Nourhan
JF-Expert Member
- Apr 7, 2023
- 1,196
- 3,026
Poa nita ku tagAisee mbona hatuitani huku...mwala peke yenu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Poa nita ku tagAisee mbona hatuitani huku...mwala peke yenu
Huwezi amini sioni tags now days...
PoleHuwezi amini sioni tags now days...
Thanx dear
HatariiiiCHAPTER 9
baada ya kuandika barua nikaambiwa nitoke staff nimsubiri mama na sister wanaongea na teacher lakini mda natoka nje pale nje nikakutana na mjomba..
mjomba aliniambia " mjomba umeyatafuta matatizo"
nikamjibu " mjomba sijayatafuta matatizo ila matatizo yamenitafuta mimi ila najutia sana na naona nimemkosea mama na familia kiujumla "
mjomba akaniambia kitu kimoja ambacho kilinishtua kidogo " tulia mjomba yangu mambo madogo tu haya tunayamaliza na umenifurahisha sana[emoji16][emoji16][emoji16]"
INAENDELEAAAA....
nikamuuliza kwanini mjomba lakini hakunijibu akarusha mada. na mpaka upleo hii ajanipa jibu nimemfurahisha kivipi.
lakini baada ya mama na sister kutoka ikabidi sisi sote tuongozane nyumbani kwa sister na mjomba pia akiwemo.
kufika kikao kikaanza mda uo nina barua yangu safi kabisa ya suspension. mama mda uo alikaa kimya tu sister ndo alikuwa ananisema sana.
maamuzi yaliyotoka kuwa nitafutiwe tution niwe naenda kusoma ili kufidia mda wa suspension nisikae bure bure tu lakini pia nikaambiwa kuhusu maisha ya ghetto niyasahau sitoruhusiwa tena kwenda kukaa kule. so nitakaa kwa sister lakini mjomba akaomba mimi nikakae kakwe.
hilo alikuwa alikupigwa hata na mtu mmoja lakini acha niwaambie mjomba alikuwa na mtoto wa kiume mmoja tu anaitwa Sadamu gape la miaka baina ya mimi na sadamu ni tofauti kama ya miaka 2 hivi sadamu ni mdogo kwangu.
lakini sadamu ni mtukutu balaa japo baba mdogo anakipato kidogo coz anapoga kazi manispaa anakusanya kusanya ushuru masokoni.
enzi hizo alipambana sana sadamu asome lakini ilikuwa kinyume chake sadamu alikataa shule mapema sana.
mjomba kwanza alimpeleka shule hizi za kata za kawaida performance ya sadamu ikawa ovyo akampeleka shule ya msingi bunge lakini alipofikia form 1 akaacha shule kabisa akasema akasema anataka mtaji wa pesa afanye biashara yoyote ile.
mjomba akampotezea akaona toto pimbi ili akampotezea dogo kusugua sugua mtaani akaanza kutumia bangi ,mara anaiba ndani pesa ndefu alafu aonekani miezi, mara siku nyingine halali nyumbani.
dakika ya mwisho likatoka wazo asomewe dua akasomewa dua fresh tu.
sasa likaja na wazo kuwa kama vipi apelekwe veta kuna mtu mjomba anajuana nae wanampokea kiujanja ujanja hivi bora sadamu asome japo ufundi kuliko kumpa biashara wakati dogo sana anaweza kutia hasara biashara yote msingi akaonga na mtaji akalewea.
So, baada ya kikao kuisha me nikaenda zangu maghetto nikasepa zangu kwa mjomba na swala la deni la ada mjomba akasema sister na mama waachane nalo analilipa yeye na hiyo pesa ya tution atalipa yeye pia.
kufika kwa mjomba nikakutana na mjomba , aunty na sadamu mwenyewe sadamu mdomo mweusi balaa yani kawa bangi mtu.
kitu ambacho niligundua mjomba kutaka nikakae kwake, kuwa anataka sadamu na mimi tukae karibu labda mimi naweza nikamshawishi sadamu na yeye akapenda shule kiasi fulani. daaaah kilichotokea ni kitu tofauti kabisa.
