Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Watu unaodhani wapo na wewe hawapo na wewe,hilo ni kundi lenye itikadi ya mrengo wa kushoto.
Ni kundi Toxic,lililoathiriwa na fifth phase administration,ni kundi linaloamini Tofauti na unavyoamini wewe.
Hata namna unavyoendesha Serikali hili kundi linakupinga kimya kimya, Report ya CAG wanaamini imelenga kumchafua Hayati, wanaamini wewe ulikuwa kinyume na Hayati ndo maana CAG kaanika hayo madudu.
Kwanza hawaamini kuwa kifo cha Magufuli ni kazi ya Mungu bali wanaamini kuwa kuna hujuma imefanyika.
Hili ni kundi ambalo baadhi yao wengi Tu umewapa vyeo vikubwa.
Baadhi yao wanadiriki kusema kuwa wewe siyo CCM halisi,Eti utakuwa CHADEMA ,yote hii hawataki wala kusikia Hayati anakosolewa.
Walimuona mungu mtu asiyeweza kukosea lolote.
Hawa ndo wanajipanga kuusaka Urais 2025, ndo hawa hawa waliokuwa wanakupiga majungu usifike ili usifike hapo ulipo.
Wataalamu wa ujasusi wana slogan yao inasema,"once an enemy always an enemy".
Usitarajie hao watu wakakupenda au kukuunga mkono, Kwanza hapo walipo wamechanganyikiwa,hawajui la kufanya,hawana uwezo tu kwa sababu upo juu yao.
Ushauri wangu kwako, ni huu.
1.Ifumue TISS yote kuanzia DGS hadi chini yaani from the Top to the Bottom.
2.Teua mawaziri wapya wote sambamba na wakuu wa mikoa na wilaya.
3.Usipuuze mawazo ya wapinzani
MUHIMU
CDF aendelee kuwa Mabeyo,na hata muda wake ukiisha mwongezee,na zaidi ya yote huyu mzee mwongeze mshahara,anakufaa sana,IGP hana shida yoyote pia.
Message sent and Delivered
Hawa wachonganishi ,kwa kawaida ni watu wenye wivu,fitina na roho mbaya.Hawa ni wengi sana makazini.Hawa ,baadae ndio watampinga mama pia.
 
Please I do not want your ignorance, and do not follow me the great mule you

Tuheshimiane tafadhari
Ukiandika ujknga lazima utapingwa kwa lugha ileile uliyo itumia.
 
Habari za wakti huu;

Kwanza kabisa nimpe Pole mama yangu ,Samia Hassan Suluhu kwa kuondokewa na Boss wake,Lakini zaidi nimpe hongera kwa kupata fursa ya kuwa RAIS wa Jamhuri katika kipindi ambacho Jemadari mwendazake JPM alikuwa ameweka moja kati ya malengo makubwa sana(Most ambitious goals of the Modern Tanzania) ya kutaka kufanya Tanzania iwe nchi ya kisasa.Lakini Pia niseme tu kwamba Mwendazake JPM amemuachia TAIFA ambalo kwanza ni divided yet united.Lakini pia anayo kazi ya Pembeni ya kufanya Damage control and healing

Sasa nirudi kwenye mada kuhusu nzi.Kuna nzi wengi sana ambao wamezagaa na najua mpaka wakati huu wengi tayari wameshaanza kujisogeza karibu.Kuna nzi wa aina mbili ambao wanajisogeza kwa kasi sana karibu na RAIS wetu Mama Samia Suluhu Hasan

Nzi wa Aina ya kwanza ni wale ambao walinufaika na Mfumo uliokuwepo zama za Magufuli ambao wanatafuta kila namna kuhakikisha kwamba Maslahi na fursa walizokuwa nazo kisiasa,kijamii na kiuchumi zinaendelea kuwepo na kuna wale Nzi ambao hawakupendezwa na mfumo ule na wengine hata kama waliufaidi lakini hawakuupenda na wengine ambao waliumia na hawakunufaika nao na ambao nao wanasogea kwa kasi kabisa ili waweze kubadili uelekeo wa Upepo.Hawa nzi wote ni nzi hatari sana kwa mustakabali wa taifa letu.

