Pre GE2025 Makonda: Dereva wangu alikuwa anafunga namba za RC DSM na kutapeli watu

Pre GE2025 Makonda: Dereva wangu alikuwa anafunga namba za RC DSM na kutapeli watu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Jana kwenye nyama choma aliyoandaa kwa Wakuu wa Mashirika Mjini Arusha, anasema alipokuwa RC Dar, wakati yeye yupo amepumzika ndani, Dereva wake alikuwa anakuja kuchukua gari kisha kuweka namba za RC Dar na bendera kisha kwenda kwa matajiri kuomba/ kuchukua fedha kwa jina lake.

My Take:
Huyu anatafuta kujisafisha tu, ila iko siku atatuambia alimficha wapi Roma na alimzika wapi Ben Saanane
Alimchukulia hatua gani huyo dereva?
 
Alichokisema Makonda ni kweli, watu wengi sana wametapeliwa na bado wanaendelea kutapeliwa kwa huo mtindo. Mungu akufunulie uelewe. Wafanya biashara wanataabika sana. Yaani kumuona kiongozi wanatozwa hela nyingi mno na wafanya wasaidizi wa viongozi na usishangae kukuta kiongozi hata kama alikuwa rafiki yako akaacha kupokea simu vile vijamaa vinamtia sumu maana vyenyewe ndiyo gate valve ya kupokea hela za rushwa kumuona kiongozi. Yaani huo mchongo ni deep state kwa ufupi. Ila ukienda Zanzibar huo ujinga hawana. You can just walk ukaonana na waziri katibu mkuu ila njoo huku bara, yaani kumuona katibu mkuu, waziri au mkuu wa shirika wasaidizi wao ambao ni vetted watakutoza hela tena kama shida yako ni kubwa na hela ni kubwa na mbaya kiongozi anakuwa hajui.

Sio kweli.. ukiona hivyo ujue kuna namna kiongozi huyo anabariki huo uhuni. Kama hataki haiwezi kuwa hivyo.
 
Alichokisema Makonda ni kweli, watu wengi sana wametapeliwa na bado wanaendelea kutapeliwa kwa huo mtindo. Mungu akufunulie uelewe. Wafanya biashara wanataabika sana. Yaani kumuona kiongozi wanatozwa hela nyingi mno na wafanya wasaidizi wa viongozi na usishangae kukuta kiongozi hata kama alikuwa rafiki yako akaacha kupokea simu vile vijamaa vinamtia sumu maana vyenyewe ndiyo gate valve ya kupokea hela za rushwa kumuona kiongozi. Yaani huo mchongo ni deep state kwa ufupi. Ila ukienda Zanzibar huo ujinga hawana. You can just walk ukaonana na waziri katibu mkuu ila njoo huku bara, yaani kumuona katibu mkuu, waziri au mkuu wa shirika wasaidizi wao ambao ni vetted watakutoza hela tena kama shida yako ni kubwa na hela ni kubwa na mbaya kiongozi anakuwa hajui.
Hujawahi kuwa Kiongozi wewe, wacha uwongo.

Kama kuna Kiongozi wa umma, watu wanapitia wasaidizi wake kujitengenezea pesa, na yeye HAJUI, basi HAFAI KUWA KIONGOZI.

There is no any excuse on this aspect
 
Anaweza akaongea ukweli, ila hapo muongo ni yeye kutaka kujitenga na hayo matukio. Ukiona dereva alithubutu kufanya hivyo, basi jua hiyo ndiyo ilikuwa michezo ya boss wake, so ilikuwa ni michezo yao kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake.
Absolutely correct. Bashite ni pimbi kabisa. Wanaposema ni ZEROBRAIN kweli ni zero. Kanyimwa akilikapewa
 

Attachments

  • Screenshot_20240830_113710_Chrome.jpg
    Screenshot_20240830_113710_Chrome.jpg
    143.2 KB · Views: 5
Tumemsikia yule aliyekuwa Konda kwenye ile Kampuni ya mabasi awaku ile akimrushia lawama aliyekuwa Dereva.
Je, ametumia fasihi katika kumrushia lawama aliyekuwa dereva wake kwamba maovu yale yalifanywa na yule dereva ila lawama ma chuki akarushiwa yeye?

Je, Inawezekana huu ni mwendelezo ambao kila anayepewa nafasi ya kuhudumu kwenye kampuni hii ya sasa ya mabasi chini ya Dereva wake Mpya, amekuwa akijaribu kujitakasa kwa kumtumia lawama yule aliyekuwa Dereva wa mabasi ya kipindi kile.

Safari hii tumemsikia aliyekuwa Kindakta kipindi kile akisimama hadharani na kuamua kumtupia lawama aliyekuwa Dereva wake, ingawa lawama hizo amejaribu kutumia fasihi na tafsida kiasi kwamba wengi wanadhani anayelaumiwa ni Dereva kwa maana ya Dereva, ila kiuhalisia nianayerushiwa lawama na huyu Kondakta ni Dereva.
Masikini Dereva yule, mwisho wa siku hata waliomuwezesha kuipata ile ajira na wenyewe watamiana.
Umeandika tafsida (satire) lakini kichwa cha Bashite hakina uwezo wa kutengeneza fasihi ya namna hiyo. Yeye alipewa mshipa wa kuvuruga na kuua tu
 

Jana kwenye nyama choma aliyoandaa kwa Wakuu wa Mashirika Mjini Arusha, anasema alipokuwa RC Dar, wakati yeye yupo amepumzika ndani, Dereva wake alikuwa anakuja kuchukua gari kisha kuweka namba za RC Dar na bendera kisha kwenda kwa matajiri kuomba/ kuchukua fedha kwa jina lake.

My Take:
Huyu anatafuta kujisafisha tu, ila iko siku atatuambia alimficha wapi Roma na alimzika wapi Ben Saanane
Mpaka Dereva anachukua gari na kuondoka ww hujui kweli?au ulikua unamruhusu?
 
Back
Top Bottom