Malezi ya sasa hivi ni mabovu kabisa

Malezi ya sasa hivi ni mabovu kabisa

Wazazi hamuongei na binti zenu.

Ishu sio kujiamulia hata asipojiamulia kama hana maarifa mimba atapata tu.
Ufinyu wa maarifa ndio huzalisha hizo mimba mfululu, kama baba/mama unaona aibu kumfundisha binti yako ajikinge vipi na mizagamuo usitegemee miaka hii ya technology vitisho vyako vitamzuia kupigwa pipe.

Assume unaishi jiji kama Dsm, Mwanza,Arusha eti umfukuze binti kigori wa miaka 17 utegemee atakosa pa kwenda, utaishia kumpoteza zaidi.

Maisha yanabadilika wakuu, tusipokubali kubadilika na kuzidi kusolve matatizo kizamani basi tutazidi kukuza tatizo.
Ndani ya humo Dar,Arusha, Mwanza kuna mabinti kibao wenye maadili mema na mazuri.
Suala la mtoto kuwa na tabia nzuri au mbaya haina mahusiano na anapo ishi ndo maana hata huko manyara vijijini kabisa kuna watoto wana tabia mbaya kuliko hata ya wanao ishi kwenye hiyo miji uliyo itaja.
Tabia ya mtoto huwa ina akisi ni aina gani ya wazazi alio nao.
Mtoto hutakiwi kumfundisha kuzuia mimba bali unatakiwa kumfundisha madhara ya uzinzi kwa ujumla maana hakuna ambaye alisha endekeza uzinzi akawa na mwisho mwema awe kwa mwanamke au mwanaume.
Wewe utakapo mfundisha namna ya kuzuia mimba ina maana umempa ruhusa ya kuanza kubugia map2 ambayo itamsababishia utasa ambao ni hasara kwake mara 200000000 kuliko usingo mother.
Wazazi wa siku hizi hamuwajibiki kwenye malezi ya watoto wenu mkatae mkubali.
Kingine ni karma kama ww kipindi cha ujana wako ulikuwa bingwa wa kuchezea mabinti za watu usitegemee wa kwako kubaki salama.
 
Malez ya sasa ni ovyo mtoto anakula chakula hatuliii mara kaacha kashika iki kile sebre yote inatapakaa chakula mama unasikia muache ndio kula yake

Halafu hata hawanyang'anyani chakula, wala hakuna mashtaka ya kukomba mboga. Mii siku hiyo nikiwepo home ni mwendo wa kuyakimbiza mpaka yanasema poo. Muda wa kula ni 7 - 10 min, baada ya hapo tunageukia mada nyingine
 
Mkuu kama una watoto wa kike basi wana hasara kubwa ya kupata baba kama ww.
Ww unasema watoto wa kike hawawezi kujizuia vipi kuhusu watoto wa kiume ndo wenye uwezo wa kujizuia?
Mlinzi wa kwanza wa mwili wako ni ww mwenyewe maana ndo unajua thamani yako na si kutegemea mtu ambaye mmekutana ukubwani eti akulindie thamani ya mwili wako huo utakuwa ni upumbavu wa hali ya juu.

% 95 ya masingo mother ,usingo mother wao walijitakia tena waliutafuta kwa nguvu.
Kati ya hao masingo mother wapo ambao kipindi cha ubinti wao walisha fuatwa na wanaume kibao wa maana wenye nia nzuri ya kujenga nao familia lakini waliwakataa kwa kisingizio cha hawana hisia nao sijui ni washamba alafu wakaenda kutembea na mabad boy wanyoa viduku,bodaboda,wabani sidii,wavuta bangi.
Wapo walio fuatwa na wanaume wenye nia nzuri ya kuwaowa wakawakataa badala yake wakaenda kufanya umalaya na waume za watu huku wakiwa wanajua kabisa.
Wapo masingo mother walio onywa juu ya mienendo yao na watu wazima wao wakajibu mimi nimesha kuwa mtu mzima nina uwezo wa kujiamlia.
Kinacho ponza wanawake wa siku hizi ni tamaa na uzungu wa kipumbavu na ndio maana hata baada ya kuolewa bado wanaendelexa umalaya wakati ana mme ndani.

