Mahakama yatoa amri Paul Makonda atangazwe gazetini na Kolomije kupata taarifa za kesi
Nakuelewa maana maovu waloyofanya wakubwa wote kama hawakuhusika angalau walijua.

Kumkamata na kumfunga Bashite nchi itaanguka.
Wamemficha atapotea kama balali Ili kuficha maovu ya wakubwa wakiruhusu akamatwe atamwaga mboga yote.
 
Ha ha ha ha .maigizo haya,yaani mahakama imeshindwa kumpata ,Hadi waombe gazeti liwatafutie makonda.maigizo haya,ukiona hivyo hapo hakuna kesi ni Kiki tu!!
Jipe moyo!! toka lini mahakama ndio inayomtafuta mtuhumiwa, utaratibu wa kisheria uko wazi pale mtuhumiwa anaposhindwa kuonekana mahakamani, hizo ndizo taratibu zilizopo!!kweli maisha haya yaani makonda ndani ya mwaka mmoja tu ni wakuishi kama digidigi, leee fieldmarshal!!
 
Ukitaka kujua kwa nini magufulists hawampendi samia ni kwa mambo kama haya. Wapwani ndio wafanyaji wakubwa wa madawa ya kulevya.
Mama anaacha aliyekua mtumishi mwakilishi wa rais mkoa wa dar kunyanyasika na kubakia katika hali ya mashaka kwa kazi aliyofanya kupambana na dawa za kulevya. Ni kisasi tu wala sio lingine.
Mama mwenyewe ni walewale,huoni anavyoufumbia macho upigaji wa kina Makamba.
 
Wamemficha atapotea kama balali Ili kuficha maovu ya wakubwa wakiruhusu akamatwe atamwaga mboga yote.
Hakuna mtu anayemficha Makonda, kwa kuwa aliyekuwa anamtuma kufanya uovu ni Mwendazake ambaye ametangulia Jehanam.

Makonda atakuwa kisha kimbia Nchi au kama yupo ata commit suicide tu, hamna namna atakubali kushtakiwa kama Ole Sabaya
 
Mahakama ya Kinondoni leo Jumanne imetoa amri ya kutangazwa gazetini, nyumba aliyoishi Masaki na au kijijini kwao Kolomije kwa aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ili apate taarifa za kesi iliyofunguliwa dhidi yake na Mwandishi wa Habari, Saed Kubenea. Kesi itatajwa 2 Machi 2022.

Pia soma > Paul Makonda ashindwa kufika Mahakamani katika kesi inayomkabili. Kesi yaahirishwa hadi 08 Feb 2022

Shauri hilo limetajwa kufuatia Mahakama hiyo kushindwa kusikiliza hapo awali baada ya shughuli kuingiliana.

----

Akizungumza mahakamani hapo Leo Wakili wa upande wa waleta maombi Nyaronyo Kicheere, ameeleza kwamba wameshindwa kumpata mjibu maombi namba 3 ambaye ni Paul Christian Makonda kwa kuwa Masaki alikokuwa anakaa amekwishahama na namba yake ya simu haipatikani na hivyo kuiomba Mahakama hiyo iwapatie hati ya kumsaka maeneo mbalimbali.

Aidha wameomba kupewa hati za wito ambazo zitapelekwa alipokuwa akifanyia kazi kwa mara ya mwisho, kwenye nyumba aliyokuwa anaishi kwa mara ya mwisho, maeneo anayotembelea mara kwa mara na nyingine iwekwe katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, nyingine ipelekwe bandarini, Kolomije, Misungwi mkoani Mwanza na ya mwisho ipelekwe kwenye gazeti la Kiswahili na la kingereza.

Wakili ameongeza kuwa lengo la kufanya hivyo ni kutaka mjibu maombi hayo ambaye ni Paul Makonda apate taarifa juu ya uwepo wa kesi hiyo mahakamani.

Kwa upande wake Hakimu wa mahakama hiyo Aron Ryamuya, ameeleza kuwa hoja ya kwenda kubandika hati hizo katika viwanja vya ndege na bandarini ni kinyume cha sheria na ni uchafuzi wa mazingira na badala yake akakubali matangazo hayo yapelekwe kwenye nyumba yake ya Masaki aliyokuwa akiishi, kwenye gazeti na kijijini kwao Koromije pekee.

Kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2022, imeahirishwa hadi Jumatatu ya Machi 2, 2022.

Chanzo: EATV
Na hapa huu ni mtego mkubwa sana Kwa Mahakama.Anachotaka kuonyesha hapa ni kwamba yeye haguswi na Wala hakuna Cha kumfanya.Mimi siamini hata kidogo kwamba yeye hajui kama anatafutwa na Mahakama.Ni jeuri hiyo hiyo ndiyo aliitumia kufanya Yale aliyoyafanya mpka Leo anatafutwa na Mahakama.
Sasa kwakweli Kwa maoni yangu Mahakama ifanye Kila liwezekanalo huyu jamaa akipatikane.
Kama kaenda nje ya nchi taarifa za uhamiaji sizingepatikana?
Huyu asiitanie Mahakama kabisa
 
Yule bwana angefufuka leo, angekufa tena maana mambo yanaenda kasi mno, Wafuasi wake wametawanywa kwa njia saba

JPM kawazidi sana. Kafa Lakini mnateseka sana kama ma x. JPM alikuwa Rais sio mchungaji au yesu au mtume. Kama kumbukumbu yangu iko Sawa. Makonda aliibuliwa bunge la Katiba. ( Sijui JPM alihusika) Then Kikwete akamteua kuwa mkuu wa Wilaya. Watu walimsifia kama mkuu wa Wilaya kijana na mchapa kazi. Alikutana na makundi ya watu nk. JPM aliwateua wakuu wa Wilaya Vijana sio kwa kuwajua personally bali kwa channel za utendaji nk. Iwe kwa kupenyezewa au Basi kuwa kwenye mzunguko. Katika kugombea Urais alimteua Pia mama yetu mgombea mwenza. Sasa Rais wetu. Tabia ya mtu Ni Kama ngozi tu. Wewe hatukujui ndo mana una uwezo wa kutangaza ya wengine. Katika miaka 5 na miezi yake ya JPM Kuna watu wema wengi na wazalendo aliowateua kupitia machinery zake. Wema na uzalendo wao hauwezi kutoka kwa JPM. Ni maisha na malezi yao.

Tatizo kubwa la watu kama wewe Ni ugonjwa. Ukiona mtu ambaye hata humjui. Hujui Undani Wake na tena Sasa Ni marehemu anakusumbua akili na moyoni ujue unapaswa kuwahi kulazwa haraka. Wanaojinyonga wanaanza kama wewe. As kwa makonda kama binadamu Ana yake Wacha mahakama itaamua.

Katibiwe mkuu.
 
Back
Top Bottom