Mafanikio ya Utawala wa Jakaya Kikwete ndani ya Miaka 10

Mafanikio ya Utawala wa Jakaya Kikwete ndani ya Miaka 10

Ila la kutumia mabilioni yetu katika mchakato wa Katiba mpya kisha kuitupa kapuni hili limeharibu yote mema aliyofanya. Katuachia msala mkubwa sana.

Nani kaitupa katiba mpya kapuni?
JPM ndo kazuia mchakato usiendelee mbele, JK aliacha phase ya kura ya maoni ifuate, JPM kaja kapiga chini process nzima!.

Kama ulitaka ile ya Warioba ndo iwe yenyewe bila kupelekwa katika bunge la katiba na kufanyiwa marekebisho basi inaelekekea hukusoma sheria ya mabadiriko ya katiba inasema nini!. Sidhani kama ulitaka JK aingilie kati na kuimpose view yake katika jambo nyeti kama lile!.

Sheria ilitaka bunge la katiba liwepo, na likawepo, sasa yaliyotokea huko ukimlaumu JK utakuwa haumtendei haki labda kama ulitaka awapige rungu CCM wafuate anavyotaka yeye!!!
 
Lakin aliepewa hiyo nafasi mbona anamchukulia poa tu
Hili uliloliona wengi wanajifanya hawalioni, JK anapashwa kupongezwa kwa kulisaidia Taifa na kutoruhusu lile kundi lake kuingia Ikulu, JK angeamua Lowassa awe Rais na ampiganie leo hii EL angekuwa Ikulu..

JK ndiye angepaswa atembee na ulinzi wa kutosha kwa kitendo kile cha kuwageuka wenzake mapema kabisa but he did not zaidi ya kutumia akili za kimedani nafikiri wazee akina Butiku nk wanafahamu risk aliyokuwanayo JK wakati ule.
 
Sasa mnaposema kuwa miaka minne ya magufuli amefanya makubwa kuliko awamu zote mnapatawa jeuri hiyo?
 
Umenena vyema.

Kwa haya uliyoyaandika na yaliyoorodheshwa na mleta mada, nina hakika awamu hii mpaka sasa hawajafikia hata 10%. Hata kama wakiongezewa miaka iliyobakia, sidhani kama watafikia hata 30%.

Awamu hii wamekwishaharibu kwenye eneo la uchumi, ari ya utendaji kazi na uzalishaji, kamwe hawawezi kufanya makubwa.

Kikwete alifanikiwa kwa vile kulikuwa na fedha. Uwekezaji wakati wa kikwete ulifikia ukuaji wa 28%, sahizi ni 4% tu! Uwekezaji huongeza pesa ya kodi lakini pia huleta fedha toka mataifa ya nje na kuhuisha uchumi wa ndani. Huyu amefukuza uwekezaji wa nje na hata kuondosha ambao tayari ulikuwepo ndani ya nchi. Angalia akina Bakhresa walivyowekeza SA, Burundi, Zambia n.k. Angalia viwanda vya cement vinavyojengwa na Watanzania nchini Msumbiji. Angalia vituo vya mafuta vinavyojengwa na Watanzania nchini Zambia, n.k. Angalia wawekezaji waliokuwepo Tanzania walioenda kuwekeza Mauritius. Wawekezaji wamekosa confidence ya mazingira ya uwekezaji Tanzania. Ni vigumu sana kuwarudisha au hata kuwaleta wapya.

Kikwete aliongeza sana uzalishaji na mauzo ya nje ya zao la korosho. Pesa hiyo ilisaidia mzunguko wa fedha na uletaji wa fedha za kigeni. Huyo ameua mauzo ya nje ya zao la korosho. Taarifa ya BoT inaonesha thamani ya mauzo ya mazao ya nje yameingia kwenye negativr growth. Haijawahi kutokea tangu uhuru.

Kikwete alijitahidi sana kuendeleza sekta ya utalii. Utalii ulifikia ukuaji wa 15%. Ongezeko la ukuaji wa utalii, liliifanya sekta ya utalii kuongoza katika uingizaji wa fedha za kigeni, ikifuatiwa na sekta ya madini. Huyu wa sasa ameushusha ukuaji wa sekta ya utalii mpaka 3.6%. Sasa hata wakija watalii 500, inatangazwa nchi nzima ili tujue kuwa watalii bado wanakuja!

