Mambosasa ajibu maswali ya Rais Magufuli kuhusu kutekwa Mo Dewji

Mambosasa ajibu maswali ya Rais Magufuli kuhusu kutekwa Mo Dewji

Hii move ni ngumu sana kuliko move zote wachezazo,maana kipengele kigumu ni kumpata Mzungu halisi wa kucheza episode 3.Heri wangekaa kimya ipite hivyo hivyo, s
 
wangezungumzia pia na ubora wa zile picha za cctv camera
 
Mambosasa alihitimisha kazi yake vizuri sana kwa kunywa chai na mhanga! Sijui mnataka aseme nini zaidi.
 
Mambosasa hupaswi kumjibu mkuu wako wa kazi namna hiyo.

Hiyo tunaita Gross Insubordination! !
 
Kwa hiyo rais hayupo informed? By the way kuna mambo ambayo Mambosasa hajaya ongelea ambayo rais aliya lalamikia.
1. Mazingira ya upatikanaji ya mtekwaji
2. Mambosasa kuonekana anakunywa chai na mtekwaji.
Hayo ndiyo alitakiwa kuyatolea ufafanuzi
 
Kwetu sisi wataalam wa Lugha na itifaki za Kiserikali, kauli ya mambo sasa ni utovu wa nidhamu si tu kwa Mkuu wa nchi Bali kwa Amiri Jeshi Mkuu.

Mambo sasa alipaswa kusema "maneno yaliyosemwa na Mkuu ya nchi si ya kupuuzwa bali yanapasa kitutafakarisha kama kuna sehemu tumekosea au tulikosea tujisahihishe". Hiyo ingekuwa kauli ya Afisa wa Jeshi kwa amiri Jeshi Mkuu.

Otherwise Mambosasa anapaswa kuchukuliwa hatua stahiki, tusubiri tuone!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mambonow kagoma kuwa mbuzi wa kafara. Hii movie ni kama ile ya Kikokotoo.

Kawaida lazima atupiwe mtu pira ili mkuu awe msafi. Hili limemuangukia Mambonow

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku chache baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kuibua maswali juu ya tukio la kutekwa Mfanyabiashara Mohamed Dewji Kamanda wa Polisi Dar es salaam Lazaro Mambosasa amejitokeza na kusema yeye alishamaliza kazi yake.


Mambosasa amesema baada ya yeye kumaliza kazi yake alikabidhi kwa viongozi wake wa juu na kwa sasa wanaojua kinachoendelea ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ambaye anatakiwa kutoa taarifa za uchunguzi zilizowasilishwa kwake.

Mambosasa amesema, “kuhusu maelekezo ya Rais aliyoyatoa kuhusu kutekwa kwa Mo, maadamu aliyatoa mbele ya Mkuu wetu wa Jeshi la Polisi na DCI ambao walikuwepo, jalada hilo lilishafika kwao, huko ndiko wanakojua kinachoendelea".

“Mimi jukumu langu lilishakwisha kwa hiyo ni suala la maamuzi ya juu kuhusu hatua zilizofikiwa kwenye jalada hilo", ameongeza Kamanda Mambosasa.

Mapema juzi Ikulu akiwaapisha Makamshna wa juu wa Jeshi la Polisi, Rais Magufuli alisema, "Jeshi la Polisi linatakiwa kuelewa kuwa Watanzania sio wajinga, kama suala la kutekwa kwa Mo Dewji linaacha maswali, tuliambiwa alitekwa na wazungu lakini lilipoisha haikueleweka, mwishoni aliyetekwa alionekana anakunywa chai na Mambosasa."
Heeh! Anamjibu amiri jeshi mkuu? Maajabu haya
 
Kwetu sisi wataalam wa Lugha na itifaki za Kiserikali, kauli ya mambo sasa ni utovu wa nidhamu si tu kwa Mkuu wa nchi Bali kwa Amiri Jeshi Mkuu.

Mambo sasa alipaswa kusema "maneno yaliyosemwa na Mkuu ya nchi si ya kupuuzwa bali yanapasa kitutafakarisha kama kuna sehemu tumekosea au tulikosea tujisahihishe". Hiyo ingekuwa kauli ya Afisa wa Jeshi kwa amiri Jeshi Mkuu.

Otherwise Mambosasa anapaswa kuchukuliwa hatua stahiki, tusubiri tuone!

Sent using Jamii Forums mobile app
Na ndio ujue hata jiwe linao elites ambao wao hawaguswi wengine hakuna kuuliza. Kama kweli anapambana na rushwa IGP alipaswa kuwa nje ya ofisi hawa ndio kielelezo cha rushwa nchini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna TAASISI ambazo huwa ni kichaka cha ukiritimba ofisi ya DCI,TRA na ARDHI.Usiombe uendwe taasisi hizo hawakawii kukuambia faili lako limepotea
 
Kwa hiyo rais hayupo informed? By the way kuna mambo ambayo Mambosasa hajaya ongelea ambayo rais aliya lalamikia.
1. Mazingira ya upatikanaji ya mtekwaji
2. Mambosasa kuonekana anakunywa chai na mtekwaji.
MO AMEWEZAJE KULETWA MPAKA GYMKHANA USIKU ULE BILA WATEKAJI KUKAMATWA TENA NA GARI LINALO FANANA NA LILE LILE LA POLISI WALILOLITILIA SHAKA?
MAMBOSASA AMEWEZAJE KUNYWA CHAI KABLA YA KUWAKAMATA WATEKAJI?
 
Back
Top Bottom