Ali Nassor Px
JF-Expert Member
- May 6, 2022
- 2,384
- 3,926
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tuko pamoja 🤜🤜🤜🤜Bado nipo naendelea kuweka kambi hapa
Hilo shangazi lako lilikuwa halina hela,akati majimama huwa yanalea vijana[emoji2]Aaaah usinicheke mie omba tu na ww yasikukute
We jamaa ni msenge [emoji23][emoji23]CHAPTER 6
Ali : ila sikia nina shida mmoja naomba unisaidie, naomba nasra akae kwako japo siku mbili hivi ili nifanye utaratibu kwa arudi kwao kwa sababu pesa ya kulala guest kwa sasa sina.
Cosmas akanitazama akanijibu: hapana hilo siwezi kukusaidia
Ali: why sasa hauwezi kunisaidia na wakati ulisema mwanzo kuwa nikitaka kusepa nikuachie nasra
Cosmas : nilikuwa nakutania, kwanza dogo anaonekana mgonjwa akizidiwa tena au likitokea la kutokea nampeleka wapi , cha pili wewe unamjua mwenye nyumba yule bi mkubwa jau kichizi mtu wa dini dini, kuna mpangaji juzi tu kaamisshwa kisa kaleta demu mchana kweupe na bi mkubwa kamuona huyo demu wa jamaa. kwahiyo wewe force force dogo harudi kwao tu.
INAENDELEAAA.....
Naa baada ya kupigwa dripu zote tatu na kupata nafuu kidogo ikabidi nirudi nae lodge lakini kumbuka mda wote hapo natumia pesa ya ada na hapo teyali nishaiteketeza kama laki 3 na 70 hivi na shilingi shilingi hivi.
Ikabidi nimdanganye kuwa jamaa yako bado hajanitafuta nadhani jamaa mzinguaji sana yule. Lakini mwanzo nipo hospital pale nakumbuka kuna mda yule jamaa yake naa alinipigia simu.
Akaniuliuliza " yule msichana aliyekuazima simu yuko wapi au alishuka wapi"
Nikamwambia" aaaah kiongozi sijui maana mimi nililala sasa inawekana alishuka kwenye gari wakati amelala so itakuwa mtihani kidogo kujua yupo wapi au alishukia wapi ? "
Jamaa alilalamika sana yani sana [emoji23][emoji23][emoji23][emoji16]. Kuwa Naa mjini mgeni alafu jamaa likawa nalo linanidanganya eti ni mdogo wake.
Mae mdogo wako unaweza kumuoa kumuweka unyumba.
LWakati naendelea kuongea na Naa ikabidi sasa nimshawishi arudi kwao tu.
Ali: Sikia Naa ujue maisha aya yana misukosuko mingi sana ila yote ya yote matatizo yanapotokea tunatakiwa tujifunze kupitia matatizo na sio kulaumu watu au kujilaumu sisi."
Kama kitu kimetokea ndo kishatokea , mimi kesho nasepa shule nakaa hostel na kesho pia ndo tunafungua shule nakushauri urudi kwenu tu kwenu ni kwenu jiji la dar es salaam gumu sana kuna matukio mengi sana ya kutisha unaweza ukauliwa alafu kwenu wasijue hata kama umekufa sasa mimi nataka nikupe msaada mmoja nataka nikukatie tiketi ya bus la mkoa X urudi kwenu".
Naa alikuwa ananijibu kwa kutikisa kichwa yani dogo alikuwa anaumwa anaumwa kweli tofauti ya mwanzo alikuwa kazidiwa sana lakini baada ya zile dripu kidogo alipata uafueni.
utaratibu wangu maisha ambao nilijipangiaga mimi mwenywe week ya kwanza kufunguliwa shule siende na hata dada yangu alikuwa anajua, mara nyingi nilikuwa najitete week ya kwanza ni week ya usafi usafi tu hakuna masomo.
