.

Biblia yenyewe inasema, itafute elimu kwa maana ndio uzima wako, yaani zaidi ya utu
Mkuu utu na Elimu vitu viwili tofauti, utu unaanzia ngazi ya familia, mfano viongozi wetu si wana Elimu kubwa mbona hawana utu ?
 
MADHARA YA KUOA MWANAMKE AMBAYE HAJASOMA NA GOLIKIPA NI HAYA!

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Nimeona kuna vijana hapa wanadanganyana na kuwa na mawazo ya kizamani.

Ati wao wataoa wanawake wenye elimu duni na wasiofanya kazi isipokuwa kazi za nyumbani (golikipa).

Sasa kwa ninyi mliofanya maamuzi ninyi sina neno na nyie kwa sababu huo ni uchaguzi wenu.

Wazo hili ni zao la kizamani ambalo msingi wake ulikuwa kwa jamii isiyoamini kama Mwanamke naye ni mtu.

Lakini ujumbe huu nimeandika ni kwa wale ambao bado hawajafanya maamuzi au hawajui wachague kipi kati ya kuoa Mke aliyesoma na anayefanya kazi za taaluma au Mke ambaye hajasoma na ambaye atakuwa mama wa nyumbani.

Yafuatayo ni madhara ya moja kwa moja ambayo utayapata kwa kuoa Mwanamke ambaye hajasoma na ambaye hana kazi yaani mama wa nyumbani;

1. Atakuwa Mwanamke Cheap na wagharama nafuu Kabisa.
Hakuna kazi rahisi kama kutongoza Mwanamke ambaye hajasoma na hana kazi. Ni rahisi kama kunywa uji wa mgonjwa. Yaani shwaaa!

Moja ya vitu vinavyompa mtu thamani kwa dunia ya leo ni Elimu.

Hata wanaume watakaomtongoza mkeo watakuwa Lundo kama siafu wekundu, hawamuogopi, wamuogope kwa kipi hasa! Lakini mdada shule ipo tena anawazidi mpaka wanaume Unafikiri hapo kuna nini.

Mpeleke mkeo ambaye hajasoma na hana kazi yoyote Kwenu siku ukitokea msiba uone jinsi atakavyotumikishwa kwa kusugua masufuria na makazi yasiyo na hadhi. Wakati huo Wake wa ndugu zao wamekaa mguu juu na hakuna kima yeyote atakayewasogelea isipokuwa wao wenyewe waamue.

Jipe hadhi kijana acha woga wa kijingajinga.

Unataka familia yako iwe cheap? Unataka watoto wako wajisikieje wakimuona mama yao(mkeo) akitumikishwa kwa kazi dhalili?

2. Mwanamke kuwa Mnafiki na kushindwa kusimama katika nafasi yake ya mke na Mama.
Mke wako hana elimu alafu hana kazi. Atawezaje kusimamia majukumu yake kama mke na kama Mama?

Mke lazima awe na elimu ya kiwango fulani angalau Diploma kwa zama hizi. Kisha awe na kijikazi au kazi ya kuingiza mapato.

Mke ni Mama wa watoto wako lakini pia ni Mama yako mlezi wakati mwingine.

Lazima uwe na Mwanamke ambaye ataweza kubeba jukumu la kukutunza na kukulea kimwili na kiroho na wakati mwingine kiakili pale ambapo utakengeuka.

Sasa unachukua Mwanamke shule hana, hana kazi, Mwanamke anakuogopa badala ya kukuheshimu kisa hana kipato.

Umekengeuka kidogo hakuna wakukurudisha kwenye mstari.

Nawajua wanaume wengi ambao wao ndio chanzo cha kuvunja nyumba zao kwa kukengeuka kwao. Aidha kutumia vibaya uanaume na ubaba wao vibaya.

3. Mkeo hataheshimiwa na Watu wa nje.

Raha ya mke aheshimiwe. Sio kila siku mke anakondeana kwa kudharaulika.

Binadamu ni kiumbe mwenye dharau Sana.

