Maelezo ya Wenje yamenyooka zaidi kuliko tuhuma za Lissu! Huenda Mbowe bado ni mtu sahihi zaidi kuongoza CHADEMA

Maelezo ya Wenje yamenyooka zaidi kuliko tuhuma za Lissu! Huenda Mbowe bado ni mtu sahihi zaidi kuongoza CHADEMA

Nimesikiliza maelezo ya Ezekiel Wenje aliyetuhumiwa na Lissu kumpeleka Abdul kumuhonga pesa, ukiniuliza mimi naona maelezo ya Wenje yamenyooka sana kuliko tuhuma alizokuwa anarusha Lissu dhidi ya watu anaodai wamehongwa.

Swali ambalo limebaki sasa ni kwamba Lissu anafanya mambo haya kwa sababu au faida zipi ukizingatia inaleta mgawanyiko sana ndani ya chama chake!

Nilikuwa nasubiria kwa shauku kumsikia Mbowe atajibu vipi tuhuma za watu wake kuhongwa pesa za Abdul lakini maelezo ya Wenje yamenyooka sana, yanatosha na naona yana ukweli mkubwa kuliko tuhuma za Lissu.
Huu ni uthibitisho kuwa CHADEMA bado chama kichanga sana, kina safari ndefu kama ya miaka 25 kushika nchi.
Tuliyoyaona huko nyuma, sasa ni hali halisi kwa wanachama wote. Ni wakati wa kuisaidia CDM, kuonyeshwa njia.
 
Wenje ameelezea hilo kwamba ni kawaida duniani kote kutumia watu maarafu au walio karibu na viongozi kushawishi kukwamua mambo yanapokwama, japo hili kweli ni tatizo la kimfumo lakini sio rushwa kama inavyoelezwa na Lissu kwa maana ya "pesa za Abdul".
Kwanini alimpeleka Abdul kwa Lissu?. Kwahio alimsaidia Ili yeye Abdul baada yakumsaidia wenje yeye ananufaika vipi?.

Wajinga ni wengi na mapenzi kwa Mbowe yanawapumbaza
 
Shida ya maelezo ya Lissu ni kuwa yanataka tuamini kuwa Wenje ni mjinga kiasi ya kwenda na mtu kama Abdul kumhonga mtu ambae msimamo wake dhidi ya rushwa na mambo ovyo unajulikana na kila mtu. Ili iaminike, itakuwa basi Wenje anajua kuwa tofauti na sura ambayo Lissu anayotuonyesha wote anahongeka. Hii nayo ni ngumu kuamini. Kitu pekee ambacho Wenje anastahili kuhukumiwa ni poor judgement. Kuto kufikiri optics za kiongozi wa juu wa Chadema kuwa karibu na mtoto wa Mwenyekiti wa CCM. Labda kama alikuwa anatumika kama mole ili apate siri za upande wa pili.

Amandla...
Wenje knew exactly what he was doing....

Kama ulivyosema kuwa, Wenje amekuwa na poor judgement ktk maamuzi yake....

Walifikiri Tundu Lissu kwa kuwa anahitaji fedha sana wakati ule (may be), he couldn't have a choice zaidi ya kuzipokea tu pesa hizo, kwa kusema zileteni....

Na bila shaka inawezekana walimwambia, chukua tu na itasemwa umelipwa za matibabu yako...!

On the other hand...

Shida ya Freeman Mbowe na wapambe wake, ni kuwa, pamoja na uzoefu wake mkubwa ktk siasa za mageuzi alikuwa hajawaelewa CCM vyema kuwa ni watu wadanganyifu na wenye hadaa ya kufa mtu...

Na ona sasa, wanamwingiza katika fedheha kubwa na mbaya sana, sababu ikiwa ni pesa zilizomuuza Yesu Kristo kwa majambazi...

These people are great manipulstors...

Wameingizwa mkenge kwenye maridhiano lakini bado hawajifunzi tu....

Kama ana hekima na busara, ingekuwa bora sana akatambua makosa na udhaifu wake na kisha achukue maamuzi magumu ya kupumzika kuliko kuendelea kujifedhehesha. Na huko tuendako inawezekana akadhalilishwa zaidi..?

Kwenye hili, eleweni kuwa Wenje ni mjumbe tu. Lakini nyuma yake yuko Freeman Mbowe mwenyewe...!!
 