Naa akakubali fresh kurudi kwao sasa kidume nikawa nawaza nafanyaje lakini mda uo mfukoni nina kama laki 1 na 30- hivi, nikasema aaaah acha niitumie alafu nitapiga vizinga kwa dada na bro watanipa tu.
jumatatu jioni nikatoka nae nikaenda nae ubungo nikamkatia tiketi ya kwenda kwao ilikuwa ni shilingi elfu 45. jumatano ndo alikuwa anasafiri.
jumatano imefkia nikamsindikaza mpaka stand nikampandisha gari nikampa na elfu 30 ya kula njiani hapo kidume nazidi kula pesa ya ada tu.
lakini nadhani hapa kwenye kumpandisha gari alafu mimi nikasepa nadhani nilifanya kosa mmoja kubwa sana maana miaka kama miwili mbele nilikuja kuoanana tena na Naa akiwa na mtoto tena mtoto mwenyewe wa yule jamaa wa mbezi mwisho.
ilikuwaje kuwaje mpaka nikakutana nae na ilikuwa wapi na nilifata nini. tuendelee kusoma story.
Naa akapanda bus mimi nikasepa kwa dada kumbuka natakiwa kwenda shule na nilipe ada siku hiyo hiyo jioni mama akanipigia simu akaniuliza umeshalipa ada nikamjibu ndio mama nishalipa ada yote hapo mfukoni nika kama elfu 55 tu .
sema baada ya kumjibu ndio hakuniuliza kitu maana mama yangu alikuwa hana kawaida ya kuulizia ulizia mambo ya risiti.
Sasa kidume nikawa nawaza hii pesa nairudisha vipi. nimemfata sister kumwambia nina shida ya elfu 50 kuna kitu nataka kununua akanitolea nje sijui hana pesa akili yake haipo sawa mambo ya upatu yanamchanganya.
hapo kichwa kinaniuma balaa nikaona hapa kwa sister hapanifai. not safe ninja naweza nikajinyonga mda wowote [emoji23][emoji23][emoji23]
Kipindi nasoma form five na six nilikuwa nimepanga ghetto na marafiki zangu kama watano hivi mitaa ya Kurasini kule sasa wakati naenda ghetto nikawa na mawazo sana.
marafiki zangu wawili walikuwa wanabet sana
kuna rafiki yangu mmoja akauliza vipi mbona una mawazo sana ikabidi nimwambie tu kilichonitokea chote.
Akaniambia "Daaah wewe MSE#@₹E ni jambazi alafu umeyakanyaga yani umejipiga kisu cha kiuno wewe mwenyewe sasa hapo itabidi tubet tu".
nikamwambia " sasa tunafanyaje nitengenezee mkeka"
akaniuliza " kwani haujui kubet "
nikamwambia " mimi sijui " .
akanitengenezea mikeka miwili mkeka wa kwanza anakitengenezea mikeka miwili mkeka wa kwanza ulikuwa wa elfu 20 mwengine wa elfu 10.
Mkeka wa elfu 20 mapema tu ukachanika. ukabaki wa mkeka wa pili wa elfu 10 ukabaki nao niliubettia team moja ya kwanza dakika 40 za kwanza tu teyali ilikuwa ishafungwa goal tatu.
ikabidi nizime simu mda uo jasho linanitoka ikabidi nizime simu nilale kwanza.
Gusa hapa kupata muendelezo [emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
Post in thread 'Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike' Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Ostadhi mzima anazidiwa nguvu na mgodi [emoji23][emoji23]CHAPTER 11
daaah hatari katika lile eneo tulikutana na mauza uza ya ushirikina na uchawi hatari. pale wakati tunachimba kuna mda tunasikia kama sauti za watu hivi wanakuja kwahiyo fast sana tunatoka tunaenda kujificha alafu ukichungulia hakuna watu wala nini.
mukienda tena kinatokea kituko kingine mara musikie kama mwanamke analia hivi yani sauti fulani hivi kama mwanamke kapigwa alafu analia.
yani tulichimba kidogo tu tukaona hapa pazito tuondoke haraka sana.