Kanisani atadharaulika. Mtaani hivyohivyo. Kisa hana elimu wala hana kazi. Yaani yupo yupo tuu.

4. Kugawa Uroda kirahisi.
Ni kweli wanawake wengi hugawa uroda lakini kuna kugawa Uroda kirahisi.

Fuatilia hata jamii yenye umalaya mwingi wanawake wao hawana elimu wala hawana kazi.

Yaani Mwanamke awe mwalimu au daktari au mwanasheria alafu awe Malaya, hiyo sio rahisi.

Ila mkeo akiwa hana elimu jua kabisa hata bodaboda hawamhofii. Yaani mwanaume yeyote anaweza kuruka naye kwa sababu mkeo ni level ya chini ambaye yeyote anaweza kutunda yake.

Lakini Mwanamke mwenye elimu na kipato ni kama Mnazi. Mpaka umpate lazima jasho likutoke na wapandaji huwa wachache.

Fikiria mkeo ni mkurugenzi Unafikiri ni wafanyakazi wake wangapi wana ujasiri wa kumtongoza? Lazima wawe na hofu.

Alafu fikiria mkeo hana elimu yoyote Unafikiri kuna mtu anamhofia kumfuata?
Hakuna!

Sasa mwanamke Watu wanatakiwa Wamheshimu yeye bila hata ya uwepo wako. Sio mkeo aheshimiwe kisa umemuoa yaani ni mke wa mtu. Hapo umepigwa.

Yaani Watu wanakuheshimu tuu wewe ndio maana hawamfuati mkeo lakini ukiwa haupo Watu wanajigaragaza. Lakini Mwanamke akiwa na kazi nzuri na elimu hata asipokuwa na mume anaheshimika na wanaume hujifikiri mara mbilimbili kumfuata.

Yote kwa yote Maisha ni ubatili. Lakini Watu wanachokazana ni kuepuka ubatili wenye maumivu, dharau, majonzi na taabu.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kama mume anaheshimiwa automatically mke ataheshimiwa and vice versa
 
Umbile la mwanamke ni kukaa nyumbani hii ndio asili. Ona kinachotokea baada ya mwanamke kutolewa nyumbani ? Leo wote sisi mashahidi.
Uko sahihi. Ukimfungulia biashara mwanamke ni kama umempa lesseni ya kutafutwa na mabwana wengine. Ataanza kuchepuka mpk ushangae.
 
Kuna chizi mmoja alijichanganya akamfungulia calling point mke wake, enzi hizo watu wengi hawana simu, wanaenda kupiga simu kwenye kibanda Cha soggy doggy, haikuchukua hata mwezi kibanda alikifunga, alivyoulizwa ilikuwaje, alisema Kuna siku alisahau kitu nyumbani akiwa kazini ikabidi aruke chap kurudi kukichukua, akapita calling point kuchukua funguo kwa wife wake, Ile anatokea kapaki kigari chake pembeni Anakuta mbele ya office Kuna ndinga la vx limepaki, kabla hajashuka kwenye kigari chake ikabidi afanye servey kidogo, kupiga jicho dukani Anakuta wife wake anashikwa matako na kibosile flani mwenye Ile ndinga, alitoka mbio akamfurusha yule kibosile na pale pale duka likafungwa, mkewe alikuwa ni zile pisi kali zilizonyooka slay queen, jamaa hawezi kumuacha mkewe lakini kiduka alikifunga, jichanganye uoe Pisi kali halafu umuache aende kazini ndio itakuwa imeisha hiyoo
 
Taikon ktk makala zako toka nikufahamu 2018 kama sikosei. hii makala ulipaswa kuifuta kabisa maana umeandika mambo ya ajabu na ya hovyo sana.

Ulichokiandika mwanaume anaejielewa vizur lazima akupuuze
 
Bado alikuwa mfanyabiashara.
Khadija mpaka anakufa ni Mfanyabiashara.

Vigezo kwa uislamu vipo vitatu.
1. Uzuri wa Mwanamke
2. Mali
3. Dini na nasaba ya mwanamke
Hujajibu swali nililo kuuliza.

