#COVID19 Malaria ndio inaua zaidi kuliko COVID19, mbona nguvu nyingi ziko kwenye COVID19

#COVID19 Malaria ndio inaua zaidi kuliko COVID19, mbona nguvu nyingi ziko kwenye COVID19

Kwanza zingatia maabukizo ya covd19 na malaria ni tofauti pia hiyo asilimia 2% ya corona kuua ni ktk kipindi kifupi sana ukifananisha na malaria. pia tiba kubwa ya corona ni oxygen tiba hii pia ni aghali sana na adimu kuzidi ya maleria.
Na toka kuzaliwa hujawahi kusikia hospitali imeelemewa na wagonjwa wa maleria lakini korona hospitali zimeelemewa
Pia hajawahi kusikia wauguzi na madaktari kadhaa waliokua wanahudumia wagonjwa wa malaria wamekufa kwa malaria. Lakini korona imewabeba
Haya ni mambo machache sana yanayo tofautisha uhatari wa corona19 dhidi ya malaria kama utatuliza akili na kuchunguza zaidi uta pata mengi ya hatari zaidi ktk covid 19 dhidi ya malaria
Unajua malaria imeua waafrika wangapi kila mwaka ?
 
Bado hakuna uhakika hizo ni nadharia tu ambazo zisizokuwa na uhakika maana hakuna uhakika wa kisayansi kuwa 5% haitatengeneza au itatengeneza variants wapya watakaomaliza 5% iliyobaki.


Swali langu la msingi.

Wewe unadhani kwanini FDA huko kwenu US hawajathibitisha uthabiti wa hizi chanjo ?
Uhakika ni nini? Kuna kitu kimoja unachoweza kusema kwa uhakika? Chochote kile?

FDA ukitaka kuwahoji, hata hizo zilizopitishwa kwa uthabiti utashindwa kuzihoji?

Nikikwambia sababu kwamba kuna tofauti kati ya chanjo za kawaida na chanjo za pandemic, utajua kuzielewa kwa muktadha halisi?

Uko vitani, kawaida unasubiri amri ya ku fire bullets, ukapata emergency mkubwa wako wa kukuamrisha fire hayupo, adui yuko mbele yako, utasema unasubiri mkubwa wako akuamrishe fire bullets? Au utajilinda kwa kadiri unavyoweza kwa muda huo na kuangalia itifaki nyingine baadaye?

Wewe una uhuru, kuchanja au kutochanja.

Kuna mtu kakulazimisha?
 
Unavyosema hivyo utadhani hii chanjo ukichanjwa haupati COVID-19
Kwa nini unafikiri hivyo? Kipi kimekupa wazo hilo?

Unaelewa tofauti ya mtu anayeambukizwa Covid-19 baada ya chanjo na anayeambukizwa Covid-19 kabla ya chanjo?

Unaelewa chanjo ni nini na inafanya kazi vipi?
 
Ni muhimu kwenda na context na probabilities.

Yani mtu anakwambia leo wanaolazwa mahospitalini Marekani zaidi ya 97% ni wasiochanjwa, na zaidi ya 99% ya wanaokufa ni wasiochanjwa, halafu bado unakataa kuchanjwa kwa sababu hujui kesho variant gani itazaliwa? Na hapohapo unaambiwa kwamba kutochanjwa ni sababu kubwa ya variants mpya kuzaliwa? Huoni hapo kukataa chanjo kunakumaliza kwa sababu unaongeza nafasi ya kuugua na hata kufa?

Chanjo kama huku Marekani siku zote zimekuwa na disclaimer.Mimi nilivyoanza chuo niliulizwa rekodi za chanjo zangu za MMR. Sikuwa nazo. Nikachanjwa.Nilivyochanjwa nikapewa disclaimer kwamba kunaweza kutokea madhara.Hiki ni kitu cha kawaida hata kwa chanjo zilizokuwa fully confirmed.Ila, inabidi tuweke vitu katika muktadha sahihi. Kwa sababu unaweza kukataa chanjo kwa risk iliyo ndogo sana ya kukufanya uugue au ufariki, pia hapo hapo ukakubali kukaa bila kuchanjwa ukiwa na risk kubwa sana ya kuugua na kufa.

