Mambo ya kwa Babu LOLIONDO

Mambo ya kwa Babu LOLIONDO

Dah leo Babu Loliondo kutokana na foleni kuwa kubwa ikabidi awaambie watu wapange foleni tofauti ya UKIMWI kushoto na kisukari kulia. Unaambiwa mstari ule wa kushoto (Wa ukimwi) haukuwa na mtu hata mmoja, babu akafurahi kuwa waathirika wamepungua sasa akawa anataka kumwaga ile dawa ya ukimwi! Duh watu wakaanza kupiga kelele "hhaaaa babu usimwage bwana, huwezi jua babu acha bwana tuko hapa leo siku ya tano babu" ikabidi babu ashangae vipi tena!
 
Sifungamani na upande wowote! Anayeweza kumuepushia kiumbe taabu,mateso,maradhi n.k ni Mungu pekee. Dawa tutumiazo pamoja na njia nyingine kadha wa kadha ni sababu tu! Na ndio maana wapo wanaokunywa dawa na wakapona na wapo wanaokunywa dawa na wasipone!

Tujiulize uwezo Babu alionao umetoka wapi? Bila shaka ni Mungu ndio chanzo cha uwezo huo. Basi tuishi kwa imani, Mungu ni mkubwa!
 
Nimefuatilia kwa muda mrefu juu ya "tiba-miujiza" inayotolewa na Babu wa loliondo.Kwa wengi wanaomuunga mkono ni sabab "wanajihisi?" wameponywa na dawa hiyo kimuujiza,na wanaompinga n kutokana na asili/chanzo cha dawa hiyo.
Dawa ya babu ikipimwa kwa vigezo vya kibiblia inapwaya ndio maana wa kina kakobe,pengo,mwingra wanapinga dawa hiyo.Kwa wakristo kigezo cha muujiza wowote kutokea(kuonekana) uwe wa kupona au la si kigezo pekee/cha muhimu kujua nguv za miujiza asili yake ni Yesu,kwa kuwa hata shetan,nabii wa uongo ana ishara tena kubwa ambazo zinaweza kuwadanganya hata wateule(wakristo wa kweli)-soma Matayo 24:24, ufunuo 13:13
Biblia imeturuhus kupima nguv (roho) zinazofanya kaz kwa watu kama Babu-1 yoh 4:1,3.
Babu alijinadi kuwa ametumwa na Mungu(Yesu) na kibiblia muujiza,uponyaji,vinafanyika kwa mamlaka ya Jina la Yesu- Matendo ya mitume 3:6,filip 2:9.
Kutumia vitu ktk uponyaj kibiblia sio lazima, bali n sharti vifanywe ktk jina la Yesu maana ndilo lenye mamlaka.
HIVYO MUUJIZA WOWOTE WAWEZA KUTOKEA KWA JINA LA YESU BILA YA KUTUMIA MAJI-matendo 3:6.
Je Babu kama kweli ametumwa na Yesu anaweza kutumia jina la Yesu pekee(pasipo maji) na watu wakpata uzima?
Muujiza wa Yesu ni kwaajili ya kuwaonya watu,kuwafungua,na kuwafundisha wasitende dhambi tena-wamgeukie Yesu sio warudi makwao kama wametoka 'theatre' bila kutubu-Yohana 5:14
Tena,muujiza wa Mungu ni lazma umtukuze Yesu na sio Babu wa loliondo-matendo 3:9 ,luka 5:26,13:13
Muujiza wa Muungu hauuzwi hata kwa shiling 1-kwani mmepewa bure toen bure-kwanin babu auze?
Babu anatakiw kujib hoja kibiblia kama kweli yeye katumwa na Yesu kweli-2petro 3:15 Tuwen macho hiz n cku za mwisho.

good food for thought mpendwa. keep it up

Glory to God
 
Sijaelewa. Babu anatibu UMAK (Ukosefu wa Makombe Klabuni)?
 
