MAGARI YA UMEME: Fahamu Faida Zake, Aina na Namna Yanavyofanya Kazi

MAGARI YA UMEME: Fahamu Faida Zake, Aina na Namna Yanavyofanya Kazi

Ishu ni kudai kuwa wanatunza mazingira kupitia hizo electric cars. Lakini upatikanaji wa hio lithium battery ni worse kabisa na inatumia precious resource ambayo ni muhimu kwa viumbe hai, shughuli za uchimbaji wa lithium zinatumia MAJI mengi mno. Moja kati ya athari ya uchimbaji lithium wanasema inaweza kusababisha ukame!

Besides, kweli ukae karibia lisaa kujaza chaji betri yako? unapoteza precious time
Teknolojia zinabadilika.

Kuna documentary nimeona wanafanya tafiti ya teknolojia ya kutumia graphene kutengeneza battery ambazo zina last muda mrefu kuliko hizo za lithium.

Electric cars is the future. Ni suala la muda tu teknolojia ya battery itakuwa bora zaidi.
 
kwa TZ tuwe na campaign ya kufunga nishati ya Gas. miaka ya nyuma tulitamgaziwa tupeleke magari watufungie hiyo mifumo na vituo vikajengwa vya kujazia gas sikumbuki iliishia wapi hii campign sijasikia tena.
 
hii habari ni pigo kubwa sana kwa nchi ambazo uchumi wake unategemea mafuta na baadhi ya nchi za Africa ambapo mafuta yanazidi kugunduliwa. hata viwanda vingi kwa sasa duniani vinaelekea kwenye mifumo ya gas kujiendesha. technologia inabadilika kwa kasi sana dunuani.
 
Haya makampuni ya kuuza mafuta yanaweza kuweka charging station. Unalipia kiasi kuchaji.

Au hizi sehemu wanazouza vyakula, wanaweka charging stations huku unapiga msosi wako taratibu.

Kwahiyo ukitoka na tesla yako Dar, una uhakika wa kufika arusha bila tatizo.

Petrol station kuweka vituo vya kuchajia magari hawawezi,ni threat kwao.
 
Ishu ni kudai kuwa wanatunza mazingira kupitia hizo electric cars. Lakini upatikanaji wa hio lithium battery ni worse kabisa na inatumia precious resource ambayo ni muhimu kwa viumbe hai, shughuli za uchimbaji wa lithium zinatumia MAJI mengi mno. Moja kati ya athari ya uchimbaji lithium wanasema inaweza kusababisha ukame!

Besides, kweli ukae karibia lisaa kujaza chaji betri yako? unapoteza precious time
Niliona Documentary kule youtube,kuna nchi hapa E/Africa wao wamepiga marufuku pikipiki za kutumia mafuta wanataka za umeme tu,so wameamua kufanya majaribio kwny mji mkuu wao kwanza na kuna Co. Ya kimarekani imepewa hio Tenda.

Pikipiki hizo battery yake inaweza kutembea km 150 ndipo inaisha chaji,then hio Co. Ya Kimarekani ina vituo sehemu mbalimbali hapo mjini ambako pikipiki ikifika inabadilishiwa battery ndani ya dakika 1 inawekewa battery iliyojaa then inasepa zake inaacha hio,hakuna muda wa kusubiri kuchaji battery.

Labda model ya dizaini hii ingeletwa na kwny magari kama installation za battery hizo kwny gari zingekua ni rahisi(kitu ambacho najua ni vigumu kwa nature ya gari za umeme zilivyo).
 
Niliona Documentary kule youtube,kuna nchi hapa E/Africa wao wamepiga marufuku pikipiki za kutumia mafuta wanataka za umeme tu,so wameamua kufanya majaribio kwny mji mkuu wao kwanza na kuna Co. Ya kimarekani imepewa hio Tenda.

Pikipiki hizo battery yake inaweza kutembea km 150 ndipo inaisha chaji,then hio Co. Ya Kimarekani ina vituo sehemu mbalimbali hapo mjini ambako pikipiki ikifika inabadilishiwa battery ndani ya dakika 1 inawekewa battery iliyojaa then inasepa zake inaacha hio,hakuna muda wa kusubiri kuchaji battery.

Labda model ya dizaini hii ingeletwa na kwny magari kama installation za battery hizo kwny gari zingekua ni rahisi(kitu ambacho najua ni vigumu kwa nature ya gari za umeme zilivyo).
But Pia mkuu upo uwezekano wa Kujaa betri kwa dakika 18. Sioni Kama Ni kupoteza Muda hata ingekuwa lisaa limoja kwa range ya 500+ km.. Sababu siyo Muda wote gari inatembea.
 
Teknolojia zinabadilika.

