Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike

Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike

Pesa ya ada,ya michango,ya kanisa,ya dhamana ogopa sana do try this Zina laana Huwa hazirudi ukisema chomoa kidogo
 
Labda zamani siku hizi unampaje mwanafunzi akalipe Ada, nenda nae bank au kwa wakala mpe risiti apeleke shule
 
Labda zamani siku hizi unampaje mwanafunzi akalipe Ada, nenda nae bank au kwa wakala mpe risiti apeleke shule
Mimi wakati nasoma nimepewa sana ada hadi milioni na sikuwahi kula hata 100
 
CHAPTER 10

kumbuka aunty alikuwa na matatizo ya pressure na mashetani kuna siku mmoja akapandisha ikabidi tumpeleke kwa sheikh mmoja hivi ambae ni jirani yetu mitaa ya kigogo hapo.

yule sheikh alikuwa na tatizo mmoja anasoma soma madua yake weeeeeh alafu anatulia hivi kama anazima nadhani yale madudu yake yalikuwa yanamtuliza hivi.

sasa baada ya aunty kutulia lakini kalala hapo tumemfunika na kanga na sheikh kukaa sawa uncle si akaanzisha mada kuwa kuna sehemu yeye anaijua na kuna mada kazisikia kuna shimo linatoa madini.

ila hiyo sehemu ipo Mkoa X ndani ndani huko, sheikh akaingilia mada akasema yeye hiyo ndoto kashawahi kuiota kuwa kaongozana na watu wawili waenda kufata madini sehemu lakini yeye hajui ni sehemu gani wala sura za ao watu usingizini hakuzijua ni za kina nani ila alikuwa anaongea nao ila sura zao hakuzijua ni za kina nani.

INAENDELEAAAA....

Mada hiyo ikafa tukamchukua aunty tukarudi nae nyumbani. lakini yoyote ya yote ile mada pale kuwa kuna sehemu kuna madini kila mtu ilimchanganya akili hivi.

kwa maelezo ya mjomba kuwa huyo mtu wa kwanza kupata ayo madini alikuwa anachimba shimo la choo. dakika ya mwisho akakutana na kitu kama kigae hivi.

so aliingia hofu ila akampa mtu ambae anaenda mjini akaulizie ni nini kile kitu kwa masonara baada ya kufika mjini sasa yule jamaa aliyetumwa akaanimbiwa kweli yale ni madini.

kwahiyo akarudi kijijini tena akamshitua jamaa wakabeba na kigae kingine wakaenda kuuza mjini now jamaa ni tajiri mkubwa tu Dar es salaam.

na habari ikatapakaa kuwa sehemu fulani kuna mali habari nzuri utembea haraka serikali ikapata taarifa kwahiyo watu wakapigwa marufuku hata kusogea lile eneo lakini ndio kijijini ndani ndani uko.


hiyo story mwanzo kabisa mimi mwenyewe sikuiamini amini hivi niliona kama mjomba anatufunga kamba ila baada ya kujikuta nina shida ya pesa ya ada ya kwenda chuo na fursa nilipewa pesa ikaisha kwa jimama.

nikaona acha na mimi nijitoe sadaka tu. so siku kama ya jumamosi mimi mjomba na yule ostadh tukatoka zetu dar es salaam mpaka mkoa X tulifika kule kama mida ya saa 11 jioni hivi.

ila mjomba alitoa wazo kuwa tukae pale stand kwanza kila mtu amalize aja yake kabisa mwenye kutaka kula akale mwenye kujisaidia na pia kila mtu anunue maji yake hajisaidie hapo kila mtu mgongon ana jembe lila bila mpini sururu, panga na torch.

maana safari ya kwenda uko kwenye hilo shimo hakuna magari usafiri pekee ambae unaweza kumfikisha mtu uko ni bodaboda ila kwa vile tunaends kufanya inshu za magendo itabidi twende kwa miguu tu hakuna kuchukua bodaboda.

tukaa pale stand saa 1 tukaanza kuupiga mguu sasa kuelekea uko kijijini. uko tulipokuwa tunaenda ni mbali sana yani tulikuwa tunapiga story njiani mpaka ikafikia hatua sasa kila mtu akabaki kimya. ila safari ilichukua kama mda wa masaa manne hivi mpaka tunafika kule kijijini.

tukafika ikabidi kwanza tupumzke kama dakika kadhaa alafu tutafute miti kwa ajili ya kutengeneza mipini ya jembe.

ili iwe inatusaidia wakati tunachimba lile shimo uwenda na sisi tukabahatika kupata japo kipande cha kigae cha dini tuje mjini kula kiki kwa mrija.

