BodGanleonid
JF-Expert Member
- Nov 14, 2022
- 3,021
- 4,330
Unamhukumu vipi mtu kufa kwa ushahidi wa kimazingira tu?
Nashauri akaombe Review ya Court of Appeal, anaweza akashinda
Tumia akili hakuna muuaji aue kisha abaki na ushahidi, ataua ataiba na kwenda kuiuza pikipiki. Kwa nchi zilizoendelea kwa ushahidi huo tu, huyo jamaa angekutwa na hatia tofauti, sio ya mauwaji.
Acheni unaa...Muuaji hawezi UA, akachukua pikipiki afu kesho aiendeshe maeneo hayo hayo
Sana.Kuna kitu cha kujifunza hapa.
Labda tusaidie wewe bushlawyer amekutwa na pikipiki ya wizi ameulizwa ameipataje akasema ni yake hana viambata vyovyote hukumu ungetoajeNdo maana twasema kuna kitu hakiko sawa.
Mtu hawezi UA afu siku ifuatayo akaitumia hiyo pikipiki
Ukakasi, huyu angeshtakiwa kwa kukutwa na pikipiki ya marehemu tu muuwaji waendelee kumtafuta pengine hata kumtumia huyu kusaidia polisiKwahiyo Jamaa amehukumiwa kifo kwa sababu tu alikamwatwa na Pikipiki aliyokuwa anaendesha Marehemu?
Kwamba ameua wamethibitishaje sasa?
Tuseme kakutwa na boxer nyekundu ambayo ndio rangi ya piki piki aliyokua nayo marehemu, je boxer nyekundu ipo moja tu Tanzania so lazma ithibitishwe kuwa ndio hyo kwa marakatasi hyo ndio sheria ndio mana kuna mawakili....Kama marehemu hakuwa mmiliki halali, haki iende kwa muuaji?
Kuna kitu hakiko sawa mahaliHapa ndipo intelligence inatakiwa kuzingatia. Mtu aibe mali ya wizi tena m'miliki wake ameuwawa halafu atembee nayo mchana kweupe.
Inapotea vizuri tu, we jichanganye ndo utajua hujuiKwa nini hawezi? Wapo watu wenye uthubutu huo- mfano ndo huyo njemba.
Halafu kumbuka damu ya mtu haipotei kihivi-hivi. Mbona hasemi bayana aliipata-pataje hiyo pikipiki??. Wahenga walisema "anayekutwa na ngozi ndiye mwizi"
Mkuu, sisi humu Jf tumepata digested story tu na si mchakato mzima wa kesi ulivyokwenda.Hakuna mtu anaeua afu kesho akaendelea kua hapo hapo, wengi hukimbia mazingira huyu kesi sio yake kilichomponza ni bodaboda aelezee alipoitoa kinachombana kuonekana yeye ndio mhusika ni hio bodaboda, angeeleza vizuri bodaboda imekuaje akawa nayo yeye na sio yake
Kuna wakati kesi inakuwa kubwa hadi watuhumiwa wanafeli utetezi ulio wa wazi kabisa, huyu jmaa keshakaa rumande muda mrefu , rumande kuna wanasheria bubu wanaweza kumis lead mtu akaogopa kusema ukweli . Akodhani atasalimikaSasa ndio angesema kwamba hiyo pikipiki kanunua kutoka kwa watu au mtu fulani ili asalamike na mauaji, mbona ni jambo rahisi sana. Kinachoonekana naye alihusika moja kwa moja katika hilo tukio.
Hapo Kuna shida kubwa Sana.Yeye aliomba TRA waje thibitisha umiliki wa pikipiki, TRA hawajatokea
Muuaji hawezi tumia chombo cha moto cha Marehemu.Hapo Kuna shida kubwa Sana.
Nadhani hiyo ni assumption, Cha msingi alikamatwa na hiyo pikipiki. Inawezekan Kuna mtu alimchoma au walimshuku kuwa ndio muuaji.Ndo maana twasema kuna kitu hakiko sawa.
Mtu hawezi UA afu siku ifuatayo akaitumia hiyo pikipiki
Basi yaonesha kashindwa jitetea au akilini ni MjingaNadhani hiyo ni assumption, Cha msingi alikamatwa na hiyo pikipiki. Inawezekan Kuna mtu alimchoma au walimshuku kuwa ndio muuaji.
