Magufuli angekuwepo sio tu vitu vingepanda bei, vingeadimika kabisa

Magufuli angekuwepo sio tu vitu vingepanda bei, vingeadimika kabisa

Kwa watetezi wa Magufuli najua mna hisia kali sana, lakini hebu jaribuni kujibu hoja kwa hoja, sio matusi

Hebu niambieni ni mambo gani Magufuli angefanya au alishafanya ambayo yangeshusha bei za vitu
Asingeweka tozo za ovyoovyo,angetafuta mafuta cheap kutoka Russia,angezuia vyakula kusafirishwa nje ya nchi hivyo kutokuongezeka Kwa bei ya vyakula.sasa hivi yote Haya yanatokea Kwa sababu ya uongozi dhaifu wa Rais samia.acha chuki zisizokuwa na maana.
 
Asingeweka tozo za ovyoovyo,angetafuta mafuta cheap kutoka Russia,angezuia vyakula kusafirishwa nje ya nchi hivyo kutokuongezeka Kwa bei ya vyakula.sasa hivi yote Haya yanatokea Kwa sababu ya uongozi dhaifu wa Rais samia.acha chuki zisizokuwa na maana.
Point alafu kwanini tumkisie ange fanya hivi au inge kua hivi wao ndio walikua wanamuongoza au ndio elimu zetu za kukariri na kubet (siidharau elimu ila nina mashaka na tunaotafuta elimu)

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Huyu Magufuli naanza kuona licha ya kutawala kwa muda mfupi, lakini anaonekana ndie ataongoza kutawala vichwa vya wengi zaidi ya marais waliopita.

Ukiuliza kwanini anasemwa hivi, utajibiwa lazima asemwe kwa mabaya yake, naona wajinga siku hizi wanajificha kwenye kivuli cha ubaya wa Magufuli, ili wao waonekane/wajione watakatifu, huku ni kujidanganya tu.

Magufuli hakuwa malaika, lazima kama mwanadamu wa kawaida alikuwa na mazuri na mabaya yake, lakini kwa baadhi hili hawalioni, wao kwao Magufuli alikuwa ni shetani tu, this is insanity & mental slavery.

Nikitizama vizuri hoja za mleta mada, naona ameamua kulaumu kwa kujua/kutojua, ili aendeleze tu kasumba ya kumsema vibaya Magufuli.

Mfano, anazungumzia sakata la sukari 2016 lililosababisha bei ya bidhaa kupanda, analaumu uamuzi wa Magufuli kuzuia uagizwaji wa sukari toka nje, kwamba huo ndio ulisababisha bei ya sukari kupanda.

Kwangu haya ni mawazo ya mtu anayefikiria kwa upande mmoja tu, tena negatively; kwasababu kama angeamua kufikiria positively ule uamuzi wa Magufuli kuzuia sukari toka nje, naamini angepata jibu zuri tu, kwamba alikuwa ana promote viwanda vyetu vya ndani, na kukuza ajira.
Safi
 
Hata yeye angekuwepo bei bado ingekuwa juu. Kwa taarifa yako mafuta ya kula yalianza kupanda wakati wake baada ya yeye kuvuruga soko la mafuta. Usidhani kuwa tumesahau alipojifanya anapiga marufuku mafuta toka nje. Toka wakati huo mpaka leo hayajawahi kushuka. Sukari ilipanda bei akawa anatumia kina Makonda kupitia kwenye godowns za wafanyabishara. Sasa hivi hali ndio ingekuwa mbaya zaidi. Bora Mungu aliingilia kati.
Pambaneni na wakati uliopo. Mnaanza kumkumbuka wakati hayupo. Amegoma kufa.
 
To me mwenye chembechembe za upinzani...MAGUFULI ni mtu na nusu
REST IN PARADISE DADA!
Sera za mzee hazikuwahi kugusa maslahi ya mwenye kipato cha chini (na hawa ndo wapiga kura )
Baba ali-deal na mapapa waliokuwa wanatupangia namna ya kuishi
 
Mazao ya wakulima yamepanda bei haijawahi kutokea, unadhani ni kwa nini? Mfano ni kahawa, mwaka 2015 kg1=2000, mwaka 2016-2021 kg1=950, mwaka 2022 kg1= 2150 (mkoa wa Kagera)
 
Na tozo watu wangelipa na hakuna wa kunyanyua mdomo..

Ujue mkiwa na Rais mwenye kiburi huwa ni disaster,imagine ndani ya miaka yake 5 mafuta ya magari yaliwahi adimika mara 2,sukari mara 2 na saruji mara 1 na hakukuwa na balaa kama za Uongozi wa Sasa..

