Leo niliwaza miradi hii mipya mikubwa ya maendeleo kama Airbus , Stieglers na SGR ni miujiza ya karne ya Mh Rais, niliwaza ili bongo tuendelee kwa kasi tunahitaji Rais wetu awe na taaluma ya ualimu (discipline mbele "we mhuni kuja hapa, kwanini hujachomekea shati unatuletea bangi hapa si mahali pake kima we, shika chini , pa pa pa! , kimbia mjinga wewe, mara! "sijaona kijana mjinga na legelege kama wewe baba yako si ni professa wewe , mbona we unafeli hivi , kazi kudai pocket money tu na kukazania Instagram na videmu mjinga mkubwa wewe baba yako ni rafiki yangu nitamtafuta nimwambie ujinga wako huku shuleni", mara "we msichana tembea kwa ukakamavu huoni uko smart area , kuja hapa haraka kazi kufuga makucha tu kama shetani ndo mwanzo wa uhuni huu na kutoa mimba za utotoni mjinga kabisa wewe! piga magoti ita jua!!) hizi tabia za walimu kuhakikisha usafi na discipline mashuleni sasa tunashuhudia ndo kiboko ya majizi na mazembe yaliyoko serikalini manake Bwana Mkubwa hakwepeshi anawatumbua tu na huu ni utamaduni mpya uliotukuka , unaohitajika na uliokosekana na unaopaswa kusifiwa na kuenziwa daima milele, nawasihi viongozi wangu waandae hidden policy ya chama chetu Rais lazima awe mwalimu kitaaluma na asitokane na zile koo za mafisadi na zile koo zenye majina ambazo mtu mzito tu akitekwa ndo wako mbele mbele na kiherehere na pia Rais asitokane na zile koo za wale wazee waliochanga pesa mwana TANU namba moja akaenda kuhutubia UN! Wenye akili watanisoma!