Nyinyi wenye tabia za kuwaaminisha wanawake kuwa watatizo yao yana sababishwa na wanaume ndo waharibifu wakubwa wa wanawake wa kizazi cha sasa.
Familia za sasa zimeharibika si kwa watoto wa kiume wala wa kike kwasababu nyinyi wazazi mmeendekeza uliberali kwenye familia.
Mimi bado sijabahatika kuwa na mtoto ila nikibahatika nitajitahidi kwa kiwango changu kumlea katika namna ile ambayo nataka awe huku nikiwa najua kuna umri fulani akifikia mambo mengi yatabaki kuwa mikononi mwake na watu wengine ambao atawaamini kama ambavyo ananiamini mimi...

Ndoa ni swala la maisha na maisha ukomo wake ni kifo so before ya ukomo inatakiwa uyafurahie maisha yako so huwezi walaumu waliowakataa wanaume kwa sababu ya kutokuwapenda, mwisho wa siku Kila mtu anamachaguo yake, namimi nawapongeza kwa hilo kwa maana huwezi kujilazimisha kuishi na mtu ilimradi na wewe uonekane uko ndani ya ndoa wakati haufurahii ndoa yako... Halafu huu nao ni ukandamizaji wawazi, haiwezekani wanaume ndio wao wawe wenye machaguo pekee kuliko wanawake kwenye maswala haya ya ndoa, hata kama wanaume ndio waoaji ila Binti nae anatakiwa achague ni nani wa kuolewa nae kati ya wale wanaomfuata kwa lengo hilo.

Lakini pia umeelezea vizuri sana hapo kuanzia kumkataa mtu fulani na kwenda kumkubali mtu fulani kwa maana hii ndio ile aina ya upendo niliyoizungumzia ya kwamba mwanamke akipenda huwa anakua msikilizaji zaidi ya kuamua, na hao wanaojiita bad boys kwasababu huwa wako na swags na wanajua hawa wanawake wanataka nini ndio maana mara nyingi huwa wanawin, kwasababu mapenzi ni mchezo wa hisia zaidi kuliko akili.

And naomba nisisitize hili, siko hapa kumtetea mwanamke wala kumkandamiza mwanamume, ila nnachojaribu kusema hapa ni kwamba swala hili la kuzalia nyumbani haliwezi kuzuiliwa na mtoto wa kike pekee bali kwa wote kwa maana ya mtoto wa kike na wakiume.

So, wafunzeni hao vijana wenu wanaojiita mabad boy, wajaribu kuwalinda hao wanawake zao, kwa maana wao ndio huwa wanadrive hii game so wanachoamua wao mara nyingi huwa ni kama Sheria kwa hao wanawake na ndio mimba nyingi zinaanzia hapo.

Narudia tena, hili tatizo la kuzalia nyumbani haliwezi kupungua kama wanaume tutaamua kulikwepa na kujiona sisi hatuhusiki na kuelekeza lawama zote kwa hawa mabinti, ila tukiwajibika ipasavyo nadhani kwa sehemu kubwa sana haya mambo yatapungua.

Tujaribu kujiona na sisi pia ni sehemu ya hili tatizo halafu tuangalie namna ya kukabiliana nalo, najua umeshakua kwenye mahusiano mara kadhaa na yapo ambayo ulikua unamlaghai Binti ilihali ukijua fika hakuna future yoyote kati yenu ila upo nae kwaajiri ya kuendesha muda tu, lakini huyo Binti alikua anaamini karibia yote uliyokua unamwambia, sometimes unamlazimisha aje mfanye mapenzi hata akiwa kwenye siku zake za hatari tena bila kinga kwa kisingizio cha kumwaga nje na kwakua anakupenda na anajua wewe ndio future yake anakukubalia kwa moyo mmoja.... (Aisee hili tatizo hatuwezi kulikwepa kaka, na sitajari watu wanasemaje kwenye huu Uzi ila Mimi nitabaki na msimamo wangu ya kwamba tukubali kuwajibika ili tuwasaidie hawa mabinti) nukta!
 
