Mahakama yaamuru Eng. Hersi aachie ngazi Yanga!

Mahakama yaamuru Eng. Hersi aachie ngazi Yanga!

Potelea mbali. Guede aende tu. Maana hakuna namna nyingine. Na huyo Magoma hana uwezo wa kushindana na wananchi wote. Ni suala tu la muda kabla ya kumshughulikia ipasavyo. 😡
Hapo swala ni Magoma au katiba? Unamuonea bure mzee Magoma yeye anataka katiba ifatwe hata wananchi wote mnamkubali hersi. Vinginevyo malizeni transformation
 
Hapo swala ni Magoma au katiba? Unamuonea bure mzee Magoma yeye anataka katiba ifatwe hata wananchi wote mnamkubali hersi. Vinginevyo malizeni transformation
Simba ilimaliza transformation? Mbona Mo alisema kainunua Simba na wala hatujaona mahakama ikilishupalia? Serikali ilishasema kuwa lazima kuwe na wawekezaji wasiopungua watatu je kuna namna imetokea kwa Mo kuvuliwa kitengo Simba? Katiba ya Simba haikupitishwa na Mo anaendesha Simba kama kawaida kama mwekezaji. Hapa kilichopo ni siasa ya kuifanya Yanga ipoteane baada ya kuona mambo magumu ndani ya uwanja.
 
Simba ilimaliza transformation? Mbona Mo alisema kainunua Simba na wala hatujaona mahakama ikilishupalia? Serikali ilishasema kuwa lazima kuwe na wawekezaji wasiopungua watatu je kuna namna imetokea kwa Mo kuvuliwa kitengo Simba? Katiba ya Simba haikupitishwa na Mo anaendesha Simba kama kawaida kama mwekezaji. Hapa kilichopo ni siasa ya kuifanya Yanga ipoteane baada ya kuona mambo magumu ndani ya uwanja.
Yaani unachojaribu kufanya hapo ni kulikimbia tatizo nyumbani kwako na kushupalia matatizo ya jirani. Hapa hoja ni zee magoma na sakata la hersi kuipora utopolo nje ya katiba ya utopolo. Ya simba waachioe simba, zimeni moto wa nyumbani kwenu kwanza.
 
Simba ilimaliza transformation? Mbona Mo alisema kainunua Simba na wala hatujaona mahakama ikilishupalia? Serikali ilishasema kuwa lazima kuwe na wawekezaji wasiopungua watatu je kuna namna imetokea kwa Mo kuvuliwa kitengo Simba? Katiba ya Simba haikupitishwa na Mo anaendesha Simba kama kawaida kama mwekezaji. Hapa kilichopo ni siasa ya kuifanya Yanga ipoteane baada ya kuona mambo magumu ndani ya uwanja.
Wakitokea watu wa kushtaki Mahakama itafuata sheria,Mahakama haiwezi kuendesha kesi isiyo na msingi kutoka kwa walalamikaji
 
MAULID KITENGE ALIVYOMUHOJI MZEE MAGOMA

Kwa Mujibu wa Mzee Magoma amesema ameamua kuwa mstari wa Mbele kutafuta Haki ya Klabu ya Yanga Kwa sababu anaona inaendeshwa kishkaji na Wanachama wengi wapo kimya hawalioni Hilo Kwa Sasa

Follow ukurasa wetu wa Instagram kuisoma zaidi hukumu hiyo ya mahakama 👇

.
@followers
#followers
#followers
#yangasc
#Wazee
#mzeemagoma
#HABARI
#Halisimediatz
#genzmemes
 
View attachment 3044226

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam, imeamuru Uongozi wa Club ya Yanga ukiongozwa na Rais wa Yanga Injinia Hersi Saidi na wenzake, kuachia ngazi na kuondoka kwenye Club hiyo kwakuwa Katiba ya Yanga haitambui uwepo wao.

