Mahakama yaridhia kunyongwa aliyemuua Dereva Bodaboda

Mahakama yaridhia kunyongwa aliyemuua Dereva Bodaboda

Habari iliyoko hapa ni kwamba amehukumiwa kunyongwa kwa kukutwa na pikipiki ambayo wanasema ni ya marehemu. Lakini pia kabla ya kusema pikipiki hiyo ameipata wapi, ni lazima kwanza wathibitishe kuwa pikipiki iliyokamatwa ndiyo hiyo aliyokuwa akiiendesha marehemu. Na hili linawezekana kwa kupata taarifa za umiliki kutoka TRA.

Na inaonekana hakuulizwa hilo swali la kuwa kaipata wapi hiyo pikipiki. Na sababu ni kwamba mahakama yenyewe Haika om na ushahidi kutoka TRA kuthibitisha umiliki.

Soma hapo chini…

“Walibainisha miongoni mwa hoja za mrufani kupinga adhabu hiyo ilikuwa ni kwamba Mahakama Kuu ilikosea kumhukumu kwa kutumia ushahidi wa kukutwa na vitu vya marehemu huku kukiwa hakuna ushahidi iwapo wakati Msimbe anauawa alikuwa akitumia pikipiki aliyokutwa nayo yeye”


Mimi sio mtaalamu sana wa mambo ya sheria lakini Katika shauri hilo kuna kesi mbili, ya kwanza ni mauaji ambayo ni kubwa na ya pili ni uporaji, kesi kubwa huwa inameza kesi ndogo.

Kesi ya huyo mhusika ilikuwa ni kesi ya mauaji, hivyo ninachokiona mimi ni kwamba alishindwa kujitetea jinsi alivyopata hiyo pikipiki ndio maana katiwa hatiani hata kama hakuhusika na hayo mauaji.
 
Hiyo ni common sense !! Bahati mbaya sana watanzania hatuna uwezo wa kutumia common sense , akili ya mwanzo kabisa ambayo mwanadamu kapewa bure kabisa bila ya kwenda darasani.
Unaona hata kwenye huu mjadala baadhi ya watu hawajaitumia common sense , wanahukumu tu .bila kuhoji
Kwahiyo aliuziwa bila ushahidi wa watu wala wa kimaandishi ?

Aliyemwuzia si angejulikana ?
Pikipiki ya wizi kuna vibali flani inakosa na inajulikana ni ya wizi.

Mwenye pikipiki alitoa ushahidi wa vibali na wa maneno kuwa Marehemu alikuwa anatumia pikipiki kwa ruhusa yake ya kutafuta pesa. Na baadhi ya vibali alikuwa navyo.

Sasa Mjomba unanunua pikipiki kama unavyonunua Embe unategemea nini ?

Ndio maana kesi imedumu muda mrefu ni kwamba Mahakama ilitaka kujiridhisha.

Na mara zote kesi ya Mauaji mtuhumiwa anapewa Wakili wa Serikali bure ili kumsaidia kuepusha kumwadhibu mtu kwa kubahatisha.
 
Mimi sio mtaalamu sana wa mambo ya sheria lakini Katika shauri hilo kuna kesi mbili, ya kwanza ni mauaji ambayo ni kubwa na ya pili ni uporaji, kesi kubwa huwa inameza kesi ndogo.

Kesi ya huyo mhusika ilikuwa ni kesi ya mauaji, hivyo ninachokiona mimi ni kwamba alishindwa kujitetea jinsi alivyopata hiyo pikipiki ndio maana katiwa hatiani hata kama hakuhusika na hayo mauaji.
Mbona umejichanganya?

Unasema wewe siyo mtaalamu wa sheria, lakini hapo hapo unasema “kesi kubwa huwa inameza kesi ndogo”

Lakini hapo hapo unataka kesi ndogo(ushahidi wa kukutwa na pikipiki), ndiyo itumike kutoa hukumu ya kesi kubwa(mauwaji)?

Kama kukutwa na pikipiki ni kesi ndogo, kwanini itumike kutoa hukumu ya mauwaji ambayo ndo kesi kubwa kwa mujibu wa maelezo yako?
 
