Maeneo ambayo Waislam wanawapiga Bao Wakristo

Maeneo ambayo Waislam wanawapiga Bao Wakristo

Naunga mkono ila hapo kwenye mahali tu nna chakusema

Ni kweli mahali anataja mlengwa mwenyewe ambaye anatakiwa kuolewa ila siku hizi baadhi ya waislam wengi wanapindisha hapo kwenye mahali naomba wakemewe yaani viongozi wa dini wakemee kipengele cha mahali

Unakuta binti ametaja vizur tu kiwango/kitu anachohitaji kama mahali ila wazee nao wanaongeza wanachotaka kiufupi haipendezi- tunaghahiri sana kuoa kutokana na hali ngumu ya maisha na hawa wazee wa kiislam kuongeza cha juu , haipendezi wakemewe watatuua na kuzini maana binti zao bado wanamiminika maghetoni Kwa masela na wao wenyewe ndio wanatia ugumu
Kumbuka pamoja na dini Kuna Mila za makabila. Mfano sisi wa Kurya mahari ni ya wazazi. Inaanza harusi kimila the dini baadae.
 
Mkuu nashukuru Kwa mchango wako.

Kuhusu suala la usafi Hilo mbona lipo wazi Kabisa.
Angalia Binti za kiislam (sio wote) akiingia chooni hata kukojoa, mtazame utakufa kabeba kopo Dogo lenye maji ya kujisafisha Baada ya kukojoa. Hii pia inatumika Kwa wanaume wa kiislam (sio wote) Ila ni wengi ukilinganisha na Wakristo ambao hawafanyi hivyo.

Njoo chooni, Waislam wakienda chooni wanamalapa ya chooni ambayo ukifika utayakuta pale. Waislam hawaingii na viatu ndani ya nyumba zao. Waislam hawaingii na viatu katika nyumba za ibada ikiwemo misikitini.
Lakini Wakristo hufanya kinyume na wao.

Usafi ni pamoja na vyakula, Waislam hawali Nguruwe, Waislam hawaruhusiwi kushika hata wanyama ambao ni najisi. Hiyo ni Kwa Imani Yao. Lakini vipi Wakristo? Achana na wasabato ambao ni kundi Dogo. Nazungumzia Wakristo katika ujumla wao.

Waislam wakienda kuswali lazima wajiswafi, watawadhe miguu Yao, suruali zenye mikojo au nguo za ndani zenu mikojo hazitakiwi misikitini.
Lakini vipi Kwa Wakristo?
Ukristo wenyewe unadai usafi wa Roho, lakini uislam umejikita kwenye usafi kuanzia kwenye Mwili, rohoni Hawana uthibitisho.

Ukiambiwa usafi sio tuu kuoga, ni zaidi ya Hapo.

Usiwaonee Wivu ninapowasifia Mkuu, Kwa sababu kunawakati pia ninawaponda na kuwakosoa Kwa Yale ambayo ninayona kwao wamepuyanga.
Angalau hapa sasa umepunguza ile mihemko ya mwanzo, umeanza kutumia maneno sio wote, tofauti na mwanzo.

Hao wanawake wa kiislamu unaosema wakiingia chooni watakuwa na maji ya kujisafisha, mbona hilo ni kawaida tu kiafya, wanawake wote wanashauriwa kwasababu za maumbile yao, wahakikishe sehemu zao za siri zinakuwa safi kila wakati, hili hata kwa wanawake wakristu nimelishuhudia mara nyingi, hivyo napinga unavyotumia kigezo hiki kuwafagilia wanawake wa kiislamu.

- Suala la malapa ya chooni, hapa napo nakushangaa, hii sio sababu ya kuhalalisha usafi wa wanawake wa kiislamu, kwasababu, malapa yoyote, ilimradi yawe masafi, mtu yeyote anaweza kuingia nayo chooni, hii mentality yako ni kama vile mtu kila mara akiingia chooni anaenda kukanyaga mavi, wacha haya mawazo, hata vyumbani mwao, wanaingia na viatu vikiwa safi, haina maana wanakanyaga vumbi/tope na kuingia nalo ndani, hapa napo nakupinga.

- Nakuona unagusia mpaka suala la najisi, sijui umeyatoa wapi hayo mamlaka, katazame nini maandiko ya biblia yanasema kuhusu najisi. Mambo ya nguo za ndani kutonuka mikojo, kwahiyo kuna wanawake wakristu huingia kanisani na chupi zinazonuka mikojo? hii mada yako haina uthibitisho wa vingi.

Huo usafi wa zaidi ya hapo ni upi ambao wanawake wakristu hawana?

Ninapoona mapungufu ya wazi kwenye hoja zako, nakuonesha upungufu huo, halafu unaniambia nawaonea wivu, ndio nazidi kuona vile uliandika hii mada yako ili kutafuta sifa tu, usifiwe na hao unaowapamba, lakini sio kuelimisha, ndio maana mwanzo nikakwambia, ulielemewa sana na mihemko wakati ukiandika haya.