Mambo yamegeuka na hapo hajaolewa, atazaa tena na mwanaume mwingine, kipindi cha nyuma wanawake wakiambiwa ni kiwanda cha kuzalisha walikuwa wanakuwa wakali, sasa saizi binti anapewa mimba, anazaa mwanaume anaingia mitini, anakuja mwanaume mwingine anaweka anasepa anakuja mwanamke mwingine naye anasepa
Mwisho wa siku mama anaondoka kwenda kuishi kwa bwana anaacha watoto wake kwa babu yao..
 
Nimelelewa na baba sijui malez ya mama Wala upendo wake japo yupo hai ila niseme Mzee ametulea kwenye malez ya kuogopa Kila kitu kwenye ukuaji wetu Sheria ziliwekwa na ukivunja unalo Tena unalo haswa saut ya baba ilituingia Hadi kwenye ubongo ukikosea au kuharibu jambo utajutia sio malez ya kidini ila malez ya kutii adabu na heshima pamoja na busara zake
Najivunia ukuaji wangu haukua na hekaheka za Dunia na ni malez naenda kuwapa watoto wangu sitataka wajifiche kwenye kivuli Cha kitu chochote sauti yangu itawaongoza wao sio Kwa mabavu Wala vitisho
 
Watoto wa siku hizi,
Ni wa kuwakabidhi mikononi mwa Mungu tu!


NIMEKUA NIKISIKIA WAZAZI WENGI WANAONGEA HIVI.
INANIPA PICHA YA MTU MZIMA ALIYEKOMAA MWILI NA VIUNGO VYA UZAZI (VIFANYIO) ILA AKILI HANA.

"mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee" (Mithali 22:6).
 
Mambo yamegeuka na hapo hajaolewa, atazaa tena na mwanaume mwingine, kipindi cha nyuma wanawake wakiambiwa ni kiwanda cha kuzalisha walikuwa wanakuwa wakali, sasa saizi binti anapewa mimba, anazaa mwanaume anaingia mitini, anakuja mwanaume mwingine anaweka anasepa anakuja mwanamke mwingine naye anasepa
Ni noma na hao watoto wanakuja kuwa machawa..
 
Watu wapo busy kutafuta pesa 24/7, unadhani wataweza kubalance kutafuta pesa na kulea watoto?
 
Mimi bado sijabahatika kuwa na mtoto ila nikibahatika nitajitahidi kwa kiwango changu kumlea katika namna ile ambayo nataka awe huku nikiwa najua kuna umri fulani akifikia mambo mengi yatabaki kuwa mikononi mwake na watu wengine ambao atawaamini kama ambavyo ananiamini mimi...

Ndoa ni swala la maisha na maisha ukomo wake ni kifo so before ya ukomo inatakiwa uyafurahie maisha yako so huwezi walaumu waliowakataa wanaume kwa sababu ya kutokuwapenda, mwisho wa siku Kila mtu anamachaguo yake, namimi nawapongeza kwa hilo kwa maana huwezi kujilazimisha kuishi na mtu ilimradi na wewe uonekane uko ndani ya ndoa wakati haufurahii ndoa yako... Halafu huu nao ni ukandamizaji wawazi, haiwezekani wanaume ndio wao wawe wenye machaguo pekee kuliko wanawake kwenye maswala haya ya ndoa, hata kama wanaume ndio waoaji ila Binti nae anatakiwa achague ni nani wa kuolewa nae kati ya wale wanaomfuata kwa lengo hilo.

Lakini pia umeelezea vizuri sana hapo kuanzia kumkataa mtu fulani na kwenda kumkubali mtu fulani kwa maana hii ndio ile aina ya upendo niliyoizungumzia ya kwamba mwanamke akipenda huwa anakua msikilizaji zaidi ya kuamua, na hao wanaojiita bad boys kwasababu huwa wako na swags na wanajua hawa wanawake wanataka nini ndio maana mara nyingi huwa wanawin, kwasababu mapenzi ni mchezo wa hisia zaidi kuliko akili.

And naomba nisisitize hili, siko hapa kumtetea mwanamke wala kumkandamiza mwanamume, ila nnachojaribu kusema hapa ni kwamba swala hili la kuzalia nyumbani haliwezi kuzuiliwa na mtoto wa kike pekee bali kwa wote kwa maana ya mtoto wa kike na wakiume.

