Maelezo ya Wenje yamenyooka zaidi kuliko tuhuma za Lissu! Huenda Mbowe bado ni mtu sahihi zaidi kuongoza CHADEMA

Maelezo ya Wenje yamenyooka zaidi kuliko tuhuma za Lissu! Huenda Mbowe bado ni mtu sahihi zaidi kuongoza CHADEMA

Pia na sisi tumemtazama na kumsikiliza vyema....

Kama umemwelewa na kumwamini Hezekia Wenje akiwawakilisha wenzake waliokula naye mlungula, nachelea kusema kuwa udadisi na ufahamu wako una kasoro...

Kwanini kabla hujaja na conclusion ya namna hii ukajipa nafasi ndogo tu kujiuliza maswali madogo na rahisi tu haya:

1. Tundu Lissu aliumia akiwa kazini. Ni kwanini unadhani serikali haitaki kulipa madai ya fedha za Tundu Lissu alizotumia kujitibu huku akiwa mbunge (mtumishi wa umma) ambaye yuko entitled na haki hiyo ya kutibiwa kwa gharama za serikali...?

2. Kumbe Wenje alimkopesha Tundu Lissu kwenye pesa hizo za matibabu. Na kumbe struggle ya Wenje na wenzake (akiwemo Freeman Mbowe aliyemtuma Wenje) hadi kuamua kujiuza kwa Rais Samia Suluhu Hassan kupitia kwa mwanae Abdul. Sasa kwanini naye anasema hilo leo? Je, Tundu Lissu anajua kuwa anadaiwa na Wenje? Shilingi ngapi..?

3. Hivi, malipo halali ya serikali hufanyika kwa njia wanayotumia Abdul na Wenje?

4. Na je, madai ya Tundu Lissu (fedha za kujitibu alizopaswa kulipiwa na serikali) ni halali au batili/ hayakidhi vigezo vya kulipwa na serikali...?

5. Kama madai yake ni halali kabisa, ni haki yake alipwe fedha hizo, huyu Abdul na Wenje wanaingia hapo kama kina nani? Walikwenda kufanya nini kwa Tundu Lissu? Wana influence gani serikalini?

6. Kama madai ya Tundu Lissu siyo halali, serikali imeshawahi kumjibu kwa maandishi kuwa hutalipwa fedha zako za madai ya matibabu yako kwa hayakidhi vigezo vya malipo 1, 2, 3, 4 nk...?

##Ukiweza kujibu maswali ndiyo utaelewa Hezekia Wenje na Genge lake ni wakweli kiasi gani...!
Yoda njoo unyooshe maelezo hapa
 
Kwamba alionana na Abdul kwenye event,siku hiyo hiyo wakafahaniana na akaanza kumuelezea suala la Lissu,inaingia akilini kweli? Yaani uonane na mtu siku hiyo hiyo uzoeane naye kwa haraka tena kwenye sherehe? Anyway tutajua mengi
Inategemea na wepesi wa kichwa chako kilivyo, sioni ugumu wa haya unayouliza ukizingatia suala la Lissu limekuwa mjadala muda mrefu katika nchi, ni kitu rahisi tu kuanzisha small talk inayohusiana na nchi inavyokwenda na kisha kuchomekea hilo.
 
Pia na sisi tumemtazama na kumsikiliza vyema....

Kama umemwelewa na kumwamini Hezekia Wenje akiwawakilisha wenzake waliokula naye mlungula, nachelea kusema kuwa udadisi na ufahamu wako una kasoro...

Kwanini kabla hujaja na conclusion ya namna hii ukajipa nafasi ndogo tu kujiuliza maswali madogo na rahisi tu haya:

1. Tundu Lissu aliumia akiwa kazini. Ni kwanini unadhani serikali haitaki kulipa madai ya fedha za Tundu Lissu alizotumia kujitibu huku akiwa mbunge (mtumishi wa umma) ambaye yuko entitled na haki hiyo ya kutibiwa kwa gharama za serikali...?

2. Kumbe Wenje alimkopesha Tundu Lissu kwenye pesa hizo za matibabu. Na kumbe struggle ya Wenje na wenzake (akiwemo Freeman Mbowe aliyemtuma Wenje) hadi kuamua kujiuza kwa Rais Samia Suluhu Hassan kupitia kwa mwanae Abdul. Sasa kwanini naye anasema hilo leo? Je, Tundu Lissu anajua kuwa anadaiwa na Wenje? Shilingi ngapi..?

3. Hivi, malipo halali ya serikali hufanyika kwa njia wanayotumia Abdul na Wenje?

4. Na je, madai ya Tundu Lissu (fedha za kujitibu alizopaswa kulipiwa na serikali) ni halali au batili/ hayakidhi vigezo vya kulipwa na serikali...?

5. Kama madai yake ni halali kabisa, ni haki yake alipwe fedha hizo, huyu Abdul na Wenje wanaingia hapo kama kina nani? Walikwenda kufanya nini kwa Tundu Lissu? Wana influence gani serikalini?