Kwahiyo Jamaa amehukumiwa kifo kwa sababu tu alikamwatwa na Pikipiki aliyokuwa anaendesha Marehemu?

Kwamba ameua wamethibitishaje sasa?

Na amini kuna zaidi, mfano kashindwa toa maelezo ya msingi na yanayoeleweka kusema aliitoa wapi, hapo panaweza amua kama yeye ni muuwaji.

Mfano, akijaribhwu kubisha kwamba pikipiki ni yake anayo miaka mingi, na ikathibitika ni ya marehemu, kwa nini aseme uongo
 
Mbona umejichanganya?

Unasema wewe siyo mtaalamu wa sheria, lakini hapo hapo unasema “kesi kubwa huwa inameza kesi ndogo”

Lakini hapo hapo unataka kesi ndogo(ushahidi wa kukutwa na pikipiki), ndiyo itumike kutoa hukumu ya kesi kubwa(mauwaji)?

Kama kukutwa na pikipiki ni kesi ndogo, kwanini itumike kutoa hukumu ya mauwaji ambayo ndo kesi kubwa kwa mujibu wa maelezo yako?


Ni hivi; Mtu aliyeuawa (kama inavyoelezwa) aliuawa na kuporwa pikipiki, yaani sababu ya kuuawa kwake ni ili aporwe pikipiki au aliuawa katika mazingira ya kupambana ili asiporwe pikipiki, kesi hapo inakuwa ni ya Mauaji na hiyo ya uporaji inakufa kifo cha mende, Uchunguzi lazima uwe na mwanzo na mwanzo wake ndio hapo kwamba; siku ya pili TU baada ya tukio ndipo mtu kakutwa/kakamatwa na pikipiki ile ile aliyokuwanayo mtu (bodaboda) aliyeuawa, sasa ilikuwa ni jambo rahisi tu kwa huyo mtu kujibu hili swali; Pikipiki hii umeipataje?? --- bila shaka ni majibu ya swali hili ndiyo yamemtia hatiani kwenye mauaji ya dereva wa boda boda.
 
Mahakama ya Rufani Morogoro, imetupilia mbali rufani ya Justine Chamashine aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kosa la kumuua dereva wa bodaboda, Joseph Frorence 'Msimbe'.

Uamuzi huo ulitolewa wiki iliyopita na Jopo la Majaji watatu likiongozwa na Jaji Mkuu Profesa Ibrahimu Juma. Majaji wengine ni Augustine Mwarija na Othman Makungu.

Chamashine alikata rufani kupinga hatia na adhabu aliyopewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam. Majaji hao walisema baada ya kupitia hoja za pande zote mbili wamebaini hoja za rufani hazina mashiko na Mahakama Kuu ilimhukumu mrufani kwa usahihi. Walibainisha miongoni mwa hoja za mrufani kupinga adhabu hiyo ilikuwa ni kwamba Mahakama Kuu ilikosea kumhukumu kwa kutumia ushahidi wa kukutwa na vitu vya marehemu huku kukiwa hakuna ushahidi iwapo wakati Msimbe anauawa alikuwa akitumia pikipiki aliyokutwa nayo yeye.

Pia, alidai hakuna ushahidi wa malalamiko unaomuunganisha mrufani na pikipiki iliyoibwa kwasababu upande wa Jamhuri umeshindwa kumuita Ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuthibitisha umiliki wake.
Wakizichambua hoja hizo, Majaji walisema Jaji wa Mahakama Kuu alikuwa sahihi kusema mrufani ndiye aliyemuua Msimbe. Aidha, walisema ushahidi unaonyesha mrufani alikamatwa na polisi akiwa anamiliki pikipiki hiyo ilithibitishwa na mmiliki wake halali ambaye alimkabidhi Msimbe kufanya biashara ya kubeba abiria Januari 6, mwaka 2017.

Ilielezwa Januari 9, mwaka 2017, Msimbe aliuawa na siku iliyofuata saa 7:30 mchana askari walimkamata mrufani akiwa anaendesha pikipiki hiyo, ndipo walipomfungulia shtaka la mauaji kwasababu alikutwa na pikipiki iliyokuwa inaendeshwa na Msimbe.​

Majaji hao walisema kwa ushahidi huo, hawaoni hitimisho lingine isipokuwa kama Jaji wa mahakama ya chini alivyoeleza kwamba mrufani alihusika na mauaji ya Msimbe na kuiba pikipiki.

