Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unataka uletewe chakula mdomoni?Ila havijamsaidia masikini kujinasua na njaa.
Mapatobyameongezeka yamenisaidia kusomesha bure wanangu,pia mtoto wa shangazi yangu kapata mkopo wa chuoHayo mapato yaloongezeka, yamekusaidiaje wewe na ukoo wako? Yameleta tija gani kwa taifa?
Apandishe mishahara kwa tija ipi?Hajapandisha mishahara na madaraja miaka mnne sasa. Maisha ya wafanyakazi ameyafanya kuwa magumu sana.
Kwa Kifupi Kikwete kafanya Mambo mengi sema kosa alilofanya ni kuruhusu watu wamchezee sharubu
Kikwete Kaongeza Hospital kadhaa
While za Kata
Nyumba za watumishi wa Umma kama Polisi na Walimu
Vivuko nchi nzima
Barabara za kutosha
Kajenga Mwendo kasi
Kajenga uwanja wa Ndege terminal 3 japo JPM kaja kuizindua tu
Kajenga viwanja vya ndege Songwe, Bukoba, Mbeya, na Mwanza
Mkuu umeua kabisaaa...Yaani ni Pwentiii tupu ila hebu tudukiscuss hiyo namba 42 kuhusu mikopo!?? Hapo Kuna ukakasi kidogo hivi tukisema una watoto 10 ukawahudumia 9.. ilihali mwenzio kaja na watoto 20 akawahudumia 17.. hivi nani apo atakuwa kafanya kazi kubwa!! Ukidiscuss kwa figure ileile ambapo kimsingi ni ngumu kulingana na wakati ingeleta logic ila hapo siungi mguu hoja!!!
Baadhi ya hospitali za mkoa nazozijua ni hospitali ya rufaa ya mkoa wa singida,alipanua hospitali ya mkoa wa Mbeya na songea
Kati ya sekta ambazo Jk alifanya vizuri ni barabara,elimu,diplomasia,demokrasia na uchumi kiujumla ila shida yake kuu hakuwabana vilivyo aliowateua na kitendo cha demokrasia na uhuru wa kujieleza kuwa mkubwa kilisababisha viongozi wa serikali kushindwa kuelezea mafanikio ya serikali maana kwa sasa hata zahanati ikijengwa lazima tujue
Teh! Elimu bure. Duh!Mapatobyameongezeka yamenisaidia kusomesha bure wanangu,pia mtoto wa shangazi yangu kapata mkopo wa chuo
Uchumi wa kikwete ulikuwa ni wa ujanja ujanja ukiwa unafahamiana na wakubwa wewe unakuwa sawa vinginevyo kun watu bado walikuwa wanashindia mlo mmoja wengi tu.
Kwani awamu zilizopita zilowaletea watu chakula mdomo.Ukianza kujitegemea utaelewa acha kula kulala kwa shemeji.Sera mbovu uleta njaa,tajiri akisomeshwa namba aishi kishetani masikini kafa kabisa.Unataka uletewe chakula mdomoni?
Tofauti ya JK na JPM ni kuwa JK alifanya jambo lolote lile alilioona lina manufaa kwa wananchi ndio maana yapo yanayoonekana kwa macho na yasiyo onekana kwa macho Mfano kuruhusu Bunge Live ni ujasiri mkubwa sana ambao JPM kashindwa kwa sababu bunge live ni kuruhusu serikali yako ikosolewe huku wananchi wanaona.Kuruhusu ripoti ya CAG kusomwa bungeni na kujadiliwa ni jambo la kishujaa ambalo bila shaka ilikua ni njia ya matumizi bora ya fedha za umma.Kujenga chuo kikuu na kulegeza masharti ya mikopo nalo lilikua jambo jema angeweza kuacha ili anunue ndege.Kuamua ujenzi wa barabara na kumwachia waziri wake afanye kwa utashi bila kulazimisha aonekane anafanya yeye ni uongozi bora.Hivyo JK alifanya yale yasiyo ya sifa tofauti na wakati huu ambao tumeng'ang'ana na vitu vichache na kujipa sifa kede kede wakati vitu vingi vya manufaa kwa Umma tumeviacha.Wote wana mazuri na madhaifu lakini kwa kuwa wapambe wa JPM wanataka tuamini kua maendeleo yameanza wakati huu wa JPM, wakati sote tunauweza wa kutazama na kuona,kupima na kulinganisha ni unafiki.flyover ya Tazara na Daraja la salender JK alikua na uwezo wa kuzindua au kuweka mawe ya msingi lakini hakujali kwa kua alijua serikali ni ile ile japo kila kitu alikuwa amesharatibu.
Unauhakika kufunga Vyuo vingi ndio kupungua idadi ya Wanafunzi vyuoni umefatilia udahili wa UDSM tu kwa miaka ya hivi karibuni ukilinganisha na enzi za JK!? Hapo sijataja UDOM Mkuu wangu!?mkuu magufuli kafunga vyuo vingi sana, kwaio idadi ya vijana wanaoingia vyuo vikuu imepungua!
Naomba uniwekee list hapa hizo hospitali zimejengwa wapi? Hakuna hospital hizo ni vidispensary tu. Nitajie ziko wapiMagufuli kajenga hospitali 65 kwa miaka mitatu
Elimu bure kabisa
Kapandisha mapato toka B800 mpaka 1.3 trilion
Kafufua Atc
Kafufua Ttcl na inatoa gawio
Mapato ya madini yameongezeka
Kaongeza nidhamu serikali
Kupanga ni kuchagua
Nikukumbushe, bunge live mchakato wa kulizima ulianza na kikwete baada ya kuona kelele zinazidi na mbele kuna joto la uchaguzi akarudi nyuma likaendelea kwa hiyo haikuwa ajenda ya jpm, huyu katekeleza tu.