Mwendazake angekuwepo Hali ingekuwa mbaya na angekuwa katili zaidi akiogopa kupinduliwa.
Nonsense,😎
 
Huu ni ujinga mkubwa, ingekatisha tamaa watu kulima kwa kuwa soko likiwa zuri wanazuiwa

Afadhali serikali ya Samia inanunua mahindi ya akiba na kuyatoa kipindi ambacho kuna uhaba, kitu ambacho Magufuli alisema ni ujinga
Sasa unapofunga mpaka ni kwa manufaa ya nani? Yaani mkulima alime kwa mahangaiko afu umpangie bei ya na pa kuuza? Mkulima kwa sasa analamba asali, mazao yamepanda bei ko wanaokaa mijini bila kupambana lazma walie. Mfano ndizi zilifikia hatua hata mnunuzi hayupo zinaozea mashambani, Leo mkulima wa Businde Kyerwa anafuatwa na mnunuzi shambani mkungu unaanzia elfu tano. Hapo mkulima utamwambia nini zaidi ya Samiah alofungua mipaka.
 
Siku watanzania watakapoamua kufanya kazi kabisa na kuacha kupambana na kivuli cha Magufuli, kuendelea kulinganisha utendaji wa viongozi, na ushabiki wa vitu vya hovyo kama Simba na yanga, taifa litapiga hatua kubwa sana.
 
Mtoa mada anajaribu kutetea udhaifu wa mama kushughulikia changamoto kubwa zinazolikabili taifa letu.

Analinganisha uhalisia na nadharia ambayo haipo na haitawahi kuwepo maana anayetaka kumlinganisha hayupo tena.

Anajaribu kutuamisha kwamba kwa Kukusanya kodi Kupitia maskini kwa Kuwatoza tozo kubwa ndiyo njia sahihi ya kuendesha nchi na siyo Kuwatoza kodi stahili wafanyabiashara wakubwa.

Kwa vile Magufuli hayupo kuelezea angewezaje ku deal na Mfumuko wa bidhaa na kupanda kwa gharama za maisha basi si vema kumnanga na Kumsema negatively.

Ninachojua na ambacho ni dhahili ni kwamba kwa kipindi chote cha miaka yake mitano bei za bidhaa nyingi hazikupanda kabisa na kwenye real estate business bei zilipungua sana ukilinganisha na kipindi cha 2010 to 2015
 
Na tozo watu wangelipa na hakuna wa kunyanyua mdomo..

Ujue mkiwa na Rais mwenye kiburi huwa ni disaster,imagine ndani ya miaka yake 5 mafuta ya magari yaliwahi adimika mara 2,sukari mara 2 na saruji mara 1 na hakukuwa na balaa kama za Uongozi wa Sasa..

Mwendazake angekuwepo Hali ingekuwa mbaya na angekuwa katili zaidi akiogopa kupinduliwa.
Kama aliweza kushusha bei za umeme, maji na bidhaa za vyakula ikiwemo mchele, unga nk, hizo tozo zingepitia mlango upi? kwa akili yako unafikiri wazo la kuleta tozo limeibuka juzi tu, lilikuwepo toka enzi za Magu, kwanini lianzishwe mara tu baada ya Magu kuondoka?
 
Tunahitaji ni Katiba mpya kwa sasa
 
Hpn inflation ingekuwa moderate Sana mnk mzee yule anacheza na maskini kuliko matajiri hvyo ,alikuwa tayari kuona tajiri anatezeka in expenses za masikini magu mjanja Sana anatafutiwa attention kwa walala hoi ndio maana mzee hajatupeleka lock down alijuwa watao tezeka Ni maskni tu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kama aliweza kushusha bei za umeme, maji na bidhaa za vyakula ikiwemo mchele, unga nk, hizo tozo zingepitia mlango upi? kwa akili yako unafikiri wazo la kuleta tozo limeibuka juzi tu, lilikuwepo toka enzi za Magu, kwanini lianzishwe mara tu baada ya Magu kuondoka?
20,000 ya Kitambulisho Cha Machinga ilipitia mlango gani?

Lini alishusha hivyo vitu wakati Sukari na Saruji vilimshinda? Hivyo vitu automatic vilishuka kwa sababu za Soko,,hakuna mwaka hata mmja Nchi jirani zilikubwa na Ukame ambayo ungelazimisha Bei za bidhaa kuwa juu,Wala hakuna mwaka hata mmja was Mwendazake Nchi ilipata mvua kidogo Ili kuathiri Bei..

Mwisho Mwaka 2021 wakati SSH anaingia bajeti ilikuwa tayari imeandaliwa na tozo zilianzishwa na Serikalini ya Mwendazake unless hujui mchakato was bajeti ndio unaweza ongea hayo..

Narudia kukwambia tozo mungelipa,na bidhaa zingeadimika huku Jiwe akishupaza shingo maana hata mkopo wa covid 19 ukichukukiwa Ili kuongeza hazina ya forex ambayo ilianguka na ambavyo Jiwe aliharibu Biashara Tzn ingeshakuwa kibra saizi maana Jiwe alitegemea zaidi mapato ya bandari na kupora pesa..
 
Back
Top Bottom