Mbowe ni mfanyabiashara kwenye siasa kuna maslahi yake, Mbowe akiamua kuwa serious na siasa na dhamira ya kweli binafsi naamini anaweza kuwa Rais wa nchi.

Mbowe ni genius lakini bahati ndio hiyo hayuko serious kivilee kama tunavyofikiria.

Tundu jana sifa za kuwa kiongozi, kitaaluma hasa kwenye field yake ya Sheria anawezakuwa anajua sana lakini huku kwingine analazimisha tu, uwezo wake ni mdogo sana.

Narudia tena Mbowe hayuko siasa ni biashara kwake na anajua anachokifanya, kichwani ni genius na anajua mambo mengi sana (ana exposure kubwa na he is well informed na mambo ya nchi hii) ukimfananisha na Lissu.

Binafsi ukiniambia nipange kumi Bora za watu wanaofaa kuwa maRais wa nchi hii basi Mbowe nitamuweka ila sio Lissu.
Chawa pro max
 
Nipe mfano wa kesi moja ya hao watoto wa malkia huko Uingereza kama lilivyokuwa suala la Wenje, Abdul na Lissu ikawasabishia hao watoto wa malkia kuingia katika matatizo.

Wewe unafikiria leo mama, shangazi au dada yake Lissu akiwa amestaafu anafuatilia mafao/pensheni yake halafu anazungushwa hatamfuata Lissu ili ampigie Waziri husika, Waziri mkuu au hata Rais??

Lissu alipokutana na Rais kuwasilisha madai yake Ubelgiji ulikuwa ni utaratibu sahihi au kwa sababu wanajuana kwa ukaribu na anawesa kumfikia Rais kwa urahisi, kama ni kufuata utaratibu ilipaswa akomae na bunge na mahakama tu.
Kwa mawazo yako unafikiri kweli Abdul alikwenda nyumbani kwa lissu kumsaidia? Yaani mtoa msaada anamfata mtu anaetaka kumsaidia nyumbani kwake hivi hivi. Kwanza Wenje muongo ni hivi lissu aliogopa kwenda kule hotelini ndo maana akawambia waje nyumbani wala sio kwamba alikuwa anaumwa.
 
Maelezo ya Lissu kama nimemuelewa vizuri ni haya:
1. Wenje aliongozana na Abdul kwenda nyumbani. Sijui kama alikuwa tayari na appointment na Wenje au la.
2. Alipofika Wenje akamtambulisha Abdul ambae Lissu alikuwa hamjui.
3. Wenje au Abdul wakamwambia Lissu kuna zawadi yake kama atapunguza makali dhidi ya serikali.
4. Ili kuthibitisha kuwa wana nia njema wakamtajia wengine ambao wamepewa zawadi. Ingawa haijasemwa lakini katika hao waliotajwa ni lazima Boss wake Lissu alikuwemo pamoja na wengine.
5. Lissu akawafurumusha na kuwaambia kuwa haongeki.

Inaelekea pia Lissu alishtaki kwa Boss wake lakini kwa mshangao akaona hamna hatua iliyochukuliwa dhidi ya Wenje. Ndio akajua kuwa kweli kuna wakubwa nyuma ya Wenje. Kwa vile alitoa hizo shutma kwenye Kamati Kuu ya chama chake kuna wenzake ambao nao walianza kukosa imani na uongozi wa chama. Halafu, hamadi, huyo huyo Wenje mtoa rushwa anatangaza nia ya kugombea nafasi ambayo Lissu ameishika. Lissu kwa kutambua kuwa Wenje ni mtu wa Boss na kujua uwezo wa Boss wa kucheza foul akajua kuwa kibarua chake kitaota nyasi. Ndio maana akaamua kushambulia nafasi ya Boss kwa sababu alijua hilo hawatalitegemea na attack is the best form of defence. Ndio maana tumefika hapa tulipo.

Amandla...
Umesahau Wenje walikutana na Abdul katika shughuli/sherehe fulani, wakawa wamekaa meza moja lakini Wenje akiwa hamjui ni nani, ndipo akatambulishwa huyu ni mtoto wa Rais katika kupiga story ndipo akamuuliza kwa nini lakini Serikali ya mama yake haitaki kumlipa Lissu madai yake, Abdul akasema mbona anafahamu ameshalipwa ndipo Wenje akampigia Lissu simu baada ya sherehe amthibitishie Abdul kwamba bado hajalipwa pesa zake anazoidai Serikali ndipo wakapanga hadi huko kukutana Lissu akiwa na nyaraka za matibabu ili Abdul asaidie kufanikisha hilo jambo.
 
