Maelezo ya Wenje yamenyooka zaidi kuliko tuhuma za Lissu! Huenda Mbowe bado ni mtu sahihi zaidi kuongoza CHADEMA

Maelezo ya Wenje yamenyooka zaidi kuliko tuhuma za Lissu! Huenda Mbowe bado ni mtu sahihi zaidi kuongoza CHADEMA

Umesahau Wenje walikutana na Abdul katika shughuli/sherehe fulani, wakawa wamekaa meza moja lakini Wenje akiwa hamjui ni nani, ndipo akatambulishwa huyu ni mtoto wa Rais katika kupiga story ndipo akamuuliza kwa nini lakini Serikali ya mama yake haitaki kumlipa Lissu madai yake, Abdul akasema mbona anafahamu ameshalipwa ndipo Wenje akampigia Lissu simu baada ya sherehe amthibitishie Abdul kwamba bado hajalipwa pesa zake anazoidai Serikali ndipo wakapanga hadi huko kukutana Lissu akiwa na nyaraka za matibabu ili Abdul asaidie kufanikisha hilo jambo.
Na wewe umeamini kabisa hii porojo? kwamba Abdul anajua Lissu ameshalipwa pesa zake wakati hajalipwa ukizingatia Lissu amekuwa akipiga kelele juu ya pesa zake kwa muda mrefu tu?
 
Na wewe umeamini kabisa hii porojo? kwamba Abdul anajua Lissu ameshalipwa pesa zake wakati hajalipwa ukizingatia Lissu amekuwa akipiga kelele juu ya pesa zake kwa muda mrefu tu?
Abdul hawezi kuwa anafuatilia kila siku kujua kama Lissu ameshalipwa pesa zake, Abdul ana maisha yake na ishu zake nyingine.
 
Kuna Kitu Chadema huwa hamkielewi Kwa sababu wengi wenu ni watoto wa juzi tu

Hata hamjui nani waliasisi Chadema na Kwa sababu gani!!

Hamjui kwanini Mwita Waitara, Patrobas Katambi na Cecil Mwambe wakiletwa Chadema

Tena hamjui kwanini Shibuda na Marando 😄😄😄

Niishie hapo 🐼
Ni kawaida sana kwenye siasa dola kuinfiltrate moles wa vyombo vya usalama na hii sio dhambi ni jukukumu la msingi la vyombo.
 
Nimesikiliza maelezo ya Ezekiel Wenje aliyetuhumiwa na Lissu kumpeleka Abdul kumuhonga pesa, ukiniuliza mimi naona maelezo ya Wenje yamenyooka sana kuliko tuhuma alizokuwa anarusha Lissu dhidi ya watu anaodai wamehongwa.

Swali ambalo limebaki sasa ni kwamba Lissu anafanya mambo haya kwa sababu au faida zipi ukizingatia inaleta mgawanyiko sana ndani ya chama chake!

Nilikuwa nasubiria kwa shauku kumsikia Mbowe atajibu vipi tuhuma za watu wake kuhongwa pesa za Abdul lakini maelezo ya Wenje yamenyooka sana, yanatosha na naona yana ukweli mkubwa kuliko tuhuma za Lissu.
Nadhani hukumsikiliza vizuri!!

Wenje ni dalali kweli!! Why aambatane na Abdul kwenye madai halali ya Lissu?

Rais alishakubali kumshughulikia madai ya Lissu, ni vipi Wenje kujitwika jukumu la kumtafuta Abdul? Kwanini hakufuata taratibu za kiserikali? Wenje ajitoe kugombea umakamu wa Mwenyekiti haraka sana
 
Wenje kajikanyaga kanyaga ovyo ovyo tu hajaeleza kile kinachodaiwa

Mara Abdul alisema Lissu tayari kashalipwa mara wakaenda kwa Lissu wakachukua nyaraka

Hapo kuna kitu behind the scenes tumefichwa.
Hivi ndivyo wafanya biashara walivyo. Wao ni pesa tu, wala hakuna cha kutetea wanyonge.
Watanzania wana akili san, ndio maana kila uchaguzi wanawapotezea mbali.
 