Narudia tena kusema, kuna watu wengi waliokataa chanjo wamepata ugonjwa, wamelazwa, wanalilia chanjo baada ya kuugua. Wanaambiwa chanjo haifanyi kazi hivyo, inatakiwa uchanjwe kabla hujaumwa. Wengine wanafariki.

Disclaimer si ujinga, ujinga ni kutoelewa nature ya disclaimer, kutoelewa proportionality, kutoelewa context.

Kwa jamii zetu ambazo hazijazoea kusoma disclaimer, hazijazoea nuance, hazijazoea transparency, disclaimer inaweza kuonekana ujinga.Lakini hilo ni tatizo la ujinga wa jamii, si tatizo la ujinga wa dislaimer.

Kwenye nchi legalistic kama US unaweza kutoa vaccine kwa watu milioni mia moja, akafa mtu mmoja tu.

Kama hujatoa disclaimer ambaye ingeokoa maisha ya huyo mtu mmoja, familia yake inaweza kushitaki serikali serikali ikalipa mamilioni ya dola na kuonekana haikufuata compliance ya disclosure, trasnparency na disclaimer.

Kwa hivyo wenzetu wanajua mambo haya, sisi tunaona ajabu kwa sababu tunalazimishwa na international conventions tu. Watu wetu wengi illiterate, innumerate, hawajui proportion, hawajui context, hawajui nuance, ndiyo maana disclaimer inaweza kuonekana ujinga.
Kama usemayo yana chembe ya ukweli, kwanini mamlaka ya madawa ya huko US hawaithibitishi ubora wa hizi chanjo ?

Kama kitu ni salama kwanini kisithibitishwe kwaajili ya matumizi na watu waende kuchanja !
 
Kwa nini unafikiri hivyo? Kipi kimekupa wazo hilo?

Unaelewa tofauti ya mtu anayeambukizwa Covid-19 baada ya chanjo na anayeambukizwa Covid-19 kabla ya chanjo?

Unaelewa chanjo ni nini na inafanya kazi vipi?
Kabla sijakujibu nataka nijue, unakataa kuwa mtu akichanjwa hapati Covid au vipi?
 
Uhakika ni nini? Kuna kitu kimoja unachoweza kusema kwa uhakika? Chochote kile?

FDA ukitaka kuwahoji, hata hizo zilizopitishwa kwa uthabiti utashindwa kuzihoji?

Nikikwambia sababu kwamba kuna tofauti kati ya chanjo za kawaida na chanjo za pandemic, utajua kuzielewa kwa muktadha halisi?

Uko vitani, kawaida unasubiri amri ya ku fire bullets, ukapata emergency mkubwa wako wa kukuamrisha fire hayupo, adui yuko mbele yako, utasema unasubiri mkubwa wako akuamrishe fire bullets? Au utajilinda kwa kadiri unavyoweza kwa muda huo na kuangalia itifaki nyingine baadaye?

Wewe una uhuru, kuchanja au kutochanja.

Kuna mtu kakulazimisha?
1. Vipo vitu vingi sana ninavyoweza kusema venye uhakika

2.Sioni popote ulipotoa majibu kwanini FDA hawajathibitisha uthabiti wa hizi chanjo.
 
Ni muhimu sana twende kwa proportion.

Unaelewa kwamba hakuna kitu kama "100%", kwamba hiyo ni dhana ya kinadharia tu?

Unaelewa leo watu wanasema Polio imetokomezwa kwa chanjo, lakini hilo halimaanishi kwamba hakuna mtu anayeumwa Polio leo?

