Mafanikio ya Rais Magufuli 2015 - 2021
Matrafik wamegeuka kuwa wakusanya kodi kushinda hata TRA.
 
Dar Dar Dar Mwanza Dar Dar Dar Chato Dar....... kweli sisi watu wa Njombe tulilaaniwa
 
Shahidi yako Mange Kimambi?

Hata siku ukilivua Kahaba Makaburi ya Kinondoni usiku Mange akikwambia huyo ni Bikra utaamini
Itakuwa chizi kama unaonyeshwa chassis namba za gari hiyohiyo ikiwa na namba tofauti na kisha kutoamini ni gari moja. Haya endelea kusubiri malaika akuthibitishie ikiwa clouds haikuvamiwa au ilivamiwa. Huu unafiki mlionao pamoja na elimu zenu ndio unaoleta shida nchi.
 
Utekaji wa raia ni moja ya jambo lililofanikiwa kwa kiwango cha hali ya juu
 
Yote hayo yamemsaidia vipi mwananchi alieko Tandahimba?
Kampelekea umeme hadi kijijini..kazi kwake afungue saluni, aweke mashine ya kusaga..tena nikuambie sasa hivi huku wananchi wamefungua projects za kukodisha miziki kwenye sherehe..yaani Jamaa kaleta Mwanga Mpya katika maisha..
 
rushwa hajakomesha na hatoweza!kuhusu nidhamu makazini ni kweli tuna nidhamu ya UOGA!
Bora hiyo nidhamu ya woga kuliko ile ya mwanzo mliyokuwa nayo ya kutubinulia midomo wananchi tukihitaji huduma.
 
Ha ha imebidi nicheke. na kelele zote hizi haya ndio kayafanya. Kukomesha rushwa how , nidhamu makazini unaweza kuniambia how, airport mwanza na Dar pamoja na flyovers ni on going projects alizikuta. Alichofanya yeye ni kununua bombardier used 2 ,kujenga hostels ya wanafunzi na kupanua hicho kipande cha barabara ya moroko.
Nyingine tunasikia kila siku ni mikwara , vitisho na ubabe ,kabaki kusema fanyeni kazi. Tutaona hiyo 2020. Hajaanza hata km 50 ya lami toka aingie ikulu
Hutaelewa hadi utakapotumia akili yako.
 
Hutaelewa hadi utakapotumia akili yako.
Tatizo kubwa ni kushindwa kutenganisha siasa na mambo mengine.
Kiuhalisia Magufuli Anandoto nzuri na anajitahidi kuzifikia.
Tumpe ushirikiano maana ndiye Rais kwa sasa ili tusipoteze Muda na ieleweke Muda haurudi ukishapita.
 
Ukijaribu kufanya mambo mazuri kwa malengo mabaya/mkono wa hila utakutana na upinzani daima...watu sio maboga wana vichwa...!!!
 
1.Mradi wa Airport terminal 3 ni wa siku nyingi mchakato wake ulianza enzi za Mkapa (waulize wakazi wa Kipawa na Mamlaka ya Viwanja.vya ndege) na Ujenzi ulianza wakati wa Kikwete sioni kwa namna gani unautaja kama sehemu ya mafanikio ya Mheshimiwa Magufuli
2. TAZARA flyover ni msaada wa Mjapani
3. UBUNGO interchange ni msaada wa World Bank unaingizaje hii kuwa mafanikio.
4. Dar Metropolitan City mradi wa barabara zote za ndani ni ufadhili wa IDA
5.Kununua ndege sio mafanikio,mafanikio ni kuendesha ATC kwa faida. (kuanzisha biashara ni jambo moja na kufanya biashara kwa mafanikio ni jambo lingine)

Najua yapo mafanikio kwa serikali ya Mheshimiwa Magufuli lakini ungeegemea katika bajeti ya 2016/2017 je wametekeleza miradi mingapi ya maendeleo?
1.Ulisikiliza bunge la bajeti mwaka jana?(nina kalabrasha hapa la orodha ya miradi ambayo.iliombewa pesa ili itekelezwe)
2.Serikali imekiri kuwa imetekeleza kwa asilimia ishirini tu orodha yote ya miradi ya mwaka wa fedha unaoisha. Bado unaona haya ni mafanikio?
Embu tuwe serious kidogo!
3.Umesikiliza au kusoma muhtasari wa ripoti ya CAG bado unaona kuna tofauti na miaka iliyopita?
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
Dawa hakuna hospitalini.uchaguzi ZNZ .sukari being juu.demokrasia imedumaa.kutekwa watu.kula rambirambi Kagera.Bunge live nk..naona mengi mabaya kuliko unyapara wa ujenzi
 
Na anapojidanganya huyu hajui kuwa watumishi wa umma sio watumishi wa Chama, hawana chakupoteza hata upinzani ukichukua nchi, polisi, walimu, madaktari, watabaki na kazi zao kama kawaida, kwahiyo ajue kabisa 2020 huyu akipata 30% ya kura zote nahama nchi hata kama upinzani utashinda
Wewe ni mpuuzi na lofa asiyejua siasa za Tanzania. Wapinzani wachukue Nchi? Baba, mama na mkeo wataipigia CCM. Wewe na viroba vyako utabaki na wahuni wenzako!!
 
Back
Top Bottom