Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huyu mama angetulia tu nyumbani na Rais Mstaafu Jakaya ingetosha, ameshakaa ikulu kama First Lady kwa miaka 10 na hatimaye kama mbunge wa kuteuliwa kwa miaka mitano. Ridhiwani anatosha kuweka alama ktk familia sasa ktk familia.Salma Kikwete ambaye ni Mke wa Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete amechukua fomu ya kuwania kuteuliwa kugombea ubunge Jimbo la Mchinga mkoani Lindi kupita Chama cha Mapinduzi (CCM).
Wakumbushwe kutia nia nafasi za udiwani pia. Sio wote wanataka ubunge tu.watia nia wamekuwa wengi kushinda hata wapiga kura jamani au mnaonaje?
Kuna watu bila vyeo vya kisiasa wanajiona hawajakamilika.Sina chuki na mama lakini ukweli lazima usemwe, akichaguliwa yeye ni upotevu wa nafasi bure tu.
Mama angeweza kufanya mambo mengine na mataasisi yao akaachia wengine hiyo nafasi ya bungeni.
Kwanza yeye na mumewe wote wanapata huduma za serikali vizuri tu hana njaa ya pesa.
Kama anajiona bado kijana hapendi kukaa hivi hivi angejikita hata kwenye miradi ya kilimo na ufugaji ya familia. Watu wenye mitaji na mitandao (Business network connections) kama hawa ndio hufaa kuonesha mfano wa kufanya biashara kubwa za kusafirirsha nje bidhaa au mazao ya kilimo na ufugaji kwenda nje ya nchi. Huko atazalisha ajira nyingi sana.
Siasa awaachie wanawe akina Ridhiwan a.k.a Riz-moko (Riz1).
Wanazidi kukusanya kura za kusini. Nasikia muna chama kinadai kura za kusini ni za kwaoSalma Kikwete ambaye ni Mke wa Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete amechukua fomu ya kuwania kuteuliwa kugombea ubunge Jimbo la Mchinga mkoani Lindi kupita Chama cha Mapinduzi (CCM).
Kazi gani Bill Gates anayofanya ya kutafuta pesa hivi sasa?Mkuu Ingekuwa hivyo akina billgate wasingekuwa wanaumiza vichwa kutafuta pesa,moyo wa binadamu ni shimo kubwa lisilolizika
Bill Clinton alifanya..... si kitu ya ajabu.Hahah wazee watamaindi kishenzi.
Hivi mkuu kwa hio huyo mama akipita kwny mchujo mume wake(JK) atakua nae anakuja kupanda jukwaani kumnadi sio?
Angegombea kwa ticket ya CDM angeshinda.Salma Kikwete ambaye ni Mke wa Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete amechukua fomu ya kuwania kuteuliwa kugombea ubunge Jimbo la Mchinga mkoani Lindi kupita Chama cha Mapinduzi (CCM).
Acha fikra potofu mkuu, watu wanaoamini mtu hutafuta nafasi ya uongozi ili kujipatia pesa hafai kuwa kiongozi.Sina chuki na mama lakini ukweli lazima usemwe, akichaguliwa yeye ni upotevu wa nafasi bure tu.
Mama angeweza kufanya mambo mengine na mataasisi yao akaachia wengine hiyo nafasi ya bungeni.
Kwanza yeye na mumewe wote wanapata huduma za serikali vizuri tu hana njaa ya pesa.
Kama anajiona bado kijana hapendi kukaa hivi hivi angejikita hata kwenye miradi ya kilimo na ufugaji ya familia. Watu wenye mitaji na mitandao (Business network connections) kama hawa ndio hufaa kuonesha mfano wa kufanya biashara kubwa za kusafirirsha nje bidhaa au mazao ya kilimo na ufugaji kwenda nje ya nchi. Huko atazalisha ajira nyingi sana.
Siasa awaachie wanawe akina Ridhiwan a.k.a Riz-moko (Riz1).
Kwani shida itakuwa wapi?Kuna watu bila vyeo vya kisiasa wanajiona hawajakamilika.
Usishangae akajifanya Hilary Clinton kutaka kugombea urais.