Pili, hivyo sio vigezo kwa Uislamu inaonekana huujui Uislamu. Ile hadithi inaongelea kwa kawaida watu huwa wanaoa kwa kuangalia vigezo vya :

1. Uzuri wa mwanamke
2. Nasaba ya mwanamke
3. Mali

Ila Mtume akasema katika hayo yote angalieni dini ya mwanamke kwani Mikono yako haitagusa michangana kwa maana hautaanguka au kupata madhila.

Mama Khadija alipo olewa na Mtume biashara zake alimuachia Mtume na yeye akawa nyumbani.

Jaribu kuwa unasoma na usiwe unasikia au kuokoteza mambo kwa ambao hawajui Uislamu.
 
Elimu ya dunia inachochea Akili ya asili.

Ndio maana Watu wanapelekwa shule.
Hii sio kweli basi hao waitwao au wenye akili wasingekuwa wanafanya mambo yenye kudhuru akili zao. Akili kijana haipimwi kwa kusoma secular itakuwa hujui akili ni nini.

Watu wanapelekwa shuleni sababu ya kasumba na kupata hela tu na nafasi.

Elimu ya dini ndio inafanya mtu kuwa smart na makini zaidi.
 
Kwa sababu Mwanamke naye ni mtu.
Sifa ya mtu lazima afanye kazi.
Vinginevyo labda asiwe mtu.

Moja ya sheria ya Mungu au ya asili ni kufanya kazi kwa mwanaume na Mwanamke.
Swali anafanya kazi wapi na kazi gani ?

Hakuna aliye pinga hilo la kufanya kazi shida mnaona kazi ni za maofisini na kutafuta hela. Hili sio umbile la mwanamke ndio maana kama akili yako inafanya kazi vizuri utaona Kuna faida chache na hasara kubwa mno.
 
Ukiwa na hela utaheshimika wewe mkeo atapata heshima kupitia wewe lakini yeye kama yeye bila wewe hana heshima yake mwenyewe.

Siku ukifa na pesa zako ndio utajua kama huyo mkeo asiye na elimu wala kazi ataheshimiwa au ndio ile kunyanyaswa na kuteseka.
Akiwa amesoma na hamna pesa? Unafikiria vitu kibwege sana wife material hapimwi kwa elimu yake. Ndoa sio ajira ya ofisini
 
MADHARA YA KUOA MWANAMKE AMBAYE HAJASOMA NA GOLIKIPA NI HAYA!

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Nimeona kuna vijana hapa wanadanganyana na kuwa na mawazo ya kizamani.

Ati wao wataoa wanawake wenye elimu duni na wasiofanya kazi isipokuwa kazi za nyumbani (golikipa).

Sasa kwa ninyi mliofanya maamuzi ninyi sina neno na nyie kwa sababu huo ni uchaguzi wenu.

Wazo hili ni zao la kizamani ambalo msingi wake ulikuwa kwa jamii isiyoamini kama Mwanamke naye ni mtu.

Lakini ujumbe huu nimeandika ni kwa wale ambao bado hawajafanya maamuzi au hawajui wachague kipi kati ya kuoa Mke aliyesoma na anayefanya kazi za taaluma au Mke ambaye hajasoma na ambaye atakuwa mama wa nyumbani.

Yafuatayo ni madhara ya moja kwa moja ambayo utayapata kwa kuoa Mwanamke ambaye hajasoma na ambaye hana kazi yaani mama wa nyumbani;

1. Atakuwa Mwanamke Cheap na wagharama nafuu Kabisa.
Hakuna kazi rahisi kama kutongoza Mwanamke ambaye hajasoma na hana kazi. Ni rahisi kama kunywa uji wa mgonjwa. Yaani shwaaa!

Moja ya vitu vinavyompa mtu thamani kwa dunia ya leo ni Elimu.

Hata wanaume watakaomtongoza mkeo watakuwa Lundo kama siafu wekundu, hawamuogopi, wamuogope kwa kipi hasa! Lakini mdada shule ipo tena anawazidi mpaka wanaume Unafikiri hapo kuna nini.