Sadamu aliuliwa kwa tukio la kupora bodaboda.
siku hiyo nakumbuka sadamu ajarudi nyumbani kama siku 2 hivi siku aliyorudi tukaonana fresh sema alikuja kama mnyonge mnyonge hivi sio kawaida yake kabisa .
akaja tukaongea ongea sana tu dakika ya mwisho akasema " oi me natoka tena "
nikamjibu " fresh"
akaondoka zake siku hiyo mjomba na aunty walikuwa wameenda shughulini, kwahiyo baada ya sadamu kuja tukawa wawili ila baada ya kuondoka nikajikuta nyumba nzima nipo peke yangu.
mida ya saa 3 au 4 hivi hivi, mjomba anakuja kuniamsha kuwa kuna matatizo yametokea niaamka fresh kwenda kumsikiliza.
inshu ya sadamu kuuliwa alianza kuniambia mimi kabla ya kumuambia aunty, tukitoka nje tukaenda kukaa sehemu ya mbali kidogo na nyumbani lakini pia akutoka yeye tu lakini pia simu ya aunty aliichukua akanipanga inshu nzima kuwa sadamu kashauliwa inasemakana kachomwa moto yeye na mwenzake mitaa ya kitunda huko.
daaah ile siku niliudhunika sana.
kwanza niliudhunika kwa mambo mawili ndo siku ya kwanza kumuona mjomba akilia kile kilio chenye uchungu mzito ndani yake lakini pia kumpoteza sadamu ambae mchana nilikuwa nae na kauli ya mwisho aliniambia " natoka".
mjomba aliongea sana na alilia sana kama mzazi ila tutafanya nini sasa na jambo lishatokea lakini pia kuna mda hauwezi kupindisha mipango ya mungu.
kuna mda utatamani kutoa msaada kwa mgonjwa lakini mgonjwa hawezi kumeza dawa hata kama una huruma kiasi gani hauwezi kumeza dawa wewe ili yeye hapone.
Aunty mkewe mjomba alikuwa na matatizo mawili yanamsumbua sana cha kwanza alikuwa na pressure lakini cha pili mashetani.
mjomba akaniambia kuwa mimi nibaki nyumbani na aunty ila nisimwambie kitu chochote aunty mpaka mwili ufike kwa vile mda ule aunty kalala nisimuamshe ila akiamka kama akija kwangu nisimwambie chochote kile kilichotokea.
kweli bhana aunty hakuamka japo kuna siku alisema kuwa siku ile waliyoenda harusini mchana kitovu kilikuwa kinamvuta sana.
maiti ilikuja home yani daaah kuna mambo sikieni sadamu alikuwa kachomwa moto ile kaungua kikweli kweli vuta picha binadamu kachomwa mtoto alafu ukimshika hivi ile nyama yake anabanduka kama nyama ya ngombe yenye mafuta mengi iliyoiva sana.
kiufupi tu ilikuwa ngumu sana kumtazama mara mbili mbili, hata kuosha mwili wake ilikuwa ngumu nani sasa unadhani anakubali kuosha binadamu kachomeka moto anatokota mafuta kiasi kile. tulimzika bila hata kumuosha na kumkafini
yani siku zote nikimkumbuka sadamu mood inakata kabisa nikikumbuka alivyoniaga nikikumbuka nilivyouona mwili wake uliochomwa moto.
mpaka leo hii aunty hayupo sawa kabisa tunaishi nae tu lakini daaah.... wakina mama wanapitia magumu mengi sana.
life lilienda nikamaliza form 6 fresh tu nikiwa nasubiri matokeo ya form 6 kwenda chuo nikachaguliwa kwenda JKT KIGOMA.
nikaona jau kwenda JKT mjomba akaniambia niende nikapige nae kazi ya kukusanya ushuru soko la vietnal na tandika me.nilikuwepo upande wa tandika kwa mwezi nilikuwa napata kama laki 3 hivi, kaa kaa pale sokoni nikajikuta naingia kwenye penzi la mama ntilie jimama moja hivi jeupe lina lafudhi ya kizanzibar lina watoto 3 moja alikuwa darasa la 3 mwengine form 2 lakini huyu alubahatika kumaliza alipigwa mimba na mwengine alikuwa yupo form 4.
iki kisa nitawasimulia siku nyingine lakini nilionga mpaka mashati mawili ya shule na viatu, nikawa namlipa kodi hapo kumbuka mimi ni dogo tu hapo lakini nina date na limama lenye miaka kama 40 hivi.
piga piga kazi matokeo yakatoka nimefaulu natakiwa ni apply chuo. lakini mda uo pesa ya chuo sina yani licha ya kukusanya laki 3 kila mwisho wa mwezi. lakini nilijikuta kama nina laki 3 na nusu tu, na hapo sokoni teyal nishapiga kazi kama miezi 4 hivi.
kumbuka aunty alikuwa na matatizo ya pressure na mashetani kuna siku mmoja akapandisha ikabidi tumpeleke kwa sheikh mmoja hivi ambae ni jirani yetu mitaa ya kigogo hapo.
yule sheikh alikuwa na tatizo mmoja anasoma soma madua yake weeeeeh alafu anatulia hivi kama anazima nadhani yale madudu yake yalikuwa yanamtuliza hivi.
sasa baada ya aunty kutulia lakini kalala hapo tumemfunika na kanga na sheikh kukaa sawa uncle si akaanzisha mada kuwa kuna sehemu yeye anaijua na kuna mada kazisikia kuna shimo linatoa madini.
ila hiyo sehemu ipo Mkoa X ndani ndani huko, sheikh akaingilia mada akasema yeye hiyo ndoto kashawahi kuiota kuwa kaongozana na watu wawili waenda kufata madini sehemu lakini yeye hajui ni sehemu gani wala sura za ao watu usingizini hakuzijua ni za kina nani ila alikuwa anaongea nao ila sura zao hakuzijua ni za kina nani.
