Mafanikio ya Utawala wa Jakaya Kikwete ndani ya Miaka 10

Mafanikio ya Utawala wa Jakaya Kikwete ndani ya Miaka 10

Hujaeleweka,wewe unalinganishaje mafanikio kati ya JK na JPM?
Mimi naona JK yupo mbali sana ukilinganisha na huyu wa sasa,yapi.maoni yako
Unalinganisha kwa mizani gani? Miaka minne kea miaka kumi?
Tuache ubabaishaji
 
Hivi JK angesimama upande wa EL mnafikiri CCM mngeweza kuudhibiti ule moto, EL kagombea kupitia upinzani mmeona ule moto wake sasa ingekuwa yuko ndani na anaungwa mkono na JK mnafikiri mngemuweza na jinsi mlivyowanafiki..

JK ashukuruwe kwa uzalendo wake na kujitenga na kundi lake japo aliwatumia kama ngazi halafu akawabwaga..
 
bora hako kakundi hakakuathiri mishahara wala biashara za watu
Hebu niambia kwa sasa Kabila zima kila kona kila wilaya, hata wakwere umewasikia kwenye ukurugenzi wowote?
Akili Kama hizi ni matope au makamasi!? VP, PM, Speaker, Hawa ni wakabila lake!? Wakifika mawaziri Wa5 yaan Full minister wanatoka kabila lake anagalau andiko lako tulipe uhalali!?? Ukiondoa CDF tu , IGP, CGP, CGF, CGI hawa n wakabila lake!?? Njoo Mpk Boss wa TISS nae ni wakabila lake!??


Mkuu kuna wakati wewe na wapumbavu wengine wenzio huwa mnaamua tu kutype chochote baada ya kuvimbiwa kande!!!
 
Waalimu walikua wanapata matunzo sana (Shemeji)
Kumekuwepo na vijembe na lugha za kejeli zinazotolewa na baadhi ya viongozi kutuhumu awamu zilizopita hasa awamu ya tano kana kwamba wao waliiba na hakuna maendeleo waliyoyafanya.

Orodha ni ndefu mimi nayakumbuka haya.

1. Daraja la Kigamboni
2. Daraja La Kilombero
3. Daraja la Umoja
4. Daraja la Maragarasi
5. Chuo Kikuu cha Dodoma
6. Hospitali ya Mloganzila
7. JNIA terminal III
8. DART(Mwendo kasi)
9. Sekondari za Kata nchi nzima kila kata ina shule.
10. Mradi mkubwa wa maji wa Ziwa Victoria
11. Songwe Airport
12. Kigoma Airport
13. Tabora Airport
14. Umeme wa REA
15. Benjamin Mkapa hospital Dodoma
16. Chuo kikuu cha Nelson Mandela Arusha
17. Dangote industry
18. Bomba la gesi Mtwara Dar
19. Kinyerezi I&II
20. Hospitali ya Moyo
21. MOI
22. Nchi nzima kuunganishwa kwa barabara za lami(zaidi km 14000 zilijengwa nchi nzima)
23. Umeme kwa makao makuu ya wilaya
24. Kuvusha Umeme Zanzibar
25. Ujenzi wa Mkongo wa taifa wa mawasiliano(leo tunajimwambafai na internet matunda ya JK)
26. JNICC Conference center(Ukumbi wa kisasa)
27. Hata CCM wenyewe aliwajengea ukumbi wa kisasa Dodoma.
28. Nyongeza ya mishahara kwa watumishi kila mwezi julai
29. Ajira kila mwaka
30. Annual Increment ilikuwa haki ya Mtumishi.
32. Diplomasia ya kimataifa ilikuwa juu katika ukanda wa maziwa makuu.
33. Demokrasia iliyopevuka
34. Aliwagomea CCM na kuwaambia hoja za kisiasa hujibiwa kisiasa, sio kwa kipigo cha polisi.
Hayo ni machache ya Mwamba Jakaya Mrisho Khalfani Kikwete lakini hakujimwambafai.

Hawa wanaomtukana na kusema kuwa hakufanya chochote zaidi ya wizi na ufisadi walikuwa wanaishi nchi gani?

Hivi huyo wanaemtukuza amefanya jambo gani kubwa linalofikia hata robo ya mkubwa aliyoyafanya Kikwete?