Tuliondoka lakini mipango yetu tukae siku kadhaa turudi tena kule kijiji kujaribu bahati yetu kwa round ya pili.
Daaah hii round ya pili ndo ilikuwa ngumu zaidi kuliko ile ya kwanza.
INAENDELEAAAA...
Tulifika mpaka mjini hapo mimi nawaza madini tu lakini kiupande mwengine naona kama fix.com hivi.
na vituko vya kule shimoni ndo nikawa sipati majibu kabisa. tukakaa mjini kama week mbili hivi sasa tukaamua kurudi tena mimi ostadh na mjomba. round hii tulisema lazima turudi na madini.
tukatoka zetu Dar es salaam. mpaka mkoa x safar yetu mda ni ule ule kule kwenye shimo mpaka stand ya mjini ni mwendo wa masaa minne kwa miguu.
tofauti ya round hii na round ya kwanza round hii tulianza kusoma dua tukiwa tupo huku huku Dar es salaam. tukapanga tukifika tena tunasoma dua then kazi inaanza fast fast.
lakini pia round hii hatutorudi stand kuna sehemu tutaenda ni kijiji cha pili jirani kuna mtu mjomba anajuana nae tutaenda kulala hapo mpaka asubuhi. ikifika asubuhi tutaanza safari yetu sasa ya kurudi mjini.
lengo la kwenda kulala kijiji jirani na sio porini ni kuwa tusikutwe na raia wa kijiji pale asubuhi. maana lile eneo limepigwa marufuku kuchimbwa.
kwahiyo tukapiga mguu mpaka kijijini pale shimoni tukakata miti kwa ajli ya mipini kama kawaida. dua zikaanza pale ostadh kama kawaida yake dua dua mwisho wa siku akazima ikabidi sasa mimi na mjomba tuiingie shimoni.
jamani kupata utajiri ni kazi ngumu sana na ukisikia kuna utajiri unapatikana kiurahisi rahisi tu basi unatakiwa ujifikilie mara mbili sheria ya pesa siku zote kila inavyozidi kuwa nyingi na maumivi yake pia yanakuwa makubwa.
piga sululu piga jembe piga sululu piga jembe hiyo mida ya saa 5 usiku inakimbilia saa 6 vituko vikaanza mara tusikie sauti za mtoto mchanga mara mwanamke analia kama ana kwikwi hivi.
tunatoka shimoni tunatazama huyo mwanamke na mtoto wako wapi sasa alafu tukitazama kweupe hakuna kitu wala nini.
tunaingia tena shimoni tunafanya kazi kidogo tu.vituko vinaanza upya mara tusikie sauti kama watu wanakuja hivi tukichomoka shimoni hakuna mtu anae kuja wala nini kiufupi usiku ule siwezi kuusahau katika maisha yangu mpaka kifo changu.
inafika mida ya saa 9 usiku tukamuasha ostadh tusepe. akatuuliza mumepata chochote jibu la mjomba " hatujapata kitu kama tulivyokuja ndo tunavyoondoka "
ostadh alitikisa kichwa akasema " hapa pazito sana sijui kama kafara lake haijavuja damu ya binadamu"
mjomba akauliza " kafara la binadamu kivipi"
ostadh akajibu " inawezekana kana hapa haliuliwa binadamu ili kulinda hizi mali zilizopo hapa yani hapa inawezekana munafanya kazi lakini munafumbwa macho nyie mwenyewe hamujui munachokifanya"
mjomba na ostadh waliongea ongea sana dakika ya mwisho ikabidi tusepe tu. sasa njiani wakati tunatembea kuna mda tukamuona ostadh kama kasimama hivi alafu akatuambia tupiteni njia za maporini huku barabarani leo inaonekana pazito sana.
aaah sisi hatukuweza kumpinga. tembea tembea ostadh akasema " munajua kwanini tumewaambia tupite njia za porini"
tukamjibu " tujui kwanini"
hakasema hamuwezi kuamini nimemuona mtu analoga yupo uchi wa mnyama". ostadh mda uo anaongea maneno hayo lakini anatetemeka yani hayupo katika hali ya kawaida kabisa.
yani anatetemeka kama mtu ambae kakamatwa na baridi kweli kweli. anatetemeka mpaka meno ya juu na ya chini yanagong'ana.