Gusa hapa kupata muendelezo[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
Post in thread 'Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike' Mama yangu mzazi aliwahi kuniambia bora nife tu apumzike
Aaaah usinicheke mie omba tu na ww yasikukuteMkuu jimama lilikupurusa ada[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
😁😁😁😁😁Duuuuuh history
Leo sitokusahau nitakupa tagsHuwezi amini sioni tags now days...
Thanx dear
Yah wana tunazama chini ya ardhi kuufata utajirNi muda wa kuchimba madini🔦⛏️⛑️
Shukrani sana Allii leo nipo on mapema sanaaa... !!
Nasikia migodini kuna mauzauzaa balaaa....!!CHAPTER 11
daaah hatari katika lile eneo tulikutana na mauza uza ya ushirikina na uchawi hatari. pale wakati tunachimba kuna mda tunasikia kama sauti za watu hivi wanakuja kwahiyo fast sana tunatoka tunaenda kujificha alafu ukichungulia hakuna watu wala nini.
mukienda tena kinatokea kituko kingine mara musikie kama mwanamke analia hivi yani sauti fulani hivi kama mwanamke kapigwa alafu analia.
yani tulichimba kidogo tu tukaona hapa pazito tuondoke haraka sana.
Tuliondoka lakini mipango yetu tukae siku kadhaa turudi tena kule kijiji kujaribu bahati yetu kwa round ya pili.
Daaah hii round ya pili ndo ilikuwa ngumu zaidi kuliko ile ya kwanza.
INAENDELEAAAA...
Tulifika mpaka mjini hapo mimi nawaza madini tu lakini kiupande mwengine naona kama fix.com hivi.
na vituko vya kule shimoni ndo nikawa sipati majibu kabisa. tukakaa mjini kama week mbili hivi sasa tukaamua kurudi tena mimi ostadh na mjomba. round hii tulisema lazima turudi na madini.
tukatoka zetu Dar es salaam. mpaka mkoa x safar yetu mda ni ule ule kule kwenye shimo mpaka stand ya mjini ni mwendo wa masaa minne kwa miguu.
tofauti ya round hii na round ya kwanza round hii tulianza kusoma dua tukiwa tupo huku huku Dar es salaam. tukapanga tukifika tena tunasoma dua then kazi inaanza fast fast.
lakini pia round hii hatutorudi stand kuna sehemu tutaenda ni kijiji cha pili jirani kuna mtu mjomba anajuana nae tutaenda kulala hapo mpaka asubuhi. ikifika asubuhi tutaanza safari yetu sasa ya kurudi mjini.
lengo la kwenda kulala kijiji jirani na sio porini ni kuwa tusikutwe na raia wa kijiji pale asubuhi. maana lile eneo limepigwa marufuku kuchimbwa.
kwahiyo tukapiga mguu mpaka kijijini pale shimoni tukakata miti kwa ajli ya mipini kama kawaida. dua zikaanza pale ostadh kama kawaida yake dua dua mwisho wa siku akazima ikabidi sasa mimi na mjomba tuiingie shimoni.
jamani kupata utajiri ni kazi ngumu sana na ukisikia kuna utajiri unapatikana kiurahisi rahisi tu basi unatakiwa ujifikilie mara mbili sheria ya pesa siku zote kila inavyozidi kuwa nyingi na maumivi yake pia yanakuwa makubwa.
piga sululu piga jembe piga sululu piga jembe hiyo mida ya saa 5 usiku inakimbilia saa 6 vituko vikaanza mara tusikie sauti za mtoto mchanga mara mwanamke analia kama ana kwikwi hivi.
tunatoka shimoni tunatazama huyo mwanamke na mtoto wako wapi sasa alafu tukitazama kweupe hakuna kitu wala nini.
tunaingia tena shimoni tunafanya kazi kidogo tu.vituko vinaanza upya mara tusikie sauti kama watu wanakuja hivi tukichomoka shimoni hakuna mtu anae kuja wala nini kiufupi usiku ule siwezi kuusahau katika maisha yangu mpaka kifo changu.
