Mambo tata matatu, Uteuzi wa Jaji Kiongozi Siyani

Mambo tata matatu, Uteuzi wa Jaji Kiongozi Siyani

Mama sijui ana mataizo gani! Kulikua kuna ulazima gani wa kufanya uteuzi wakati mchakato wa kesi ukiendelea?
Kwa hiyo kesi ikichukua mwaka na jamaa asipande cheo kwa muda wote huo? Kumbuka mpaka sasa wapo kwenye kesi ndogo kesi ya msingi aijaanza kusikilizwa
 
Kipi
Uteuzi wa Jaji Siyani kuwa Jaji Kiongozi una sura tatu tata sana.

1) Ikiwa Jaji Kiongozi Mh Siyani atalazimika kuachia Jaji mwingine hii kesi ya Mh Mbowe, Athari za kuteuliwa jaji mwingine kwenye kesi hii ni kwamba ajaye anaweza kutoa maamuzi kwaniaba ya mamlaka za uteuzi ili nae apendelewe kupata ulaji wa ujiaji kiongozi... Hi ni dhana yangu tu tata.

(2) Ikiwa Jaji Kiongozi Siyani licha ya kuteuliwa kuwa Jaji Kiongozi ataendelea kusikiliza kesi ya Mh Mbowe, Upande wa Pili wa dhana yangu tata nikwamba, athari za Jaji Siyani anayesikiliza kesi hii ikiwa maamuzi yatakuwa kinyume na "UMMA", itatafsiriwa kwamba kapata asante kuwa jaji Kiongozi kabla hata kazi haramu ambayo mteuaji alishahukumu mbele ya dunia kupitia BBC Swahili hajaimaliza.

(3) Na kwa asilimia ndogo sana ikiwa Jaji Kiongozi Mh Siani ataendelea kusikiliza kesi kama kawaida, inaweza kuwa sasa ni ahueni kwa "umma" kwakuwa Jaji kiongozi atakuwa huru zaidi kuamua kwa haki bila hofu ya kuingiliwa tofauti na awali alipokuwa jaji wa mahakama kuu tu.

Kwa mizani hii mitatu na kwa asili ya siasa za kiutawala za Dar es Salaam, tuendelee kupiga magoti kila mtu kwa imani yake haki itendeke na ionekane kutendeka.

Na Yericko Nyerere
View attachment 1968603
Je kipi cheo kikubwa kati ya jaji mkuu wa Zanzibar na jaji wa mahakama ya rufaa Tanzania
 
Kuna mambo kama huyajui bora kuuliza tu kwa wanaojua ndugu. Yaani hoja unazotaka kulazimisha hapa sioni jinsi zitakavyoathiri utendaji wa Jaji. Judges wote wanateuliwa na huyo huyo Rais, yaani hoja zako hapa zinaonekana kuwa ni kituko tu. Strangely kuna watu bado wataona umeandika vitu vya maana kumbe ni pumba tupu
 
Uteuzi wa Jaji Siyani kuwa Jaji Kiongozi una sura tatu tata sana.

1) Ikiwa Jaji Kiongozi Mh Siyani atalazimika kuachia Jaji mwingine hii kesi ya Mh Mbowe, Athari za kuteuliwa jaji mwingine kwenye kesi hii ni kwamba ajaye anaweza kutoa maamuzi kwaniaba ya mamlaka za uteuzi ili nae apendelewe kupata ulaji wa ujiaji kiongozi... Hi ni dhana yangu tu tata.

(2) Ikiwa Jaji Kiongozi Siyani licha ya kuteuliwa kuwa Jaji Kiongozi ataendelea kusikiliza kesi ya Mh Mbowe, Upande wa Pili wa dhana yangu tata nikwamba, athari za Jaji Siyani anayesikiliza kesi hii ikiwa maamuzi yatakuwa kinyume na "UMMA", itatafsiriwa kwamba kapata asante kuwa jaji Kiongozi kabla hata kazi haramu ambayo mteuaji alishahukumu mbele ya dunia kupitia BBC Swahili hajaimaliza.

(3) Na kwa asilimia ndogo sana ikiwa Jaji Kiongozi Mh Siani ataendelea kusikiliza kesi kama kawaida, inaweza kuwa sasa ni ahueni kwa "umma" kwakuwa Jaji kiongozi atakuwa huru zaidi kuamua kwa haki bila hofu ya kuingiliwa tofauti na awali alipokuwa jaji wa mahakama kuu tu.

Kwa mizani hii mitatu na kwa asili ya siasa za kiutawala za Dar es Salaam, tuendelee kupiga magoti kila mtu kwa imani yake haki itendeke na ionekane kutendeka.

Na Yericko Nyerere
View attachment 1968603
Athari kubwa zaidi ya Jaji kuteuliwa kuwa JK ni kwamba kesi hii itaenda taratibu sana.

