Majasusi wa Urusi (FSB) wambaini m-Ukraine aliyetega bomu Urusi na kumuua binti mwandishi wa habari (Darya Dugina)

Kama wamemfahamu muhusika ni vyema ila wangeweza kuzuuia tukio kama wangekua na ' Intel..' za kutosha.

Wanao sana ila kuna watu muhimu wengi sana na wanao Chungwa ni wengi mno ila Labda huyo hakuwa katika list
Sio suala la intelijensia kwani wengine hawachungwi bali wajichunge wao

Kama target imeandaliwa ni vigumu kujua Labda Siri ivuje tu
 
Hua wanakamata wairan wenzako waliowahi kushirkiana au kutumiwa na mossad (halafu wakija kwenye media wanajikwambafai) sijawahi ona Iran kamkamata mossad agent aliyefanya tukio.
Haya,nimekupa na wengine waliotaka kulipua maeneo nyeti wakadakwa!
 
Hahaha pro Russia wanateseka sana.
Kwanza huu waweza kuwa uzushi yaani wafuatolie hizo footage zote na wasimkamate?

Hii ni baada ya mlipuko ndio wakafanya uchunguzi na kumjua kwa kuangalia cctv na mienendo yote mpaka kujua aliingia lini

Hatuwezi kusema kwanini hawakudhibiti kwa sababu hakuwa anachungwa
Ushahidi ni baada ya kuanza utafutaji wa evidences
Hata hivyo wako vizuri wakati sisi hatuoni umuhimu wa cctv au tunazitoa baada ya tukio
Au umeme unakata kutwa
 
Ni vigumu kumpata kwani Estonia ni mwanachama wa NATO ingawa Russia wameomba extradiction ya huyo mwanamke.

Pia Estonia pana majeshi ya NATO na vifaa vyote hivyo Russia inawawia vigumu kuchukua hatua ya haraka.
Watu wanafuatwa mpaka ndani ya uingereza Kama Yule jamaa aliyepewa sumu?warusia wanaingia popote.
 
Je nikisema aliuliwa Russians mwenyewe nitakuwa muongo?.........kwamba kwa nafasi ya babaake, magharibi wali collaborate naye, alafu wa Russia wakabaini hilo na kukata kitovu kwa namna Ile.
 
Ni vigumu kumpata kwani Estonia ni mwanachama wa NATO ingawa Russia wameomba extradiction ya huyo mwanamke.

Pia Estonia pana majeshi ya NATO na vifaa vyote hivyo Russia inawawia vigumu kuchukua hatua ya haraka.
Hata kama Yuko upande wa NATO ni mhalifu kama wahalifu wengine,nchi atakayopatikana itaombwa imtoe ashitakiwe.
Kama nchi ikikataa maana yake nchi hiyo inaunga mkono vitendo vya kigaidi.
Na Ugaidi ni dhambi kubwa sana kwa nchi za NATO.
Sasa hapo ndiopo mzani utakapokataa kubalance.

Nakumbuka Skipal,yule Mrusi na Binti yake waliopewa sumu huko London.
Lkn bahati hawakufa.
Wacha tuone.
 
Je nikisema aliuliwa Russians mwenyewe nitakuwa muongo?.........kwamba kwa nafasi ya babaake, magharibi wali collaborate naye, alafu wa Russia wakabaini hilo na kukata kitovu kwa namna Ile.
Ndugu yangu ,usitake kupoteza muda wako Bure,
FSB wameshamaliza kazi,wameshapata details zake zote.wameshajua Kila kitu kinachomhusu.
Usifikiri FSB ni Akina Siro kuwa wanasubiri mpaka wampate dereva wa Lisu ndio wamjue aliempiga risasi.
Usijaribu kupotosha,Wala FSB sio wapotoshaji
Kama wale wa kusema CDM ndio waliompiga mtu wao na vyuma.
Hapa kwa FSB upele umepata mkunaji.
 
Labda wataiteka tena
 
Kama alipitia ukaguzi mkali kabla ya kuingia Russia ina maana bomu kalipata akiwa ndani ya Russia. Ivyo ndani ya Russia kuna mapandikizi ya Ukraine walishirikiana nae kufanikisha mission.
Hakuna kitu Urusi kakosea kama kuchukua Wananchi wa Ukraine kama wakimbizi, afu yeye ndo mvamizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…