Unaelewa kwamba inawezekana hiyo 5% yako ambayo inakataa chanjo inaweza kutengeneza new variants zitakayoiua hiyo 5% mpaka 5% yote ikafa na 95% ikaendelea kuishi bila kuathirika?
Hii inakataa coz hiyo 5% ikizalisha variant inayoi battle chanjo means we will be back to early 2020 era, yaan maambukizi yanaanza upyaaaa, polio iko contained coz

1-vaccine ina efficiency kubwa (sikumbuki %)

2- polio virus wana chance ndogo ya mutation
 
What is "long run" ?

The Economist John Maynard Keynes was asked about the long run, you know what was his answer?

In the long run, we all die.

Kwani ukichanjwa maana yake hutakufa?
Sizungumzii "long run" kwa maana ya "infinity", nazungumzia long term in biosafety context

Hakuna chanjo ya kutokufa, ila tunachanja tusipate au tuwe na probability ndogo ya kupata ugonjwa flani.
 
Uko vitani, unaona unalengwa na risasi, unasubiri kamati ya ulinzi ikae na kutoa itifaki ya miezi sita ya kupitishwa na majenerali zitumwe kwako kukushauri jinsi ya kukwepa risasi. Utakufa!

Soma, jielimishe, uliza pointed questions.Tutakujibu. Ukileta ubishi napo sawa tu, ni haki yako ya kikatiba.
Na wala hatuhitaji kubishana nawe sana kuku convince upige chanjo, suala la usalama wako mwenyewe.

Kama hutaki kuchanja usichanje, kwani umelazimishwa? Si Majaliwa kasema chanjo ni hiyari? Umeambiwa lazima?

Umelazimishwa kuchanja?

Mimi natetea haki za wote wanaokataa kuchanjwa wasichanjwe. Hususan kwa sababu, wanaochanjwa, so far, wanalindwa dhidi ya kuumwa na kuwa hospitalized. Wasiochanjwa ndio wanaoumwa, wanaolazwa na wanaokufa.Marekani zaidi ya 97% ya wanaolazwa hospitali ni wasiochanjwa. Zaidi ya 99% wanaofariki ni wasiochanjwa.

Inawezekana kutochanjwa kwao kutasababisha vifo vingi vya wajinga na vizazi vyao kufutika, vizazi vinavyofuata vitakuwa na wajinga wachache zaidi.

Kama unaleta ubishi kwenye jambo linalosababisha vifo, mimi siwezi kukulazimisha usikifuate kifo.

Mimi nitakuelimisha tu, ukikataa elimu sina jinsi, itabidi upigwe tu.

Na mimi wala sitakulilia, kwa sababu utakuwa umeyataka mwenyewe.
C'mon big bro,

Hebu kunywa maji kidogo, naona unaanza kupanick!

Mbona umekata upepo mapema,au sio wewe kuna mtu anatype kwenye account yako!!!
 
Uko vitani, unaona unalengwa na risasi, unasubiri kamati ya ulinzi ikae na kutoa itifaki ya miezi sita ya kupitishwa na majenerali zitumwe kwako kukushauri jinsi ya kukwepa risasi. Utakufa!

Logically sawa, ila huna uhakika wa hiyo silaha yako kama itakukinga either kwa muda mrefu, mfupi ,isikukinge au ikageuka kukuback fire pia...you have no safety & efficacy data , so you don't have any right ya kuishikia bango hii chanjo..as you always speak "no research no right to speak".
 
Soma, jielimishe, uliza pointed questions.Tutakujibu. Ukileta ubishi napo sawa tu, ni haki yako ya kikatiba.
Na wala hatuhitaji kubishana nawe sana kuku convince upige chanjo, suala la usalama wako mwenyewe.

Kama hutaki kuchanja usichanje, kwani umelazimishwa? Si Majaliwa kasema chanjo ni hiyari? Umeambiwa lazima?

Sasa si hapo juu umesema wasiochanja wanatengeneza new variants, means hata wasio chanja wanakuhusu ndo maana mmechanjwa still mnavaa barakoa nk kama ambao hawajachanja!!
 
.

Inawezekana kutochanjwa kwao kutasababisha vifo vingi vya wajinga na vizazi vyao kufutika, vizazi vinavyofuata vitakuwa na wajinga wachache zaidi.