So, wafunzeni hao vijana wenu wanaojiita mabad boy, wajaribu kuwalinda hao wanawake zao, kwa maana wao ndio huwa wanadrive hii game so wanachoamua wao mara nyingi huwa ni kama Sheria kwa hao wanawake na ndio mimba nyingi zinaanzia hapo.

Narudia tena, hili tatizo la kuzalia nyumbani haliwezi kupungua kama wanaume tutaamua kulikwepa na kujiona sisi hatuhusiki na kuelekeza lawama zote kwa hawa mabinti, ila tukiwajibika ipasavyo nadhani kwa sehemu kubwa sana haya mambo yatapungua.

Tujaribu kujiona na sisi pia ni sehemu ya hili tatizo halafu tuangalie namna ya kukabiliana nalo, najua umeshakua kwenye mahusiano mara kadhaa na yapo ambayo ulikua unamlaghai Binti ilihali ukijua fika hakuna future yoyote kati yenu ila upo nae kwaajiri ya kuendesha muda tu, lakini huyo Binti alikua anaamini karibia yote uliyokua unamwambia, sometimes unamlazimisha aje mfanye mapenzi hata akiwa kwenye siku zake za hatari tena bila kinga kwa kisingizio cha kumwaga nje na kwakua anakupenda na anajua wewe ndio future yake anakukubalia kwa moyo mmoja.... (Aisee hili tatizo hatuwezi kulikwepa kaka, na sitajari watu wanasemaje kwenye huu Uzi ila Mimi nitabaki na msimamo wangu ya kwamba tukubali kuwajibika ili tuwasaidie hawa mabinti) nukta!
Kumbe wana haki ya kuchagua wanacho kipenda?, sasa mbona uanze kulaumu wengine baada ya kupata matokeo ya walicho jiona wana haki ya kukichagua na ulicho kipenda?
Kama yeye aliona wanaume wenye nia ya kujenga familia naye hawana maana kwake bali wahuni wenye swaga ndo wenye maana kwake kwanini kuwe na lawama baada ya mavuno ya machaguo yake?
Yaani upande mahindi alafu kipindi cha mavuno ukivuna mahindi ulalamike kwa kusema ulitegemea kuvuna mchele?
Yaani ufirisike kwa sababu ya pombe uanze kuwalaumu wamiliki wa baa ni kwanini walikuwa wanakubali kukuuzia pombe?
Yeye alichagua swaga lakini kuna mabinti wenzake walichagua kuwa na kujenga familia hivyo kila mtu anakula matokeo ya alicho kipanda.

Jukumu la mzazi ni kumfundisha mtoto
jinsi ya kuwaepuka hao watu wenye mienendo mibovu na sio kuwategemea hao wenye mienendo mibovu ndo wamlinde binti yako utakuwa mpumbavu wa hali ya juu.
Jukumu la mzazi ni kuhakikisha anamfundisha namna ya kufanya maamuzi sahihi na wakati sahihi kwa ajili ya manufaa ya maisha yake.
Ni jukumu la mzazi kumfundisha mtoto wake kufanya maamuzi kwa kutumia akili badala ya hisia maana ukufanya maamuzi kwa hisia una %99 ya kufeli.

Yaani mvuta bangi asiye thamini mwili wake kila siku anaumezesha mimoshi ndo unategemea akulindie binti yako?
Muendesha boda asie thamini maisha yake anaendesha pikipiki akiwa ameninginiza miguu angani ndo atamthamini binti yako?

Wazazi wajibikeni kwenye malezi ya watoto acheni visingizio.
 