Imedaiwa kuwa uamuzi huu wa Mahakama umekuja baada ya Kundi la Wazee wachache waliowahi kuwa Wazee wa Yanga kipindi cha nyuma, kushitaki Mahakamani likidai uwepo wa Viongozi wa sasa wa Yanga (Injinia Hersi na wenzake) ni batili na haujafuata Katiba ya Club hiyo.

Kutokana na Wazee hao kushinda kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, inamaana kuwa Rais wa Yanga Injinia Hersi na Viongozi wenzake wanatakiwa kuachia ngazi na kukabidhi Ofisi kuanzia sasa.

Injinia Hersi alianza kuiongoza Yanga kama Rais miaka miwili iliyopita baada ya kushinda nafasi hiyo akiwa ni Mgombea pekee July 2022 na kumfanya kuwa Rais wa kwanza wa Yanga SC toka kuanza kwa mfumo mpya wa mabadiliko ambapo alitangazwa kuwa atakuwa madarakani kwa miaka minne ( hadi 2026 ) kwa mujibu wa Katiba ya Club hiyo.

Source: #MillardAyoUPDATES
PIA SOMA
- Yanga: Mkutano na wanahabari tar 17.07.204

====

Source nyingine:
Wanachama wawili wa Yanga SC JUMA MAGOMA na GEOFREY MWAIPOPO walishinda kesi waliyofungua katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar mwaka jana mwezi Agosti. Kesi yao ilikuwa dhidi ya Baraza la wadhamini la klabu hiyo kuikabidhi klabu kwa mtu wasiyemjua wala asiyekuwa Mwanachama wakati kesi inafunguliwa mwezi Mei mwaka 2022 siku moja kabla ya uchaguzi mkuu wa klabu uliomuweka madarakani Rais wa Yanga Eng Hersi Said. Awali walifungua kesi hiyo Mahakama ya Wilaya ya Ilala iliyopo Kinyerezi jijini Dar, kabla ya kushauriwa kuihamishia katika Mahakama ya Kisutu.

Walipinga kutumika kwa katiba ya mwaka 2020 ambayo ilitumika kwenye uchaguzi Mkuu uliouweka uongozi uliopo madarakani wakisema katiba hiyo sio halali. Inasemekana RITA waliitwa kutoa ushahidi na wakasema wanaifahamu katiba ya mwaka 2011 ambayo ipo ofisini kwao na hiyo ya mwaka 2020 hawaitambui.

Baada ya kupata hukumu yao mwezi Agosti mwaka 2023 JUMA MAGOMA NA GEOFREY MWAIPOPO wameona hakuna utekelezaji wa hukumu hiyo hata baada ya kuwasilisha kwa wahusika wakaamua kufungua kesi ya kukazia hukumu ambapo itatolewa maamuzi mwezi Agosti tarehe 5 mwaka 2024, ili hukumu hiyo ianze kufanya kazi. Ambapo inategemewa Mkutano Mkuu wa Yanga kuitwa ambao utajumuisha WANACHAMA WOTE HAI sio wawakilishi wa matawi pekee (kama ilivyo sasa) na kwenda kwenye uchaguzi mkuu wa uchaguzi wa viongozi wa klabu kwa kufuata katiba ya mwaka 2011.

Kama hili litatokea manake Eng Hersi na timu yake watakuwa wameondoshwa madarakani kwakuwa watakuwa wameingia isivyo halali.
View attachment 3044242

Pia soma==>> Je, Mahakama Ina Mamlaka ya Kumwondoa Rais wa Yanga Hersi?
Hukumu hii haiwezi kuwa ni "final & binding" pasipo uwepo na nafsi ya kukata rufaa.
 
Yanaanzaga hivi hivi hizi timu mbili zina siasa sanaaaaa , ngoja uone hapo linatengenezwa zengwe timu isitawalike wakati wa Yanga kuhenya unakaribia ,
Hapo simba nae atatambaaa weeee wakati ukifika zengwe tena hahahaa
 
Back
Top Bottom