Kikwete aliimarisha sana mahusiano ya nje. Licha ya kupata fedha kutoka kwenye uchumi uliokuwa unanawiri lakini pia aliweza kupata fedha nyingi za misaada na mikopo rahisi bila shida. Kwa nchi kama ya kwetu huwezi kupaa kiuchumi bila kutumia mbinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na misaada na mikopo. Ni wakati wa Kikwete, Tanzania ilikuwa ndiyo nchi ya kwanza katika Afrika kuweza kupata msaada mkubwa toka Marekani, ikifuatiwa na Ghana. Huyu alipokuja kutokana na mambo ya hovyo aliyoanza nayo pesa hiyo TZS 1.3 trillion tuliyokuwa tukiioata kila mwaka, ikapotea. Wenzetu Ghana walibahatika kupata mwendelezo mzuri wa uongozi, wanaendelea kupata mpaka leo, na Ghana inaongoza kwa ukuaji wa uchumi Afrika, na kuna wakati iliongoza kwa ukuaji wa uchumi Duniani. Ujerumani, ni kati ya mataifa yenye uchumi mzuri sana Duniani lakini ili kupiga hatua za maendeleo, baada ya vita kuu ya Dunia, ilipewa misaada. Misaada siyo mibaya, kama utaitumia kama mtaji.

Katika ujumla wake, ukiyatazama ambayo yalifanyika wakati wa Kikwete, tuwe wakweli wa nafsi zetu, yanayofanyika sasa ni kidogo sana yasiyostahili hata ulinganifu, lakini kelele ya kuyasifia imekuwa kubwa kuliko uhalisia. Nini cha ajabu kilichofanyika awamu hii ambacho hakikuwahi kufanyika?

Mwalimu Nyerere aliipokea nchi ikiwa haina grid ya Taifa. Alijenga grid ya Taifa. Alijenga mabwawa kama kidatu na Mtera. Kikwete akaongeza vyanzo vipya vya umeme wa gas. Kwa hiyo ujenzi wa bwawa jingine jipya awamu hii siyo kitu cha muujiza. Ni jambo la kawaida kwa nchi inayokuwa na ongezeko la watu.

Mwalimu Nyerere alinunua ndege 14 mpya, hakuna pangaboi hata moja. Sasa ndege za safari hii ni muujiza?

Wakati wa mwalimu kulijengwa reli toka Dar mpaka Kaprimposhi Zambia, karibia 2,000km. Sasa hii ya 300km ndiyo uwe muujiza?

Hospitali kama Muhimbili, na karibia zote za mikoa zilijrngwa wakati wa Mwalimu. Kikwete kioindi chake kulijengwa hospitali kubwa na uimarishaji wa hudumu za afya kwa kuboresha miundombinu yake. Sasa zahanati za awamu hii ziwe muujiza?

Hatujafikia pakulinganisha miradi ya awamu hii na ile ya awamu ya kwanza au awamu ya nne. Bado sana. Nauliza mambo machache:

1) Miaka 4 imepita, barabara km ngapi za lami zimejengwa awamu hii linganisha na 14,000km wakati wa Kikwete?

2) Madaraja makubwa mangapi yamejengwa awamu hii linganisha na madaraja 6 wakati wa Kikwete?

3) Ongezeko la la makusanyo ya serikali kwa 500% wakati wa Kikwete linganisha na ongezeko la sasa la makusanyo ya serikali

4) Linganisha ujenzi wa hospitali kubwa tatu (Mkapa, JK taasisi ya moyo na Mloganzila) zilizojengwa wakati wa Kikwete linganisha na awamu hii (hakuna hata moja labda ununuzi wa vifaa)

5) Linganisha ongezeko la wanafunzi wa vyuo vikuu lililoendana na ongezeko la mikopo, ujenzi wa UDOM na ubadilishaji wa vyuo vya kawaida kuwa vyuo vikuu, kutoka wanafunzi 3,000 mpaka 14,000. Ongezeko la 466%. Huyu wa sasa ameongeza wangapi?

6) Uletaji wa wawekezaji wakubwa kama Dangote wa zaidi ya $700m ulioendana na ajira za Watanzania 10,000. Huyu wa sasa ameleta uwekezaji gani ambao hata wa kufikia angalao $500m, na ajira za mara moja japo 5,000 tu? Au ndiyo vile viwanda 4,000 vilivyoajiri watu 12,000 (yaani kila kiwanda kina wafanyakazi 3!!!)