Kuna documentary nimeona wanafanya tafiti ya teknolojia ya kutumia graphene kutengeneza battery ambazo zina last muda mrefu kuliko hizo za lithium.

Electric cars is the future. Ni suala la muda tu teknolojia ya battery itakuwa bora zaidi.
Tafiti ndio hazija maliza, kwa sasa wanatumia lithium na wanaendelea kuproduce lithium batteries na kuharibu mazingira vile vile.

Kweli wanataka battery iwe future.

Kuna swali najiuliza, hivi gari za electric zinapotembea wakati yale maringi yanazunguka kwanini hayarudishi chaji kwenye battery?
 
Niliona Documentary kule youtube,kuna nchi hapa E/Africa wao wamepiga marufuku pikipiki za kutumia mafuta wanataka za umeme tu,so wameamua kufanya majaribio kwny mji mkuu wao kwanza na kuna Co. Ya kimarekani imepewa hio Tenda.

Pikipiki hizo battery yake inaweza kutembea km 150 ndipo inaisha chaji,then hio Co. Ya Kimarekani ina vituo sehemu mbalimbali hapo mjini ambako pikipiki ikifika inabadilishiwa battery ndani ya dakika 1 inawekewa battery iliyojaa then inasepa zake inaacha hio,hakuna muda wa kusubiri kuchaji battery.

Labda model ya dizaini hii ingeletwa na kwny magari kama installation za battery hizo kwny gari zingekua ni rahisi(kitu ambacho najua ni vigumu kwa nature ya gari za umeme zilivyo).
Hio Idea ni nzuri lakini battery zina degrade. Atakuja mtu aweke battery yake ishaanza kufifia. Unapewa battery fully charged lakini unaona unakwenda short distance
 

Magari ya umeme ndiyo magari yanayotazamiwa kutumika zaidi siku za usoni. Serikali nyingi barani Ulaya zinaahidi kusaidia utengenezaji wa magari yenye kiwango cha chini cha uzalishaji wa hewa sumu, huku makampuni ya Mazda na Maserati yakiwa tayari yametengeneza au kuweka mipango ya kutengeneza magari ya umeme.

Suala la utengenezaji wa magari yatumiayo umeme si jipya kama inavyodhaniwa na wengi. Gari la kwanza la umeme lilitengenezwa mnamo 1837 huko Aberdeen, Uskochi. Teknolojia hiyo ilipata mafanikio kiasi ya kwamba teksi zilizotumia betri za umeme zilianza kutumika katika mitaa ya London na New York mwishoni mwa karne ya 19.

Hata hivyo, jambo la kusikitisha ni kuwa umaarufu wake haukudumu kwani bei ya mafuta ilipungua na hivyo kuyafanya magari ya petroli na dizeli kutawala barabara mpaka leo hii.

Sasa enzi mpya ya magari ya umeme imekuja. Pamoja na teknolojia kukua haraka, miundo inazidi kuvutia macho na ulimwengu unazidi kuwa na ufahamu zaidi wa mazingira.

Mnamo 2008 Tesla Roadster ilifikia kiwango cha kilomita 350 na kutoa msukumo kwa makampuni mengine ya utengenezaji wa magari kuingia katika soko hilo. Hivi sasa kampuni kama Volvo imetangaza kuwa kila gari wazalishalo kuanzia 2019 litatumia kabisa au litahusisha angalau mfumo kidogo wa kutumia umeme.

Hata hivyo ripoti zanadai kuwa mpaka kufikia mwaka 2035 magari yote mapya yatakayouzwa barani Ulaya yatakuwa yale yatumiayo umeme.

Je, magari ya umeme hufanya vipi kazi?
Badala ya tanki la mafuta, gari la umeme lina betri ya ndani ambayo huchajiwa kupitia usambazaji wa umeme na kisha huhifadhi na kutumia nguvu hiyo kuwezesha mota ya umeme na kusukuma magurudumu. Inamaanisha kuwa magari haya hayana haja ya clutch na mfumo wa gia au bomba la kutolea moshi, jambo linaloyafanya yawe yasiyotoa sauti kubwa kama yale ya mafuta. Waendeshaji wengi wa magari haya wanasema ni laini sana kuendesha.

Likiwa fully charged, gari la kawaida la umeme sasa linaweza kwenda zaidi ya kilomita 400 kabla ya kuhitaji kuchajiwa tena. Hiyo inaweza isiwe umbali unaopata kutoka kwenye magari ya petroli, lakini safari nyingi bado zinaweza kutekelezwa kwa urahisi kwenye gari la umeme.

