Mambosasa ajibu maswali ya Rais Magufuli kuhusu kutekwa Mo Dewji

Mambosasa ajibu maswali ya Rais Magufuli kuhusu kutekwa Mo Dewji

Afwande Mambosasa umeeleweka sana tu
Afande.jpeg
 
Hii nchi ina sinema nyingi sana...
Ndio maana tunashika nafasi ya pili Afrika kwa kuzalisha filamu kwa wingi. Nigeria wanaongoza. Lakini kwa hali hii tunaweza kuwapiku muda si mrefu. Tatizo la filamu zetu ni ubora.
 
Haifiki ijumaa atapangiwa kazj nyingine believe me.
 
undefinedasije tu kwenda kuwa constable kule Nanyumbu...undefinedIla kafanya vizuri kunawa mikono
Pamoja na jibu alilotoa halitampendeza malaika, ila kafanya jambo jema kujitoa
 
Kwetu sisi wataalam wa Lugha na itifaki za Kiserikali, kauli ya mambo sasa ni utovu wa nidhamu si tu kwa Mkuu wa nchi Bali kwa Amiri Jeshi Mkuu.

Mambo sasa alipaswa kusema "maneno yaliyosemwa na Mkuu ya nchi si ya kupuuzwa bali yanapasa kitutafakarisha kama kuna sehemu tumekosea au tulikosea tujisahihishe". Hiyo ingekuwa kauli ya Afisa wa Jeshi kwa amiri Jeshi Mkuu.

Otherwise Mambosasa anapaswa kuchukuliwa hatua stahiki, tusubiri tuone!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata kama Anasingiziwa Achutame tuuu....!?, huyo anaekosea-kosea kwa kuto shaurika atajuaje kama anakosea?.ama ye ni Malaika Mweusi aishie juu ya ubinadamu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiofisi ni vizuri boss au junior kuwasiliana kiofisi kulikoni kujibizana au kutuhumiana hadharani .Naona kuna kitu hakiko sawa.Public sio ofisi.Mafaili yapo boss aandike junior ajibu.Haya mambo ya kuanikana hadharani na kujibizana hadharani kati ya mabosi na ma subordinate wao ni ukosefu wa nidhamu za kiofisi na lazima ukataliwe usiote mizizi . Taratibu za mawasiliano ya kiofisi yaheshimiwe na yatumike kwa wote mabosi na juniors.Kitu haliko sawa uliza kiofisi ujibiwe na junior kama kuna kitu hukioni sawa kiekezee kiofisi.Ndio maana vyuo vyote hufundisha business communication kwa kozi zote za sayansi na Arts ili zitumike zaidi

Jiwe ndio tatizo kwa kutaka kick public. Huu ni udhibitisho vyombo vya kimamlaka huwa haviwajibiki kwa umma bali kwa rais kwenye maagizo toka juu. Hayo rais aliyomuambia Mambosasa huwa tunahoji humu jukwaani kila siku lakini hamna majibu zaidi ya ubabaishaji. Leo rais kahoji ndio mambo sasa anaona ni wakati wa kujibu.
 
Mambosasa angekaa kimya tu,wenye akili zetu,tunajua hapa anatafutwa MTU wa kutolewa kafara,
Haiwezekani,ishu ya Mo,IGP asijue,DCI asijue,TISS wasijue,na wote wana ripoti kwa Mkulu,
Hii ni kama Ishu ya kikokotozi cha mafao,upuuzi ulifanywa na Waziri,Mkurugenzi wa SSRA akatolewa kafara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa muda nilivaa viatu vya rais halafu nikawa nasoma alichonijibu, nikajikuta napandwa na hasira kali, nikachukua simu nimpigie igp ili ampeleke akawe analinda magodown, ndipo nikagundua mimi si rais na hata namba ya igp sina, dah!

Rais si Mungu.
 