Halafu anagombea Makamu mwenyekiti endapo atashinda na Lisu akashinda hawa watafanya kazi kama mtu na msaidizi wake?
Hapo ndipo chama kitakaposambaratika. Kwa akili ya kawaida lazima viongozi wenye hekima na busara wamshauri mmoja ajitoe au apingwe ili asishinde kwa manufaa ya chama (Uma).
 
Nimesikiliza maelezo ya Ezekiel Wenje aliyetuhumiwa na Lissu kumpeleka Abdul kumuhonga pesa, ukiniuliza mimi naona maelezo ya Wenje yamenyooka sana kuliko tuhuma alizokuwa anarusha Lissu dhidi ya watu anaodai wamehongwa.

Swali ambalo limebaki sasa ni kwamba Lissu anafanya mambo haya kwa sababu au faida zipi ukizingatia inaleta mgawanyiko sana ndani ya chama chake!

Nilikuwa nasubiria kwa shauku kumsikia Mbowe atajibu vipi tuhuma za watu wake kuhongwa pesa za Abdul lakini maelezo ya Wenje yamenyooka sana, yanatosha na naona yana ukweli mkubwa kuliko tuhuma za Lissu.
shenzi hayo maelezo yakowapi?
 
Screenshot_20241220_214816_Instagram.jpg
 
Pia na sisi tumemtazama na kumsikiliza vyema....

Kama umemwelewa na kumwamini Hezekia Wenje akiwawakilisha wenzake waliokula naye mlungula, nachelea kusema kuwa udadisi na ufahamu wako una kasoro...

Kwanini kabla hujaja na conclusion ya namna hii ukajipa nafasi ndogo tu kujiuliza maswali madogo na rahisi tu haya:

1. Tundu Lissu aliumia akiwa kazini. Ni kwanini unadhani serikali haitaki kulipa madai ya fedha za Tundu Lissu alizotumia kujitibu huku akiwa mbunge (mtumishi wa umma) ambaye yuko entitled na haki hiyo ya kutibiwa kwa gharama za serikali...?

2. Kumbe Wenje alimkopesha Tundu Lissu kwenye pesa hizo za matibabu. Na kumbe struggle ya Wenje na wenzake (akiwemo Freeman Mbowe aliyemtuma Wenje) hadi kuamua kujiuza kwa Rais Samia Suluhu Hassan kupitia kwa mwanae Abdul. Sasa kwanini naye anasema hilo leo? Je, Tundu Lissu anajua kuwa anadaiwa na Wenje? Shilingi ngapi..?

3. Hivi, malipo halali ya serikali hufanyika kwa njia wanayotumia Abdul na Wenje?

4. Na je, madai ya Tundu Lissu (fedha za kujitibu alizopaswa kulipiwa na serikali) ni halali au batili/ hayakidhi vigezo vya kulipwa na serikali...?

5. Kama madai yake ni halali kabisa, ni haki yake alipwe fedha hizo, huyu Abdul na Wenje wanaingia hapo kama kina nani? Walikwenda kufanya nini kwa Tundu Lissu? Wana influence gani serikalini?

6. Kama madai ya Tundu Lissu siyo halali, serikali imeshawahi kumjibu kwa maandishi kuwa hutalipwa fedha zako za madai ya matibabu yako kwa hayakidhi vigezo vya malipo 1, 2, 3, 4 nk...?

##Ukiweza kujibu maswali ndiyo utaelewa Hezekia Wenje na Genge lake ni wakweli kiasi gani...!
Njia aliyotumia Wenje inaweza kuwa ina shida lakini ameelezea sababu ni zipi ilikuwa hivyo na akatolea mfano jinsi nchi hii contractor anaweza akajenga na kukamilisha mradi vizuri kabisa akiwa na certificates zote lakini akawa anazungushwa katika malipo yake ndipo ambapo watu wanatumia watu wanaowajua watu wenye mamlaka ili tu kukwamua haki zao. Kumtumia Abdul ili kushawishi malipo halali ya Lissu yalipwe na serikali japo ni jambo la hovyo lakini sio rushwa kama anavyoelezea Lissu kuhongwa "pesa za Abdul".
 