.

What if waliochanja after a time "t" watapata serious adverse effect na kupotea wote,


Besides, kutokuchanja ndio unakua mjinga???????!!!!!!!!!
 
Hususan kwa sababu, wanaochanjwa, so far, wanalindwa dhidi ya kuumwa na kuwa hospitalized. Wasiochanjwa ndio wanaoumwa, wanaolazwa na wanaokufa.Marekani zaidi ya 97% ya wanaolazwa hospitali ni wasiochanjwa. Zaidi ya 99% wanaofariki ni wasiochanjwa.

Hizi data nazo zina walakini, what if ikawa only 2% ya wasiochanjwa ndio wamepata hiyo morbidity ya kuwa hospitalized, na only % ya waliopata morbidity ndio wamefariki then ukifanya simpo analysis ndio ukaandika ulivyo andika, mtu asipo translate vizuri data zako anaweza kufikiri 97% chances ya kulazwa na 99% ya kufa usipo chanjwa,


NB:nlifanya quick analysis kwa data za marekani mortality rate ni less than 2 kwa general population (average ya states zaid ya 5) tena humo kuna wazee, vijana wagonjwa wa immunosuppressive diseases etc!
 
Kwa nini unafikiri hivyo? Kipi kimekupa wazo hilo?

Unaelewa tofauti ya mtu anayeambukizwa Covid-19 baada ya chanjo na anayeambukizwa Covid-19 kabla ya chanjo?

Unaelewa chanjo ni nini na inafanya kazi vipi?
Mbona huko kwenu duniani, number ya maambukizi inazidi kwenda juu badala ya kushuka ilhali mmeshachanja % kubwa ya watu kuliko huku kwetu mashenzini ?
 
Ni muhimu kwenda na context na probabilities.

Yani mtu anakwambia leo wanaolazwa mahospitalini Marekani zaidi ya 97% ni wasiochanjwa, na zaidi ya 99% ya wanaokufa ni wasiochanjwa, halafu bado unakataa kuchanjwa kwa sababu hujui kesho variant gani itazaliwa? Na hapohapo unaambiwa kwamba kutochanjwa ni sababu kubwa ya variants mpya kuzaliwa? Huoni hapo kukataa chanjo kunakumaliza kwa sababu unaongeza nafasi ya kuugua na hata kufa?

Chanjo kama huku Marekani siku zote zimekuwa na disclaimer.Mimi nilivyoanza chuo niliulizwa rekodi za chanjo zangu za MMR. Sikuwa nazo. Nikachanjwa.Nilivyochanjwa nikapewa disclaimer kwamba kunaweza kutokea madhara.Hiki ni kitu cha kawaida hata kwa chanjo zilizokuwa fully confirmed.Ila, inabidi tuweke vitu katika muktadha sahihi. Kwa sababu unaweza kukataa chanjo kwa risk iliyo ndogo sana ya kukufanya uugue au ufariki, pia hapo hapo ukakubali kukaa bila kuchanjwa ukiwa na risk kubwa sana ya kuugua na kufa.

Narudia tena kusema, kuna watu wengi waliokataa chanjo wamepata ugonjwa, wamelazwa, wanalilia chanjo baada ya kuugua. Wanaambiwa chanjo haifanyi kazi hivyo, inatakiwa uchanjwe kabla hujaumwa. Wengine wanafariki.

Disclaimer si ujinga, ujinga ni kutoelewa nature ya disclaimer, kutoelewa proportionality, kutoelewa context.

Kwa jamii zetu ambazo hazijazoea kusoma disclaimer, hazijazoea nuance, hazijazoea transparency, disclaimer inaweza kuonekana ujinga.Lakini hilo ni tatizo la ujinga wa jamii, si tatizo la ujinga wa dislaimer.

Kwenye nchi legalistic kama US unaweza kutoa vaccine kwa watu milioni mia moja, akafa mtu mmoja tu.