6. Kama madai ya Tundu Lissu siyo halali, serikali imeshawahi kumjibu kwa maandishi kuwa hutalipwa fedha zako za madai ya matibabu yako kwa hayakidhi vigezo vya malipo 1, 2, 3, 4 nk...?

##Ukiweza kujibu maswali ndiyo utaelewa Hezekia Wenje na Genge lake ni wakweli kiasi gani...!
Maelezo mazuri sana..nilikuwa najiuliza kwanini CDM inadidimia..kumbe akina wenje wamepewa pesa ndio maana wanakaa kimya watu wakitekwa..
 
Wenje knew exactly what he was doing....

Kama ulivyosema kuwa, Wenje amekuwa na poor judgement ktk maamuzi yake....

Walifikiri Tundu Lissu kwa kuwa anahitaji fedha sana wakati ule (may be), he couldn't have a choice zaidi ya kuzipokea tu pesa hizo, kwa kusema zileteni....

Na bila shaka inawezekana walimwambia, chukua tu na itasemwa umelipwa za matibabu yako...!

On the other hand...

Shida ya Freeman Mbowe na wapambe wake, ni kuwa, pamoja na uzoefu wake mkubwa ktk siasa za mageuzi alikuwa hajawaelewa CCM vyema kuwa ni watu wadanganyifu na wenye hadaa ya kufa mtu...

Na ona sasa, wanamwingiza katika fedheha kubwa na mbaya sana, sababu ikiwa ni pesa zilizomuuza Yesu Kristo kwa majambazi...

These people are great manipulstors...

Wameingizwa mkenge kwenye maridhiano lakini bado hawajifunzi tu....

Kama ana hekima na busara, ingekuwa bora sana akatambua makosa na udhaifu wake na kisha achukue maamuzi magumu ya kupumzika kuliko kuendelea kujifedhehesha. Na huko tuendako inawezekana akadhalilishwa zaidi..?

Kwenye hili, eleweni kuwa Wenje ni mjumbe tu. Lakini nyuma yake yuko Freeman Mbowe mwenyewe...!!
Na hawa chawa wake ndiyo wanazidi kumpaka kinyesi kwani kadiri wanavyozidi kumtetea na kutoa maelezo ya janja janja ndiyo wanafungua milango ya watu wenye akili kuzidi kuchimba ili kuufikia ukweli halisi. Mbowe kwa uzoefu wake nilidhani angeliona hili mapema na kutangaza mapema kuwa yeye anaheshimu kauli yake aliyotoa 2019 kuwa hatagombea tena hivyo hawa wapambe nuxi wasingekuwa na kiherehere. Naona mbele ya safari Mbowe akienda kudhalilika sana. Hawa wapambe hawana cha kupoteza sana zaidi ya manufaa binafsi waliyokuwa wanapata kwa Mbowe kuwa mwenyekiti, lakini Mbowe ataathirika zaidi kwani heshima aliyojingea kwa miaka 30 inaenda kuyeyuka kama tofali la barafu kwenye jua kali.
 
Yes Mbowe ukimchambua anaonekana ni MTU sahihi Ila wakati aliopo ndo sio sahihi.

Lissu anatembea na Wave (Wimbi) la watu wanaotaka kuona mabadiliko ya kweli na siasa za ushindani. Hivyo hawataki kumchambua na kuangalia weakness areas zake.

Hii ndo Kama ile 2015 - kuna watu wengi walipata ubunge na udiwani kupitia Wimbi la mabadiliko Ila katika uwezo walikuwa hawana uwezo wowote .

Means unaweza kuwa MTU sahihi Ila ukawa haupo katika wakati sahihi.

Mbowe inambidi aachie ngazi hii itamjengea Heshima sana. Asibishane na wakati
Mkuu, hii ya 'Asibishane na wakati' ndilo jibu lenyewe, maana " WAKATI ni UKUTA"
 
Umesahau Wenje walikutana na Abdul katika shughuli/sherehe fulani, wakawa wamekaa meza moja lakini Wenje akiwa hamjui ni nani, ndipo akatambulishwa huyu ni mtoto wa Rais katika kupiga story ndipo akamuuliza kwa nini lakini Serikali ya mama yake haitaki kumlipa Lissu madai yake, Abdul akasema mbona anafahamu ameshalipwa ndipo Wenje akampigia Lissu simu baada ya sherehe amthibitishie Abdul kwamba bado hajalipwa pesa zake anazoidai Serikali ndipo wakapanga hadi huko kukutana Lissu akiwa na nyaraka za matibabu ili Abdul asaidie kufanikisha hilo jambo.
Na wewe ukaamini huu uzushi,Lissu ndiye mwenye shida kwani Abdul ndiye afunge safari kumfuata mtu anyehitaji msaada na isiwe vice versa?
 