Kwakuhitimisha Kikwete alifanya makubwa na Mikopo aliyokopa kila mmoja ananufaika nayo na vitu vinaonekana.

Naomba nawe utukumbushe Mambo makubwa yaliyofanywa enzi za Jakaya.

Tiririka .....
Hali kwa sasa ni ngumu (Shemeji)
 
Kwani wewe unadhani hawajui kuwa JK kafanya kazi nzuri sana
Ila tu inabidi wamshushe kwa sababau wasipofanya hivyo viatu vya JK ni vikubwa sana kwa wao kuvivaa!

Ngoja niongeze vitu vingine katika achievement za JK

35. Zana nzito za kutisha za jeshi letu
36. Mfumo wa IT wa kukusanya mapato wa Halmashauri na e-Government
37. Ajira kwa vijana (Bodaboda, Bajaji, M-Pesa, Tigo-Pesa, HalotelMoney)
38. Kununua Vivuko kibao nchini kwa mfano kununua MV Magogoni, MV Utete, ununuzi wa MV Pangani, MV Kinesi etc
39. Kufanyia repair vivuko kibao kama vile MV Alina, MV Kigamboni, MV Sebgerema etc
40. Miradi kibao ya Kilimo kwa mfano kufungua chuo kuu cha kilimo cha Mwalimu Nyerere huko Butiama
41. Miradi ya maji ya bomba na visima kibao, mfano Maji ya bomba ni mradi kama wa Ruvu chini unaosupply Bagamoyo, Bunju na Makongo
42. Kuongezeka kwa wanafunzi wanaopata mkopo chuo kikuu, Ikumbukwe JK ndo aligeuza vyuo vinavyotoa advanced diploma kuwa vya digree na alitoa mikopo kwa wanafunzi wengi mno katika utawala wake
43. Kwenye afya alipambana vilivyo na ugonjwa wa Malaria,
44. Kwenye Kilimo wakulima wa Kahawa, Korosho, Mbaazi, Alizeti, walipata neema sana
45. Aliibadirisha sheria ya madini ile ya mzee Ben angalau tukaanza kunufaika na madini (Achilia mbali sarakasi za kina mruma za kudai tunadaiwa trilion 425 ambazo hatupewi ng'o)
46. Aliukarabati uwanja wa mpira wa Uhuru (Shamba la Bibi) siku hizi una majukwaa na pitc nzuri sana
47. Aliwekeza pia ktk michezo kwa mfano, kutuletea makocha wa nje kama vile Maximo na kusaidia kuleta Hamasa ya mpira na watu kuipenda timu yao ya Taifa
48. Aligawa chakula kwenye majanga kama vile njaa, penye ukame aligawa chakula, alisema hakuna ambaye angekufa kwa njaa
49. Kijeshi alitupa heshima, Aliwatwanga M23, Alimnyoosha Kanali Bacar wa Anjuani Comoro
50. Aliipa heshima TZ kidiplomasia, alisuluhisha migogoro mingi ya majirani wetu kama vile Kenya etc
51. Aliongeza ukusanyaji wa mapato kutoka shilingi bilion 160 kwa mwezi mwaka 2005 hadi shilingi bilion 850 kwa mwezi mwaka 2015
52. Ujenzi wa nyumba za sehemu mbalimbali nchini kwa mfano huko Kimbiji, Tabata n.k
53. Mafanikio ya NHC na NSSF kwenye kujenga nyumba nzurinzuri nchi nzima za bei nafuu
53. Angalau alitutoa ushamba kwa kuvutia investment kama vile Mlimani City na Mashopping malls mbalimbali katika miji mikuu
53. Angalia daraja kama la Furahisha mwanza
54. Miradi ya stendi mbali mbali kama vile ile ya Mbezi Mwisho, Stendi ya Tegeta kwa gari zinazoenda Bagamoyo
55. Kwa mara ya kwanza tangu nchi hii ipate uhuru aliruhusu taarifa za CAG ziwe zinasomwa na kujadiliwa bungeni
56. Alituruhusu tuone Bunge Live, siku hizi wananchi hawaelewi sana kinachoendelea huko bungeni
Mkuu umeua kabisaaa...Yaani ni Pwentiii tupu ila hebu tudukiscuss hiyo namba 42 kuhusu mikopo!?? Hapo Kuna ukakasi kidogo hivi tukisema una watoto 10 ukawahudumia 9.. ilihali mwenzio kaja na watoto 20 akawahudumia 17.. hivi nani apo atakuwa kafanya kazi kubwa!! Ukidiscuss kwa figure ileile ambapo kimsingi ni ngumu kulingana na wakati ingeleta logic ila hapo siungi mguu hoja!!!
 