Abdul hawezi kuwa anafuatilia kila siku kujua kama Lissu ameshalipwa pesa zake, Abdul ana maisha yake na ishu zake nyingine.
Kwamba Wenje,mwanasiasa mashuhuri kabla ya mwezi wa 10 mwaka jana alikuwa hamjui kabisa Abdul ndio akatambukishwa ukumbini wakati watu wengi tu huku mtaani wanamfahamu Abdul hasa ukizingatia miezi miwili kabla (August) mwaka jana zilisambaa habari kwenye media nyingi nchini juu ya Abdul kuiwakilisha serikali ya Tanzania nchini Uganda na picha zake kusambaa kwa wingi kwenye mitandao
 
Hili ni tatizo kutokana na mfumo dhaifu wa utendaji haki nchini na urasimu uliopitiliza, hii ndio inapelekea watu kujaribu kutumia "watu wanaowajua watu" lakini pia kwa maelezo ya Wenje Lissu alikuwa pamoja akitoa ushirikiano katika mchakato wote huo wa kumtumia Abdul kushawishi serikali imlipe madai yake halali.
kwahiyo kwa akili zako ulitaka wenje ajisemeeje??
 
Lissu alisema Abduli alikuwa anataka kumpa RUSHWA ili aache kumkomalia Mama yake.

Wenje anasema alimpeleka Abduli ili Tundu Lissu alipwe madai yake sasa nadhani Lissu anatakiwa anyooshe zaidi maneno yake ili tujue nini ni nini na lipi ni lipi.
 
Kwamba Wenje,mwanasiasa mashuhuri kabla ya mwezi wa 10 mwaka jana alikuwa hamjui kabisa Abdul ndio akatambukishwa ukumbini wakati watu wengi tu huku mtaani wanamfahamu Abdul hasa ukizingatia miezi miwili kabla (August) mwaka jana zilisambaa habari kwenye media nyingi nchini juu ya Abdul kuiwakilisha serikali ya Tanzania nchini Uganda na picha zake kusambaa kwa wingi kwenye mitandao
Hata wewe kuna mazingira ukikutana na Abdul unaweza usimjue kama ni yeye .
 
Umesahau Wenje walikutana na Abdul katika shughuli/sherehe fulani, wakawa wamekaa meza moja lakini Wenje akiwa hamjui ni nani, ndipo akatambulishwa huyu ni mtoto wa Rais katika kupiga story ndipo akamuuliza kwa nini lakini Serikali ya mama yake haitaki kumlipa Lissu madai yake, Abdul akasema mbona anafahamu ameshalipwa ndipo Wenje akampigia Lissu simu baada ya sherehe amthibitishie Abdul kwamba bado hajalipwa pesa zake anazoidai Serikali ndipo wakapanga hadi huko kukutana Lissu akiwa na nyaraka za matibabu ili Abdul asaidie kufanikisha hilo jambo.
Hiyo shughuli iliyowakutanisha ilikuwa haramu? Kama haikuwa haramu aitaje! Vinginevyo unatusikitisha sana wewe mtu mzima kuuamini uongo wa mchana kweupe.

Hivi Kwa mfano wasingekutana kwenye hiyo shughuli Wenje angeweza kunisaidia vipi Lissu kuhusu madai yake halali?

Pengine wewe mwandishi wa mada hii ni Wenje
 
Nimesikiliza maelezo ya Ezekiel Wenje aliyetuhumiwa na Lissu kumpeleka Abdul kumuhonga pesa, ukiniuliza mimi naona maelezo ya Wenje yamenyooka sana kuliko tuhuma alizokuwa anarusha Lissu dhidi ya watu anaodai wamehongwa.

Swali ambalo limebaki sasa ni kwamba Lissu anafanya mambo haya kwa sababu au faida zipi ukizingatia inaleta mgawanyiko sana ndani ya chama chake!