Atakuwa na majukumu ya kiutawala ambayo ni mengi sana hivyo kesi haitasikilizwa mfululizo tena.

Hii kesi kama Jaji kiongozi ataendelea nayo itaisha 2023.
 
Kuna mambo kama huyajui bora kuuliza tu kwa wanaojua ndugu. Yaani hoja unazotaka kulazimisha hapa sioni jinsi zitakavyoathiri utendaji wa Jaji. Judges wote wanateuliwa na huyo huyo Rais, yaani hoja zako hapa zinaonekana kuwa ni kituko tu. Strangely kuna watu bado wataona umeandika vitu vya maana kumbe ni pumba tupu
Pumba ambazo imekulazimu uzisome na kuweka pumba kubwa zaidi ya zile zilizowekwa mwanzo!

Haya ndiyo maajabu ya nchi yetu hii ya 'Mama Mizinguo'!
 
Athari kubwa zaidi ya Jaji kuteuliwa kuwa JK ni kwamba kesi hii itaenda taratibu sana.

Atakuwa na majukumu ya kiutawala ambayo ni mengi sana hivyo kesi haitasikilizwa mfululizo tena.

Hii kesi kama Jaji kiongozi ataendelea nayo itaisha 2023.
Huu ni upande ambao wengi wetu hatujaupa uzito stahiki, lakini naona mantiki yake ni nzito.

Maana yake ni kwamba Mbowe atakuwa jela kwa muda wote huo, na hapo hapo wakitegemea kuikata miguu CHADEMA wakati Mwenyekiti wao akiwa jela.

Inawezekana sana.
 
Huu ni upande ambao wengi wetu hatujaupa uzito stahiki, lakini naona mantiki yake ni nzito.

Maana yake ni kwamba Mbowe atakuwa jela kwa muda wote huo, na hapo hapo wakitegemea kuikata miguu CHADEMA wakati Mwenyekiti wao akiwa jela.

Inawezekana sana.
Watu wengi hawajaona hiyo side nyingine wanaangalia ngonjera na ramli tu.

Mwenyekiti wa Chama atakuwa ndani kwa muda wote huo huku Jaji anayesikiliza kesi akiwa kwenye majukumu mengine ya kiutawala.

Kibaya zaidi mkutano mkuu wa kikatiba wa chama ulitakiwa kufanyika July mwaka huu haujafanyika na msajili wa vyama ameshaanza chochoko za kuuliza kwanini chama hakijatoa maamuzi juu ya rufaa za kina Mdee.
 
Jaji kiongozi atazunguka hii nchi kufanya majukumu ya kiutawala, kesi itapigwa tarehe hadi basi, mwishowe Mbowe atoke 2024 huko
 
Nimekumbuka hypothesis formulation....
You have to create "VIRUS" and then "ANTIVIRUS".

Make sure also your "SUSPENSION" its well shaken.

NOTABENE: Make sure that your results of data interpretation & data recording are well buried.
 
Yericko umeandika kwa uchungu sana hadi umesahau kuweka bei ya kitabu cha UJASUSI WA KIUCHUMI.

Vyovyote itakavyokuwa maneno ya naibu balozi wa Ujerumani kwa Mbowr yataapply..."NEVER GIVE UP".
 
ILA NISEME KITU HAWA WOTE WENYE MAMLAKA NA WATEULIWA NA HIZO MAMLAKA UINGIA MISIKITINI NA MAKANISANI KUJINYENYEKEZA KWA MUNGU, ILA KWA KIGEZO CHA SIASA HAKUNA DHAMBI INAHALALALISHWA KUPITIA HUMO....AIDHA WAWE WANAFIKI (KAMA MAFARISAYAO) MBELE YA UMMA NA DINI WASIPOTENDA HAKI TUNA UFAHAMU NA LAANA ITAANZA HAPA KABLA YA KUFARIKI KWAO...WITNESS JIWE
 
Lakini haiwezi ikatafsiriwa kuwa ni rushwa ili atende anayotaka mteuzi, endapo kama cheo chake hicho kipya kitamwonyesha kubadilika na alivyokuwa mwanzo?

Matumaini yangu ni kwamba, huyu mtu ataendelea kufuata sheria, no matter what, na hiyo itamjengea heshima zaidi, kama alivyoanza kujipambanua wakati wa kesi ndogo.

Hata hivyo, lakini, kwa nini nia ya mteuzi iangaliwe katika upande mmoja tu wa kesi, kwamba uteuzi umepewa msukumo na kesi inayosikilizwa kwa upande wa mashtaka pekee?

Mteuzi anaweza kuwa kalenga upande wa utetezi.
Baada ya kuona kesi ilvyosimama, mteuzi naye anatafuta sehemu ya kudandia ili aonekane kuwa upande wa utenda HAKI!
Hapo atakuwa anajitafutia yeye na serikali yake sifa za kuonekana kuwa wanasimamia mabadiliko.
una hoja
 
Back
Top Bottom