Mafanikio ya Utawala wa Jakaya Kikwete ndani ya Miaka 10

Mafanikio ya Utawala wa Jakaya Kikwete ndani ya Miaka 10

Kumbe hujui hata IPTL ilianza lini...? IPTL ipo toka miaka ya tisini kwa taarifa yako.
IPTL JK kaikuta nenda kasome historia..Kuna case za IPTL mahakamani London toka miaka ya tisini kasome historia vizuri..
Wewe hujui historia ya IPTL kaa kimya!! Kikwete ameiasisi kampuni ya IPTL kabla hajawa Rais; wakati huo alikuwa naibu waziri wa Nishati na Madini chini ya Al Noor Kasum
 
Jk alikuwa hana Promo tu ila mengi kafanya HUYU ANALIPA WATU WA KUMFANYIA PROMO NA PRAISE TEAM NAYO INA MKUZA SANA.JK KAFANYA YOTE BILA KUATHIRI KIPATO NA MAISHA HUKU MTAANI.
Kumekuwepo na vijembe na lugha za kejeli zinazotolewa na baadhi ya viongozi kutuhumu awamu zilizopita hasa awamu ya tano kana kwamba wao waliiba na hakuna maendeleo waliyoyafanya.

Orodha ni ndefu mimi nayakumbuka haya.

1. Daraja la Kigamboni
2. Daraja La Kilombero
3. Daraja la Umoja
4. Daraja la Maragarasi
5. Chuo Kikuu cha Dodoma
6. Hospitali ya Mloganzila
7. JNIA terminal III
8. DART(Mwendo kasi)
9. Sekondari za Kata nchi nzima kila kata ina shule.
10. Mradi mkubwa wa maji wa Ziwa Victoria
11. Songwe Airport
12. Kigoma Airport
13. Tabora Airport
14. Umeme wa REA
15. Benjamin Mkapa hospital Dodoma
16. Chuo kikuu cha Nelson Mandela Arusha
17. Dangote industry
18. Bomba la gesi Mtwara Dar
19. Kinyerezi I&II
20. Hospitali ya Moyo
21. MOI
22. Nchi nzima kuunganishwa kwa barabara za lami(zaidi km 14000 zilijengwa nchi nzima)
23. Umeme kwa makao makuu ya wilaya
24. Kuvusha Umeme Zanzibar
25. Ujenzi wa Mkongo wa taifa wa mawasiliano(leo tunajimwambafai na internet matunda ya JK)
26. JNICC Conference center(Ukumbi wa kisasa)
27. Hata CCM wenyewe aliwajengea ukumbi wa kisasa Dodoma.
28. Nyongeza ya mishahara kwa watumishi kila mwezi julai
29. Ajira kila mwaka
30. Annual Increment ilikuwa haki ya Mtumishi.
32. Diplomasia ya kimataifa ilikuwa juu katika ukanda wa maziwa makuu.
33. Demokrasia iliyopevuka
34. Aliwagomea CCM na kuwaambia hoja za kisiasa hujibiwa kisiasa, sio kwa kipigo cha polisi.
Hayo ni machache ya Mwamba Jakaya Mrisho Khalfani Kikwete lakini hakujimwambafai.

Hawa wanaomtukana na kusema kuwa hakufanya chochote zaidi ya wizi na ufisadi walikuwa wanaishi nchi gani?

Hivi huyo wanaemtukuza amefanya jambo gani kubwa linalofikia hata robo ya mkubwa aliyoyafanya Kikwete?

Kwakuhitimisha Kikwete alifanya makubwa na Mikopo aliyokopa kila mmoja ananufaika nayo na vitu vinaonekana.

Naomba nawe utukumbushe Mambo makubwa yaliyofanywa enzi za Jakaya.

Tiririka .....
 
