Tetesi: Majadiliano ya Makinikia: Tanzania inapumulia mashine

Tetesi: Majadiliano ya Makinikia: Tanzania inapumulia mashine

tutapata majibu baada ya majadiliano. kuja kwao ACACIA kwenye meza ya mduara ni hesha kubwa kwetu kama taifa. na kuwa sisi siyo wa mchezomchezo kwenye Tanzania ya JPM

haya ndio mawazo ya kijinga ya waafrika. hujui hata wakoloni walipotaka kututawala walitufuata hukuhuku? hujui kama Mali zetu walizifuata hukuhuku? acha kujisifia eti wamekufuata. cha kujisifia ni jinsi gani utafaidikia na ujio wao. je matarajio yetu yatatimia
 
Mkuu..unapozungumzia "noah"...be specific..ni noah kibasi?au mnyama pendwa?...kama ni mnyama pendwa nadhan kwa idadi yetu ya watz mil..54 tunaweza pewa kila mtu..sio gari!

Sent using Jamii Forums mobile app

trilioni 400s siyo hela kidogo. zinatosha kununua Noah ya gari kqa kila mtz
 
Acha tupumulie mashine maana ndo furaha yako, hata tukiwa `win' wewe hutafaidika lolote.
 
Mawakala wa mafisadi wanatapa tapa tu.
Hakitoki kitu mpaka siku ya mwisho
 
Mtu asiposifu na kushangilia ni wakala wa fisadi tayari?
Subirini watu wajadiliane mtafanya assessments zenu baada ya matokeo,kupiga piga kelele kwa sasa mnajionesha jinsi gani mlikua mnataka kututoa kwenye reli ili tufeli mapema mtubeze
 
Haswa hiki ndio cha mhimuuuuu!!!!

Tusubiri kushinda kama ile Meli ya Masamaki.Maana kama hata ile kesi ya akina Masamaki tumeshindwa kabla hata haijaanza tukaona nyota tumewatoa wazee wa Rushwa na ufisadi wako mjini wanatanua kama kawa.

Hata hili tutapigwa kimya kimya tutaomba radhi maisha yataendelea,ilikuwa kick tu usijali,kuonekana magazetini hakujawahi mwacha mtu salama
 
Ukimya uliotanda juu ya maendeleo ya majadiliano ya makinikia yana mshindo Mkuu. Taarifa nilizopenyezewa na mtu ninayemwamini inasemekana jamaa wamekomaa kwelikweli na wanajua kupangua hoja. Inasemakana kuwa Hoja zetu zinazojikita kwenye tuhuma na siyo uhalisia zinasagwa na kuyeyushwa kama chuma.

Kana kwamba hiyo haitoshi hata maprofesa walioko kwenye kamati ya Makinikia kutoka Tanzania wameanza kuzilaumu kamati zilizoundwa kuchunguza Makinikia hayo kwani wanashindwa kupangua hoja za Mzungu katika majadiliano hayo ambayo yametawaliwa na rejea kutoka katika matokeo ya kamati mbili za Rais ambayo yalitiliwa shaka na wengi .

Ngoja tusubiri trilioni 300 na zaidi. Tanzania isipokuwa tajiri kwa pesa zote hizo tutakuwa tuna laana.
Ukimya gani? Mbona umeishayapata na sisi kupitia kwako tumeyapa? Kumbuka kushinda au kushindwa ni kwa Watanzania!
ujitafakari!
 
nasubiria NOAH yangu nimeshaioda kabisa

Angalia tu usije ukaishia kufa kwa kihoro pale utakapoambiwa deni unalodaiwa limezidi la NOAH yaani unadaiwa deni la New Model MB
 
Back
Top Bottom