Je, kuna faida gani za kutumia gari la umeme?
Kuna sababu nyingi kwanini mtu angetaka kuwa na gari la umeme. Moja ya sababu kubwa zaidi ni utunzaji wa mazingira. Magari haya yanazalisha kiasi kidogo cha hewa chafu na yana ufanisi zaidi kwani 95% ya nishati inayozalishwa hutumika katika mfumo wa kusukuma gari, wakati injini za mafuta zikiwa na ufanisi wa 30% tu -- nishati inayobaki inapotea kama joto au kelele.

Lakini kuna faida zingine pia. Kuna gharama za chini za uendeshaji kwani kuchaji betri hadi kujaa kabisa hutumia gharama za chini zaidi kulinganisha na kujaza tanki la petroli.

Kumbuka kuwa, ingawa kwa sasa ni gharama zaidi kununua gari la umeme kuliko gari la kawaida, kuna motisha na mipango maalumu ya serikali nyingi duniani iliyowekwa ili kukabiliana na hii.

Je, ni zipi aina tofauti za magari ya umeme?
Kwa ujumla kuna aina tatu za magari ambayo huchukuliwa kama 'ya umeme'.
  • Conventional Hybrids kama vile Toyota Prius ambayo yanahitaji tanki la petroli lakini pia ina mota ya umeme inayotumiwa na betri ambayo huchaji wakati gari linapofunga breki.
  • Plug-in Hybrids ambayo pia yana injini za petroli na mota za umeme lakini inaweza kuingizwa ili kuchaji na kwa ujumla inaweza kukimbia kwa muda mfupi kwa nguvu ya umeme kabla ya betri kuishiwa chaji.
  • Battery Electric Vehicles ndio huenda unafikiria zaidi unapofikiria magari ya umeme. Magari haya yanaendeshwa kwa umeme tu. Watengenezaji wengi wakubwa wa magari hutengeneza haya -- kuanzia Renault hadi wazalishaji wataalam wa magari ya umeme kama Tesla.
Je, unachaji vipi gari la umeme?
Tutachaji magari yetu kama vile tunachaji simu zetu kabla ya kwenda kulala ama wakati zinapoishiwa chaji, kwa kutumia soketi zile zile unazotumia kuwasha televisheni yako au mashine ya kunyolea.

Kasi ya kuchaji hutegemea aina ya gari ulilo nalo na aina ya usambazaji wa umeme ulioliunganisha nao.

Lakini, kawaida kuna aina tatu za kuchaji:
  • Kuchaji polepole (slow charging): hii inachukua kama masaa 5 mpaka kujaa kabisa.
  • Kuchaji haraka (fast charging): hii huchukua saa moja.
  • Kuchaji haraka zaidi (rapid charging): hii unaweza kuchaji gari lako kwa dakika 20 tu. Sehemu za huduma za kuchaji zinapatikana karibu na barabara kuu au kwenye vituo vya huduma za magari karibu na barabara.
Enzi mpya ya magari ya umeme
Ni wazi kwamba tunaingia kwenye enzi mpya ya magari ya umeme. Miundombinu ya huduma za magari haya zitakuwa zimeboreshwa sana katika miaka michache ijayo. Kuendesha gari la umeme itakuwa kawaida kwa wengi katika miaka ijayo na serikali na makampuni ya kuzalisha nishati yanaweka malengo makubwa kusaidia hilo kutekelezeka.
  • Nchini Ujerumani, serikali inaangalia uwezekano wa kuhama kabisa kutoka matumizi ya dizeli na petroli hadi umeme katika siku za usoni.
  • Ufaransa na Uingereza tayari wamepanga kupiga marufuku uuzaji wote wa magari ya petroli na dizeli ifikapo mwaka 2040.
  • Denmark sasa ina vituo vingi zaidi vya kuchaji magari ya umeme kuliko vituo vya mafuta.
  • Italia imesamehe wamiliki wa magari ya umeme ushuru wa kila mwaka na ushuru wa umiliki kwa miaka mitano tangu tarehe ya usajili wao wa kwanza.

Credits: E.ON
Shida kubwa kwa Tanzania ni hii teknolojia kuwa mpya, si kwa EV tu hata hizi hybrid. Hebu jaribu nenda kwa fundi wako muulize nataka agiza Prius ana maoni gani uone atakavyo kujibu.... Bila shaka atakwambia gari mbovu zile... Hazitengenezeki nk uvivu wa mafundi wetu ndio unapelekea tunaendelea ishi na teknolojia ya zamani. Mfano mwaka huu ni 2021 eti unaenda nunua toyota starlet ya mwaka 1999 na wewe unvimba barabani una gari, kweli? Au sababu fundi wako alikwambia gari hilo ni gumu (sijui ukigongana haliumii) na lina injini nyepesi kitengenezeka? Huwezi fanana na mtu alie nunua toyota ractis ya mwaka 2012 japo gari ya 2012 kwa wenzetu ina teknolojia ya zamani lakini kwetu utaitwa una "new model" lakini uko watembea na teknolojia ya kisasa ya gari yako na usalama wako, gari za kisasa zina mifumo mingi ya usalama, ulaji mzuri wa mafuta (economy) comfort nk.