Tuorodheshe na mizigo aliotuachia,
1. Escrow
2. Kila nyumba ilikuwa na jenereta umeme haukuwa wa uhakika.
3. Iptl
4. Watu walijichukulia pesa ya umma wanavyotaka.
5. Ufisadi ulishamiri.
6. Shirika la ndege lilikufa
7. Shirika la reli lilikufa
8. Kampuni ya huduma za meli nayo ilikuwa taabani
9. Madeni ya wafanyakazi yaliongezeka
10. Mikopo ya vyuo kutofika kwa wakati hadi maandamano
11. Wizi ulishamiri hasa mabenki na mabasi kuvamiwa
12. Uraisi ilikuwa wa familia.
13. Miradi ilikuwa ya gharama kubwa kuliko uhalisia
14. Taiga walipanda ndege na hakujulikana aliyewapandisha.
15. Tembo na wanyama wengine walipungua kwa mask.
16. Maji yalikuwa Shida.
17. Mikataba mingi mibovu ilisainiwa.
18.

Bomba la gesi tulipigwa ile mabaya bomba la bilion 200 tukajengewa kwa 1.2T ,
 
Wale waliotuhakikishia kipindi cha awamu ya nne kuwa Kikwete hajafanya lolote ndio leo wamegeuka na kuanza kuorodhesha yote aliyofanya.
Wale waliosema ccm tangu uhuru haijawahi kufanya chochote leo wamekuwa waimba pambio wa kusifia mambo yaliyofanywa na awamu nne zilizopita.

Kikwete na Mkapa ni viongozi ovyo kuwahi kutokea nchi hii, hata yule baba yenu wa taifa naye ovyo japo yeye alijitahidi compared to those couple above.
Nikiona watu leo wanamsifia Kikwete nachoka kabisa na kujiuliza how stupid these black people are.

Nikisema Waafrika wengi ni viumbe wapumbavu mnaanza kulia mara ooh Sir Khan mbaguzi.
Magufuli wanyooshe hawa watu mpaka akili ziwarudie.
Kuna wakati unaweza kudhani wenzako ni wajinga kumbe ni kwa sababu wewe umeshikwa na uwendawazimu.

Vichaa huwa wanaamini wana akili kuwazidi wenye akili, na pia wanaamini wana nguvu kuliko chochote, ndiyo maana huweza kusimama hata katikati ya barabrara wakiamini wana nguvu kuyazidi malori yanayoitumia hiyo barabara.

Waulize ndugu na marafiki zako kama wanakuona ni mzima. Mara nyingi magonjwa ya akili, dalili ya kwanza ni kuamini una akili kuwazidi watu wengine wote.
 
Wewe hujui historia ya IPTL kaa kimya!! Kikwete ameiasisi kampuni ya IPTL kabla hajawa Rais; wakati huo alikuwa naibu waziri wa Nishati na Madini chini ya Al Noor Kasum

Yanazungumziwa mafanikio ya urais wake, wewe unaleta habari za uwaziri.. Kama dhambi kuanzia watu walivyokuwa huko chini wengi wanazo.. Unajua kama IPTL ipo toka mwaka 1994 Rais ni Mwinyi tumuache tumlaumu JK wakati mwenye mamlaka yupo.
 
Kikwete alijitahidi sana. Na kwa kipimo chochote huwezi kumlinganisha na huyu wa sasa.

Tulimlaumu Kikwete kwa baadhi ya mambo. Tulitarajia tumpate kiongozi atakayekuwa bora kuliko yeye lakini kwa bahati mbaya tukampata huyu wa sasa.

Kosa kubwa la Kikwete ambalo mimi namlaumu ni kuruhusu mtu awauzie vimada na ndugu zake, nyumba za serikali kwa bei za kutupa (sh 10m nyumba iliyopo Upanga!). Halafu mtu huyo huyo badala ya kumpeleka Segerea, unampa nafasi ya kupewa madaraka ya juu zaidi. Huo ni udhaifu wa hali ya juu.
 
Mimi ongeeni yooote ila kubwa namshukuru sana mzee JK alinikopesha nkasoma elimu ya juu tena bila shida yoyote. Wazee wangu wasingeweza ila JK aliweza.
Ni jambo Jema, umalize mkopo wako kama bado wengine nao wafaidike.
 