Mpeleke mkeo ambaye hajasoma na hana kazi yoyote Kwenu siku ukitokea msiba uone jinsi atakavyotumikishwa kwa kusugua masufuria na makazi yasiyo na hadhi. Wakati huo Wake wa ndugu zao wamekaa mguu juu na hakuna kima yeyote atakayewasogelea isipokuwa wao wenyewe waamue.

Jipe hadhi kijana acha woga wa kijingajinga.

Unataka familia yako iwe cheap? Unataka watoto wako wajisikieje wakimuona mama yao(mkeo) akitumikishwa kwa kazi dhalili?

2. Mwanamke kuwa Mnafiki na kushindwa kusimama katika nafasi yake ya mke na Mama.
Mke wako hana elimu alafu hana kazi. Atawezaje kusimamia majukumu yake kama mke na kama Mama?

Mke lazima awe na elimu ya kiwango fulani angalau Diploma kwa zama hizi. Kisha awe na kijikazi au kazi ya kuingiza mapato.

Mke ni Mama wa watoto wako lakini pia ni Mama yako mlezi wakati mwingine.

Lazima uwe na Mwanamke ambaye ataweza kubeba jukumu la kukutunza na kukulea kimwili na kiroho na wakati mwingine kiakili pale ambapo utakengeuka.

Sasa unachukua Mwanamke shule hana, hana kazi, Mwanamke anakuogopa badala ya kukuheshimu kisa hana kipato.

Umekengeuka kidogo hakuna wakukurudisha kwenye mstari.

Nawajua wanaume wengi ambao wao ndio chanzo cha kuvunja nyumba zao kwa kukengeuka kwao. Aidha kutumia vibaya uanaume na ubaba wao vibaya.

3. Mkeo hataheshimiwa na Watu wa nje.

Raha ya mke aheshimiwe. Sio kila siku mke anakondeana kwa kudharaulika.

Binadamu ni kiumbe mwenye dharau Sana.

Kanisani atadharaulika. Mtaani hivyohivyo. Kisa hana elimu wala hana kazi. Yaani yupo yupo tuu.

4. Kugawa Uroda kirahisi.
Ni kweli wanawake wengi hugawa uroda lakini kuna kugawa Uroda kirahisi.

Fuatilia hata jamii yenye umalaya mwingi wanawake wao hawana elimu wala hawana kazi.

Yaani Mwanamke awe mwalimu au daktari au mwanasheria alafu awe Malaya, hiyo sio rahisi.

Ila mkeo akiwa hana elimu jua kabisa hata bodaboda hawamhofii. Yaani mwanaume yeyote anaweza kuruka naye kwa sababu mkeo ni level ya chini ambaye yeyote anaweza kutunda yake.

Lakini Mwanamke mwenye elimu na kipato ni kama Mnazi. Mpaka umpate lazima jasho likutoke na wapandaji huwa wachache.

Fikiria mkeo ni mkurugenzi Unafikiri ni wafanyakazi wake wangapi wana ujasiri wa kumtongoza? Lazima wawe na hofu.

Alafu fikiria mkeo hana elimu yoyote Unafikiri kuna mtu anamhofia kumfuata?
Hakuna!

Sasa mwanamke Watu wanatakiwa Wamheshimu yeye bila hata ya uwepo wako. Sio mkeo aheshimiwe kisa umemuoa yaani ni mke wa mtu. Hapo umepigwa.

Yaani Watu wanakuheshimu tuu wewe ndio maana hawamfuati mkeo lakini ukiwa haupo Watu wanajigaragaza. Lakini Mwanamke akiwa na kazi nzuri na elimu hata asipokuwa na mume anaheshimika na wanaume hujifikiri mara mbilimbili kumfuata.

Yote kwa yote Maisha ni ubatili. Lakini Watu wanachokazana ni kuepuka ubatili wenye maumivu, dharau, majonzi na taabu.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
I hope
Mambo yanawaendea easy huko na mkeo
Mwenye Phd
 
Back
Top Bottom