What about "men". So it's okay for them kuzaa hovyo hovyo cause hawabebi ujauzito?.. Kwa nini all the blame should be taken by women while men are the predators
Siku hizi wanawake wanajipa mimba wenyewe. Mwanaume hahusiki 😅😅😅
 
Kumbe wana haki ya kuchagua wanacho kipenda?, sasa mbona uanze kulaumu wengine baada ya kupata matokeo ya walicho jiona wana haki ya kukichagua na ulicho kipenda?
Kama yeye aliona wanaume wenye nia ya kujenga familia naye hawana maana kwake bali wahuni wenye swaga ndo wenye maana kwake kwanini kuwe na lawama baada ya mavuno ya machaguo yake?
Yaani upande mahindi alafu kipindi cha mavuno ukivuna mahindi ulalamike kwa kusema ulitegemea kuvuna mchele?
Yaani ufirisike kwa sababu ya pombe uanze kuwalaumu wamiliki wa baa ni kwanini walikuwa wanakubali kukuuzia pombe?
Yeye alichagua swaga lakini kuna mabinti wenzake walichagua kuwa na kujenga familia hivyo kila mtu anakula matokeo ya alicho kipanda.

Jukumu la mzazi ni kumfundisha mtoto
jinsi ya kuwaepuka hao watu wenye mienendo mibovu na sio kuwategemea hao wenye mienendo mibovu ndo wamlinde binti yako utakuwa mpumbavu wa hali ya juu.
Jukumu la mzazi ni kuhakikisha anamfundisha namna ya kufanya maamuzi sahihi na wakati sahihi kwa ajili ya manufaa ya maisha yake.
Ni jukumu la mzazi kumfundisha mtoto wake kufanya maamuzi kwa kutumia akili badala ya hisia maana ukufanya maamuzi kwa hisia una %99 ya kufeli.

Yaani mvuta bangi asiye thamini mwili wake kila siku anaumezesha mimoshi ndo unategemea akulindie binti yako?
Muendesha boda asie thamini maisha yake anaendesha pikipiki akiwa ameninginiza miguu angani ndo atamthamini binti yako?

Wazazi wajibikeni kwenye malezi ya watoto acheni visingizio.
Hiyo scenario ya kuvuna na kupanda sidhani kama inaweza kuingia hapo kwenye kitendo cha kumkataa au kumkatalia huyu kwasababu hajapendezwa nae na kumkubali ambae amependezwa nae, kwasababu anapomkataa huyu na kumkubali yule haimaanishi kwamba eti anajua huyu nnaemkataa ni Bora kuliko huyu nnaemkubalia na endapo ingekua hivyo sidhani kama wangejiingiza kwenye matatizo kwa hali ya kujua (ubaya wa mtu huwa hauonekani siku moja hasa mtu huyo akiwa na jambo lake ambalo bado hajatimiza huwa anageuka na kuwa malaika).

Na mengine hayo uliyoyaandika hapo sijui kwenye bodaboda mara wavuta bangi sijajua umeweka haya kwa mlengo gani ila kama umetumia hao watu ili uweze kuelezea bad boys ni watu wa aina gani basi uko wrong.

Kwa maana kuna wavuta bangi ambao ni walezi wazuri wa familia zao lakini pia kuna bodaboda ambao ni walezi wazuri wa familia zao... Bad boy ni character ambayo mtu anakua nayo ila kuvuta bangi ni starehe tu kama starehe zingine.

Na point yako ya mwisho ya kusema watu walee watoto wao waache visingizio si sawa, kwasababu mtu kupata ujauzito na kuzalia nyumbani haimaanishi wazazi wake walimlea vibaya.

Lakini pia unavyosema watoto wafunze kutumia akili na sio hisia hii nayo inaonesha ni kwa jinsi gani hauelewi namna mapenzi yanavyowork, ni wachache sana wenye uwezo wa kuzuia hisia zao au kuzishinda pale wanapopenda kiukweli.

Kuna watu wanapenda kiasi cha kupambana hata kwa kutumia resources zote walizonazo ili walikeep penzi liendelee kuwepo, na si kwamba eti hawana akili nope ila ni vile hisia za mapenzi zinapomzidia mtu huwa akili haifanyi kazi sawa sawa (ungewahi kupenda at least mara moja basi ungekielewa hiki nnachokwambia)

Kwahiyo punguzeni lawama lakini pia mkubali ya kwamba hakuna mwanamke anaejipa mimba mwenyewe, so mfunze mwanao wa kiume ili aachane na tabia ambazo umezitaja hapo juu kama kweli unaamini watu wa hivyo ndio waharibifu basi kumbe unarudi kwenye point yangu ya kwamba malezi yasiwe ya upande mmoja ila yawe kwa pande zote ili kuwapunguza hao waharibifu waache uharibifu wao.