Kumekuwepo na vijembe na lugha za kejeli zinazotolewa na baadhi ya viongozi kutuhumu awamu zilizopita hasa awamu ya tano kana kwamba wao waliiba na hakuna maendeleo waliyoyafanya.

Orodha ni ndefu mimi nayakumbuka haya.

1. Daraja la Kigamboni
2. Daraja La Kilombero
3. Daraja la Umoja
4. Daraja la Maragarasi
5. Chuo Kikuu cha Dodoma
6. Hospitali ya Mloganzila
7. JNIA terminal III
8. DART(Mwendo kasi)
9. Sekondari za Kata nchi nzima kila kata ina shule.
10. Mradi mkubwa wa maji wa Ziwa Victoria
11. Songwe Airport
12. Kigoma Airport
13. Tabora Airport
14. Umeme wa REA
15. Benjamin Mkapa hospital Dodoma
16. Chuo kikuu cha Nelson Mandela Arusha
17. Dangote industry
18. Bomba la gesi Mtwara Dar
19. Kinyerezi I&II
20. Hospitali ya Moyo
21. MOI
22. Nchi nzima kuunganishwa kwa barabara za lami(zaidi km 14000 zilijengwa nchi nzima)
23. Umeme kwa makao makuu ya wilaya
24. Kuvusha Umeme Zanzibar
25. Ujenzi wa Mkongo wa taifa wa mawasiliano(leo tunajimwambafai na internet matunda ya JK)
26. JNICC Conference center(Ukumbi wa kisasa)
27. Hata CCM wenyewe aliwajengea ukumbi wa kisasa Dodoma.
28. Nyongeza ya mishahara kwa watumishi kila mwezi julai
29. Ajira kila mwaka
30. Annual Increment ilikuwa haki ya Mtumishi.
32. Diplomasia ya kimataifa ilikuwa juu katika ukanda wa maziwa makuu.
33. Demokrasia iliyopevuka
34. Aliwagomea CCM na kuwaambia hoja za kisiasa hujibiwa kisiasa, sio kwa kipigo cha polisi.
Hayo ni machache ya Mwamba Jakaya Mrisho Khalfani Kikwete lakini hakujimwambafai.

Hawa wanaomtukana na kusema kuwa hakufanya chochote zaidi ya wizi na ufisadi walikuwa wanaishi nchi gani?

Hivi huyo wanaemtukuza amefanya jambo gani kubwa linalofikia hata robo ya mkubwa aliyoyafanya Kikwete?

Kwakuhitimisha Kikwete alifanya makubwa na Mikopo aliyokopa kila mmoja ananufaika nayo na vitu vinaonekana.

Naomba nawe utukumbushe Mambo makubwa yaliyofanywa enzi za Jakaya.

Tiririka .....
DART ilianzishwa na kuzinduliwa JPM
Barabara zilitekelezwa na bado zinatekelezwa na JPM

Daraja la Kigamboni (Nyerere Bridge) lilianzishwa na kuzinduliwa na JPM. E.t.c.

Na kwa kweli miradi ambayo ilikamilika kwa ufanisi chini ya Kikwete mingi ni ile iliyosimamiwa na JPM kama waziri ndiyo maana tulimpa Urais. Over.
 
JK aliachia nchi inaenda kwa auto pilot. It was a disaster. It was very painful experience.
Amepumzika sasa. Tumpe heshima yake na kumuacha apumzike kwa amani
Nchi ingekuwa kwenye autopilot hali isingekuwa ilivyo sasa. Autopilot ndo ilikuwa unalipa mishahara na kujenga barabara? Autopilot ndo. Iliwaangamiza m23? Autopilot ndo imefaya hayo yote mleta mada aliyosema? Upo sahihi mzee aachwe apumzike maana hatuna Shukrani.
 
DART ilianzishwa na kuzinduliwa JPM
Barabara zilitekelezwa na bado zinatekelezwa na JPM

Daraja la Kigamboni (Nyerere Bridge) lilianzishwa na kuzinduliwa na JPM. E.t.c.