Nimekwambia, pita huko uswahili uyaone maisha wanayoishi hao unaowasifia hapa, halafu rudi usome hiki ulichoandika hapa uone kama kina mantiki, ndio maana nikakuuliza, unavyosema "wamewaacha mbali mno" kwenye mazingira gani? haya tunayoishi, au kuna mengine kichwani mwako?

Kama wewe ni mstaarabu, waombe radhi wanawake wakristu kwa namna ulivyowaandika hapa.
 
Kumbuka pamoja na dini Kuna Mila za makabila. Mfano sisi wa Kurya mahari ni ya wazazi. Inaanza harusi kimila the dini baadae.

Hapo imezungumziwa dini mkuu, tena ni dini ya kiislam hatujafika kwenye tamaduni za makabila , tukifika upande wa tamaduni za makabila tutakushtua Chief
 
Umesahau na waislam mwanamke kazi yake ni kukazwa tuu haruhisiwi aende hata sokoni hii ni kazi ya mwanaume tuu
 
Angalau hapa sasa umepunguza ile mihemko ya mwanzo.

Hao wanawake wa kiislamu unaosema wakiingia chooni watakuwa na maji ya kujisafisha, mbona hilo ni kawaida tu kiafya, wanawake wote wanashauriwa kwasababu za maumbile yao, wahakikishe sehemu zao za siri zinakuwa safi kila wakati, hili hata kwa wanawake wakristu nimelishuhudia mara nyingi, hivyo napinga unavyotumia kigezo hiki kuwafagilia wanawake wa kiislamu.

- Suala la malapa ya chooni, hapa napo nakushangaa, hii sio sababu ya kuhalalisha usafi wa wanawake wa kiislamu, kwasababu, malapa yoyote, ilimradi yawe masafi, mtu yeyote anaweza kuingia nayo chooni, hii mentality yako ni kama vile mtu kila mara akiingia chooni anaenda kukanyaga mavi, wacha haya mawazo, hata vyumbani mwao, wanaingia na viatu vikiwa safi, haina maana wanakanyaga vumbi/tope na kuingia nalo ndani, hapa napo nakupinga.

- Nakuona unagusia mpaka suala la najisi, sijui umeyatoa wapi hayo mamlaka, katazame nini maandiko ya biblia yanasema kuhusu najisi. Mambo ya nguo za ndani kutonuka mikojo, kwahiyo kuna wanawake wakristu huingia kanisani na chupi zinazonuka mikojo? hii mada yako haina uthibitisho wa vingi.

Ninapoona mapungufu ya wazi kwenye hoja zako, nakuonesha upungufu huo, halafu unaniambia nawaonea wivu, ndio nazidi kuona vile uliandika hii mada yako kutafuta sifa tu, usifiwe na unaowapamba, lakini sio kuelimisha, ndio maana mwanzo nikakwambia, ulielemewa sana na mihemko wakati ukiandika haya.

Mkuu unaposema kiafya inashauriwa, Huko kwenye afya Nani mshauri?
Uislam hata kusingekuwa na mambo ya delta za afya uislam upo bayana Kwa hayo. Uislam hautegemei ushauri wa madaktari katika suala la usafi wa Mwanamke na Mwanaume.

Kuhusu mihemko,,,, hapo unajadili Kwa Maoni yako na sio hoja.
Mimi nimetoa hoja ambazo hazihitaji ufafanuzi kwani zipo wazi Kwa Watu wote wasiolemewa na ushabiki.

Mimi sio muislam, lakini haifanyi nisione mazuri ya Waislam.
Mimi ni Mkristo lakini hainifanyi nisione madhaifu ya upande niliopo.
Hiyo haimaanishi kwenye uislam hakuna madhaifu. Ndio maana kuna Wakati naandikaga mapungufu ya uislam.

Ni ishu ya kàwaida.
 
Mkuu unaposema kiafya inashauriwa, Huko kwenye afya Nani mshauri?
Uislam hata kusingekuwa na mambo ya delta za afya uislam upo bayana Kwa hayo. Uislam hautegemei ushauri wa madaktari katika suala la usafi wa Mwanamke na Mwanaume.

Kuhusu mihemko,,,, hapo unajadili Kwa Maoni yako na sio hoja.
Mimi nimetoa hoja ambazo hazihitaji ufafanuzi kwani zipo wazi Kwa Watu wote wasiolemewa na ushabiki.

Mimi sio muislam, lakini haifanyi nisione mazuri ya Waislam.
Mimi ni Mkristo lakini hainifanyi nisione madhaifu ya upande niliopo.
Hiyo haimaanishi kwenye uislam hakuna madhaifu. Ndio maana kuna Wakati naandikaga mapungufu ya uislam.