Kama hujatoa disclaimer ambaye ingeokoa maisha ya huyo mtu mmoja, familia yake inaweza kushitaki serikali serikali ikalipa mamilioni ya dola na kuonekana haikufuata compliance ya disclosure, trasnparency na disclaimer.

Kwa hivyo wenzetu wanajua mambo haya, sisi tunaona ajabu kwa sababu tunalazimishwa na international conventions tu. Watu wetu wengi illiterate, innumerate, hawajui proportion, hawajui context, hawajui nuance, ndiyo maana disclaimer inaweza kuonekana ujinga.
Mabandiko yako ya kwenye huu uzi yangeprintiwa yakawekwa kila kona ya barabara zote za dunia nzima

Natamani watu wote duniani tupate elimu kama hii kuhusu covid vaccination hakika tungeudhibiti huu ugonjwa haraka sana

Mods wangeunganisha hizi posts wakaweka sticky mwanzoni juu kabisa ya jukwaa hili watu wasome wapate kuelimika

Your contribution is highly appreciated and extremely valuable as it may save a life or two. Keep doing this

Thank you.
 
Logically sawa, ila huna uhakika wa hiyo silaha yako kama itakukinga either kwa muda mrefu, mfupi ,isikukinge au ikageuka kukuback fire pia...you have no safety & efficacy data , so you don't have any right ya kuishikia bango hii chanjo..as you always speak "no research no right to speak".
Chanjo hazijafanyiwa research?

Unataka research ifanywe kwa miaka mingapi ili uikubali?

Na kwa miaka yote hiyo unayosubiri research ikamilike utakubali kufa kwa Corona tu kwa sababu research ya miqka kadhaa haijamalizika? Hqtq kqmq chanjo imepatikana na inafanya kazi?

Ukisubiri miaka 10 ya kuiangalia chanjo, halafu mtu akasema hiyo miaka 10 haitoshi, kwa sababu hatujui madhara ya miaka 15 na 20, utakataa hiyo vaccine?

Nishasema, kama hutaki chanjo, usichanje.

Kwani kuna mtu kakulazimisha kuchanja?
 
Sasa si hapo juu umesema wasiochanja wanatengeneza new variants, means hata wasio chanja wanakuhusu ndo maana mmechanjwa still mnavaa barakoa nk kama ambao hawajachanja!!
Mpaka sasa hakuna new variant ambayo imeshinda vaccine.

Wewe kataa chanjo utengeneze new variant tu.

Ni haki yako ya kikatiba.

Kuna mtu kakulazimisha kuchanja?

Hujanijibu swali hili.
 
Hizi data nazo zina walakini, what if ikawa only 2% ya wasiochanjwa ndio wamepata hiyo morbidity ya kuwa hospitalized, na only % ya waliopata morbidity ndio wamefariki then ukifanya simpo analysis ndio ukaandika ulivyo andika, mtu asipo translate vizuri data zako anaweza kufikiri 97% chances ya kulazwa na 99% ya kufa usipo chanjwa,


NB:nlifanya quick analysis kwa data za marekani mortality rate ni less than 2 kwa general population (average ya states zaid ya 5) tena humo kuna wazee, vijana wagonjwa wa immunosuppressive diseases etc!
Sawa.

Wewe ndiye unajua. Hizo data zina walakini.

Usichanje.

Kwani kuna mtu kakulazimisha kuchanja?

Usichanje.

Mtu akikulazimisha kuchanja nitatetea haki yako ya kukataa kuchanja.

Umekataa kuchanja, kwa sababu zako zozote zile, zenye msingi au zisizo na msingi. Hakuna wa kukuingilia katika haki yako hii. Akikuingilia mtu tutatetea haki yako hii hata kama hatukubaliani nawe kuhusu chanjo.

Tatizo liko wapi?
 
Mbona huko kwenu duniani, number ya maambukizi inazidi kwenda juu badala ya kushuka ilhali mmeshachanja % kubwa ya watu kuliko huku kwetu mashenzini ?
@Kiranga jibu hili kwanza, achana na kusema ni haki yangu kikatiba
 
Back
Top Bottom