Kama huna malengo na mtu au hauna malengo ya kulea huyo mtoto atakae zaliwa kwanini umshawishi mtoto wa mwenzio ambae amekuamini mfanye mapenzi bila kinga? Halafu baada ya hapo unamkimbia na zigo la lawama lote unamuacha nalo yeye.

Kama mnavyojikinga na ukimwi basi pia hivyo hivyo mjikinge na mimba hasa mkijua bado hamko tayari kuwa baba. Ukifanya hivyo hakuna mwanamke atakae kulazimisha na endapo atafanya hivyo basi unatakiwa umsaidie kwa maana hapo kwake zitakua ni hisia badala ya akili.
 
Ndani ya humo Dar,Arusha, Mwanza kuna mabinti kibao wenye maadili mema na mazuri.
Suala la mtoto kuwa na tabia nzuri au mbaya haina mahusiano na anapo ishi ndo maana hata huko manyara vijijini kabisa kuna watoto wana tabia mbaya kuliko hata ya wanao ishi kwenye hiyo miji uliyo itaja.
Tabia ya mtoto huwa ina akisi ni aina gani ya wazazi alio nao.
Mtoto hutakiwi kumfundisha kuzuia mimba bali unatakiwa kumfundisha madhara ya uzinzi kwa ujumla maana hakuna ambaye alisha endekeza uzinzi akawa na mwisho mwema awe kwa mwanamke au mwanaume.
Wewe utakapo mfundisha namna ya kuzuia mimba ina maana umempa ruhusa ya kuanza kubugia map2 ambayo itamsababishia utasa ambao ni hasara kwake mara 200000000 kuliko usingo mother.
Wazazi wa siku hizi hamuwajibiki kwenye malezi ya watoto wenu mkatae mkubali.
Kingine ni karma kama ww kipindi cha ujana wako ulikuwa bingwa wa kuchezea mabinti za watu usitegemee wa kwako kubaki salama.
Mzeebaba umeibugia kama ilivyo..
Mimi sikumaanisha kukaa nae kumfundisha kuzuia mimb pekee.

Na pia sikumaanisha mikoa tajwa ndio yenye watoto wenye tabia mbovu ila ni kua mjini vishawishi ni vingi na njia illegal za binti kusurvive ni nyingi pia.
 
Yaani saa hii ni shida. kuna moja ilitokea huyo singo maza alikuwa na watoto wawili moja wa kike na mwingine wa kiume huko kanda ya ziwa. Wakubwa wote wako chuo kikuu. Sasa mara binti kabebeshwa mimba huko chuoni. Kapambana, kajifungua baada ya muda fulani mtoto kaachiwa bibi, yaani mama wa binti, ili binti aendelee na masomo. Mara baada ya muda fulani, naye wa kiume akabebesha mimba binti huko chuoni alikokuwa anasoma. Wakalea mimba kimya kimya, mara yule binti wa watu akajifungua. Sasa ukitaka kujua hawa watoto vichwa vibovu, naye akapanga na mzazi mwenzake kwamba mtoto tukamuache kwa maza, bila hata kumuonea huruma kwamba mama yao ni singo maza. Basi kijana akawa anampigia mama yake, "halo mama shikamoo, kuna mjukuu wako namleta hapo home". Mama naye "mjukuu wangu yupi?". Kuna binti nasoma naye ndiyo tumezaa. Maa akamchenjia. "Huyo mjukuu simjui, kaeni naye nyie wenyewe". Lile likijana lilivyo lijinga, likaanza kusema, mbona mtoto wa dada yangu uko naye. kwa nini unamkataa huyu mtoto wangu. Mama akasema hiyo mimi sijui. Likijana lile lilvyo lipuuzi likajiua. Likamuachia mama yake majonzi yasiyopimika. Hao ndiyo aina ya watu wanaoitwa gen-zii, yaani ni zii kweli
changamoto sana
 
Back
Top Bottom