Wana JF kuhusu tiba ya Loliondo na kauli tata kutoka makanisa ya kiroho msimamo wangu ndiyo huu,

  1. Kama babu ni roho itokayo kuzimu, nchi hii tuna mitume na manabii wengi kwa nini wasiombe Mungu wao akawajulisha kuhusu ukweli wa mchungaji mstaafu huyo badala ya kutoa hoja zisizo na mashiko. Mbona Kakobe alishawahi kusema kuwa Mrema ni chaguo la Mungu anashindwa nini kuomba Mungu ampe maono juu ya tiba hiyo kisha akawatangazia umma ili kutoa nusra kwa watu wanaokwenda kupata tiba. Kushindwa kuweka maono hii ni ishara ya kushindwa na kuanza kuona wivu wa kihuduma!
  2. Kama babu angejuwa tapeli asingekubali ku - charge Tshs 500.00 kwani roho ya kitapeli hujali mali, sifa na umimi kuliko hofu ya Mungu. Pia watu wasingekwenda kule ambako barabara na miundo mbinu ni mibovu kuliko maelezo, kisha uniambie watu wengi wawe wajinga kukubali shida na taabu bila mafanikio.
  3. Kutokana na hilo, upo uwezekano mkubwa wa kuchakachua huduma ile kwa kupanda mamluki kibao ambao watajifanya wanatoa huduma inayofanana na hiyo lakini mwisho wa yote kweli itajitenga.
  4. Mwisho, basi hao wachungaji wanaomuombea mabaya mchungaji Mungu wao hasikii, iwaje jambo nyeti kama hili ashindwe kuwajibu hali ya kuwa watu wanaendelea kupotea kwa mujibu wa mitazamo yao.
Ukisikiliza ushuhuda toka kwa watu waliotoka Loliondo ni lazima uwepo wa Mungu utakuwepo kule.
 
Inaonekana hakuna mtu aliye na ukweli juu ya tiba ya loliondo ila ni Mungu peke yake. Naomba tusitishe mjadala huu tujadili mambo mengine. Hii ni kwa sababu imefika hatua ya wengine kuwarushia wengine matusi badala ya kujibu hoja! Tumwachie Mungu atoweka wazi ukweli! Days will tell the truth. Mbarikiwe.
 
Adha ya maradhi ajuwaye ni mgonjwa. Tusikurupuke kulaumu na kukandia kwa kusukumwa na kiburi kinacholetwa na kuwa na afya njema. Taratibu jamani..taratibu.
 
Nimefuatilia kwa muda mrefu juu ya "tiba-miujiza" inayotolewa na Babu wa loliondo.Kwa wengi wanaomuunga mkono ni sabab "wanajihisi?" wameponywa na dawa hiyo kimuujiza,na wanaompinga n kutokana na asili/chanzo cha dawa hiyo.
Dawa ya babu ikipimwa kwa vigezo vya kibiblia inapwaya ndio maana wa kina kakobe,pengo,mwingra wanapinga dawa hiyo.Kwa wakristo kigezo cha muujiza wowote kutokea(kuonekana) uwe wa kupona au la si kigezo pekee/cha muhimu kujua nguv za miujiza asili yake ni Yesu,kwa kuwa hata shetan,nabii wa uongo ana ishara tena kubwa ambazo zinaweza kuwadanganya hata wateule(wakristo wa kweli)-soma Matayo 24:24, ufunuo 13:13
Biblia imeturuhus kupima nguv (roho) zinazofanya kaz kwa watu kama Babu-1 yoh 4:1,3.
Babu alijinadi kuwa ametumwa na Mungu(Yesu) na kibiblia muujiza,uponyaji,vinafanyika kwa mamlaka ya Jina la Yesu- Matendo ya mitume 3:6,filip 2:9.
Kutumia vitu ktk uponyaj kibiblia sio lazima, bali n sharti vifanywe ktk jina la Yesu maana ndilo lenye mamlaka.
HIVYO MUUJIZA WOWOTE WAWEZA KUTOKEA KWA JINA LA YESU BILA YA KUTUMIA MAJI-matendo 3:6.
Je Babu kama kweli ametumwa na Yesu anaweza kutumia jina la Yesu pekee(pasipo maji) na watu wakpata uzima?
Muujiza wa Yesu ni kwaajili ya kuwaonya watu,kuwafungua,na kuwafundisha wasitende dhambi tena-wamgeukie Yesu sio warudi makwao kama wametoka 'theatre' bila kutubu-Yohana 5:14
Tena,muujiza wa Mungu ni lazma umtukuze Yesu na sio Babu wa loliondo-matendo 3:9 ,luka 5:26,13:13
Muujiza wa Muungu hauuzwi hata kwa shiling 1-kwani mmepewa bure toen bure-kwanin babu auze?
Babu anatakiw kujib hoja kibiblia kama kweli yeye katumwa na Yesu kweli-2petro 3:15 Tuwen macho hiz n cku za mwisho.
Uchambuzi wako umekaa kimaslahi zaidi just like those statements from Pengo et al.