Kazi ya mtuhumiwa ni kudis approve allegations. Sasa inaonekana imemshindwa.Sio kazi ya mtuhumiwa kusaidia upande wa mashtaka kuprove kesi yao
Kuaangalia umiliki siyo lazima sana hadi uwende tra,hata kwenye simu tu unaweza angalia!!Hapo Kuna shida kubwa Sana.
Kaiba pikipiki halafu aliyeibiwa kauawa kwenye tukio, aliyeiba ndio muuaji mwenyewe.Kesi ya mauwaji haijathibitishwa.
Wangethibitisha ya wizi, (kwamba mshitakiwa/mrufani ndiye aliye iba pikipiki), basi wangeweza kuthibitisha ya mauwaji.
Kesi yake hapo ni kupatilkana na mali ya wizi.
Naona mahakama imetumia tu “short cut”
There is no “guilty beyond a reasonable doubt” sentencing here.
Kumuhukumu mtu adhabu ya kifo kwa kukutwa na mali ya wizi ni uvivu wao mahakama, waendesha mashtaka pamoja na wapelelezi wa kesi ya wizi na mauwaji.
Usiseme hivyo kwa kua hayajakukuta, watu wanaua na wanakwenda Bank wanachukua Mali za Marehemu bila hata ya uwoga na kujimilikisha!!Ndo maana twasema kuna kitu hakiko sawa.
Mtu hawezi UA afu siku ifuatayo akaitumia hiyo pikipiki
Mahakama ya Rufani Morogoro, imetupilia mbali rufani ya Justine Chamashine aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kosa la kumuua dereva wa bodaboda, Joseph Frorence 'Msimbe'.
Uamuzi huo ulitolewa wiki iliyopita na Jopo la Majaji watatu likiongozwa na Jaji Mkuu Profesa Ibrahimu Juma. Majaji wengine ni Augustine Mwarija na Othman Makungu.
Chamashine alikata rufani kupinga hatia na adhabu aliyopewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam. Majaji hao walisema baada ya kupitia hoja za pande zote mbili wamebaini hoja za rufani hazina mashiko na Mahakama Kuu ilimhukumu mrufani kwa usahihi. Walibainisha miongoni mwa hoja za mrufani kupinga adhabu hiyo ilikuwa ni kwamba Mahakama Kuu ilikosea kumhukumu kwa kutumia ushahidi wa kukutwa na vitu vya marehemu huku kukiwa hakuna ushahidi iwapo wakati Msimbe anauawa alikuwa akitumia pikipiki aliyokutwa nayo yeye.
Pia, alidai hakuna ushahidi wa malalamiko unaomuunganisha mrufani na pikipiki iliyoibwa kwasababu upande wa Jamhuri umeshindwa kumuita Ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuthibitisha umiliki wake.
Wakizichambua hoja hizo, Majaji walisema Jaji wa Mahakama Kuu alikuwa sahihi kusema mrufani ndiye aliyemuua Msimbe. Aidha, walisema ushahidi unaonyesha mrufani alikamatwa na polisi akiwa anamiliki pikipiki hiyo ilithibitishwa na mmiliki wake halali ambaye alimkabidhi Msimbe kufanya biashara ya kubeba abiria Januari 6, mwaka 2017.
Ilielezwa Januari 9, mwaka 2017, Msimbe aliuawa na siku iliyofuata saa 7:30 mchana askari walimkamata mrufani akiwa anaendesha pikipiki hiyo, ndipo walipomfungulia shtaka la mauaji kwasababu alikutwa na pikipiki iliyokuwa inaendeshwa na Msimbe.
Majaji hao walisema kwa ushahidi huo, hawaoni hitimisho lingine isipokuwa kama Jaji wa mahakama ya chini alivyoeleza kwamba mrufani alihusika na mauaji ya Msimbe na kuiba pikipiki.
Majaji hao walisema kutokana na hali hiyo wameona hoja za mrufani hazina mashiko, hivyo wanaitupa rufani kama ilivyokatwa. Chamashine alitenda kosa hilo, Januari 9, mwaka 2017, eneo la Kikwaraza, Kata ya Mikumi, Wilaya ya Kilosa, Morogoro.
Hata Mimi naona kashindwa kujitetea.Basi yaonesha kashindwa jitetea au akilini ni Mjinga