Najua wachache wa nzi hawa unawajua ila pia najua kuna ambao huwajua au hujaweza kuwatambua ila jihadhari nao.Mheshimiwa RAIS ninapoandika waraka huu ninawaona jinsi wanavyoweka mikakati, wengine wanafuatilia historia yako kujua kama kuna kitu wanaweza kukitumia ili kukufikia kwa urahisi uweze kusikia ushauri wao. Mimi nakusisitizia waepuke hawa nzi.Kazi uliyo nayo ni kubwa sana.

Mheshimiwa RAIS, Wewe ni mrithi wa Magufuli na jamii haitakuelewa kama utaachia kusimamia yale mema ambayo Mwendazake Magufuli aliyasimamia.Usije kushawishika kudharau kukamilisha baadhi ya miradi ambayo ina tija ambayo iko katika hatua za utekelezaji kwani utajishushi heshima yako wewe na utakuwa umeitukana kumbukumbu ya mtangulizi wako JPM ambaye kifo chake kimekupa nafasi ya kuwa rais wa nchi.

Hata hivyo usiogope kuonesha tofauti hasa katika maeneo ambayo kwa hakika Mtangulizi wako hakuwa sahihi.Ndio hakuwa mkamilifu.Kuna baadhi ya mambo mengi sana yanahitaji kurekebishwa na usiogope kuwa tofauti kwani wewe unayo haki ya kuweka tone ya uongozi wako.

Naendelea kukusisitiza kwamba kwa sasa litazame Baraza la Mawaziri, kuna watu hawatakiwa kabisa kuwa humo,watakuvuruga.Kumbuka moja kati ya heshima kubwa uliyo nayo ni kuwa makamu mwenyekiti wa Bunge la Katiba Mpya.Nafasi hio inakupa jukumu moja kubwa nalo ni kuukamilisha mchakato ule na kuhakikisha sauti ya wananchi inasikiwa.

Mama Samia, Wewe ni Mzanzibari, tena Mzanzibari kweli kweli Usisahau hilo.Fanya Jambo kuhusu Zanzibar

Sitaki kusema zaidi ila kama nikajaliwa nitaongeza mengine ila kwa sasa nikutakie kila la heri katika kazi yako ya kuendesha nchi yetu

Mungu Ibariki Tanzania

Mungu Mbariki Mh. Samia H. Suluhu

Rais wa JMT
Huwa napenda kuona mtu anayebalansi habari/uchambuzi.
Pakukosea anakosea na pa kusifia anasifia pia
 
