Uchaguzi 2020 Mama Salma Kikwete achukua fomu ya kuwania kuteuliwa kugombea jimbo la Mchinga kupitia CCM

Kuna mtu anauliza eti huyu mama yupo singo kwa sasa? Yumkini anatafuta ubunge ili aweze kuendesha maisha yake kivyake maana hela za wanaume si za kutegemea😜😜😜😜😜 Anyway shikamoo mama, ukatutetee huko mjengoni ili tujiajiri tusitegemee ajira
 
Inafikirisha sana, kwa umri wake alitakiwa atulie nyumbani ajitunzie heshima yake, sasa aaenda kuoambana na watoto huko bungeni
Kwa sasa ameshaonja utamu wa siasa(apart from being a first lady) naona amenogewa sasa.
 
Kujiajiri nyie wanyonge ndio mnapaswa mjiajiri.
 
Sheria ya kugombea ubunge ibadilishwe ikiwa ni pamoja na umri wa kugombea maana naona wazee safari hii wamekomaa
Hahah wazee watamaindi kishenzi.

Hivi mkuu kwa hio huyo mama akipita kwny mchujo mume wake(JK) atakua nae anakuja kupanda jukwaani kumnadi sio?
 
Iswali gumu sana kujibu, labda Riziwani
Hahah wazee watamaindi kishenzi.

Hivi mkuu kwa hio huyo mama akipita kwny mchujo mume wake(JK) atakua nae anakuja kupanda jukwaani kumnadi sio?
 
Hii inaonyesha mumewe hawezi kum-controll/kumpiga stop mipango anayotaka kufanya mkewe,wote wawili ni short-sighted au wanamjaribu mwenyekiti.

Nadhani mumewe angemwambia hapana hapana, acha kabisa sasa, hata ile tokea mwanzo, mtu umekuwa First Lady for 10 yrs, unahangaika hangaika na ubunge ya nini? Haya umepewa ubunge bure viti maalum 5 years, bado unang'ang'ana ya nini? Kuna tatizo mahali lazima
 
Kila lenye kheri mama.Nafurahi watu wanavyochukua form.Demokrasia inakua.

Demokrasia inakua? Huku tumeshatahadharishwa kuhusu watakaopata na kukosa; hata idadi ya viti kwa kila chama imepangwa! Mwenyewe unaona jinsi watu wanavyoikimbia CHADEMA kama kirusi cha covid 19 chenyewe. We’ll see.
 
Ni kukosa Shukrani pia kwa miaka hio 5 aliyopewa kwa heshima ya mumewe.
 
Nyie wachangiaji humu mitazamo yenu midogo sana. Kugombea kwa huyu mama si kwa sababu anataka ubunge. Hapo kuna zaidi ya ubunge.
 
twende kazi twende kazi . . ngoja na bado maana wengine nawa-zoom tu kwa mbali wakienda kuchukua fomu kwa bodaboda
 
Anajidhalilisha tu
 
ni haibu kwa mama aliyekaa ikulu miaka 10, kwenda kudhalilishwa jukwaan kwa ajili ya ubunge! saa nyingine muwe mnaridika nakuwaachia wengine nao wale.
 
Acha aingie ulingoni apewe matusi ya kutosha/achafuliwe kwa sana tu ndipo atapata akili vizuri.

Wamekalia kuwaambia watoto wa maskini wajiajiri lkn wao kutwa kulilia ubunge.

Mkuu naona bado unafikiri safari hii kampeni zitafanya kama zamani. Hakuna mgombea wa CCM atakayetukanwa au kudhalilishwa na upinzani. Hujastukia ziara za Siro zinazoendelea kuhamasisha “amani na utulivu” wakati wa uchaguzi. Na kampeni zimeshaanza tayari.

Jua safari hii wagombea wa upinzani hasa CDM wameandaliwa vichapo vya uhakika kila watakapoonyesha hata mbwembwe tu (acha matusi) kwenye mikutano yao ya kampeni. Itakuwa ni mwendo wa kushushwa majukwaani, vichapo, selo, na kupumzishwa (suspension) hadi wajue safari hii wanaotakiwa kusikika pekee na kueleweka ni kina nani. Very hard times are coming.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…