Awamu hii wafanye kazi lakini hawajafikia popote kiasi cha kujilinganisha na awamu iliyopita au awamu ya Mwalimu Nyerere. Wameharibu mambo mengi kwenye uchumi, wajisahihishe ili Mungu akiwajalia uhai, warekebishe katika kipindi cha pili. Kwa kipindi hiki their performance is very minimum, below our expectation.
Dah nimekusoma vyema mkuu umefunguka vyema sana
 
Akili Kama hizi ni matope au makamasi!? VP, PM, Speaker, Hawa ni wakabila lake!? Wakifika mawaziri Wa5 yaan Full minister wanatoka kabila lake anagalau andiko lako tulipe uhalali!?? Ukiondoa CDF tu , IGP, CGP, CGF, CGI hawa n wakabila lake!?? Njoo Mpk Boss wa TISS nae ni wakabila lake!??
Mkuu kuna wakati wewe na wapumbavu wengine wenzio huwa mnaamua tu kutype chochote baada ya kuvimbiwa kande!!!
acha UPUNGA wewe hawa
Ukiondoa CDF tu , IGP, CGP, CGF
hawa ni wakwere?
mbona unaPANIC au kichwa tupu mnajimwambafy
tulia dawa ikuingie hakuna zaidi ya mkwere hata kwa Roho nzuri
 
Kwa Kifupi Kikwete kafanya Mambo mengi sema kosa alilofanya ni kuruhusu watu wamchezee sharubu

Kikwete Kaongeza Hospital kadhaa
While za Kata
Nyumba za watumishi wa Umma kama Polisi na Walimu
Vivuko nchi nzima
Barabara za kutosha
Kajenga Mwendo kasi
Kajenga uwanja wa Ndege terminal 3 japo JPM kaja kuizindua tu
Kajenga viwanja vya ndege Songwe, Bukoba, Mbeya, na Mwanza
Hii pia ilimsaidia sana kuwa na uwazi katika serikali. Maana mijadala huru hadi kupelekea kashfa nyingi kuibuliwa. Wristleblowers tulivujisha sana habari nzito na zikatikisa nchi.

Deal zilikuwa nyingi sana tena bila mizengwe.
 
Kumekuwepo na vijembe na lugha za kejeli zinazotolewa na baadhi ya viongozi kutuhumu awamu zilizopita hasa awamu ya tano kana kwamba wao waliiba na hakuna maendeleo waliyoyafanya.

Orodha ni ndefu mimi nayakumbuka haya.

1. Daraja la Kigamboni
2. Daraja La Kilombero
3. Daraja la Umoja
4. Daraja la Maragarasi
5. Chuo Kikuu cha Dodoma
6. Hospitali ya Mloganzila
7. JNIA terminal III
8. DART(Mwendo kasi)
9. Sekondari za Kata nchi nzima kila kata ina shule.
10. Mradi mkubwa wa maji wa Ziwa Victoria
11. Songwe Airport
12. Kigoma Airport
13. Tabora Airport
14. Umeme wa REA
15. Benjamin Mkapa hospital Dodoma
16. Chuo kikuu cha Nelson Mandela Arusha
17. Dangote industry
18. Bomba la gesi Mtwara Dar
19. Kinyerezi I&II
20. Hospitali ya Moyo
21. MOI
22. Nchi nzima kuunganishwa kwa barabara za lami(zaidi km 14000 zilijengwa nchi nzima)
23. Umeme kwa makao makuu ya wilaya
24. Kuvusha Umeme Zanzibar
25. Ujenzi wa Mkongo wa taifa wa mawasiliano(leo tunajimwambafai na internet matunda ya JK)
26. JNICC Conference center(Ukumbi wa kisasa)
27. Hata CCM wenyewe aliwajengea ukumbi wa kisasa Dodoma.
28. Nyongeza ya mishahara kwa watumishi kila mwezi julai
29. Ajira kila mwaka
30. Annual Increment ilikuwa haki ya Mtumishi.
32. Diplomasia ya kimataifa ilikuwa juu katika ukanda wa maziwa makuu.
33. Demokrasia iliyopevuka
34. Aliwagomea CCM na kuwaambia hoja za kisiasa hujibiwa kisiasa, sio kwa kipigo cha polisi.
Hayo ni machache ya Mwamba Jakaya Mrisho Khalfani Kikwete lakini hakujimwambafai.

Hawa wanaomtukana na kusema kuwa hakufanya chochote zaidi ya wizi na ufisadi walikuwa wanaishi nchi gani?