Kwa mawazo yako unafikiri kweli Abdul alikwenda nyumbani kwa lissu kumsaidia? Yaani mtoa msaada anamfata mtu anaetaka kumsaidia nyumbani kwake hivi hivi. Kwanza Wenje muongo ni hivi lissu aliogopa kwenda kule hotelini ndo maana akawambia waje nyumbani wala sio kwamba alikuwa anaumwa.
Inawezekana Abdul alikuwa akitaka kumsaidia Lissu lakini akiwa na ajenda zake nyingine za ziada za kisiasa, inawezekan alikuwa anamtaka amsaidie kwa huruma tu lakini pia inawezekana alitaka kumsaidia kama mtoto wa mwenye mamlaka tu kujisikia vizuri kushawishi mamlaka, hilo ni la Abdul sasa.

Kuhusu kuumwa Wenje anasema Lissu alikuwa anaumwa tangu wanatoka Arusha kurudi Dar kuelekea siku ya kukutana na Abdul, kama Lissu alidanganya hilo ni lake Lissu pia.
 
Swali ambalo limebaki sasa ni kwamba Lissu anafanya mambo haya kwa sababu au faida zipi ukizingatia inaleta mgawanyiko sana ndani ya chama chake!
Nimeshawaambia lisu ni mtu mbinafsi sana, sijui kwa nini nyie hamuelewi tu. Anafanya hayo kwa manufaa yake binafsi ili apate sympathy toka kwa nyumbu na hatimaye apigiwe kura kuwa mwenyekiti wa chama. Hizo ni calculated moves zake ili apate kura za huruma. Yuko tayari kusema au kufanya lolote kwa manufaa yake binafsi.
 
Umesahau Wenje walikutana na Abdul katika shughuli/sherehe fulani, wakawa wamekaa meza moja lakini Wenje akiwa hamjui ni nani, ndipo akatambulishwa huyu ni mtoto wa Rais katika kupiga story ndipo akamuuliza kwa nini lakini Serikali ya mama yake haitaki kumlipa Lissu madai yake, Abdul akasema mbona anafahamu ameshalipwa ndipo Wenje akampigia Lissu simu hapo hapo amthibitishie Abdul bado hajalipwa pesa zake anazoidai Serikali ndipo wakapanga hadi huko kukutana.
Nimeiweka ili kuonyesha how ridiculous the whole thing is. Wenje, seriously, aende kumhonga Lissu nyumbani kwake? Atakuwa mjinga namba moja.

Amandla...
 
Wenje knew exactly what he was doing....

Kama ulivyosema kuwa, Wenje amekuwa na poor judgement ktk maamuzi yake....

Walifikiri Tundu Lissu kwa kuwa anahitaji fedha sana wakati ule (may be), he couldn't have a choice zaidi ya kuzipokea tu pesa hizo, kwa kusema zileteni....

Na bila shaka inawezekana walimwambia, chukua tu na itasemwa umelipwa za matibabu yako...!

On the other hand...

Shida ya Freeman Mbowe na wapambe wake, ni kuwa, pamoja na uzoefu wake mkubwa ktk siasa za mageuzi alikuwa hajawaelewa CCM vyema kuwa ni watu wadanganyifu na wenye hadaa ya kufa mtu...

Na ona sasa, wanamwingiza katika fedheha kubwa na mbaya sana, sababu ikiwa ni pesa zilizomuuza Yesu Kristo kwa majambazi...

These people are great manipulstors...

Wameingizwa mkenge kwenye maridhiano lakini bado hawajifunzi tu....

Kama ana hekima na busara, ingekuwa bora sana akatambua makosa na udhaifu wake na kisha achukue maamuzi magumu ya kupumzika kuliko kuendelea kujifedhehesha. Na huko tuendako inawezekana akadhalilishwa zaidi..?

Kwenye hili, eleweni kuwa Wenje ni mjumbe tu. Lakini nyuma yake yuko Freeman Mbowe mwenyewe...!!
It still does not make any sense. Hasa ukimuingiza Mbowe ambae bila shaka alikuwa anajua kuwa Lissu ameanza kupoteza imani nae. Na kwa nini leo? Na kwa nini amhonge Lissu? Ili anyamaze? Hamjui Lissu? Hapa Lissu ameingia choo cha kike. Nia yake ni kummaliza mtu ambae alidiriki kusema wazi kuwa atashindana nae. Ego yake imempeleka pabaya.

Amandla...
 
Back
Top Bottom