Malengo yangu mwaka 2021 ni kuacha pombe, umalaya na ku-bet

Asee umetema yai apo nime elewa neno You tu apo. Au umetutukana [emoji16]

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
 
Una mipango mizuri ambayo itakutoa hapo ulipo na kukupeleka hatua nyingi sana mbele.

Mimi nilishaweza kutoka hapo no2, ila nikarudi tena,nikatoka tena,halafu nikarudi tena tena. Ila baadaye nikaweza kutoka mazima. Ni jambo ambalo lazima nikiri halikuwa rahisi.ninachoweza kusema Mungu mwenyewe alinishindia baada ya kumuomba msaada wa Roho Mtakatifu through maombi ya nguvu na ya kufunga.

Nilichofanya nikapata muda mwafaka wa kutafakari kwa nini vitu vya kijinga kama hivyo vinifarakanishe na Mungu wangu.kwamba niukose uzima wa milele kwa vistarehe ambavyo hata hivyo vina ni-cost financially na psycologically.

Labda ni kwambie, ni hivi utakavyotangaza kuacha uzinzi na mambo hayo yote uliyodhamilia,umetangaza vita na ufalme wa giza, atakurudishia fursa nyingi kutenda uovu. utashangaa.yaani wale wasichana uliwahi watongoza zamani wakakutosa watakutafuta wenyewe,walio kuacha wemyewe ukiwa bado unawapenda utakuta wanarudi wenyewe kukuomba msamaha ili muendelee.Kama kuna mtu ulikuwa unapata vikwazo vya kumpata utashangaa vikwazo vinayeyuka vyenyewe.inakuwa easy kumpata.

Sasa ukishatangaza hiyo vita,ujue unahitaji usaidizi wa Mungu haraka,

Nenda sehemu unapodhani wanamwabudu Mungu wa kweli kajiungamanishe hapo( Ingawa hata hapo pia unaweza pata vishawishi vya kukurudisha nyuma)
2.Jisemee moyoni mwako na kinywani mwako kwa kumaanisha kwamba umeenda hapo kupata msadaa wa kufunguliwa ktk vifungo vya dhambi(maana hivyo ni vifungo)
3.Hudhuria Ibada na uwashuhudie hao wote ambao ni marafiki zako wa zamani kwamba wewe umekata shauri,umeamua kuacha dhambi
4.Tafuta marafiki wengine wapya wanaoamini (kuwa makini hapa pia,kwa sababu wapo wanaoonekana wanaamini,kumbe ni machoni tuu)

5.Hudhuria vipindi vya ibada katikati ya wiki,pata mafundisho sahihi ya kukujenga kiimani ,sima neno la Mungu kila wakati,usisubiri jumapili tuu,sababu utapoa
6.Badilisha utaratibu wa familia yako,kwa kumweka Mungu mbele.Anza kumuweka mkeo na watoto wako karibu zaidi(sababu watakutia moyo) jitahidi katika matembezi yako uwe na mkeo kama ikiwezekana.

7.Endelea kuichukia hiyo tabia mbaya,penda kulinda huo uaminifu utakaokuwa umesha utengeneza baada ya kuwambia washikaji zako na max wako kwamba wewe umeshaacha hayo mambo.

8.Fanya yote haya kwa kumaanisha,kama ni mkristo endelea kulitumania jina La YESU,sababu linayo nguvu ya ajabu sana



Lastly,maisha yako yatabadilika mpaka kila mtu atakushangaa.uchumi wako utaimarika sana,sababu utakuwa umebarikiwa

Narudia tena,kuacha mambo hayo na mengineyanayofanana na hayo si jambo rahisi Ila pia ni jambo linalowezekana,kata shauri kwa faida yako mwenyewe.
 
Mkuu umesema ukweli mtupu. Hongera na asante
 
Sema una pumzika. [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji28][emoji28][emoji28][emoji1787]
 
Mimi binafsi swala la pombe kwakweli linanitesa sana, niko katika mchakato wa kupunguza iwe napiga Friday na Saturday tu
 
Nakushauri usiache, ila punguza kwa asilimia 50, hapo kwenye 500k utabakiwa na chenji utafanya maendeleo mengine.
 
Chagua dhambi moja iwe kipaumbele chako na ufanye sana, maana unamjazia shetani mafaili mengi wakati dhambi nyingine unafanya kidogo.
 
Watu wakiwa wamefulia wanakuwa na mawazo mazuri ngoja sasa warudi kwenye hali zao washike mahela yao watasahau kila kitu walichosema
Ha ha ha ha haha[emoji23][emoji1787][emoji1787]

Nimecheka kifala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…