Hivi huyo wanaemtukuza amefanya jambo gani kubwa linalofikia hata robo ya mkubwa aliyoyafanya Kikwete?

Kwakuhitimisha Kikwete alifanya makubwa na Mikopo aliyokopa kila mmoja ananufaika nayo na vitu vinaonekana.

Naomba nawe utukumbushe Mambo makubwa yaliyofanywa enzi za Jakaya.

Tiririka .....
Tuachane na utoto, Mwinyi aliwahi kusema kwamba kila kitabu kina zama zake, hivyo alikuwepo Nyerere, na uzuri wake na Mapungufu yake, akawa Mwinyi na uzuri wake na Mapungufu yake, akaja Mkapa hivyo hivyo na JK tukawa na mategemeo yetu ya ukijana na modernity etc na sasa Magufuli na "ushamba" wake anayo mazuri yake na Mapungufu yake , mwisho wa siku naye atasemwa kwa uzuri wake na wengine kwa mapungufu yake. Hivyo hakuna haha ya kuingia kwenye malumbano ya kitoto ya kwamba Baba au Mama wa fulani ni Not a zaidi ya Wazazi wa fulani.
 
  • Thanks
Reactions: nao
[Kajenga nyumba za jwtz nchi nzima
QUOTE="britanicca, post: 33128597, member: 290488"]
Kwa Kifupi Kikwete kafanya Mambo mengi sema kosa alilofanya ni kuruhusu watu wamchezee sharubu

Kikwete Kaongeza Hospital kadhaa
While za Kata
Nyumba za watumishi wa Umma kama Polisi na Walimu
Vivuko nchi nzima
Barabara za kutosha
Kajenga Mwendo kasi
Kajenga uwanja wa Ndege terminal 3 japo JPM kaja kuizindua tu
Kajenga viwanja vya ndege Songwe, Bukoba, Mbeya, na Mwanza
[/QUOTE]
Miradi yote aliyotekeleza Kikwete gharama zake hazifikii gharama za mradi mmoja wa bwawa la umeme linalojengwa na Magufuli achilia mbali miradi mingine mingi iliyomalizika na inayoendelea.
 
Tuachane na utoto, Mwinyi aliwahi kusema kwamba kila kitabu kina zama zake, hivyo alikuwepo Nyerere, na uzuri wake na Mapungufu yake, akawa Mwinyi na uzuri wake na Mapungufu yake, akaja Mkapa hivyo hivyo na JK tukawa na mategemeo yetu ya ukijana na modernity etc na sasa Magufuli na "ushamba" wake anayo mazuri yake na Mapungufu yake , mwisho wa siku naye atasemwa kwa uzuri wake na wengine kwa mapungufu yake. Hivyo hakuna haha ya kuingia kwenye malumbano ya kitoto ya kwamba Baba au Mama wa fulani ni Not a zaidi ya Wazazi wa fulani.

Mkuu haya yamekuja baada ya kuona Mzee wetu kila siku anasimangwa na makada wenzie kana kwamba hakuna alichofanya hivyo sio vyema likapita hivihivi bila ukweli kusemwa ili kila kitu kijulikane maana wengine inawezekana ni wadogo hawakuishi zama za JKN, AM, BWM na JK..

La Msingi pia ni makada,wafuas na wapenzi wa CCM kuacha unafiki na kugeukana kwa kuangalia upepo baadala yake wasimamie ukweli, haki na wawe wazalendo wa kweli..

Raisi wetu JPM afahamu pia amezungukwa na wanafiki wa CCM wapo kimaslahi na kuangalia mvumo wa upepo hata kesho tu upepo ukibadirika watamgeuka hata yeye na kumsema ila ni sisi wazee wa fact ndio tutasimama naye na kuwaambia makada wenzie mnamuonea Mzee wetu alitenda hili na lile jema kwa Taifa yetu na mumuache Mzee wetu apumzike... Makada wa CCM wanahistoria mbaya juu ya wazee wetu kuanzia JKN, Mwinyi, BWM na JK ikumbukwe mpaka mzee Warioba alikulaga vibao wakati fulani kilichotokea kwa JKN wakati wa ubinafsishaji kila mtu anajua...
 