tukapata miti ya mipini fresh kumbuka tupo kijijini lakini porini sana na hiyo ilikuwa kama mida ya saa 5 usiku hivi.

kijijini kimetulia na nyumba moja ipo hapo nyingine ipo mbali sana kama kilometres mbili hivi hadi tatu.

ostadh akatoa wazo kuwa kabla hatujaingia mule shimoni kuanza kazi lisomwe dua maana mara nyingi mambo ya mali mali majini nao hawachezi mbali anaweza akaingia mtu shimoni likamvaa jinu ikawa mtihani sasa na kule ni porini hakuna msaada wa mtu.

vuta picha kutoka hapo mpaka stand kwa miguu ni masaa manne sasa unadhani itakuwaje au nani ataweza kumbeba mtu masaa yote yao sindo munajuikuta mpaka asubuhi mupo njiani tu wana kijiji wanakuja kuwakamata kirahisi.

ostadh akapiga visomo vyake soma soma somaaaa weeeeh. dakika ya mwisho tukamuona kazima katulia tuli tukajua mambo teyali sasa sisi wawili mimi na mjomba tuzame shimoni moja aende chini mwengine akae juu kucheck usalama.

daaah hatari katika lile eneo tulikutana na mauza uza ya ushirikina na uchawi hatari. pale wakati tunachimba kuna mda tunasikia kama sauti za watu hivi wanakuja kwahiyo fast sana tunatoka tunaenda kujificha alafu ukichungulia hakuna watu wala nini.

mukienda tena kinatokea kituko kingine mara musikie kama mwanamke analia hivi yani sauti fulani hivi kama mwanamke kapigwa alafu analia.

yani tulichimba kidogo tu tukaona hapa pazito tuondokue haraka sana.

Tuliondoka lakini mipango yetu tukae siku kadhaa turudi tena kule kijiji kujaribu bahati yetu kwa round ya pili.

Daaah hii round ya pili ndo ilikuwa ngumu zaidi kuliko ile ya kwanza.

Gusa hapa kupata muendelezo [emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
Post in thread 'Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike' Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike
Very interesting
 
Katika kitu ambacho najisifu mpka leo ni kupita salama kipindi cha utotoni na kipindi cha mihemuko cha form 2,3,4,5&6 bila kudinywa...hapa watu watakataaa hahaha [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38]
Hongera kama ni kweli
 
CHAPTER 12

mguu kwa mguu mpaka kwa mganga tukamkuta mganga yupo macho anafanya tiba tiba zake kuna moto unawaka pale nje kwake lakini pia tulimkuta mwanamke nadhani yule ni mkewe nilimjua kama mkewe baada ya story story hapo mbele lakini pia tulimkuta mwanamke jimama la nguvu jeupe limekaa pale pembeni ya moto hivi.

kichwani nywele zipo wazi ana kitambaa cheusi kajifunga kama taulo kiunoni hivi lakini kifuani yupo wazi kabisa. yani kifua kinaonekana kabisa mitindi unaiona ile pale.

siku hiyo baada ya kuliona lile tukio ndo nikaamini kama uchawi upo na wanawake wanapenda ushirikina kuliko hata wanaume....


INAENDELEAAAA....

Lile tukio liliniogopesha kiasi fulani hivi ila ilinibidi nijikaze tu maana ndo tumleta mgonjwa tena.

wakati mganga akiendelea endelea na tiba zake nilikuwa nasikiliza maongezi yake akiwa kapandisha na lile jimama jeupe lililo nusu uchi.

Katika maongezi yake na mganga nilitambua kuwa lile jimama shida zake ni mbili na ndo maana yupo pale kwa mganga shida ya kwanza alikuwa naitaji mtoto ndoa yake ina kama miaka 17 hivi lakini hakubahatika kupata mtoto na manyanyaso na maneno yamekuwa mengi sana upande wa mumewe.

Lakini pia mganga alimwambia kuwa amelogwa lakini mganga akasita kidogo akamuuliza vipi unataka kumjua aliyekuroga akasema

"Ndio namtaka kumjua"

Jibu lilotoka kuwa aliyemroga ni mama yake mzazi. Lile jimama alikushtuka sana kivile maana sijui kama lile janamke sio dangaji la mjini.

Mambo yao yakaendelea weeeh mda uo me na uncle tunatazama mchezo tu lile jimama likamaliza tiba na yule mganga likavaa nguo zake hilo likaondoka zake. Kabla hakujapambazuka vizuri.