Lile picha walilocheza wakimuhusisha dreva teksi la kishamba sana. Yaani limewaacha uchi kabisa na kituko mbele ya jamii.
Kwa sasa ni afadhali wanyamaze tu maana watu washamwachia Mungu.
Wakijaribu kuleta muvi nyingine maana naona mkuu wa kaya keshaichomekea wataumbuka zaidi na kutonesha kidonda ambacho kishageuka kovu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku chache baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kuibua maswali juu ya tukio la kutekwa Mfanyabiashara Mohamed Dewji Kamanda wa Polisi Dar es salaam Lazaro Mambosasa amejitokeza na kusema yeye alishamaliza kazi yake.


Mambosasa amesema baada ya yeye kumaliza kazi yake alikabidhi kwa viongozi wake wa juu na kwa sasa wanaojua kinachoendelea ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ambaye anatakiwa kutoa taarifa za uchunguzi zilizowasilishwa kwake.

Mambosasa amesema, “kuhusu maelekezo ya Rais aliyoyatoa kuhusu kutekwa kwa Mo, maadamu aliyatoa mbele ya Mkuu wetu wa Jeshi la Polisi na DCI ambao walikuwepo, jalada hilo lilishafika kwao, huko ndiko wanakojua kinachoendelea".

“Mimi jukumu langu lilishakwisha kwa hiyo ni suala la maamuzi ya juu kuhusu hatua zilizofikiwa kwenye jalada hilo", ameongeza Kamanda Mambosasa.

Mapema juzi Ikulu akiwaapisha Makamshna wa juu wa Jeshi la Polisi, Rais Magufuli alisema, "Jeshi la Polisi linatakiwa kuelewa kuwa Watanzania sio wajinga, kama suala la kutekwa kwa Mo Dewji linaacha maswali, tuliambiwa alitekwa na wazungu lakini lilipoisha haikueleweka, mwishoni aliyetekwa alionekana anakunywa chai na Mambosasa."
Sikujua kama jpm ni muigizaji mzuri kiasi hiki!
 
Kumbe rais ndiye anatuona watanzania ni wajinga. IGP anayempa maagizo ya kuwashughulikia maRPC wazembe kama Mambosasa ndiye aliyekalia taarifa. Shubamiti!
 
Mambosasa hawezi kutumbuliwa kwani anaijua picha yote na wakizidi kumprovoke ataharibu kila kitu kuhusu scandal name huenda akawataja wahusika ili kama mbwai na iwe!
Nami namtia moyo kuwa usikubali kulibeba peke yako na ikibidi itisha press ujisafishe!
Nyakati nyingine, ninyi watu wazima mliobakisha miaka miwili au mitano kustaafu mbona kama akili zenu mnaziachaga home wakati wa kwenda kazini? Mnakubalije kufanya dili na watoto wadogo?
 
Mambosasa angekaa kimya tu,wenye akili zetu,tunajua hapa anatafutwa MTU wa kutolewa kafara,
Haiwezekani,ishu ya Mo,IGP asijue,DCI asijue,TISS wasijue,na wote wana ripoti kwa Mkulu,
Hii ni kama Ishu ya kikokotozi cha mafao,upuuzi ulifanywa na Waziri,Mkurugenzi wa SSRA akatolewa kafara

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa akikaa kimya si ndio lawama zitamwangukia??
Jiwe anajua kila kitu ila anapangua kishamba.
 
Kwetu sisi wataalam wa Lugha na itifaki za Kiserikali, kauli ya mambo sasa ni utovu wa nidhamu si tu kwa Mkuu wa nchi Bali kwa Amiri Jeshi Mkuu.

Mambo sasa alipaswa kusema "maneno yaliyosemwa na Mkuu ya nchi si ya kupuuzwa bali yanapasa kitutafakarisha kama kuna sehemu tumekosea au tulikosea tujisahihishe". Hiyo ingekuwa kauli ya Afisa wa Jeshi kwa amiri Jeshi Mkuu.

Otherwise Mambosasa anapaswa kuchukuliwa hatua stahiki, tusubiri tuone!

Sent using Jamii Forums mobile app
Serikali za kinafiki ndio watendaji wake wanabeba lawama za wakubwa.
Sasa wewe ulitaka Polisi ichukue lawama wakati tatizo sio lao??
Huu unafiki hautatui matatizo.
 
Back
Top Bottom