Makonde plateu
JF-Expert Member
- Nov 19, 2022
- 1,443
- 3,480
Kufuatia kifo cha ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoani Arusha, Richard Walalaze aliyedaiwa kujiua kwa kujirusha kutoka ghorofani, familia ya marehemu imeibua mpya baada ya kuuona mwili wake katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Bombo na kufuatilia mahali ulipokutwa mwili huo hotelini.
Familia hiyo imesema haiamini kama kweli alijirusha na kueleza kuwa kifo chake kinatia shaka na kubainisha kuwa imejikuta ikiwa na maswali mengi yasiyo na majibu, hivyo inasubiri taarifa ya uchunguzi wa mwili itakapotolewa na Serikali.
Msemaji wa familia hiyo, kaka wa marehemu, Godfrey Walalaze, ambaye ni mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki amesema hayo akiwa katika Hospitali ya Bombo na kubainisha kuwa mazingira ya kifo cha ndugu yao yanatia shaka iwapo ni kweli alijirusha kutoka ghorofani au la.
"Tumeuchunguza mwili tunapata shaka, sababu ukiacha kovu kichwani, mwili wote hauna mchubuko wala hakuna kiungo chochote kilichovunjika, lakini hata pale hotelini ulipokutwa mwili na michirizi ya damu inatupa maswali mengi mno," alisema Walalaze.
Kitenge Updates
Familia hiyo imesema haiamini kama kweli alijirusha na kueleza kuwa kifo chake kinatia shaka na kubainisha kuwa imejikuta ikiwa na maswali mengi yasiyo na majibu, hivyo inasubiri taarifa ya uchunguzi wa mwili itakapotolewa na Serikali.
Msemaji wa familia hiyo, kaka wa marehemu, Godfrey Walalaze, ambaye ni mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki amesema hayo akiwa katika Hospitali ya Bombo na kubainisha kuwa mazingira ya kifo cha ndugu yao yanatia shaka iwapo ni kweli alijirusha kutoka ghorofani au la.
"Tumeuchunguza mwili tunapata shaka, sababu ukiacha kovu kichwani, mwili wote hauna mchubuko wala hakuna kiungo chochote kilichovunjika, lakini hata pale hotelini ulipokutwa mwili na michirizi ya damu inatupa maswali mengi mno," alisema Walalaze.
Kitenge Updates