Nilikuwa nasubiria kwa shauku kumsikia Mbowe atajibu vipi tuhuma za watu wake kuhongwa pesa za Abdul lakini maelezo ya Wenje yamenyooka sana, yanatosha na naona yana ukweli mkubwa kuliko tuhuma za Lissu.
Kwa ambao hawana akili kama wewe ni sawa
 
Mbowe ni mfanyabiashara kwenye siasa kuna maslahi yake, Mbowe akiamua kuwa serious na siasa na dhamira ya kweli binafsi naamini anaweza kuwa Rais wa nchi.

Mbowe ni genius lakini bahati ndio hiyo hayuko serious kivilee kama tunavyofikiria.

Tundu jana sifa za kuwa kiongozi, kitaaluma hasa kwenye field yake ya Sheria anawezakuwa anajua sana lakini huku kwingine analazimisha tu, uwezo wake ni mdogo sana.

Narudia tena Mbowe hayuko siasa ni biashara kwake na anajua anachokifanya, kichwani ni genius na anajua mambo mengi sana (ana exposure kubwa na he is well informed na mambo ya nchi hii) ukimfananisha na Lissu.

Binafsi ukiniambia nipange kumi Bora za watu wanaofaa kuwa maRais wa nchi hii basi Mbowe nitamuweka ila sio Lissu.
Hivi vichekesho huwa mnavipataje?
 
Nimesikiliza maelezo ya Ezekiel Wenje aliyetuhumiwa na Lissu kumpeleka Abdul kumuhonga pesa, ukiniuliza mimi naona maelezo ya Wenje yamenyooka sana kuliko tuhuma alizokuwa anarusha Lissu dhidi ya watu anaodai wamehongwa.

Swali ambalo limebaki sasa ni kwamba Lissu anafanya mambo haya kwa sababu au faida zipi ukizingatia inaleta mgawanyiko sana ndani ya chama chake!

Nilikuwa nasubiria kwa shauku kumsikia Mbowe atajibu vipi tuhuma za watu wake kuhongwa pesa za Abdul lakini maelezo ya Wenje yamenyooka sana, yanatosha na naona yana ukweli mkubwa kuliko tuhuma za Lissu.
Lissu hakumtaja kwa jina.
 
Nimesikiliza maelezo ya Ezekiel Wenje aliyetuhumiwa na Lissu kumpeleka Abdul kumuhonga pesa, ukiniuliza mimi naona maelezo ya Wenje yamenyooka sana kuliko tuhuma alizokuwa anarusha Lissu dhidi ya watu anaodai wamehongwa.

Swali ambalo limebaki sasa ni kwamba Lissu anafanya mambo haya kwa sababu au faida zipi ukizingatia inaleta mgawanyiko sana ndani ya chama chake!

Nilikuwa nasubiria kwa shauku kumsikia Mbowe atajibu vipi tuhuma za watu wake kuhongwa pesa za Abdul lakini maelezo ya Wenje yamenyooka sana, yanatosha na naona yana ukweli mkubwa kuliko tuhuma za Lissu.

Lazima tujiulize maswali haya ,Wenje kwa muda mrefu alikua hana jina kubwa hasa kipindi hiki cha Awamu ya Tano inayojiita ya sita ,imekuwaje mtoto mdogo kama Abdul amtafute Wenje ili amfukie Lisu?
Je, Abdul ni nani kwenye CCM na kwa nini aanze kuwatafuta watu Baada ya Kashfa ya DP World?
Je, hii haionyeshi wazi kuwa ni watu wengi hasa viongozi wa CHADEMA wa kanda walipewa fedha za DP World kuzima maandamano yaliyokuwa yameitishwa na Mwabukusi na wanaharakati wengine?

Ikumbukwe kuwa Wanaharakati waliitisha maandamano kupinga kuuzwa kwa bandari ya DSM .

Wanaharakati akiwemo Dr.Slaa wakaanza kutumia jukwaa la Chadema kuratibu maandamano , Wanaharakati wakaviomba vyama vya siasa viungane nao kuhamasisha na kupanga maandamano nchi nzima . CHADEMA wakajitokeza kukanusha kuwa wao hawa mpango wa kushiriki kwenye maandalizi wala kuhamasisha wanachama wao kuandamana nchi nzima kupinga uuzwaji wa Bandari . Maandamano ya Mwabukusi yakakosa nguvu kubwa . Bandari inauzwa kizembe kabisa nchi ikiwa na chama kikubwa kabisa kinachosema kina kubalika nchi nzima bila kuandamana wala kushiriki kwenye maandamano yaliyoandaliwa na wanaharakati ,wasiokuwa na vyama .