Na kwa kweli miradi ambayo ilikamilika kwa ufanisi chini ya Kikwete mingi ni ile iliyosimamiwa na JPM kama waziri ndiyo maana tulimpa Urais. Over.
Na hili ndo kosa kubwa, watu wanafikiri aliyepita akipewa heshima yake anayostahili basi aliyopo anapungukiwa na sifa, wakati ukweli uliopo ni kwamba kila mtu anafanya yake kwa wakati wake. Kwani ni lazima mafanikio yaliyopita uyaunganishe na yanayofanyika?
 
Umenena vyema.

Kwa haya uliyoyaandika na yaliyoorodheshwa na mleta mada, nina hakika awamu hii mpaka sasa hawajafikia hata 10%. Hata kama wakiongezewa miaka iliyobakia, sidhani kama watafikia hata 30%.

Awamu hii wamekwishaharibu kwenye eneo la uchumi, ari ya utendaji kazi na uzalishaji, kamwe hawawezi kufanya makubwa.

Kikwete alifanikiwa kwa vile kulikuwa na fedha. Uwekezaji wakati wa kikwete ulifikia ukuaji wa 28%, sahizi ni 4% tu! Uwekezaji huongeza pesa ya kodi lakini pia huleta fedha toka mataifa ya nje na kuhuisha uchumi wa ndani. Huyu amefukuza uwekezaji wa nje na hata kuondosha ambao tayari ulikuwepo ndani ya nchi. Angalia akina Bakhresa walivyowekeza SA, Burundi, Zambia n.k. Angalia viwanda vya cement vinavyojengwa na Watanzania nchini Msumbiji. Angalia vituo vya mafuta vinavyojengwa na Watanzania nchini Zambia, n.k. Angalia wawekezaji waliokuwepo Tanzania walioenda kuwekeza Mauritius. Wawekezaji wamekosa confidence ya mazingira ya uwekezaji Tanzania. Ni vigumu sana kuwarudisha au hata kuwaleta wapya.

Kikwete aliongeza sana uzalishaji na mauzo ya nje ya zao la korosho. Pesa hiyo ilisaidia mzunguko wa fedha na uletaji wa fedha za kigeni. Huyo ameua mauzo ya nje ya zao la korosho. Taarifa ya BoT inaonesha thamani ya mauzo ya mazao ya nje yameingia kwenye negativr growth. Haijawahi kutokea tangu uhuru.

Kikwete alijitahidi sana kuendeleza sekta ya utalii. Utalii ulifikia ukuaji wa 15%. Ongezeko la ukuaji wa utalii, liliifanya sekta ya utalii kuongoza katika uingizaji wa fedha za kigeni, ikifuatiwa na sekta ya madini. Huyu wa sasa ameushusha ukuaji wa sekta ya utalii mpaka 3.6%. Sasa hata wakija watalii 500, inatangazwa nchi nzima ili tujue kuwa watalii bado wanakuja!

Kikwete aliimarisha sana mahusiano ya nje. Licha ya kupata fedha kutoka kwenye uchumi uliokuwa unanawiri lakini pia aliweza kupata fedha nyingi za misaada na mikopo rahisi bila shida. Kwa nchi kama ya kwetu huwezi kupaa kiuchumi bila kutumia mbinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na misaada na mikopo. Ni wakati wa Kikwete, Tanzania ilikuwa ndiyo nchi ya kwanza katika Afrika kuweza kupata msaada mkubwa toka Marekani, ikifuatiwa na Ghana. Huyu alipokuja kutokana na mambo ya hovyo aliyoanza nayo pesa hiyo TZS 1.3 trillion tuliyokuwa tukiioata kila mwaka, ikapotea. Wenzetu Ghana walibahatika kupata mwendelezo mzuri wa uongozi, wanaendelea kupata mpaka leo, na Ghana inaongoza kwa ukuaji wa uchumi Afrika, na kuna wakati iliongoza kwa ukuaji wa uchumi Duniani. Ujerumani, ni kati ya mataifa yenye uchumi mzuri sana Duniani lakini ili kupiga hatua za maendeleo, baada ya vita kuu ya Dunia, ilipewa misaada. Misaada siyo mibaya, kama utaitumia kama mtaji.