RAIS SAMIA ATAFANYA YAFUATAYO KATIKA UONGOZI WAKE

1. Kudhibiti mfumuko wa bei.

2. Kuboresha mazingira ya uwekezaji.

3. Kuimarisha uzalishaji na usalama wa chakula.

4. Kuimarisha upatikanaji wa mbolea nchini.

5. Kuimarisha mbinu za kupambana na nzige.

6. Kuimarisha kilimo cha umwagiliaji.

7. Kuimarisha vyama vya ushirika.

8. Kuimarisha uzalishaji wa mbegu zinazoongeza upatikanaji wa malighafi zinazotumiwa kutengeneza mafuta ya kula.

9. Kuhamasisha ufugaji wa kisasa.

10. Kuimarisha uvuvi wa bahari kuu.

11. Kuimarisha sekta ya utalii.

12. Kuimarisha uwekezaji wa kimkakati katika madini.

13. Kuwaendeleza wachimbaji wadogo wa madini.

14. Kusimamia masoko ya madini.

15. Kusimamia usambazaji umeme vijijini.

16. Kusimamia ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima (Uganda) hadi Chongoleani (Tanga, Tanzania).

17. Kuimarisha sekta ya viwanda.

18. Kupanua wigo wa masoko ya ndani na nje ya nchi ili wakulima na wafanyabiashara wanufaike.

19. Kutekeleza mipango ya upangaji, upimaji na umilikishaji ardhi.

20. Kujenga madaraja maeneo mbalimbali.

21. Kujenga na kukarabati viwanja vya ndege.

22. Kununua ndege tatu mpya.

23. Kujenga na kukarabati barabara.

24. Kujenga na kukarabati nyumba na majengo ya serikali.

25. Kuendeleza ujenzi wa reli ya kisasa (SGR).

26. Kuingiza nchini vichwa vya treni na mabehewa.

27. Kuboresha bandari za Dar, Mtwara na Tanga.

28. Kuongeza matumizi ya teknolojia ya mawasiliano ya kasi.

29. Kuinua kiwango cha ubora wa elimu.

30. Kuimarisha utoaji mikopo ya elimu ya juu.

31. Kujenga na kukarabati miundombinu ya elimu ili kuongeza fursa za upatikanaji wa elimu nchini.

32. Kusambaza vifaa vya kufundishia na kujifunzia.

33. Kutoa mafunzo kazini kwa walimu na wakufunzi.

34. Kukamilisha miradi 924 ya maji inayoendelea kujengwa nchini.

35. Kuanza utekelezaji wa miradi ya maji katika miji 28.

36. Kuboresha huduma za maji jijini Dodoma kwa kujenga bwawa la Farkwa.

37. Kutekeleza mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi mkoani Simiyu.

38. Kutekeleza miradi ya maji na mazingira Dar, Mara, Kilimanjaro, Arusha na Mwanza.

39. Kuendeleza utekelezaji wa Hospitali za Rufaa za Kanda mbalimbali na Hospitali maalumu.

40. Kuendeleza ujenzi na ukarabati wa hospitali za Halmashauri 102, vituo vya afya 487 na ujenzi wa zahanati 1,198.

41. Kununua mitambo 12 yenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya mitungi 200 ya hewa ya oksijeni kwa siku.

42. Kuendelea kuimarisha huduma za kibingwa nchini.
43. Kuendeleza uboreshaji wa miundombinu ya vituo vya kutolea huduma za afya unaoendelea kote nchini.

44. Kuendelea kuliimarisha na kuliongezea uwezo JWTZ na Majeshi mengine.

45. Kuendelea kuboresha mazingira ya kazi na wafanyakazi.

46. Kuziimarisha taasisi za Hifadhi ya Jamii ili ziwanufaishe wafanyakazi.

47. Kuhakikisha asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri inawafikia walengwa.

48. Kuendelea kuratibu utekelezaji wa masuala ya ukuzaji ajira na kazi za staha.

49. Kuuendeleza Mji wa Serikali Mtumba – Dodoma.

50. Kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI.

51. Kuendeleza mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

52. Kuimarisha mikakati ya kuzuia, kupunguza, kujiandaa na kukabili maafa pindi yanapotokea.

53. Kuimarisha mikakati ya kuhifadhi mazingira.

54. Kuendeleza vita dhidi ya rushwa na ufisadi.

55. Kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali za muungano.

56. Kuimarisha mahusiano baina ya Tanzania na mataifa mengine pamoja na mashirika/jumuiya za kikanda na kimataifa.
57. Kuimarisha utamaduni, michezo na Sanaa.🇹🇿🇹🇿
 
Hizi kelele na miluzi mingi zitakuangusha ktk uongozi wako. Vunja Baraza la mawaziri unda upya, hizi kelele za kina musiba kibajaji, musukuma zitaisha. Watakuogopa.

Sasa hivi Kuna kelele nyingi wengine wanakukubali lakini lipo kundi la wachache hawakukubali kabisa.

USIPOZIBA UFA UTAJENGA UKUTA
 
Hizi kelele na miluzi mingi zitakuangusha ktk uongozi wako.
Vunja Baraza la mawaziri unda upya, hizi kelele za kina musiba kibajaji, musukuma zitaisha.
Watakuogopa.

Sasa hivi Kuna kelele nyingi wengine wanakukubali lakini lipo kundi la wachache hawakukubali kabisaaa
USIPOZIBA UFA UTAJENGA UKUTA
Haitakiwi wamuogope inapaswa wamheshimu
 
Hizi kelele na miluzi mingi zitakuangusha ktk uongozi wako.
Vunja Baraza la mawaziri unda upya, hizi kelele za kina musiba kibajaji, musukuma zitaisha.
Watakuogopa.

Sasa hivi Kuna kelele nyingi wengine wanakukubali lakini lipo kundi la wachache hawakukubali kabisaaa
USIPOZIBA UFA UTAJENGA UKUTA
Mbowe lini anavunja chadema ili aunde upya?
 
Tunafunga ramadhan kwanza. Muda huu tunatumia pia kuchuja maoni yote yakiwemo ya wenye mihemko kama wewe. Pia hatuongozwi na sosho midia isipokuwa utashi wa kiasi kadiri mama anavoamini.
 
Back
Top Bottom