Majaji hao walisema kutokana na hali hiyo wameona hoja za mrufani hazina mashiko, hivyo wanaitupa rufani kama ilivyokatwa. Chamashine alitenda kosa hilo, Januari 9, mwaka 2017, eneo la Kikwaraza, Kata ya Mikumi, Wilaya ya Kilosa, Morogoro.
Hii ni hukumu mbovu; ultimate penalty ya kifo inatakiwa itolewe kwa ushahidi solid ukiambatana na silaha iliyotumika kufanya mauaji, sio huu wa kukutwa na pikipiki ya marehemu. Inawezakana aliiba kwa mtu mwingine bila kujua kuwa ilikuwa pia imeibiwa kwingineko.

Halafu Mzuzuri Ukiwaona ditopile alipoua dereva wa daladala hivyo kwa kumpiga risasi ya papo kwa papo kukiwa na ushahidi lukuki, eti kesi yake ilibadilika na kuwa ya kuuwa bila kukusudia; ndipo uijue jinsi haki inavyotolewa na mahakama zetu.
 
Mimi sio mtaalamu sana wa mambo ya sheria lakini Katika shauri hilo kuna kesi mbili, ya kwanza ni mauaji ambayo ni kubwa na ya pili ni uporaji, kesi kubwa huwa inameza kesi ndogo.

Kesi ya huyo mhusika ilikuwa ni kesi ya mauaji, hivyo ninachokiona mimi ni kwamba alishindwa kujitetea jinsi alivyopata hiyo pikipiki ndio maana katiwa hatiani hata kama hakuhusika na hayo mauaji.
Na jamaa alitaka kuchomoka kwa kutaka izibitishwe je hyo pikipiki ndio aliyokua nayo marehemu kupitia TRA...

Sasa TRA hawajatokea hapo ushahd unaacha shaka
 
Unapozungumzia matumizi ni lazima ufafanue ni matumizi gani!!?, labda alikuwa anaitorosha kwa kuiendesha au alikuwa anaitafutia soko huku akiiendesha nk, juu ya yote kama hakuhusika na tukio la kupora na kuua angeeleza0 kaipaje hiyo pikipiki, just simple case.
Piki piki ya kuibiwa tena kwa kuuwawa mtu haiwezi kutoroshwa kwa njia rahisi kama hiyo.
Huyo ni mnunuzi wa vitu vya deal na alikuwa hajui the extent kwamba kuna siku atanunua vitu vya tukio la mauaji ,ndo yamemkuta .
Kwahiyo aliuziwa bila ushahidi wa watu wala wa kimaandishi ?

Aliyemwuzia si angejulikana ?
Pikipiki ya wizi kuna vibali flani inakosa na inajulikana ni ya wizi.

Mwenye pikipiki alitoa ushahidi wa vibali na wa maneno kuwa Marehemu alikuwa anatumia pikipiki kwa ruhusa yake ya kutafuta pesa. Na baadhi ya vibali alikuwa navyo.

Sasa Mjomba unanunua pikipiki kama unavyonunua Embe unategemea nini ?

Ndio maana kesi imedumu muda mrefu ni kwamba Mahakama ilitaka kujiridhisha.

Na mara zote kesi ya Mauaji mtuhumiwa anapewa Wakili wa Serikali bure ili kumsaidia kuepusha kumwadhibu mtu kwa kubahatisha.
Hayoo yoote uliyoesema hakuna mahala umeonyesha kuwa mtuhumiwa ndiye muuwaji, ana kesi kadhaa za kujibu ikiwepo kununua au kukutwa na mali ya wizi , ,
 
Tuanzie hapa.
Mtuhumiwa ndio mwenye pikipiki.
Tunaomba lisiti za Ununuzi wake.