Wewe ni mzungu???
Kama na wewe ni ngozi nyeusi basi jua upo kundi moja na wapumbavu maana hata ulichoandika hapa ni upumbavu
Wale waliotuhakikishia kipindi cha awamu ya nne kuwa Kikwete hajafanya lolote ndio leo wamegeuka na kuanza kuorodhesha yote aliyofanya.
Wale waliosema ccm tangu uhuru haijawahi kufanya chochote leo wamekuwa waimba pambio wa kusifia mambo yaliyofanywa na awamu nne zilizopita.

Kikwete na Mkapa ni viongozi ovyo kuwahi kutokea nchi hii, hata yule baba yenu wa taifa naye ovyo japo yeye alijitahidi compared to those couple above.
Nikiona watu leo wanamsifia Kikwete nachoka kabisa na kujiuliza how stupid these black people are.

Nikisema Waafrika wengi ni viumbe wapumbavu mnaanza kulia mara ooh Sir Khan mbaguzi.
Magufuli wanyooshe hawa watu mpaka akili ziwarudie.
 
Hivi hizo tenda si alikuwa anazisimamia mnyikulu .sijui bado anarun chini ya JPM. Hoja zote za hapo juu zinadhihirisha jinsi watanzania walivyokuwa wanafiki according to research .awamu ya nne mi karibia ingenipasua mchana kweupe.
 
JK alifanya mengi..lakini kwa haya machache nitaendelea kumkumbuka.
1. Serikali yake ambayo leo watu wanadai ilikuwa ya kifisadi ilitoa ushirikiano mkubwa kwa ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG. Mawaziri zaidi ya 13 wamepotezwa kutokana na uhuru mpana waliopewa CAG, BUNGE NA WAANDISHI WA HABARI.
2. Wakati wa utawala wa JK Wahalifu waitwao "WASIOJULIKANA" ambao wamejipatia umaarufu mkubwa kwenye zama hizi, hawakupata nafasi ya kuteka, kutesa na kuwapoteza moja kwa moja baadhi ya wananchi.
3. Pamoja na mazuri mengi aliyofanya JK hakuwahi kutumia majukwaa kujimwagia sifa, aliwaachia wananchi waseme
 
His own risk for his own choice,
and because he lost his choice, and again, on the other side the major rival also lost the battle, then he has got less risk.

Magufuli wasn't his choice,
And if in 4yrs tayari kumekucha kuanza kuwalinganisha basi kuna upande una speed inayomtisha aliyemtangulia, na wote wanaiona, yaani anayemfukuzia na anayefukuziwa,
Awamu hii inahubiri inayoyafanya ili watu waielewe awamu na kuiamini ipate support ya wananchi maana haina kundi la kisiasa la kuillinda,
Awamu inayoenda kuomba awamu bila kundi kama ilivyoingia bila kundi.
Hili uliloliona wengi wanajifanya hawalioni, JK anapashwa kupongezwa kwa kulisaidia Taifa na kutoruhusu lile kundi lake kuingia Ikulu, JK angeamua Lowassa awe Rais na ampiganie leo hii EL angekuwa Ikulu..

JK ndiye angepaswa atembee na ulinzi wa kutosha kwa kitendo kile cha kuwageuka wenzake mapema kabisa but he did not zaidi ya kutumia akili za kimedani nafikiri wazee akina Butiku nk wanafahamu risk aliyokuwanayo JK wakati ule.
 
Tuorodheshe na mizigo aliotuachia,
1. Escrow
2. Kila nyumba ilikuwa na jenereta umeme haukuwa wa uhakika.
3. Iptl
4. Watu walijichukulia pesa ya umma wanavyotaka.
5. Ufisadi ulishamiri.
6. Shirika la ndege lilikufa
7. Shirika la reli lilikufa
8. Kampuni ya huduma za meli nayo ilikuwa taabani
9. Madeni ya wafanyakazi yaliongezeka
10. Mikopo ya vyuo kutofika kwa wakati hadi maandamano
11. Wizi ulishamiri hasa mabenki na mabasi kuvamiwa
12. Uraisi ilikuwa wa familia.
13. Miradi ilikuwa ya gharama kubwa kuliko uhalisia
14. Taiga walipanda ndege na hakujulikana aliyewapandisha.
15. Tembo na wanyama wengine walipungua kwa mask.
16. Maji yalikuwa Shida.
17. Mikataba mingi mibovu ilisainiwa.
18.
 
