Majibu ya Rais Samia Suluhu hata Kama yangekuwa uongo lakini Yanaridhisha

Majibu ya Rais Samia Suluhu hata Kama yangekuwa uongo lakini Yanaridhisha

Lini ulilazimishwa na nani aliyetulazimisha? Tuwekee huu ushahidi husika.
Tatizo mnalazimisha watanzania wote waende na hii ajenda ya katiba mpya ukweli ni kwamba ... muda bado wa kuwa na katiba mpya ukifika hakutakua na haja ya kutumia nguvu nyingi.

Kuna matatizo kweli ambayo wanaweza wakayajadili na wakatengeneza ground-base kutaka kuaminisha watz kua kila tatizo ni kwasababu ya katiba mbovu hata kama ni kweli it will take time mpka tuelewe anzeni na ambayo yanamgusa kila mtu moja kwa moja
 
Wanakatwa kwa ridhaa yao?
Pengine wapo walioridhia na pengine wapo ambao hawajaridhia na wala kukubaliana na hali.

Hivyo suala libaki kila mtu ajisemee mwenyewe,kama mimi nimeshakubaliana na hali
 
Interview ya Salim Kikeke na Samia jana imefanya mambo makuu manne yafuatayo:

1.Imemfunua Samia ni nani,anataka nini na ana mpango wa kuifanyia nini Tanzania.Imemfunua kuwa ni dikteta muoga na asiejiamini.

2.Imemshusha Salim Kikeke kupindukia.

3.Imeumiza image ya BBC.

4.Imedhalilisha waandishi wa habari.
 
Pengine wapo walioridhia na pengine wapo ambao hawajaridhia na wala kukubaliana na hali.

Hivyo suala libaki kila mtu ajisemee mwenyewe,kama mimi nimeshakubaliana na hali

Ww ni mfaidika wa hizi tozo kandamizi, hivyo huwezi kuacha kuridhika.
 
Assalamu Aleykum

Nimemsikia Mhe. Rais, Mama Samia Suluhu akiwa anahojiwa na Mwandishi, Salimu Kikeke. Kwa kweli Maswali yamejibiwa vizuri Sana.
Nafahamu Siasa zilivyo, nafahamu mambo ya kiutawala Kwa kiasi kidogo, Kwa majibu ya Rais Samia ni wazi amejibu kwa kiwango cha juu mno.

Ingawaje amejibu kirahisi sana karibu maswali yote lakini majibu yake yalikuwa yanafungua majibu ya baadhi ya maswali ambayo angeulizwa Mbele.

Hata Kama Samia atakandiwa na mahasimu wake kuwa amejibu Kama mjinga, au ameongea uongo, au vyovyote watakavyo mwambia lakini ukweli ni kuwa amejibu Kwa kiwango kizuri cha juu kabisa. Kama ni uongo basi ni ule uongo unaoridhisha kabisa.

SSH moja ya majibu yake, hasa kwenye mikutano ya Kisiasa ameniongezea Jambo jipya ambalo nikiri kuwa sikuwa nalifahamu.
Jambo Hilo ni kuhusu Katiba ya Vyama vya Kisiasa ambapo ndani yake kuna vipengele vinavyoelezea idadi ya vikao na mikutano Kwa mwaka ambayo Chama kitapaswa kikae.

Mikutano hii Kwa vile IPO kikatiba(ya kila chama kulingana na Chama) ikiitishwa haina haja ya kuomba kibali Kwa polisi.
Hii Kwa kweli sikuwa nafahamu.

Kwa maelezo yake Kama nitakuwa nimekuelewa Sawia, alikuwa anamjibu Kikeke kuwa, Mikutano au vikao vya kichama inaruhusiwa ikiwa vimeorodheshwa ndani ya Katiba. Na Kama havijaorodheshwa basi sharti kuwepo na Kibali kutoka Polisi.

Kwa mujibu wa maelezo ya SSH anajaribu Kueleza kuwa baadhi ya Vyama vya Upinzani hutaka kufanya mikutano hovyo hovyo hata Kama vikao/mikutano hiyo haipo kikatiba(Katiba ya chama husika) na pia hawajaomba Kibali polisi.

Nikiri kuwa sikujua Jambo Hilo. Na niliona Wapinzani wanaonewa lakini Kama ni hivyo basi nilikuwa sipo Sahihi.

Lakini Kama SSH anadanganya basi Wanasheria mtanieleza kuhusiana na hoja hiyo aliyoisema Mhe. Rais.

Kuhusiana na Kesi ya Mbowe, siwezi elezea lolote isipokuwa naiachia Mahakama, ingawaje maswali ninaweza kuwa nayo, mathalan, iweje Mbowe akamatwe kipindi hiki akidai Katiba mpya na sio kipindi cha nyuma?

Ingawaje SSH ameeleza kana kwamba Tayari kulikuwepo na mchakato wa kesi hiyo na ndio maana Mbowe amejiingiza katika kudai Katiba mpya kujikinga na mshale wa kesi hiyo.

Yote tisa, mwisho ni majibu ya Mhe. Rais ni mepesi Sana lakini Yanaridhisha mno kiasi kwamba hata muulizaji anajikuta maswali mengine aliyonayo kichwani yanayeyuka.

