Makabila haya mtu ukifanikiwa jiandae kujaza ndugu tegemezi kwako ama kukuomba misaada kila mara, ukikataa unaonekana huna undugu

Makabila haya mtu ukifanikiwa jiandae kujaza ndugu tegemezi kwako ama kukuomba misaada kila mara, ukikataa unaonekana huna undugu

wasambaa kwa tabia hizo ndo wenyewe hao ukoo mzima utahamia kwa ndugu au kama mtoto wao kaolewa na mume mwenye unafuu wa maisha basi timu nzima itaweka kambi ya pre season hapo nyumbani
Kati ya vitu ambavyo Wasambaa hatujajaliwa, basi ni ubinafsi na uchoyo kwenye chakula. Ukioa/ukiolewa na Msambaa, kubali kuishi kijamaa.

Hayo ndiyo maisha ambayo Mwenyezi Mungu ametujalia.
 
Katika hali ya kawaida inaweza kuwa kero kwako lakini katika jicho la kibinadamu na kama Mungu amekujaalia kipato basi jitahidi kuwasaidia ndugu zako katika namna ambayo hutawadhalilisha au kuwakwaza...........

Zipo namna nyingi za kuwasaidia ndugu bila kugombana au kukwazana nao....kila mmoja ana jinsi yake ya kuyaendea maisha na kutafakari mambo yake......Kuna baadhi ya watu akili zao zimechangamka katika kuziona fursa na kuzifanyia kazi....lakini pia wapo watu ambao akili hazifanyi kazi mpaka ziamshwe kwa matendo au matukio ni hali kawaida kimaumbile kwani hatuwezi kufanana..........

Kama Mungu amekunyooshea mambo yako na una nafasi ya kumsaidia ndugu yako au hata jamaa yako wa karibu usisite kufanya hivyo kwa namna yoyote Ile ambayo itamfaa.........

Kweli maisha ni magumu vipato vyetu Wakati mwingine havikidhi mahitaji yetu lakini haimaanishi kuwa tuwatupe ndugu zetu.........

Wapo watu ambao ni wachache wa fadhila na wapo watu ambao ni wenye kushukuru na kukumbuka fadhila.....hupaswi kuhangaishwa na hayo kwani moyo wa mtu ni kiza kinene fanya wema wako kwa kadri ya uwezo wako.......

Mafanikio na hali nzuri za maisha zisitupe viburi na jeuri na kuona kuwa hatuwahitaji.....huo ni upofu wa fikra na ubinafsi......maisha ni kutegemeana na kusaidiana kwani hakuna mwanadamu anayejitegemea kwa kila kitu........asio kufaa kwa hili basi atakufaa kwa lile.......

Tuufanye wema kama kiunganishi na tuukatae ubaya kama utenganishi......


Ukubwa au udogo wa Dunia inatokana na wewe unavyoishi na binadamu wenzio......
Dah, umeongea point Sana, Mimi sipendagi wageni kwangu, hila sasa itabidi niwe mkarimu kwakweli! Nikweli binadamu tuwe na Moyo wa kusaidiana
 
😂😂😂hao ni hatari sitosahau walivyonimalizia sofa zangu, tv inaangaliwa kuanzia 12 asubuhi mpaka ngoma tisa night kali kulala nalala kwa tabuu kisa wao
na sifa ya wizi na umalaya kwa wanawake!
 
wasambaa kwa tabia hizo ndo wenyewe hao ukoo mzima utahamia kwa ndugu au kama mtoto wao kaolewa na mume mwenye unafuu wa maisha basi timu nzima itaweka kambi ya pre season hapo nyumbani
hii n kweli hua nawaona wasambaa wakishuka kwny burdan,tashrif,nacharo, shambalai, ksk na kiluwa ase anashuka babu,shangaz, mamdogo, shemeji hapo kila mmoja kaja na vitoto vyake vitatu
 
Hatukatai ndugu kuja shida mtu anakuja kukaa tu yani hawazi kazi wala nini,

Inavyotakiwa inabidi muwe na umoja lakini sio umoja wa kuanza kujazana na kuwa wategemezi, Kuna makabila mifano mizimuri kama wachaga, wakinga, wakuria, n.k yaani kama wewe ni mgeni ukienda kwa ndugu utapokelewa vizuri tu lakini itabidi uwe umeshataarifu ujio wako, shughuli iliyokuleta, ratiba yako ikoje, upo mpaka lini, mipango yako, n.k. kama ni kusalimiana wiki 2 zinatosha, sahau kuweka kambi hapo ya kudumu.



Kimbembe kipo kuna makabila wakishaona mwezao katoboa mjini, basi ndugu zake ama ndugu wa mke huhamishia kambi huko ,... wanakula na kulala hapo bila kazi maalum [emoji28][emoji28]

Makabila haya kwangu niliyoyaona ni kama.

. Watu wa pwani - wazaramo, wasambaa, wadigo

. Wanyakyusa - hawa huwa wanaendeleza undugu hata ule wa mbali, hata mke wa mjukuu wa baba mdogo wa babu bado anahesabiwa kama ndugu, kawaida sana kukuta mnyakyusa ana ndugu 100 na hao wengi hukutana misibani ama wakifika sehem wanaulizia ndugu zao wapate pa kuishi.

Wabena - hapa dada awe kalamba kitengo flani halafu yupo mjini, atatafutwa na atapatikana na wataalikana.

-wanyamwezi na wagogo,


Kuna ile kujificha nyuma ya kivuli cha undugu lakini inakuwa inazidi sasa, mtu hata maendeleo yanashuka
Wachaga hawapo?
 
Kama unakwazika na ndugu kujaa kwako bila shughuli maalumu waambie live kuwa maisha ni magumu waende kwao wakajitegemee au waende Mombasa kuna vitu vya bure wapendavyo.
Kwanini upate shida na upo home kwako.
Speak out!!
Ukonga Mombasa hii hii nnayoijua mimi au Mombasa ipi mkuu?
 
Halafu unapata pesaaa mingi! japo unalisha kundi la watu!! pia ni ufahari kutegemewa na watu wakubwa kwa wadogo! wengiiii!! najisikiaga sana....

nilipo huku nje ya nchi ili mradi tu uwe Mtanzania ninakutunza bila shida na km unaanza maisha njoo kwangu ila usiwe mwizi nina uwezo wa kujua Mwizi ni yupi! lkn shambani kama kawaida!

usiwe mvivu kufanya kazi, za shamba /viwandani, hapa nina Mgahawa wangu utakula humo lkn lipa , nitakulipa posho ya chakula na kazi za kufua vyuma na kuosha magari! kama mia tano hivi! na shamba!

kulima shambani na kuvuna, ujenzi km hujui kujenga utakuwa kibarua wa mafundi kwenye kampuni yangu ya ujenzi!! mambo yako yakiwa safi tambaa!...ukiumwa wkt uko kwangu unatibiwa hospitalini kwangu unalipia!

Ukiona kulala chini huwezi nina milki Hostel utaenda hapo utalipia hela kidogo!! hata ndugu wa damu wakija kwangu mwendo ni ni ivoivo tu! so sinaga hasara!
 
Makabila ya watu wakarimu yote wanajali sana undugu, huwa hawajali sana vitu kama msosi, sijui maisha magumu wao ndugu akija nyumbani kwake anafurahi tuu wala haoni tabu.
Katika hili, Mungu atubariki Wasambaa kwa kweli.
 
Back
Top Bottom