Maharage wa TANESCO atimuliwa kwenye kikao cha Waziri Mkuu Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu Biteko. Apewa siku tatu

Maharage wa TANESCO atimuliwa kwenye kikao cha Waziri Mkuu Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu Biteko. Apewa siku tatu

Boss wa TANESCO atimuliwa kikaoni. Sioni nyota njema kwake. Siku tatu zinamtosha kweli au ndo wanamkomoa baba wa watu?
View attachment 2756107
Na Biteko akija kujua dili za Luku atamla kichwa mazima.

Kaambiwa nenda kashughulikie Umeme. Alikuwa high Table ametabasamu na furaha zote amekaa kwenye Maonesho yanayoendelea ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam

Tarehe 25 Septemba 2021, Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Maharage Chande kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO akichukua nafasi ya Dkt. Tito Mwinuka

Kutokana na Mgao Mkubwa wa Umeme unaoendelea Nchini, Maharage anadai hakuna Mgao bali ni Upungufu wa umeme.

Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Maharage Chande aliwaomba Wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho kuna Upungufu wa Umeme unaosababisha baadhi ya Maeneo kuwa na Umeme na mengine kukosa Huduma hiyo

Maharage alisema "Katika Mtandao wa Umeme hitilafu huwa zinatokea mara kwa mara na pale zinapotokea Wateja wetu huwa tunawataarifu. Tunapopata upungufu sio Nchi nzima inakuwa haina Umeme ila ni kwa baadhi ya maeneo na huwa tunatoa taarifa"

Sasa baada ya kwambiwa aende kushughulikia umeme, nilijua ataenda site. Cha ajabu yupo Ofisini kwake Ubungo kakaa huku tai ameilegeza, inaonekana ana mawazo sana.

Tumuombee presha yake isipande.

Baadhi ya Watanzania wamesema mgao wa umeme umekuwa ukisababisha hasara katika biashara zao mara kwa mara. Na wamelitaka shirika la umeme (TANESCO), kutoa taarifa rasmi ya jinsi mgao huo unavyoendeshwa. Je, kwa sasa Tanesco inazalisha kiwango gani cha umeme? Ni upungufu wa aslimia ngapi?
Na afe
 
Huyo Maharage anaonewa bure tu, kuongoza taasisi za ki Africa ni kazi sana. Unafikiri angewagomea huyo aliyem suggest na yule aliyemtoa DSTV na kum appoint pale Tanesco.
We ndo tahira kuliko huyo makande... anaonewa nn wakati anasababishia taifa hasara
 
Watu wengi wanafikiri umeme unatosha nchi hii...
Umeme hautoshi na kwa kipindi kirefu hakukuwa na chanzo kipya cha umeme..

Tunasubiri Julius Nyerere Dam ikamilike..
Naona ile connection ya line kutoka Arusha kwenda Namanga inakaribia kuisha... Wanunue hata megawatts 400 kutoka Ethiopia unaopitia Kenya pengine unafuu utapatikana
Ulioluepo Awamu ya magufuli ulkua unatoka wapi?
 
Unaangalia tatizo hili kutoka upande mbaya.

Monopoly ndiyo tatizo.

Ukiwa na makampuni mengi ya umeme, kampuni moja likiwa na tatizo, kampuni lingine likatatua hilo tatizo, wateja wataamua kuondoka kwenye kampuni lenye tatizo na kuhamia kampuni lenye ufanisi.

Sasa hivi, TANESCO inafanya itakavyo, kwa sababu haina competition.
Bwana Yesu afiwe Mr Kiranga!! Kwa haya maelezo yako labda kwa nguvu za roho mtakatifu ndo nitakuelewa!!
Hoja yangu ni hii,, tutawezaje kuhimili miundo mbinu (nyaya, nguzo, meter nk) za kampuni za umeme wakati hizi za TANESCO zinatukera??
Tumsifu
Yesu Kristo
 
Bwana Yesu afiwe Mr Kiranga!! Kwa haya maelezo yako labda kwa nguvu za roho mtakatifu ndo nitakuelewa!!
Hoja yangu ni hii,, tutawezaje kuhimili miundo mbinu (nyaya, nguzo, meter nk) za kampuni za umeme wakati hizi za TANESCO zinatukera??
Tumsifu
Yesu Kristo
Haya. Nenda kwa huyo Roho Mtakatifu wako akueleweshe.

Maana naona umeamua kutoelewa.
 
Umeme hamna ila watu wanakaa bungeni kupitisha bajeti eti wananchi wapelekewe umeme wa REA, hiki ni kituko cha karne. Na ndo maana hadi leo watu wamekaa hawaelewi hiyo REA itawafikia karne gani yaani nchi inaendeahwa kama nyumbani kwa mganga wa kienyeji kila kitu ni kwa ramli tu
 
Maharage Chande na hata katibu mkuu wizara ya nishati hawastahili kuwa kwenye hizo nafasi zao. Wameprove failure kwenye kila eneo. Hasa huyo katibu mkuu somebody Mramba. Yaani haya majamaa hayajui connection iliyopo kati ya umeme na uchumi wa nchi? Unakata umeme tangu asubuhi ya saa 1 unarudisha saa 1 au 2 usiku. Alafu unavaa suti na tai kwa achievement gani uliyoipata?. Yule aliyekuwa waziri wa hii wizara ( january makamba) ndo ametuletea huu ujinga wote. Sehemu zote kafeli sio umeme sio mafuta. Alafu bado kapewa wizara nyingine, nako aende kuharibu pia. Mama Samia ebu ongeza ukali kidogo mama yetu. Mtaani mambo sio mambo. , Kukosekana kwa umeme wa uhakika kuna watu watafunga biashara zao.
 