Kwa Kifupi Kikwete kafanya Mambo mengi sema kosa alilofanya ni kuruhusu watu wamchezee sharubu

Kikwete Kaongeza Hospital kadhaa
While za Kata
Nyumba za watumishi wa Umma kama Polisi na Walimu
Vivuko nchi nzima
Barabara za kutosha
Kajenga Mwendo kasi
Kajenga uwanja wa Ndege terminal 3 japo JPM kaja kuizindua tu
Kajenga viwanja vya ndege Songwe, Bukoba, Mbeya, na Mwanza
kosa jengine kubwa sana ambalo limeyeyusha yale mengi alioyafanya ni pale alipoitwanga na chini rasimu ya Warioba.
 
Kumekuwepo na vijembe na lugha za kejeli zinazotolewa na baadhi ya viongozi kutuhumu awamu zilizopita hasa awamu ya tano kana kwamba wao waliiba na hakuna maendeleo waliyoyafanya.

Orodha ni ndefu mimi nayakumbuka haya.

1. Daraja la Kigamboni
2. Daraja La Kilombero
3. Daraja la Umoja
4. Daraja la Maragarasi
5. Chuo Kikuu cha Dodoma
6. Hospitali ya Mloganzila
7. JNIA terminal III
8. DART(Mwendo kasi)
9. Sekondari za Kata nchi nzima kila kata ina shule.
10. Mradi mkubwa wa maji wa Ziwa Victoria
11. Songwe Airport
12. Kigoma Airport
13. Tabora Airport
14. Umeme wa REA
15. Benjamin Mkapa hospital Dodoma
16. Chuo kikuu cha Nelson Mandela Arusha
17. Dangote industry
18. Bomba la gesi Mtwara Dar
19. Kinyerezi I&II
20. Hospitali ya Moyo
21. MOI
22. Nchi nzima kuunganishwa kwa barabara za lami(zaidi km 14000 zilijengwa nchi nzima)
23. Umeme kwa makao makuu ya wilaya
24. Kuvusha Umeme Zanzibar
25. Ujenzi wa Mkongo wa taifa wa mawasiliano(leo tunajimwambafai na internet matunda ya JK)
26. JNICC Conference center(Ukumbi wa kisasa)
27. Hata CCM wenyewe aliwajengea ukumbi wa kisasa Dodoma.
28. Nyongeza ya mishahara kwa watumishi kila mwezi julai
29. Ajira kila mwaka
30. Annual Increment ilikuwa haki ya Mtumishi.
32. Diplomasia ya kimataifa ilikuwa juu katika ukanda wa maziwa makuu.
33. Demokrasia iliyopevuka
34. Aliwagomea CCM na kuwaambia hoja za kisiasa hujibiwa kisiasa, sio kwa kipigo cha polisi.
Hayo ni machache ya Mwamba Jakaya Mrisho Khalfani Kikwete lakini hakujimwambafai.

Hawa wanaomtukana na kusema kuwa hakufanya chochote zaidi ya wizi na ufisadi walikuwa wanaishi nchi gani?

Hivi huyo wanaemtukuza amefanya jambo gani kubwa linalofikia hata robo ya mkubwa aliyoyafanya Kikwete?

Kwakuhitimisha Kikwete alifanya makubwa na Mikopo aliyokopa kila mmoja ananufaika nayo na vitu vinaonekana.

Naomba nawe utukumbushe Mambo makubwa yaliyofanywa enzi za Jakaya.

Tiririka .....
Vipi anarudi tena au una mapenzi naye tu! Maana naona kumbe hata MOI ilijengwa na Kikwete! We bomu kweli!
35. Ongeza safari za nje tulikwenda sana!
36. Tulipata posho za safari na mikutano sana!
37. Vituo vya mafuta vilijengwa sana!
38. Petroli ilichanganywa na mafuta ya taa sana!
39. Posho za bunge zilipandishwa hadi laki 3
40. Idadi kubwa ya wabunge wa CCM walishika nafasi ya uwaziri japo kidogo
41. Tuliburudika sana na madawa ya kulevya mitaani kwetu
42.

Kwa kushindwa kutuletea Katiba mpya, endelea kuandika huo uchafu unaoita ni mafanikio bila kutueleza pesa yetu ilikwenda wapi kwa miaka kumi. Kipato chetu cha sasa hakistahili kuwekewa listi ya miradi ya bilioni chache kiasi hicho wakati bajeti yetu ni ya trilioni.
 