Katika ujumla wake, ukiyatazama ambayo yalifanyika wakati wa Kikwete, tuwe wakweli wa nafsi zetu, yanayofanyika sasa ni kidogo sana yasiyostahili hata ulinganifu, lakini kelele ya kuyasifia imekuwa kubwa kuliko uhalisia. Nini cha ajabu kilichofanyika awamu hii ambacho hakikuwahi kufanyika?

Mwalimu Nyerere aliipokea nchi ikiwa haina grid ya Taifa. Alijenga grid ya Taifa. Alijenga mabwawa kama kidatu na Mtera. Kikwete akaongeza vyanzo vipya vya umeme wa gas. Kwa hiyo ujenzi wa bwawa jingine jipya awamu hii siyo kitu cha muujiza. Ni jambo la kawaida kwa nchi inayokuwa na ongezeko la watu.

Mwalimu Nyerere alinunua ndege 14 mpya, hakuna pangaboi hata moja. Sasa ndege za safari hii ni muujiza?

Wakati wa mwalimu kulijengwa reli toka Dar mpaka Kaprimposhi Zambia, karibia 2,000km. Sasa hii ya 300km ndiyo uwe muujiza?

Hospitali kama Muhimbili, na karibia zote za mikoa zilijrngwa wakati wa Mwalimu. Kikwete kioindi chake kulijengwa hospitali kubwa na uimarishaji wa hudumu za afya kwa kuboresha miundombinu yake. Sasa zahanati za awamu hii ziwe muujiza?

Hatujafikia pakulinganisha miradi ya awamu hii na ile ya awamu ya kwanza au awamu ya nne. Bado sana. Nauliza mambo machache:

1) Miaka 4 imepita, barabara km ngapi za lami zimejengwa awamu hii linganisha na 14,000km wakati wa Kikwete?

2) Madaraja makubwa mangapi yamejengwa awamu hii linganisha na madaraja 6 wakati wa Kikwete?

3) Ongezeko la la makusanyo ya serikali kwa 500% wakati wa Kikwete linganisha na ongezeko la sasa la makusanyo ya serikali

4) Linganisha ujenzi wa hospitali kubwa tatu (Mkapa, JK taasisi ya moyo na Mloganzila) zilizojengwa wakati wa Kikwete linganisha na awamu hii (hakuna hata moja labda ununuzi wa vifaa)

5) Linganisha ongezeko la wanafunzi wa vyuo vikuu lililoendana na ongezeko la mikopo, ujenzi wa UDOM na ubadilishaji wa vyuo vya kawaida kuwa vyuo vikuu, kutoka wanafunzi 3,000 mpaka 14,000. Ongezeko la 466%. Huyu wa sasa ameongeza wangapi?

6) Uletaji wa wawekezaji wakubwa kama Dangote wa zaidi ya $700m ulioendana na ajira za Watanzania 10,000. Huyu wa sasa ameleta uwekezaji gani ambao hata wa kufikia angalao $500m, na ajira za mara moja japo 5,000 tu? Au ndiyo vile viwanda 4,000 vilivyoajiri watu 12,000 (yaani kila kiwanda kina wafanyakazi 3!!!)

Awamu hii wafanye kazi lakini hawajafikia popote kiasi cha kujilinganisha na awamu iliyopita au awamu ya Mwalimu Nyerere. Wameharibu mambo mengi kwenye uchumi, wajisahihishe ili Mungu akiwajalia uhai, warekebishe katika kipindi cha pili. Kwa kipindi hiki their performance is very minimum, below our expectation.
Kwani wewe unadhani hawajui kuwa JK kafanya kazi nzuri sana
Ila tu inabidi wamshushe kwa sababau wasipofanya hivyo viatu vya JK ni vikubwa sana kwa wao kuvivaa!