Mbona maelezo ya wenje yanadai Abdul alisema alishalipwa? Alijuaje?
Alisema yeye alikuwa akifahamu Lissu ameshalipwa, labda ilikuwa ni kudhani tu kwa sababu aliona Lissu hapigi tena kelele n.k
 
Nimesikiliza maelezo ya Ezekiel Wenje aliyetuhumiwa na Lissu kumpeleka Abdul kumuhonga pesa, ukiniuliza mimi naona maelezo ya Wenje yamenyooka sana kuliko tuhuma alizokuwa anarusha Lissu dhidi ya watu anaodai wamehongwa.

Swali ambalo limebaki sasa ni kwamba Lissu anafanya mambo haya kwa sababu au faida zipi ukizingatia inaleta mgawanyiko sana ndani ya chama chake!

Nilikuwa nasubiria kwa shauku kumsikia Mbowe atajibu vipi tuhuma za watu wake kuhongwa pesa za Abdul lakini maelezo ya Wenje yamenyooka sana, yanatosha na naona yana ukweli mkubwa kuliko tuhuma za Lissu.
Wewe ni Wenje. Na uongo uliotunga unaonyesha ulivyo na akili ndogo.
 
Na wewe ukaamini huu uzushi,Lissu ndiye mwenye shida kwani Abdul ndiye afunge safari kumfuata mtu anyehitaji msaada na isiwe vice versa?
Ilikuwa wakutane hotelini, Lissu akaumwa ndio wakaamua waende nyumbani kwake.
 
Ilikuwa wakutane hotelini, Lissu akaumwa ndio wakaamua waende nyumbani kwake.
Lissu alikuzidini akili wewe na Abdul. Alijua akienda hotelini hatakuwa na ushahidi ndiyo maana akawaambia mwenda nyumbani kwake. Hili jambo siyo rahisi kukana kama unavyofikiria. Samia angetaka kumlipa Lissu wala kusingekuwepo na ulazima wa wewe na Abdul kwenda nyumbani kwake.
 
Mkuu haiondoi ukweli kuwa premise nzima ya sakata hili la udalali wa rushwa ya Abdul, kwa mujibu wa maneno ya Wenje ina rangi zote za rushwa.

Kumsaidia Tundu Lissu isiwe scapegoat, hata ingekuwa ni yeye Wenje aliyedhurika kuna mtu angemsaidia tu.

Ajitete kwa namna nyingine lakini sio kwa kuingiza madhila aliyopitia mwenzie.
Wenje, Lissu na wengine ndani ya CHADEMA walikuwa wanahongwa pesa na Abdul ili iwaje??
 
Mkuu umemskiliza Wenje lakini ? Kuna sehemu yoyote umeona amejichanganya kwenye maelezo yake?
Siyo kujichanganya tu bali umeonyesha ulivyo mpumbavu kama huyu Abdul na mama yake. Hata kama ni rushwa kuna namna ya kutoa na siyo ujinga mliofanya. Nyie mlidhani Lissu ana uchu wa fedha kama wewe na Mbowe na hatakuwa na namna ya kuzikataa.
 
Wenje, Lissu na wengine ndani ya CHADEMA walikuwa wanahongwa pesa na Abdul ili iwaje??
Mbowe na wewe mmeshachukuwa chenu. Lissu amekataa kwa sababu hataki rushwa. Samia anajua hakubaliki ndiyo maana amemhonga Mbowe akitaka asipate ushindani uchaguzi ujao. Mbowe ni dalali. Katudanganya siku nyingi lakini sasa hivi amefika mwisho wa utapeli wake.
 
Mbowe ni mfanyabiashara kwenye siasa kuna maslahi yake, Mbowe akiamua kuwa serious na siasa na dhamira ya kweli binafsi naamini anaweza kuwa Rais wa nchi.

Mbowe ni genius lakini bahati ndio hiyo hayuko serious kivilee kama tunavyofikiria.

Tundu jana sifa za kuwa kiongozi, kitaaluma hasa kwenye field yake ya Sheria anawezakuwa anajua sana lakini huku kwingine analazimisha tu, uwezo wake ni mdogo sana.

Narudia tena Mbowe hayuko siasa ni biashara kwake na anajua anachokifanya, kichwani ni genius na anajua mambo mengi sana (ana exposure kubwa na he is well informed na mambo ya nchi hii) ukimfananisha na Lissu.

Binafsi ukiniambia nipange kumi Bora za watu wanaofaa kuwa maRais wa nchi hii basi Mbowe nitamuweka ila sio Lissu.
Mkuu, heshima kwako! Je, mwaka 1985 tunge kuomba utuwekee watu 10 ambao wewe una uhakiki watakuwa Maraisi wetu WATARAJIA kwa Mujibu Taratbu zetu za kumpata RAIS wetu hadi leo 2024 ungepatia/ungekuwa sahihi?
 
Back
Top Bottom