Miradi yote aliyotekeleza Kikwete gharama zake hazifikii gharama za mradi mmoja wa bwawa la umeme linalojengwa na Magufuli achilia mbali miradi mingine mingi iliyomalizika na inayoendelea.[/QUOTE]Sasa huo mradi umekamilika au hivi kujenga barabara zalami urefu jumla klm 14000 madaraja makubwa zaidi ya klm 1 yapo zaid ya sita halafu unalinganisha namradi uliotolewa kishika uchumba cha b650 mradi t6
 
Kumekuwepo na vijembe na lugha za kejeli zinazotolewa na baadhi ya viongozi kutuhumu awamu zilizopita hasa awamu ya tano kana kwamba wao waliiba na hakuna maendeleo waliyoyafanya.

Orodha ni ndefu mimi nayakumbuka haya.

1. Daraja la Kigamboni
2. Daraja La Kilombero
3. Daraja la Umoja
4. Daraja la Maragarasi
5. Chuo Kikuu cha Dodoma
6. Hospitali ya Mloganzila
7. JNIA terminal III
8. DART(Mwendo kasi)
9. Sekondari za Kata nchi nzima kila kata ina shule.
10. Mradi mkubwa wa maji wa Ziwa Victoria
11. Songwe Airport
12. Kigoma Airport
13. Tabora Airport
14. Umeme wa REA
15. Benjamin Mkapa hospital Dodoma
16. Chuo kikuu cha Nelson Mandela Arusha
17. Dangote industry
18. Bomba la gesi Mtwara Dar
19. Kinyerezi I&II
20. Hospitali ya Moyo
21. MOI
22. Nchi nzima kuunganishwa kwa barabara za lami(zaidi km 14000 zilijengwa nchi nzima)
23. Umeme kwa makao makuu ya wilaya
24. Kuvusha Umeme Zanzibar
25. Ujenzi wa Mkongo wa taifa wa mawasiliano(leo tunajimwambafai na internet matunda ya JK)
26. JNICC Conference center(Ukumbi wa kisasa)
27. Hata CCM wenyewe aliwajengea ukumbi wa kisasa Dodoma.
28. Nyongeza ya mishahara kwa watumishi kila mwezi julai
29. Ajira kila mwaka
30. Annual Increment ilikuwa haki ya Mtumishi.
32. Diplomasia ya kimataifa ilikuwa juu katika ukanda wa maziwa makuu.
33. Demokrasia iliyopevuka
34. Aliwagomea CCM na kuwaambia hoja za kisiasa hujibiwa kisiasa, sio kwa kipigo cha polisi.
Hayo ni machache ya Mwamba Jakaya Mrisho Khalfani Kikwete lakini hakujimwambafai.

Hawa wanaomtukana na kusema kuwa hakufanya chochote zaidi ya wizi na ufisadi walikuwa wanaishi nchi gani?

Hivi huyo wanaemtukuza amefanya jambo gani kubwa linalofikia hata robo ya mkubwa aliyoyafanya Kikwete?

Kwakuhitimisha Kikwete alifanya makubwa na Mikopo aliyokopa kila mmoja ananufaika nayo na vitu vinaonekana.

Naomba nawe utukumbushe Mambo makubwa yaliyofanywa enzi za Jakaya.

Tiririka .....
Jiwe na waimba kwaya wake hawatambui hata moja hapo
 
Vipi anarudi tena au una mapenzi naye tu! Maana naona kumbe hata MOI ilijengwa na Kikwete! We bomu kweli!
35. Ongeza safari za nje tulikwenda sana!
36. Tulipata posho za safari na mikutano sana!
37. Vituo vya mafuta vilijengwa sana!
38. Petroli ilichanganywa na mafuta ya taa sana!
39. Posho za bunge zilipandishwa hadi laki 3
40. Idadi kubwa ya wabunge wa CCM walishika nafasi ya uwaziri japo kidogo
41. Tuliburudika sana na madawa ya kulevya mitaani kwetu
42.

Kwa kushindwa kutuletea Katiba mpya, endelea kuandika huo uchafu unaoita ni mafanikio bila kutueleza pesa yetu ilikwenda wapi kwa miaka kumi. Kipato chetu cha sasa hakistahili kuwekewa listi ya miradi ya bilioni chache kiasi hicho wakati bajeti yetu ni ya trilioni.
hayo yote yalifanywa na wana CCM,nawe ni muimba kwaya tu WTF
 
acha UPUNGA wewe hawa
hawa ni wakwere?
mbona unaPANIC au kichwa tupu mnajimwambafy
tulia dawa ikuingie hakuna zaidi ya mkwere hata kwa Roho nzuri
Wewe kweli ni kitomfyo...
 
Back
Top Bottom