Umeme wenyewe unategemea kudra za Mwenyezi Mungu kuleta mvua.Sasa hapo utamlaumu mtu vipi?Huyu Dotto ana roho mbaya kama mpwa wake Jiwe 🤔
 
Boss wa TANESCO atimuliwa kikaoni. Sioni nyota njema kwake. Siku tatu zinamtosha kweli au ndo wanamkomoa baba wa watu?
View attachment 2756107
Na Biteko akija kujua dili za Luku atamla kichwa mazima.

Kaambiwa nenda kashughulikie Umeme. Alikuwa high Table ametabasamu na furaha zote amekaa kwenye Maonesho yanayoendelea ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam

Tarehe 25 Septemba 2021, Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Maharage Chande kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO akichukua nafasi ya Dkt. Tito Mwinuka

Kutokana na Mgao Mkubwa wa Umeme unaoendelea Nchini, Maharage anadai hakuna Mgao bali ni Upungufu wa umeme.

Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Maharage Chande aliwaomba Wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho kuna Upungufu wa Umeme unaosababisha baadhi ya Maeneo kuwa na Umeme na mengine kukosa Huduma hiyo

Maharage alisema "Katika Mtandao wa Umeme hitilafu huwa zinatokea mara kwa mara na pale zinapotokea Wateja wetu huwa tunawataarifu. Tunapopata upungufu sio Nchi nzima inakuwa haina Umeme ila ni kwa baadhi ya maeneo na huwa tunatoa taarifa"

Sasa baada ya kwambiwa aende kushughulikia umeme, nilijua ataenda site. Cha ajabu yupo Ofisini kwake Ubungo kakaa huku tai ameilegeza, inaonekana ana mawazo sana.

Tumuombee presha yake isipande.

Baadhi ya Watanzania wamesema mgao wa umeme umekuwa ukisababisha hasara katika biashara zao mara kwa mara. Na wamelitaka shirika la umeme (TANESCO), kutoa taarifa rasmi ya jinsi mgao huo unavyoendeshwa. Je, kwa sasa Tanesco inazalisha kiwango gani cha umeme? Ni upungufu wa aslimia ngapi?
Maharage kaangushiwa jumba bovu
 
Maharage Chande na hata katibu mkuu wizara ya nishati hawastahili kuwa kwenye hizo nafasi zao. Wameprove failure kwenye kila eneo. Hasa huyo katibu mkuu somebody Mramba. Yaani haya majamaa hayajui connection iliyopo kati ya umeme na uchumi wa nchi? Unakata umeme tangu asubuhi ya saa 1 unarudisha saa 1 au 2 usiku. Alafu unavaa suti na tai kwa achievement gani uliyoipata?. Yule aliyekuwa waziri wa hii wizara ( january makamba) ndo ametuletea huu ujinga wote. Sehemu zote kafeli sio umeme sio mafuta. Alafu bado kapewa wizara nyingine, nako aende kuharibu pia. Mama Samia ebu ongeza ukali kidogo mama yetu. Mtaani mambo sio mambo. , Kukosekana kwa umeme wa uhakika kuna watu watafunga biashara zao.
Makamba anatembelea jina la baba yake,hana maajabu yeyote
 
Kwa nionavyo mimi. Tanesco iendelee kujenga miundo mbinu ya kusambaza umeme lakini isitishe zoezi la kuwaunganisha wateja wapya hadi pale vyanzo vipya vya uzalishaji umeme vitakapoanza kufanya kazi.
 
Unaangalia tatizo hili kutoka upande mbaya.

Monopoly ndiyo tatizo.

Ukiwa na makampuni mengi ya umeme, kampuni moja likiwa na tatizo, kampuni lingine likatatua hilo tatizo, wateja wataamua kuondoka kwenye kampuni lenye tatizo na kuhamia kampuni lenye ufanisi.

Sasa hivi, TANESCO inafanya itakavyo, kwa sababu haina competition.

Nakubaliana na wewe, ingeruhusiwa hata watu kuwekeza kwenye min grids kwa level hata ya mkoa au wilaya.

Umeme ni bidhaa waruhusu soko huria kama telecoms industry maana washashindwa kuleta umeme wa uhakika miaka 60 toka uhuru
 
Maharage anapwaya...

Na huyo jamaa anaendeleza Siasa; Si angemwambia kabla ya Kikao na kuokoa hizo dakika kadhaa alizotumia kwenye kikao; Au ni mwendo wa kuonyesha wanafanya kazi wakati wote wanapwaya...; Unamwambia aliyekuwepo wakati wa tatizo atatue tatizo kwa njia zipi ?
 
Nakubaliana na wewe, ingeruhusiwa hata watu kuwekeza kwenye min grids kwa level hata ya mkoa au wilaya.

Umeme ni bidhaa waruhusu soko huria kama telecoms industry maana washashindwa kuleta umeme wa uhakika miaka 60 toka uhuru
Hivi watu wamekatazwa kuwekeza kwenye Solar n.k., Wale Dowans na Symbion walikuwa sio wawekezaji ? Au unataka wafanye transmission ? Na wakifanya transmission unadhani watakwenda kule ambapo ni pagumu na hakuna faida ?

Issue kubwa sio Competition; Competition kwenye kitu kama umeme ni ngumu kutokea matokeo yake ukifanya hivyo watu wata-create opportunities za kupiga na kupanga bei (hili linaendelea huko Europe)

Kwa wingi wa vyanzo hakuna sababu ya Tanesco ku-fail; Iendelee kuwa state owned na watu kupewa targets wakishindwa mbona sheria zipo na wengine wa kujaliza nafasi wapo ?

 
Back
Top Bottom