Ungesoma posts vizuri zilizopita ungeona nini kilileta group na umekuta nilikutumia mwaliko ukajiunga.
Hakuna tabu naweza kuliamishia kwenu, nasubiri warumi ambaye pia nilimtumia kujiunga akijiunga nalihamishia kwake yeye ndie ataweza au pia nifah au mwingine yoyote.
Kuna wambea kama 10 bado hawajakubali au hawajaona request ya kujiunga wakajiunga zipo pending.
Au mtachagua nani ashike usikani. Hakuna tabu
ok nimekupata haina shida hata ukiwa wewe ulieanzishaa ,sema Tu wambea wa east Afrika hatukupewa taarifa kua group linaanza,nimekupata hakuna kinachoharibikaaa
Cheki PM, shukurani.
Jamani sio kila mtu anaalikwa, kitu cha special invitees, yani humo wambea first class tu, chezeya weye, tumepanda bei siku izi hahaa ahaha, ngoja nikajiunge kwenye website, nataka nishushe vitu matata mpaka picha humo, nataka nizindue kwa kishindooo
Hahahahahaa, hatutaki id's mpya.Na wao wajiunge waanzishe lao au wakomae huku halafu tutawaangalia kama wanafaa.
Jamani hili jambo sio mchezo, hasa tukiwa tunaelekea kwenye ile sheria inabidi tupate uhuru.
Huku jukwaani hatujiamini hadi tunaanza kuongea mafumbo mtu unachekecha kichwa kama uko kwenye chumba cha mtihani.....
Ndio maana hizi id tusizozijua tuachane nazo kabisa, wengine usalama wa taifa, ohoooo!
Hahahah nashangaa
Mnataka screen shot zangu nizirushe wapi???
Hahahah
Wambea waheshimiwa, halafu wote tukishajiunga, tunaanza kuchagua viongozi wa juu mpaka chini, ukiwa unatega sana kundini bila sababu tunaku terminate fasta, yani humo full balaa yani
Itabidi atupe taarifa.Haiwezekani wakubaliwe watu tusiowajua.
Mods wameamua kutukomesha kabisa hivi hawaoni au kuna shida gani.
Wambea waheshimiwa, halafu wote tukishajiunga, tunaanza kuchagua viongozi wa juu mpaka chini, ukiwa unatega sana kundini bila sababu tunaku terminate fasta, yani humo full balaa yani
Inabidi tujijue kwa kweli, sio kila mtu anaingia, wengine waandishi wa habar humu, maana nataka nianzishe topic hot zile kabisa kwa ajili ya kutambulisha group letu, au sio wambea wenzangu?
Ha ha ha ha ha warumi utaua watu jamani!
Basi kuna mtu huku jana tulimsema sio mbea leo nikamkuta sehemu anapiga umbea.Hili group litaleta balaa humu.
NDIOOOOOO! Uwiiiiii warumi ndio maana nakupendaga.
Tumechoka umbea wa JF kuandikwa kwa shigongo kila siku.Sasa hivi watatukoma.
Watajibeba mwaka huu *****, au sijui niweke kule instagram sasa ivi? Maana ule umbea mrefu na picha juu nakwambia, nimeweka private kule au mnaonaje?
Hahahahahaa, watajuuuta maana mimi ndiye group Admin.
Hakuna mbea mpya huko, watanichukiaje jamani?
Lawama zikizidi nitampa mtu mwingine ila kwa sasa wajipange sana.Kuna mvimba macho mmoja asahau tu hilo group maana sitomkubalia hata akiwaambia mods!....uwiiiiiii!