"mjomba akasema " sikia ali wewe beba begi la vifaa , mimi nambeba ostadh nadhani hayuko sawa hapa bado hatua kidogo tufike kijiji tunachoenda "
nikamwambia mjomba " sawa lakini si bora tujikaze twende na ostadh mjini maana huko tunapoenda kijiji cha pili hakuna hospital wala nini "
jibu halonipa mjomba " aya mambo mengine hayaitaji hospital ukimchoma mgonjwa sindano tu ndo ushamuua mazima mambo ya Kiswahili yanamalizwa kiswahili swahili tu"...
ostadh hali yake ilikuwa haieleweki kabisa kuna mda anakuwa sawa kuna mda anaanza kutetemeka mpaka tunafika iko kijiji tukichokuwa tunaenda. imeshafika saa 10 usiku.
kuna nyumba flani hivi ya udongo mjomba akaenda kupiga hodi mda uo mimi nimekaa pembeni nasoma mchezo tu.
baada ya kupiga hodi kama tatu hivi akatoka jamaa na kibukita kashika tochi mkononi na panga alivyomuona tu mjomba aaakacheka sana nadhani yule mtu alikuwa anajuana na mjomba baada ya yule jamaa kucheka mjomba nae akacheka waliongea ongea sana dakika ya mwisho akamueleza kuwa tupo na mgonjwa mwenzetu hayupo sawa tunahitaji msaada wake.
yule mtu akaja akamtazama ostadh akasema huyu kwa hali ilivyo tumpeleke KWA KOMBO ( sio jina halisi la muhusika ). huyo kombo ni mganga wa kienyeji mda huu sasa ikawa jamaa ndo kambeba ostadh hiyo safari sasa tunamuwaisha ostadh kwa mganga.
huku tunampeleka mgonjwa lakini pia story za hapa na pale zinaendelea.
nikamuuliza " mjomba ushawahi kusikia story ya yule mganga aliyejinyonga baada ya kutapeliwa "
mjomba alicheka sana akasema " acha hizo mada sasa hivi sio mda wa kuongea hizo mada zako"
mguu kwa mguu mpaka kwa mganga tukamkuta mganga yupo macho anafanya tiba tiba zake kuna moto unawaka pale nje kwake lakini pia tulimkuta mwanamke nadhani yule ni mkewe nilimjua kama mkewe baada ya story story hapo mbele lakini pia tulimkuta mwanamke jimama la nguvu jeupe limekaa pale pembeni ya moto hivi.
kichwani nywele zipo wazi ana kitambaa cheusi kajifunga kama taulo kiunoni hivi lakini kifuani yupo wazi kabisa. yani kifua kinaonekana kabisa mitindi unaiona ile pale.
siku hiyo baada ya kuliona lile tukio ndo nikaamini kama uchawi upo na wanawake wanapenda ushirikina kuliko hata wanaume....
ITAENDELEAAAA...
Hata mm nasibanduki [emoji23]Bado nipo naendelea kuweka kambi hapa
We nae 😂😂😂😂Koh koh koh......! Mmhm! Fegi hizi...
Khe khe khe ....Eeh Mhmn!We nae 😂😂😂😂
Wazazi wakitengana wanaoumia ni watoto,kina Na wapo wengi sana kwenye jamiikuna watu wanapitia magumu,,,,mama huyo dogo Naa anaona bora kutoroka home akaolewe sio jambo dogo hilo ujue🤦♀️