Maharage wa TANESCO atimuliwa kwenye kikao cha Waziri Mkuu Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu Biteko. Apewa siku tatu

Yeye ndie MD - hawezi kukimbia matatizo ya TANESCO. Ameweza kuirekebisha Customer care - iko vizuri. Sasa aangalie kuhusu upatikanaji wa huo umeme. Maana hai-make sense kuunganisha wateja wengi ambao hawapati umeme.
Nimekuuliza Maharage ndio ameleta ukame?

Maharage ndio mtoa pesa za kujenga miradi Nje ya vyanzo vya maji huko Tanesco?

Alishaleta Serikalini kinachotakiwa ni swala la kina Biteko na wenzie kuleta pesa Tanesco sio kukikosha Kwa maigizo ya kijinga.

Mwisho Biteko akiwa MD wa Tanesco anaweza leta Umeme?
 
TANESCO inaendeshwa kisiasa.

Watanzania hawalipii gharama halisi za umeme, wanalipa gharama ndogo sana, halafu, wakati kawaida ni watumiaji wakubwa wa viwandani kufidia tofauti, uchumi hauna watumiaji wakubwa wa kutosha wa kulipia the difference.

Matokeo yake, it's a vicious circle of poverty.

Umeme kukosekana inadumaza uchumi, na uchumi kudumaa kunafanya watumiaji wakubwa washindwe ku support matumizi ya umeme ya general population na umeme ukosekane.

Kwa msingi huo, hawa kina Maharage, they are set to fail.

Kitu cha kwanza kinachotakiwa ni kuondoa ukiritimba wa TANESCO kuwa na monopoly kwenye umeme.

Unategemea vipi ufanisi kwenye biashara ya monopoly?

Achia kuwe na makampuni matano ya umeme yanagombea wateja, halafu angalia competition ya kibiashara unavyomaliza matatizo.

Unategemea vipi efficiency kwenye monopoly?
 
Wamechelewa sana ku engage private sector kwenye kuzalisha na kusambaza umeme, hiki chanzo cha maji tayari kimeonyesha kuathirika na mabadiliko ya tabia nchi na hivyo serikali kupitia monopoly ya Tanesco haitaweza tena kuzalisha na kusambaza umeme effectively in a long run.
 
Na bado wamekomaa nacho..kaazi kweli kweli.
 
Acha ashughulikiwe ili apate akili
 
Kwamba kinachotakiwa ni serikali kupeleka pesa, ili zikafanye nini sasa hapo TANESCO kama kiongozi aliyepo hapo juu ni boya asiyekuwa na maono yoyote ya kuliongoza hilo shirika..?

Shida ya hii nchi sio kupeleka pesa kwenye maeneo fulani, shida ni wakina nani walioko huko zinakopelekwa? Wengi walioko kwenye mashirika na wazira mbalimbali ni wehu, wezi mabogus, wasiojua lolote. Kupeleka hela kwa aina hiyo ya watu ni UPUMBAVU usioweza kusaidia chochote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…