Nashauri watanzania tubadilike, tukumbuke gari halijaumbwa kupigwa au kugongana eti utaskia makaratasi yale, ukigongana hiyo ni ajali, kwenye ajali safety features za gari huwa ni kumlinda mtumiaji wa gari atoke salama sio gari lisiumie, endeleeni kutumia magari yakigongana uso kwa uso dereva ana banwa na steering.

Kabla hatujaamua kuanza na EV sababu ya upungufu wa charging stations (kwa east africa kuna fast charging station iko chuo cha makerere Uganda tu) basi tununue hybrids mf toyota aqua... Hichi kidudu kipo poa na bei ya kawaida tu
 
Hio Idea ni nzuri lakini battery zina degrade. Atakuja mtu aweke battery yake ishaanza kufifia. Unapewa battery fully charged lakini unaona unakwenda short distance
Uzuri ni kwamba zile battery zote ziko owned na Co.,so kwa case yoyote ile ni mtu anaipeleka hio battery karibu na kituo kilicho karibu nae wanabadilisha chap then nduki
 
Shida kubwa kwa Tanzania ni hii teknolojia kuwa mpya, si kwa EV tu hata hizi hybrid. Hebu jaribu nenda kwa fundi wako muulize nataka agiza Prius ana maoni gani uone atakavyo kujibu.... Bila shaka atakwambia gari mbovu zile... Hazitengenezeki nk uvivu wa mafundi wetu ndio unapelekea tunaendelea ishi na teknolojia ya zamani. Mfano mwaka huu ni 2021 eti unaenda nunua toyota starlet ya mwaka 1999 na wewe unvimba barabani una gari, kweli? Au sababu fundi wako alikwambia gari hilo ni gumu (sijui ukigongana haliumii) na lina injini nyepesi kitengenezeka? Huwezi fanana na mtu alie nunua toyota ractis ya mwaka 2012 japo gari ya 2012 kwa wenzetu ina teknolojia ya zamani lakini kwetu utaitwa una "new model" lakini uko watembea na teknolojia ya kisasa ya gari yako na usalama wako, gari za kisasa zina mifumo mingi ya usalama, ulaji mzuri wa mafuta (economy) comfort nk.

Nashauri watanzania tubadilike, tukumbuke gari halijaumbwa kupigwa au kugongana eti utaskia makaratasi yale, ukigongana hiyo ni ajali, kwenye ajali safety features za gari huwa ni kumlinda mtumiaji wa gari atoke salama sio gari lisiumie, endeleeni kutumia magari yakigongana uso kwa uso dereva ana banwa na steering.

Kabla hatujaamua kuanza na EV sababu ya upungufu wa charging stations (kwa east africa kuna fast charging station iko chuo cha makerere Uganda tu) basi tununue hybrids mf toyota aqua... Hichi kidudu kipo poa na bei ya kawaida tu

Nazipenda prius/honda fit hybrid(kwa ajili ya matumizi ya mafuta),ila mafundi wa kibongo kwa kukatisha tamaa wako vzr.
 
Haya makampuni ya kuuza mafuta yanaweza kuweka charging station. Unalipia kiasi kuchaji.

Au hizi sehemu wanazouza vyakula, wanaweka charging stations huku unapiga msosi wako taratibu.

Kwahiyo ukitoka na tesla yako Dar, una uhakika wa kufika arusha bila tatizo.
Kwahiyo imeshindikana kabisa kuundiwa jiko ili betri ijichaji pale gari ikiwa inatembea!?
 
Tafiti ndio hazija maliza, kwa sasa wanatumia lithium na wanaendelea kuproduce lithium batteries na kuharibu mazingira vile vile.

Kweli wanataka battery iwe future.

Kuna swali najiuliza, hivi gari za electric zinapotembea wakati yale maringi yanazunguka kwanini hayarudishi chaji kwenye battery?
Kuna gari za hybrid zinacharge battery zake.
 
Kuna gari za hybrid zinacharge battery zake.
Simaanishi hio system ilokuwemo kwenye hybrid, nazungumzia full electric car. Wakati maringi yanazunguka, kwanini mzunguko wa hayo maringi usitumike kuzalisha umeme na kurudisha chaji kwenye betri? Windmill inazunguka ndio inatowa umeme, Hydro Elctric Power turbines zinazunguka na kuzalisha umeme, vipi maringi ya gari yanazunguka lakini hayazalishi umeme?
 
Back
Top Bottom