Ni ishu ya kàwaida.
Ni mihemko kwa sababu unatumia maneno, "wamewaacha mbali mno" nikakuuliza kwenye mazingira gani, haya tunayoishi, au kuna mengine unayofikiria kichwani mwako?!

Mpaka nilipo ku challenge ndio kidogo ukabadilika, umeanza kutumia maneno "sio wote", mbona mwanzo hukuandika hivyo? tatizo lilikuwa mihemko yako tu.

Nimekwambia kapite kule uswahilini uone hao unaowasifia wanaishi vipi, halafu rudi hapa ulinganishe na ulichoandika kwenye mada yako uone kama vinafanana, ulikuwa kwenye ndoto ya mihemko ukiandika haya.

Ukisema mazuri yasifiwe sawa yasifiwe, lakini usisifie tu kama zuzu bila kufanya comparison kwenye mazingira unayoishi, wewe unasifia tu kwasababu zako za kufikirika, mimi sipo hivyo, amka ndotoni.
 
Ni mihemko kwa sababu unatumia maneno, "wamewaacha mbali mno" nikakuuliza kwenye mazingira gani, haya tunayoishi, au kuna mengine unayofikiria kichwani mwako?!

Nimekwambia kapite kule uswahilini uone hao unaowasifia wanaishi vipi, halafu rudi hapa ulinganishe na ulichoandika kwenye mada yako uone kama vinafanana, ulikuwa kwenye ndoto ya mihemko ukiandika haya.

Hukohuko uswahilini nimepita nikakuta Wakristo na Waislam nikawapima bado muislam alishinda kwenye ishu ya usafi na Stara Hilo wala sio la kubishia
 
Hukohuko uswahilini nimepita nikakuta Wakristo na Waislam nikawapima bado muislam alishinda kwenye ishu ya usafi na Stara Hilo wala sio la kubishia
Huko uswahilini ulikopita unapajua mwenyewe, nionavyo, umekuja na hii hoja kwa kukurupuka, hukujipanga vizuri, ukadhani hutakutana wapingaji wa aina yangu, next time jipange.

Lazima uvijue vigezo vya kupima huo usafi unaouzungumzia hapa, lakini sio kuandika jumla jumla tu kama ulivyofanya.
 
Kwenye MISOSI Waislam wamewazadi mbali sana Wakristo.
Mwezi wa Ramadhan FUTARI zanazouzwa huliwa sana na Wakristo kuliko Waislam wenyewe waliofunga. [emoji1787][emoji1787]
 
Kuna maelekezo ya mtume (SAW) kwamba mambo matatu ni katika dini:

1. Muumini kuwa na chanzo binafsi cha mapato.

2. Muumini kumiliki makazi yake binafsi (nyumba).

3. Muumini kumiliki usafiri wake.
Hapo 3 hutumia neno Kipando. Iwe Ngamia, farasi, gari nk?
 
Saiv ukifikwaa na msiba kwetu wakristo ni stress tupu...catering msibani..kaburi kujengewaa..sare za familiaa..mziki wa maombolezo...mpk msiba uishe upoo hoii[emoji119]wakristo tunaoverdo jamani
Ni tabia za kuiga, haya mambo ya caterers kwenye misiba mbona miaka michache iliyopita majirani na ndugu ndio walijitokeza kupika chakula na kuhakikisha wafiwa wanakula na kusaidiwa kuzika marehemu wao?

Vv
 
Kwenye suala WA wake wanne naunga mkono. Maana si kila Siku napenda nikae na mume kuna wakati sitaji hata kumuona, Kuna wakati namiss. So katika angle hii unapata fursa ya kuwa mwenyewe na watoto wako akiwa mbali Kwa wake zake wengine. Kwetu sisi kina mama tunaliona hili Kwa ukaribu zaidi
 
Sehemu Nayowapa Credit ni maswala ya UBINADAM(HURUMA NA KUSAIDIA)

Nadhani ni karibia hospital zote kubwa waislam Ndo wenye mchango mkubwa kuwasaidia wagonjwa wote bila kujali itikadi kwa kuwapa vyakula na maji.

Nilishawahi uguzaga Mgonjwa hospital mbili tofauti nikabahatika kuona hiyo hali , ilinivutia sana .Kwani ndani ya wodi alolazwa mgonjwa wangu karibia wote hawakuwa hata na ndugu wenye uwezo wa kukimu mahitaji la mlo kwa mara tatu. Hivyo ukipeleka chakula basi unazidisha angalau nae awape wenzake.Pia kupitia hizo taasisi za kiislam zilifanya wagonjwa wote kupata chakula na maji.

Nilijiuliza ni namna gani wanawasaidia watu katika hali ngumu kama ile huku imani ya pili huku ndo kwanza ni kuchangishana kwenye nyumba za ibada ili kujenga hospital alafu gharama zao ziko juuu.
Huwa wanapita mitaani na kutangaza misikitini kutoa kwa ajili ya wagonjwa
 
Back
Top Bottom