Mbona Yesu alitumia tope kumponya kipofu?Kwanini asingesema tu mimi ni Yesu,nakuamuru upate kuona?
Tatizo ni kwamba unataka ukishawahudumia watu basi na kanisa uanzishe kimaslahi,hao maaskofu wanhofu tu kuhusu congregations zao na si eti kwamba miujiza yenye Yesu haitumii vitu!

Biblia inasema kila mtu atakula kwa jasho lake,jasho la babu ni lipi?

Hata mara nyingine watu wakipitia mambo magumu ie magonjwa yanayohitaji upasuaji,halafu upasuaji huo ukawa wa mafanikio,basi huchukuliwa kama ni muujiza kwa muumini aliyefanyiwa upasuaji huo....Kuna wanaomeza dawa wakipona wanamshukuru Mungu na Yesu kwa muujiza wa uponyaji.

Tuachane na maslahi kwenye issue za kiimani.
 
Uchambuzi wako umekaa kimaslahi zaidi just like those statements from Pengo et al.

Mbona Yesu alitumia tope kumponya kipofu?Kwanini asingesema tu mimi ni Yesu,nakuamuru upate kuona?
Tatizo ni kwamba unataka ukishawahudumia watu basi na kanisa uanzishe kimaslahi,hao maaskofu wanhofu tu kuhusu congregations zao na si eti kwamba miujiza yenye Yesu haitumii vitu!

Biblia inasema kila mtu atakula kwa jasho lake,jasho la babu ni lipi?

Hata mara nyingine watu wakipitia mambo magumu ie magonjwa yanayohitaji upasuaji,halafu upasuaji huo ukawa wa mafanikio,basi huchukuliwa kama ni muujiza kwa muumini aliyefanyiwa upasuaji huo....Kuna wanaomeza dawa wakipona wanamshukuru Mungu na Yesu kwa muujiza wa uponyaji.

Tuachane na maslahi kwenye issue za kiimani.

nawahurumia watu wengi sana wanapotea kwa kukosa maarifa!

ooh, God have mercy on your people!
 
Inaonekana hakuna mtu aliye na ukweli juu ya tiba ya loliondo ila ni Mungu peke yake. Naomba tusitishe mjadala huu tujadili mambo mengine. Hii ni kwa sababu imefika hatua ya wengine kuwarushia wengine matusi badala ya kujibu hoja! Tumwachie Mungu atoweka wazi ukweli! Days will tell the truth. Mbarikiwe.

jibu liko kwenye maneno ya Mungu mpendwa. acha uvivu, kasome utaelewa. achana na watu wanaoongea kw ahisia bila ufahamu. ni neno la Mungu pekee litakalokuondolea wasiwasi. imani bila neno la Mungu si imani ya kumpendeza Mungu kwani waabudu halisi watamwabudu katika roho na kweli. zingatia kuwa kweli ni neno la Mungu, basi hakuna zaidi. si miujiza wala ndoto, ni NENO LA MUNGU.

ubarikiwe sana

Glory to God
 
Back
Top Bottom