Hapa ndipo wanapitia mashaka ya Mapeswa ya Rushwa yaliyotolewa na viongozi wa vyama vyote na wakalamba asali kimya kimya . Lisu Pekee alijitokeza hadharani kupinga rushwa ya kuuza nchi na Bandari zetu .
Lisu Pekee anaonekana wazi kuwa suala la bandari zetu kuuzwa linaloleta kuliko kuliko viongozi wote wa vyama vyote vya siasa Tanzania. Akifuatiwa na wanaharakati wazalendo pamoja na Kanisa Katoliki linalosimamia misingi ya haki kwa watu wote duniani tofauti na mengine yanayojali zaidi vipato vyao na kuziba midomo.


Lisu ni Mwanasiasa wa karne na muujiza unaotembea .
 
Nadhani hukumsikiliza vizuri!!

Wenje ni dalali kweli!! Why aambatane na Abdul kwenye madai halali ya Lissu?

Rais alishakubali kumshughulikia madai ya Lissu, ni vipi Wenje kujitwika jukumu la kumtafuta Abdul? Kwanini hakufuata taratibu za kiserikali? Wenje ajitoe kugombea umakamu wa Mwenyekiti haraka sana
Hizo taratibu za kiserikali si ndio zimeshindwa? Hivi wale ambao kila siku wanamlilia hali Rais au Makonda hawajui kuwa kuna taratibu za serikali? Hivi wewe ukiona unapigwa dana dana malipo yako haumtafuti mtu ambae ana access na anayeweza kukusaidia? Kuna kitu gani cha ajabu kwa Wenje kusema " ngoja niongee na Abdul labda anaweza kutusaidia kwa kumkubusha mama yake kuhusu ahadi yake?" Tatizo liko wapi?

Amandla...
 
Nimesikiliza maelezo ya Ezekiel Wenje aliyetuhumiwa na Lissu kumpeleka Abdul kumuhonga pesa, ukiniuliza mimi naona maelezo ya Wenje yamenyooka sana kuliko tuhuma alizokuwa anarusha Lissu dhidi ya watu anaodai wamehongwa.

Swali ambalo limebaki sasa ni kwamba Lissu anafanya mambo haya kwa sababu au faida zipi ukizingatia inaleta mgawanyiko sana ndani ya chama chake!

Nilikuwa nasubiria kwa shauku kumsikia Mbowe atajibu vipi tuhuma za watu wake kuhongwa pesa za Abdul lakini maelezo ya Wenje yamenyooka sana, yanatosha na naona yana ukweli mkubwa kuliko tuhuma za Lissu.
Unahitaji uwe kichaa ili utetee huu uchafu yaani malipo ya Lisu ayaulizie Kwa Abdul ambaye sio mfanyakazi wa serikali
 
Wenje ameelezea hilo kwamba ni kawaida duniani kote kutumia watu maarafu au walio karibu na viongozi kushawishi kukwamua mambo yanapokwama, japo hili kweli ni tatizo la kimfumo lakini sio rushwa kama inavyoelezwa na Lissu kwa maana ya "pesa za Abdul".
Sio kweli tutajie ushawahi sikia wapi pengine?
 
Hata wewe kuna mazingira ukikutana na Abdul unaweza usimjue kama ni yeye .
Kwamba Wenje amemwona kwa mara ya kwanza shereheni, hapo hapo akaanzisha suala la madai ya Lisu na kufikia hatua ya kumpigia Lisu simu. Mtu ambaye ulikuwa humjui unakutana naye mara hiyo na kumuekeza matatizo yako. Kisha yeye anajotolea kumfuata nyumbani msaidiwa badala ya kumtaka mwomba msaada kumfuata.
 
Back
Top Bottom