Mama yangu angeni-abort wakati bado niko tumboni mwake, angekuwa amenifanyia wema mkubwa sana

Mama yangu angeni-abort wakati bado niko tumboni mwake, angekuwa amenifanyia wema mkubwa sana

Balqior

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2021
Posts
2,406
Reaction score
8,039
Mama yangu angenitoa na kunitupilia mbali kipindi bado niko kwenye tumbo lake la uzazi, ingekuwa ni faida kubwa sana kwangu, ningejihesabia mwenye bahati sana, sababu nisingekuwa na haja ya kuja Duniani na kupitia mateso, usaliti, hofu, Karaha za kila namna, magonjwa, e.t.c kisha mwisho wa siku dini zinakwambia ukiteleza kidogo kwenye dhambi unaenda kuchomeka motoni milele baada ya kufa.

Kutokana na maisha na majaribu tunayopitia hapa Duniani, sisi binadamu uwezekano wa kwenda motoni baada ya kifo ni mkubwa kuliko kwenda mbinguni. Hii Dunia sio nzuri kabisaaaa, kiuhalisia ni mbaya mno na inatisha sana.

Kungekuwa na uchaguzi wa kuja Duniani au kutokuja duniani kabla ya kuzaliwa, mimi ningekataa katu katu kabisa kuja Duniani.

Najiuliza Mungu anafaidika nini kwa kutuumba sisi binadamu? Alivyotuumba amefaidika nini, na asingetuumba angepungukiwa nini? Yeye si muweza wa yote, amejikamilisha kwa kila kitu? Anatuhitaji sisi binadamu kwa ajili gani? Je, anafurahi sana kuona binadamu kila siku tunavyomkasirisha kwa dhambi, tunavyoteseka na tunavyorukaruka na sarakasi za hapa Duniani?

NB: Sina mawazo ya kujiua, na kwa sasa sina shida kubwa sana ninazopitia, maana kutokana na hii post kuna wengine watafikiria nitachukua maamuzi hayo ya kujiua, wengine watafikiria sasa hivi nina matatizo makubwa sana napitia ndio maana nimeandika hii post, la hasha, siwezi jiua maana najua ntakakoenda baada ya kujiua ni kubaya zaidi ya hapa Duniani. Mimi nimewaza tu.
 
Mama yangu angenitoa na kunitupilia mbali kipindi bado niko kwenye tumbo lake la uzazi, Ingekuwa ni faida kubwa sana kwangu, Ningejihesabia mwenye bahati sana, sababu nisingekuwa na haja ya kuja duniani na kupitia mateso, usaliti, hofu,
Okoka mkuu......usikute Hilo Ni pepo linakukatisha tamaa

Kemea pepoooo
 
Mama yangu angenitoa na kunitupilia mbali kipindi bado niko kwenye tumbo lake la uzazi, Ingekuwa ni faida kubwa sana kwangu, Ningejihesabia mwenye bahati sana, sababu nisingekuwa na haja ya kuja duniani na kupitia mateso, usaliti, hofu,
Hali mbaya sana mtaani. Mama afanye wepesi, bado kidogo tu watu waanze kuongea peke yao mabarabarani
 
Kuhusu dunia kua ni mbaya au nzuri, inategemea na hali yako. Kuna watu wanatamani kufa wakati wowote waondoke tu hapa duniani. Na kuna watu hawatamani hata kuzeeka, wanatamani waishi milele. Kwaio usiilalamikie dunia, jilalamikie mwenyewe, kama unahitaji ushauri tuambie tutakusaidia
 
Mama yangu angenitoa na kunitupilia mbali kipindi bado niko kwenye tumbo lake la uzazi, Ingekuwa ni faida kubwa sana kwangu, Ningejihesabia mwenye bahati sana, sababu nisingekuwa na haja ya kuja duniani na kupitia mateso, usaliti, hofu,
Huna shukrani, si kwa mama yako aliyekubeba miezi tisa tumboni mwake na kukuzaa kwa uchungu mwingi, wala Muumba wako aliyekupa neema ya uhai na pumzi ya kuja kuandika ulichokiandika.

Malalamiko yako yote hayana maana. Mungu akuhurumie tu!
 
Mama yangu angenitoa na kunitupilia mbali kipindi bado niko kwenye tumbo lake la uzazi, Ingekuwa ni faida kubwa sana kwangu, Ningejihesabia mwenye bahati sana, sababu nisingekuwa na haja ya kuja duniani na kupitia mateso, usaliti, hofu,
Kumbuka hayo mawazo yako ni huyo Mungu ndiye aliyekupa uhuru na ubongo huo unaotumia kutiririka haya maoni yako, kumbuka wanyama ambao wanao uhai kama wewe kamwe hawawezi kutiririka jinsi wewe ulivyotiririka, je hujiulizi tofauti yako wewe na mnyama ni ipi??, kwanini ushindwe hata kutoa shukrani kwa Mungu kukuumba mtu unayejitanbua??.

Falsafa ya adhabu sikuvya hukumu ipo hivi; Mungu mwenye huruma na upendo ni zaidi ya mzazi kwa mtoto wake, mtoto anapougua mzazi humtafutia mwanaye dawa hata kama ni chungu ilmradi tu mtoto wake apone, ni hivyohivyo Mungu kwa mtu, ile "adhabu" siku ya kiyama ni sawa na dawa chungu anayopewa mkosefu ili apone maradhi yake ya rohoni kutokana na madhambi aliyofanya akiwa duniani na adhabu ya siku ya kiyama sio ya milele bali ni ya muda.

Mrefu kulingana na wingi wa madhambi yako, baada ya adhabu kumalizika mtu hatimaye ataruhusiwa kuingia peponi kwenye raha ya milele raha ambayo hatapewa kiumbe yeyote isipokuwa mtu tu, je wewe huoni kuumbwa kwako uwe mtu badala ya mnyama au kiumbe mwingine ni Mungu kakupa upendeleo?

Basi inatakiwa umshukuru Mungu kwa jambo hilo na mitihani ya kimaisha ni njia ya kukufanya wewe umkumbuke Mungu kwa kumuomba msaada ili shida zako ziondoke kwani bila hivyo binadamu ni wasahaulifu sana, basi tumuabudu Mungu na tumshukuru kwa kila hali.
 
Back
Top Bottom