Majaliwa asema CCM kumpeleka kwa wananchi Rais Samia 2025

Majaliwa asema CCM kumpeleka kwa wananchi Rais Samia 2025

Ni kikao kilichopitisha hayo maamuzi ya hivyo.
 
Badala ya kufanya kazi wamekalia kampeni, CCM ni janga ndani ya nchi hii na maendeleo ya kweli tutaendelea kuyasikia kwa wengine tu, maana viongozi muda wote wanapambana kubaki madarakani
 
Hii sasa ni kufuru!.. Uchaguzi tumefanya miezi kumi iliyopita, Mpaka October 2025 kuna miaka minne kamili. Badala ya kuwaza namna ya kushughulikia kilichomo kwenye ilani iliyonadiwa na ahadi zilizotolewa, tunapenyezewa nyeti za nani atakayesimama kugombea?. Kampeni zimeanza mapema? 🤔 😳
 
Dodoma.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema mwaka 2025 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitampeleka kwa wananchi mtu mmoja, Rais Samia Suluhu Hassan hivyo mawaziri watambue hilo.

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Oktoba 29, 2021 katika ukumbi wa St Gasper jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa mawaziri na naibu mawaziri.

Majaliwa amewataka mawaziri na naibu wao kuwa wasemaji wakubwa wa mafanikio ya Serikali ili itakapofika 2025, Samia Suluhu Hassan (Rais) apite na kusema kidogo tu.

"Wambieni wananchi kuhusu mazuri yanayofanywa na Serikali hii, tambueni msimamo na mtazamo wa Rais ili mkawe wasemaje zaidi yeye akija awe na maneno machache ya kueleza," amesema.

Waziri Mkuu amewataka mawaziri na naibu wao kufanya kazi kwa mashirikiano na kuheshimu kauli za viongozi wakuu kwani siyo kila agizo lazima waandikiwe barua ndipo watekeleze.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amewataka viongozi hao kuwa mfano kwa mienendo yao wakianzia na mavazi, kauli na kutojiinga katika mambo yatakayowafanya wajadiliwe.

Amesema katika mitandao ya kijamii wapunguze kuzungumza mambo mengi ili kusudi wanapotamka mambo machache yaonekane kuwa na maana kwa jamii.

Chanzo: Mwananchi
Wanashinda insta na warembo wao na mavazi yao ya ajabu,utadhani ni wa bongo movie!
 
Tumuombe Mwenyezimungu atujaalie uzima hiyo 2025.
Na kama CHADEMA wakimuweka Mh. Mbowe unadhani mtanange utakuwa vipi..? (Free and Fair uchaguzi)
 
Hivi Majaliwa ni nani huko Ccm?? Maana naona ana vuka mipaka yake ya utawala..
 
Dodoma.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema mwaka 2025 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitampeleka kwa wananchi mtu mmoja, Rais Samia Suluhu Hassan hivyo mawaziri watambue hilo.

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Oktoba 29, 2021 katika ukumbi wa St Gasper jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa mawaziri na naibu mawaziri.

Majaliwa amewataka mawaziri na naibu wao kuwa wasemaji wakubwa wa mafanikio ya Serikali ili itakapofika 2025, Samia Suluhu Hassan (Rais) apite na kusema kidogo tu.

"Wambieni wananchi kuhusu mazuri yanayofanywa na Serikali hii, tambueni msimamo na mtazamo wa Rais ili mkawe wasemaje zaidi yeye akija awe na maneno machache ya kueleza," amesema.

Waziri Mkuu amewataka mawaziri na naibu wao kufanya kazi kwa mashirikiano na kuheshimu kauli za viongozi wakuu kwani siyo kila agizo lazima waandikiwe barua ndipo watekeleze.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amewataka viongozi hao kuwa mfano kwa mienendo yao wakianzia na mavazi, kauli na kutojiinga katika mambo yatakayowafanya wajadiliwe.

Amesema katika mitandao ya kijamii wapunguze kuzungumza mambo mengi ili kusudi wanapotamka mambo machache yaonekane kuwa na maana kwa jamii.

Chanzo: Mwananchi

Kuuliza si ujinga, Majaliwa asema CCM itampeleka samia kwa wananchi. Nani au kikao kipi kimekutuma useme hayo? Mwenza wa Rais haonekani, hasemi ,hajulikani aliko , wewe umetumwa na nani?​

 
Dodoma.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema mwaka 2025 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitampeleka kwa wananchi mtu mmoja, Rais Samia Suluhu Hassan hivyo mawaziri watambue hilo.

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Oktoba 29, 2021 katika ukumbi wa St Gasper jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa mawaziri na naibu mawaziri.

Majaliwa amewataka mawaziri na naibu wao kuwa wasemaji wakubwa wa mafanikio ya Serikali ili itakapofika 2025, Samia Suluhu Hassan (Rais) apite na kusema kidogo tu.

"Wambieni wananchi kuhusu mazuri yanayofanywa na Serikali hii, tambueni msimamo na mtazamo wa Rais ili mkawe wasemaje zaidi yeye akija awe na maneno machache ya kueleza," amesema.

Waziri Mkuu amewataka mawaziri na naibu wao kufanya kazi kwa mashirikiano na kuheshimu kauli za viongozi wakuu kwani siyo kila agizo lazima waandikiwe barua ndipo watekeleze.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amewataka viongozi hao kuwa mfano kwa mienendo yao wakianzia na mavazi, kauli na kutojiinga katika mambo yatakayowafanya wajadiliwe.

Amesema katika mitandao ya kijamii wapunguze kuzungumza mambo mengi ili kusudi wanapotamka mambo machache yaonekane kuwa na maana kwa jamii.

Chanzo: Mwananchi
Huyo mama akigombea sihangaiki kupiga kura yangu maana nitakuwa nimeinajisi
 
Back
Top Bottom