Kwa Kifupi Kikwete kafanya Mambo mengi sema kosa alilofanya ni kuruhusu watu wamchezee sharubu

Kikwete Kaongeza Hospital kadhaa
While za Kata
Nyumba za watumishi wa Umma kama Polisi na Walimu
Vivuko nchi nzima
Barabara za kutosha
Kajenga Mwendo kasi
Kajenga uwanja wa Ndege terminal 3 japo JPM kaja kuizindua tu
Kajenga viwanja vya ndege Songwe, Bukoba, Mbeya, na Mwanza
Baadhi ya hospitali za mkoa nazozijua ni hospitali ya rufaa ya mkoa wa singida,alipanua hospitali ya mkoa wa Mbeya na songea
Kati ya sekta ambazo Jk alifanya vizuri ni barabara,elimu,diplomasia,demokrasia na uchumi kiujumla ila shida yake kuu hakuwabana vilivyo aliowateua na kitendo cha demokrasia na uhuru wa kujieleza kuwa mkubwa kilisababisha viongozi wa serikali kushindwa kuelezea mafanikio ya serikali maana kwa sasa hata zahanati ikijengwa lazima tujue
 
Enzi za JK kwa watumishi bima ya Afya ulikuwa unaruhusiwa kumpachika yeyote unayemtaka la msingi usizidi ile idadi ya wategemezi, leo unaambiwa uwapachike mke wako,mzazi au watoto tu, huu ni upuuzi mkubwa sana, wanashindwa kujua kuwa kuna mtu hana baba wala mama mzazi ila kalelewa na ndugu na jamaa ambao leo wanahitaji msaada kutoka kwake....inasemekana serikali ilikusanya kidogo sana kulinganisha na leo, lakini naamini pesa ilikuwa kwenye mikono ya raia ndiyo maana watu waliishi maisha mazuri, walisomesha watoto, walijenga nyumba nk leo hii haya yamebaki historia. Sipendi watu kubeza jitihada za viongozi waliopita, naamini waliopita walifanya yao na waliopo pia wanafanya yao ili taifa liendelee, hakuna mtu mmoja anaweza kukamilisha kila kitu peke yake, hata JPM kwa sasa anafanya yake na wengine watakuja wafanye yao. Ila wote mnasema JK hakufanya kitu mnakosea sana.
 
Tuorodheshe na mizigo aliotuachia,
1. Escrow
2. Kila nyumba ilikuwa na jenereta umeme haukuwa wa uhakika.
3. Iptl
4. Watu walijichukulia pesa ya umma wanavyotaka.
5. Ufisadi ulishamiri.
6. Shirika la ndege lilikufa
7. Shirika la reli lilikufa
8. Kampuni ya huduma za meli nayo ilikuwa taabani
9. Madeni ya wafanyakazi yaliongezeka
10. Mikopo ya vyuo kutofika kwa wakati hadi maandamano
11. Wizi ulishamiri hasa mabenki na mabasi kuvamiwa
12. Uraisi ilikuwa wa familia.
13. Miradi ilikuwa ya gharama kubwa kuliko uhalisia
14. Taiga walipanda ndege na hakujulikana aliyewapandisha.
15. Tembo na wanyama wengine walipungua kwa mask.
16. Maji yalikuwa Shida.
17. Mikataba mingi mibovu ilisainiwa.
18.

Escrow na IPTL ni kitu kilekile kasome historia ya IPTL ilianza lini jamaa yangu na mkataba uliasainiwa lini..

Hakuna Kampuni au shirika hata moja lililomfia JK huwa mnasahau sana kasome tena historia, mashirika yalikufa awamu ya pili na ya tatu, tena awamu ya tatu ikaja kuyauza kabisa...
Ukiondoa mkataba wa Buzwagi nitajie mkataba mwingine mbovu uliosainiwa na JK, mikataba mingi mibovu inayoisumbua hii nchi ilisainiwa awamu ya tatu kama hujui pale tu sera ya ubinafsishaji ilipoanza..
 
Back
Top Bottom