Muhimu:. Tunataka Katiba Mpya Kwa kizazi kipya.
Ishu ya Katiba si suala la kiongozi kuamua liendelee ama liendelee. Ni takwa la kizazi kipya.

Taikon wa Fasihi
Turiani, Mvomero
We jamaa naona umeandika kutokana na mahaba yako au ndio mwisho wa uelewa wako ukiangalia kiundani yale mahojiano yameacha maswali mengi kuliko majibu. Pia yameonyesha namna uongozi tuliona unavyoyachukulia mambo yeye maslahi ya kitaifa katika mtazamo finyu, nikiongelea kwenye hizo point zako mbili ulizochukua÷suala la mikutano ya kisiasa na suala la kukamatwa kwa Mbowe
*Suala la mikutano, kwamba mikutano haiko kikatiba ila inaruhusiwa iwapo imeorodheshwa katika katiba ya chama husika pia inatakiwa ipate kibali cha polisi Sasa suala la kujiuliza Je vyama vya siasa kazi yake nini na vinafanyaje kazi, je sheria ya vyama vya siasa inasemaje kuhusu mikutano ya kisiasa na ni wakati gani inatakiwa ifanyike, ni wakati wa uchaguzi kutoa elimu kwa wapiga kura au wakati mwingine wowote baada ya uchaguzi ili kutoa elimu ya uraia na pia kushawishi watu ili kupata wanachama wapya?, Pia kuhusu kibali cha polisi,je polisi kazi yake kutoa kibali au kuamua kukataza au kukubali mikutano?
*Kuhusu suala la kukamatwa kwa Mbowe,kwamba alikua na kesi toka mwaka jana na wenzie walishakamatwa na walishaukumiwa, Sasa wenzie waliohukumiwa ni wakinanani, kwanini Mbowe hakukamatwa toka wakati huo akamatwe Sasa?
Kwa maoni yangu naona mama amepuyanga kwenye hayo mahojiano kwa sababu majibu yake mengi yalikua mepesi Sana pia yalikosa rejea ie kikatiba,sheria, takwimu au tafiti na pia ninavyoona siasa za Tanzania ziko biased Sana maana tunaona chama tawala wanafanya siasa za uhuru zaidi kwa kimvuli Cha serikali huku upinzani wao wanapigwa Sana danadana
 
Interview ya Salim Kikeke na Samia jana imefanya mambo makuu manne yafuatayo:

1.Imemfunua Samia ni nani,anataka nini na ana mpango wa kuifanyia nini Tanzania.Imemfunua kuwa ni dikteta muoga na asiejiamini.

2.Imemshusha Salim Kikeke kupindukia.

3.Imeumiza image ya BBC.

4.Imedhalilisha waandishi wa habari.


Maswali yalikuwa rahisi mno
 
Kuna tatizo gani upinzani wakiwa na agenda zaidi ya moja wanazozipagania katika nchi?

Upinzani hauwezi kupigania agenda ya katiba mpya, uhuru wa habari na tozo za miamala ya simu kwa pamoja?
Upinzani hawana Agenda wanayoipigania.

Ni Kama ngedere anayerukia Tawi hili na hili

Kama wangekuwa na Agenda moja wakaipigania mpaka ikakamilika huenda wangekuwa mbali.

CCM wanachoringia ni kuwa na Upinzani dhaifu sana
 
Kuna tatizo gani upinzani wakiwa na agenda zaidi ya moja wanazozipagania katika nchi?

Upinzani hauwezi kupigania agenda ya katiba mpya, uhuru wa habari na tozo za miamala ya simu kwa pamoja?

Sijakataa.

Ila wapiganie chenye soko si unajua Siasa pia ni Kama biashara
 
Wote wanaomsifia Samia ni Kwa sababu ya udini and nothing else , wanajaribu kumkingia kifua agombee tena 2025 japo indicator zinaonyesha worst to come!!! Kama nilimpinga Jiwe , sina cha kumsifia SSH madam Yale ya Maghufuli anayaendeleza Kwa udhabiti zaid
Na wewe unampinga SSH kwasababu siyo dini yako ?
 
Unaweza kuwa sahihi, ndio maana nikasema hata Kama ni uongo lakini unaridhisha
Hivi wewe ukoje, tangu lini majibu ya uongo yakaridhisha? Au ni yale mambo ya Zanzibar kuwa tumefungwa lakini chenga tumewala? Acheni uswahili simamia haki wewe.
 
Hivi wewe ukoje, tangu lini majibu ya uongo yakaridhisha? Au ni yale mambo ya Zanzibar kuwa tumefungwa lakini chenga tumewala? Acheni uswahili simamia haki wewe.


Hujawahi ona Uongo unaoridhisha
Kisha ukakutana na ukweli usioridhisha?

Waulize Mahakimu na majaji watakuambia,
Au waulize waliopo ndani ya ndoa
 
Sasa mbona unang'nga'niza wawe na bidhaa moja tu?!
Bakheresa mwenye bidhaa za juice, ice cream, hotel, unga na media biashara yake sio sustainable ?
Kila kitu duniani ni Kama biashara tuu.
Angalia soko linahitaji nini ili Biashara iwe sustainable
 
Back
Top Bottom