Kama huna tunamwomba mmiliki halali wa hiyo pikipiki uliyokutwa nayo
 
Ni hivi; Mtu aliyeuawa (kama inavyoelezwa) aliuawa na kuporwa pikipiki, yaani sababu ya kuuawa kwake ni ili aporwe pikipiki au aliuawa katika mazingira ya kupambana ili asiporwe pikipiki, kesi hapo inakuwa ni ya Mauaji na hiyo ya uporaji inakufa kifo cha mende, Uchunguzi lazima uwe na mwanzo na mwanzo wake ndio hapo kwamba; siku ya pili TU baada ya tukio ndipo mtu kakutwa/kakamatwa na pikipiki ile ile aliyokuwanayo mtu (bodaboda) aliyeuawa, sasa ilikuwa ni jambo rahisi tu kwa huyo mtu kujibu hili swali; Pikipiki hii umeipataje?? --- bila shaka ni majibu ya swali hili ndiyo yamemtia hatiani kwenye mauaji ya dereva wa boda boda.
Suala la kuthibitisha kosa si la mtuhumiwa, ni mwendesha mashtaka au mahakama kuthibitisha kuwa mtuhumiwa ana kosa.

Ni sawa nipelekwe mahakamani kwa kosa la wizi halafu mahakama iniambie nithibitishe kama mimi siyo mwizi!
 
Ni hivi; Mtu aliyeuawa (kama inavyoelezwa) aliuawa na kuporwa pikipiki, yaani sababu ya kuuawa kwake ni ili aporwe pikipiki au aliuawa katika mazingira ya kupambana ili asiporwe pikipiki, kesi hapo inakuwa ni ya Mauaji na hiyo ya uporaji inakufa kifo cha mende, Uchunguzi lazima uwe na mwanzo na mwanzo wake ndio hapo kwamba; siku ya pili TU baada ya tukio ndipo mtu kakutwa/kakamatwa na pikipiki ile ile aliyokuwanayo mtu (bodaboda) aliyeuawa, sasa ilikuwa ni jambo rahisi tu kwa huyo mtu kujibu hili swali; Pikipiki hii umeipataje?? --- bila shaka ni majibu ya swali hili ndiyo yamemtia hatiani kwenye mauaji ya dereva wa boda boda.
Umiliki wa pikipiki ulithibitishwa mahakamani?
Kama nilivyosema, labda taarifa kuhusu kesi hii iliyoletwa hapa haijakamilika.
Kulikuwa na shida gani kupata uthibitisho kutoka TRA kuhusu umuliki wa pikipiki ili ijulikane kwamba ndiyo aliyokuwa akiiendesha marehemu?
Ndiyo maana nasema labda walichukuwa ushahidi mwingine zaidi ya hiyo pikipiki na ndiyo wakautumia kutoa hiyo hukumu.
 
Na jamaa alitaka kuchomoka kwa kutaka izibitishwe je hyo pikipiki ndio aliyokua nayo marehemu kupitia TRA...

Sasa TRA hawajatokea hapo ushahd unaacha shaka


TRA wanachoweza kuthibitisha ni umiliki wa pikipiki na sio nani alikuwa anaendesha pikipiki na wakati gani.
 
Piki piki ya kuibiwa tena kwa kuuwawa mtu haiwezi kutoroshwa kwa njia rahisi kama hiyo.
Huyo ni mnunuzi wa vitu vya deal na alikuwa hajui the extent kwamba kuna siku atanunua vitu vya tukio la mauaji ,ndo yamemkuta .


Sasa ndio angesema kwamba hiyo pikipiki kanunua kutoka kwa watu au mtu fulani ili asalamike na mauaji, mbona ni jambo rahisi sana. Kinachoonekana naye alihusika moja kwa moja katika hilo tukio.
 
Kuna series of misfortunes zikikuandama unaweza jikuta umeingia kwenye matatizo makubwa kwa bahati mbaya , kuna uwezekano kuwa jamaa ni mnunuzi maarufu wa vitu vya mazabe, akaletewa pikipiki hiyo akanunua kwa bei chee bila kujua msala wake.
Piki piki mbali sana , simu ya kununua mitaani tu inaweza kukuletea msala kama huo na kwa mahakama zetu zinavyofanya kazi unaweza kunyongwa kweli
Kule Kenya kuna Dogo ni m anafunzi wa Chuo kikuu alikutwa na simy kumbe simu ilikuwa ya raia mmoja wa Uganda alie uwawa na kuporwa vitu, sasa dogo kanunua simu, hadi sasa yuko ndani
 
Back
Top Bottom