inafika mida ya saa 9 usiku tukamuasha ostadh tusepe. akatuuliza mumepata chochote jibu la mjomba " hatujapata kitu kama tulivyokuja ndo tunavyoondoka "
ostadh alitikisa kichwa akasema " hapa pazito sana sijui kama kafara lake haijavuja damu ya binadamu"
mjomba akauliza " kafara la binadamu kivipi"
ostadh akajibu " inawezekana kana hapa haliuliwa binadamu ili kulinda hizi mali zilizopo hapa yani hapa inawezekana munafanya kazi lakini munafumbwa macho nyie mwenyewe hamujui munachokifanya"
mjomba na ostadh waliongea ongea sana dakika ya mwisho ikabidi tusepe tu. sasa njiani wakati tunatembea kuna mda tukamuona ostadh kama kasimama hivi alafu akatuambia tupiteni njia za maporini huku barabarani leo inaonekana pazito sana.
aaah sisi hatukuweza kumpinga. tembea tembea ostadh akasema " munajua kwanini tumewaambia tupite njia za porini"
tukamjibu " tujui kwanini"
hakasema hamuwezi kuamini nimemuona mtu analoga yupo uchi wa mnyama". ostadh mda uo anaongea maneno hayo lakini anatetemeka yani hayupo katika hali ya kawaida kabisa.
yani anatetemeka kama mtu ambae kakamatwa na baridi kweli kweli. anatetemeka mpaka meno ya juu na ya chini yanagong'ana.
"mjomba akasema " sikia ali wewe beba begi la vifaa , mimi nambeba ostadh nadhani hayuko sawa hapa bado hatua kidogo tufike kijiji tunachoenda "
nikamwambia mjomba " sawa lakini si bora tujikaze twende na ostadh mjini maana huko tunapoenda kijiji cha pili hakuna hospital wala nini "
jibu halonipa mjomba " aya mambo mengine hayaitaji hospital ukimchoma mgonjwa sindano tu ndo ushamuua mazima mambo ya Kiswahili yanamalizwa kiswahili swahili tu"...
ostadh hali yake ilikuwa haieleweki kabisa kuna mda anakuwa sawa kuna mda anaanza kutetemeka mpaka tunafika iko kijiji tukichokuwa tunaenda. imeshafika saa 10 usiku.
kuna nyumba flani hivi ya udongo mjomba akaenda kupiga hodi mda uo mimi nimekaa pembeni nasoma mchezo tu.
baada ya kupiga hodi kama tatu hivi akatoka jamaa na kibukita kashika tochi mkononi na panga alivyomuona tu mjomba aaakacheka sana nadhani yule mtu alikuwa anajuana na mjomba baada ya yule jamaa kucheka mjomba nae akacheka waliongea ongea sana dakika ya mwisho akamueleza kuwa tupo na mgonjwa mwenzetu hayupo sawa tunahitaji msaada wake.
yule mtu akaja akamtazama ostadh akasema huyu kwa hali ilivyo tumpeleke KWA KOMBO ( sio jina halisi la muhusika ). huyo kombo ni mganga wa kienyeji mda huu sasa ikawa jamaa ndo kambeba ostadh hiyo safari sasa tunamuwaisha ostadh kwa mganga.
huku tunampeleka mgonjwa lakini pia story za hapa na pale zinaendelea.
nikamuuliza " mjomba ushawahi kusikia story ya yule mganga aliyejinyonga baada ya kutapeliwa "
mjomba alicheka sana akasema " acha hizo mada sasa hivi sio mda wa kuongea hizo mada zako"
mguu kwa mguu mpaka kwa mganga tukamkuta mganga yupo macho anafanya tiba tiba zake kuna moto unawaka pale nje kwake lakini pia tulimkuta mwanamke nadhani yule ni mkewe nilimjua kama mkewe baada ya story story hapo mbele lakini pia tulimkuta mwanamke jimama la nguvu jeupe limekaa pale pembeni ya moto hivi.
kichwani nywele zipo wazi ana kitambaa cheusi kajifunga kama taulo kiunoni hivi lakini kifuani yupo wazi kabisa. yani kifua kinaonekana kabisa mitindi unaiona ile pale.
siku hiyo baada ya kuliona lile tukio ndo nikaamini kama uchawi upo na wanawake wanapenda ushirikina kuliko hata wanaume....
ITAENDELEAAAA...
Tuko pamoja sana mwanzo mwisho 🤜🤜🤜Shukrani sana Allii leo nipo on mapema sanaaa... !!
Nsona Kitruu bado chamotroooo kabesaaa
Mauza uza mitaa ya kwao yalipozaliwa ni migodini na sehemu yoyote ile yenye maliNasikia migodini kuna mauzauzaa balaaa....!!
Ngoja niendelee kusoma!