Ngoja niongeze vitu vingine katika achievement za JK

35. Zana nzito za kutisha za jeshi letu
36. Mfumo wa IT wa kukusanya mapato wa Halmashauri na e-Government
37. Ajira kwa vijana (Bodaboda, Bajaji, M-Pesa, Tigo-Pesa, HalotelMoney)
38. Kununua Vivuko kibao nchini kwa mfano kununua MV Magogoni, MV Utete, ununuzi wa MV Pangani, MV Kinesi etc
39. Kufanyia repair vivuko kibao kama vile MV Alina, MV Kigamboni, MV Sebgerema etc
40. Miradi kibao ya Kilimo kwa mfano kufungua chuo kuu cha kilimo cha Mwalimu Nyerere huko Butiama
41. Miradi ya maji ya bomba na visima kibao, mfano Maji ya bomba ni mradi kama wa Ruvu chini unaosupply Bagamoyo, Bunju na Makongo
42. Kuongezeka kwa wanafunzi wanaopata mkopo chuo kikuu, Ikumbukwe JK ndo aligeuza vyuo vinavyotoa advanced diploma kuwa vya digree na alitoa mikopo kwa wanafunzi wengi mno katika utawala wake
43. Kwenye afya alipambana vilivyo na ugonjwa wa Malaria,
44. Kwenye Kilimo wakulima wa Kahawa, Korosho, Mbaazi, Alizeti, walipata neema sana
45. Aliibadirisha sheria ya madini ile ya mzee Ben angalau tukaanza kunufaika na madini (Achilia mbali sarakasi za kina profesa mruma za kudai kuwa tumeibiwa na ACACIA madini na kodi vyenye thamani ya trilion 425 )
46. Aliukarabati uwanja wa mpira wa Uhuru (Shamba la Bibi) siku hizi una majukwaa na pitch nzuri sana
47. Aliwekeza pia ktk michezo kwa mfano, kutuletea makocha wa nje kama vile Maximo na kusaidia kuleta Hamasa ya mpira na watu kuipenda timu yao ya Taifa
48. Aligawa chakula kwenye majanga kama vile njaa, penye ukame aligawa chakula, alisema hakuna ambaye angekufa kwa njaa
49. Kijeshi alitupa heshima, Aliwatwanga M23, Alimnyoosha Kanali Bacar wa Anjuani Comoro
50. Aliipa heshima TZ kidiplomasia, alisuluhisha migogoro mingi ya majirani wetu kama vile Kenya etc
51. Aliongeza ukusanyaji wa mapato kutoka shilingi bilion 160 kwa mwezi mwaka 2005 hadi shilingi bilion 850 kwa mwezi mwaka 2015
52. Ujenzi wa nyumba za sehemu mbalimbali nchini kwa mfano huko Kimbiji, Tabata n.k
53. Mafanikio ya NHC na NSSF kwenye kujenga nyumba nzurinzuri nchi nzima za bei nafuu
53. Angalau alitutoa ushamba kwa kuvutia investment kama vile Mlimani City na Mashopping malls mbalimbali katika miji mikuu
53. Angalia daraja kama la Furahisha mwanza
54. Miradi ya stendi mbali mbali kama vile ile ya Mbezi Mwisho, Stendi ya Tegeta kwa gari zinazoenda Bagamoyo
55. Kwa mara ya kwanza tangu nchi hii ipate uhuru aliruhusu taarifa za CAG ziwe zinasomwa na kujadiliwa bungeni
56. Alituruhusu tuone Bunge Live, siku hizi wananchi hawaelewi sana kinachoendelea huko bungeni
 
Kikwete ndio muasisi wa kampuni ya IPTL na ufisadi WOTE ulifuata ukiwamo wa ESCROW!!!
Kikwete alikuwa muwazi na kiasi kikubwa aliheshimu uhuru wa mihimili mingine.

Tuliijua Escrow na IPTL kwa sababu aliruhusu watu kujadili.

Huyu kwenye awamu yake 1.5 trillion haijulikani iliko, na hataki watu wajadili. Huyu aliyelinda upotevu wa 1.5 trillion na aliyeruhusu kujadiliwa kwa 300 billion, nani afadhali?
 
Mijitu mizimaa yanalumbana eti kwa Kingozi kufanya wajibu wake. Waafrika hatutaendelea maisha yetu tutabaki kufadhiliwa kama maiti fungua usikilize
 
Back
Top Bottom