Inshu sasa ikabaki upande wetu na ostadh. Kuna mda nilijaribu kumshauri mjomba kuwa tusiseme tulienda wapi mpaka mwenzetu akakutwa na tatizo tuseme tu kuwa tulikuwa tunawahi gari ya asubuhi tukakutana na tatizo ila dakika ya mwisho uncle akuwa upande wangu alipoulizwa imekuwaje kuwaje.

Ikabidi aseme tu kuwa tulikuwa tunatoka kule shimoni kunakosadikika kuna madini.

Mganga akasema " imekuwa vizuri kusema ukweli lakini tiba ya huyu mwenzenu inahitaji vifaa na vifaa vinahitaji pesa na laiti kama mungesema mumkimbize hospital basi hata uko hospital musingefika nae angekufa njiani , huyu mda huu kuna mdudu kamvaa mwilini ... Akuishua hapo tu akatupa na kisa kinachofanana na chetu kuwa kuna mtu hapo hapo kijijini alishawahi kukutwa na madhira kama ayo.

Jamaa alikuwa na balaa watu wakajua kashafika akaswaliwa fresh maana alikuwa muislam ila dakika ya mwisho pale kaburini wanataka kumfukia sasa jamaa akapiga chafya... Lakini maamuzi yaliyotoka kuwa watu wapeleke mchanga chini tu haina jinsi"

Daaaah hapo akili sasa nadhani ndo ilizidi kupagawa maana tulipanga tunaenda mkoa X kijiji X kwa kwenda na kugeuza lakini sasa tunaambiwa tutulie siku kadhaa mpaka mwenzetu apone.

Uncle akatoa pesa baada kidogo akatoka na mganga sikujua wameenda wapi ila walivyorudi warirudi na vitu vya kiganga ganga hivi.

Mimi wakati wanatoka nilikuwepo na mke wa mganga tukawa tunapiga story story za hapa na pale kuhusu mazingira ya pale kijijini kiujumla. Katika maongezi yetu kuna mda akapigiwa simu kuna mtu akaongea nae huyo mtu nilisikia anamuita "MAMA SOMOE"

Kwa maongezi yao nilisikia kama mama somoe anataka kuja siku ya pili yake kuja kuwatembelea lakini pia kwa ajiri ya matatizo ya mtoto wake ambae ni Somoe.

Ujue sikujiuliza sana huyo MAMA SOMOE ni nani nilidhani ni mtu wa kawaida tu lakini jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza.

Uncle akarudi na mganga mda uo ostadh yupo ndani ya banda la udongo tu. kalala tu mda wote.

baada ya kurudi na vifaa mganga alisema kuwa tiba ya ostadh itafanyika usiku lakini pia mkewe amuandalie chai mapema sana kwa ajiri ya usiku wakati wa tiba.

usiku ukafika bhana mganga akaimba imba nyimbo zake weeeh akishiriana na mkewe akawa anaitiki tu. akapandisha akaongea ongea mambo mengi sana lakini dakika ya mwisho akatoa maelezo kuwa kama tutataka kwenda tena shimoni basi twende kwake kwanza kupata dawa akataja na dawa kadhaa kwa ajiri ya ostadh inshu ya ostadh kiupande mmoja ikawa teyal imeshaisha tunasubiri apate nafuu tu tusepe mjini.

Sasa mida kama ya saa 4 asubuhi hivi inakimbilia saa 5 nipo na uncle hapo mda uo tukasikia mlio wa bodaboda mda uo sisi tulikuwa tumekaa tunapiga story nyuma ya nyumba ya mganga kwahiyo ilikuwa ngumu kumjua ni nani aliyekuja na bodaboda.

daaah kuna mambo yasikie tu kuna ile kauli inasema binadamu wanakutana ila milima ndo akiukutani ni ya kweli 100%.

ile nimenyanyuka naenda kunywa maji uso kwa uso na NAA tena round hii akiwa kabeba mtoto moyo ulipiga paaaaah kushituka na akili ikanijia fast kuwa inawezekana Naa ndio MAMA SOMOE mwenyewe ambae alikuwa anaongea na mke wa mganga siku ya jana.

Ndani ya mda mfupi nilipatwa na maswali kama yote hivi

nilijiuliza

1. NAA ATAREACT VIPI BAADA YA KUONANA NA MIMI ?

2. LAKINI IMEKUWAJE ANA MTOTO ?

3. MTOTO KAZAA NA NANI ?

4. VIPI KUHUSU SHULE ?

Gusa hapa kupata muendelezo 👇👇👇
Post in thread 'Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike' Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike
 
Back
Top Bottom